Ongezeko la Ukimwi Morogoro na sababu zake

Candid Scope

JF-Expert Member
Nov 8, 2010
11,883
6,884
Morogoro+image.jpg

images (1).jpg images (2).jpg images (3).jpg
images (4).jpg images (5).jpg images (6).jpg

Ongezeko la Ukimwi Morogoro na sababu zake

Manispaa ya Morogoro ni moja ya maeneo ambayo yameathiriwa na Ukimwi ambao kichocheo chake kikubwa ni mwingiliano wa kibiashara yakiwamo magari makubwa kama malori ambayo huegeshwa mjini humo likiwamo eneo maarufu la Itigi.

Eneo hili limekuwa maarufu kwa umalaya kwani nyakati za usiku malori mengi huegeshwa katika maeneo hayo na kuwa kishawishi kikubwa kwa baadhi ya watu wakiwamo vijana hasa wasichana ambao wamekuwa wakishiriki biashara ya ngono.

Kinadada kutoka kila kona ya Morogoro hufika Itigi kwa kufanya biashara hiyo ya uchangudoa.

Miongoni mwao wamo wanafunzi kutoka vyuo mbalimbali vilivyoko Morogoro ambao hujihusisha na ngono. Vijana hao wasomi wa vyuo vikuu mbalimbali wamekuwa wakifanya vitendo hivi bila kujali kuwa Ukimwi bado ni tishio.

Baadhi yao wanadai kuwa wanafanya hivyo kutokana na ugumu wa maisha.

Dk Getrude Lebby, mratibu wa Ukimwi Wilaya ya Morogoro Mjini anaeleza kuwa kinamama ndiyo wameambukizwa zaidi kuliko wanaume.

Dk Lebby anasema kuwa maambukizi ya Ukimwi wilayani humo yamekuwa yakisababishwa zaidi na:

Kwanza, vigodoro-harusi, ngoma za kunema wari ambazo zimekuwa zikichezwa hasa nyakati za usiku.

Pili, barabara kuu ya Iringa, Dodoma, Dar es Salaam ambayo huwezesha madereva wengi wa malori hasa ya mizigo kuegesha eneo la Msamvu.

Sababu nyingine ni wingi wa taasisi za elimu ya juu kama vile, Kigurunyembe, Mzumbe, Sokoine, Jordan na Chuo Kikuu cha Kiislamu ambazo wanafunzi wake wamekuwa wakishiriki ngono bila tahadhari.

Pia, Morogoro kuwa Kitovu cha biashara zikiwamo za mazao ya kilimo kama mchele kutoka Kilombero, Mahenge na Ifakara, viwanda vya sukari Mtibwa na Kilombero.

Viwanda mbalimbali mjini humo vinavyohitaji nguvukazi . Hivyo ni pamoja na vya tumbaku, nguo na ngozi.

Mtaalamu huyo anaeleza kitakwimu kuwa maambukizi ya VVU yamekuwa yakipanda na kushuka kila mwaka.
Amir Nondo Meya wa Morogoro anasema kuwa hana taarifa yeyote kuhusu mazingira hatarishi kama ya Itigi na Kaumba bali anachokijua kuwa maeneo hayo ni maarufu kwa kumbi za starehe. "Ninachokijua mimi ni kuwa maeneo hayo ni maarufu kwa starehe watu mbalimbali huenda maeneo hayo kwenda kuburudika na si vinginevyo"anasema Nondo.

Hata hivyo, ngono zinazofanyika Itigi ni kama mapenzi ya kuku ambayo hufanyika popote.

Uchunguzi unaonyesha kuwa chumba kimoja kidogo hutumiwa na watu zaidi ya sita kwa wakati mmoja na mmiliki wake kupata Sh1,000 kwa kila mtu anayehudumiwa.

Takwimu za maambukizi ya VVU Morogoro zinaonyesha kuwa jumla ya watu 12,482 waliopima VVU, wanaume 6,371 na wanawake 6,111, kati yao waliopatikana na maambukizi ni 668 wanaume 253 na wanawake ni 415.


Enedy Mwanakatwe, Mratibu na mshauri wa Ukimwi wilaya anasema kuwa ili kuhakikisha maambukizi ya VVU yanapungua ni wajibu wa kila mtu kuchukua hatua kwa jamii pia elimu kuhusu Ukimwi itolewe kwa wanafunzi.


"Moja ya mikakati ni kuanzisha Klabu za afya/Ukimwi kwenye vyuo vikuu, vyuo vya kawaida na shule zetu ili tuweze kupunguza maambukizi kwani Ukimwi upo na unaua,"anasema.


Mwanahawa Hamis na Happiness John na ni miongoni mwa kinadada wanaojihusisha na biashara hiyo ya ngono ambao wanasema kuwa hufanya biashara hiyo kutokana na ugumu wa maisha unaowakabili.


"Maisha bwana kila mtu anajua anavyoishi kujikimu kimaisha, wapo wanaoiba mali za watu, majambazi, mafisadi na malaya kama sisi lakini hatufanyi hivyo kwa kupenda ni ugumu wa maisha ndiyo unaosababisha japokuwa wapo wanafanya hivyo kwa tamaa zao kama wanafunzi wa vyuo," alisema Mwanahawa.


Happiness anasema kuwa ukosefu wa ajira nchini ndiyo chanzo cha yote haya kwani kila mwaka wasomi kwa kila, idara wanaongezeka, lakini hakuna ajira.


Hisani ya Mwananchi Publication

 

Attachments

  • download.jpg
    download.jpg
    13.1 KB · Views: 458
  • images.jpg
    images.jpg
    13.9 KB · Views: 434
Asante kwa taarifa

Tatzo wengi tunashikwa na kigugumuzi katika kujadili janga la ukimwi. Ikija hapa mada ya mapenzi dakika chache tu utajaa comments za kujaza kurasa kadhaa, kumbe mapenzi yayo hayo ndiyo yanayoangamiza watu kwa ukimwi. Lets discuss about it, other wise we are going to die, to avoid this discussion may be okay, but we can't avoid HIV.
 
Kukua kwa mji, biashara/viwanda kuongezeka, kunaongeza maambukizi, kivipi?
 
bwana gesti zimejaa sana moroalafu kweli wee aboodanajaza basi kila nush saa ...haiwezeka i wlte wakana kwa jema wapo wagegedaji kibao....na kaeli msamvu pamefurima totoz usiku uyadhani pale ndio morro katikati....vvu pamoja na hasara zake upunguza msongamano wa wawajinga duniani
 
bwana gesti zimejaa sana moroalafu kweli wee aboodanajaza basi kila nush saa ...haiwezeka i wlte wakana kwa jema wapo wagegedaji kibao....na kaeli msamvu pamefurima totoz usiku uyadhani pale ndio morro katikati....vvu pamoja na hasara zake upunguza msongamano wa wawajinga duniani
True that...rafik angu leo umetumia cm gan kuandika?maana umekua na mwandiko mbaya km haukusoma primary....haha
 
Huo ndio ukweli, moro sio sehemu salama jamani, wameongelea itigi na wanafunzi wa chuo ila mamesahau madereva wa bodaboda na wanafunz wa sekondar na pia madereva na makondakta wa daladala. Hawa wabodaboda na wadaladala wanatabia ya kuzungukana wenyewe kwa wenyewe. Hiyo ndio moro waungwana mkija mtumie kinga taa ya kijani imeshawaka hapa.
 
Kweli kabisa Vigodoro ni tatizo kubwa,Serikali iingilie kati suala hili ikiwezekana ipige marufuku utaratibu huu hasa wanapoamua Kukesha na Kucheza Mziki Usiku Kucha.
 
Nadhani hali hii ya ongezeko la maambukizi inatokana na ongezeko kubwa la watu kwenye mji huu wa Morogoro. Pia kwenye vyuo vikuu vyote nchini nasikia kuna idadi kubwa ya wadada wenye maambukizi, wanaosomeshwa na mfuko wa mama Salma. Wamesambazwa kwa lengo zuri la kusaidiwa kupata elimu, lakini kwa wale vijana wetu wasiokuwa makini wamekuwa wakiangukia kwenye mahusiano na wadada hao. "Tubadilike na tuwe makini, Ukimwi bado upo na unamaliza nguvukazi ya Taifa la kesho".
 
Aka kabiasha sasa hivi kila sehemu kapo aisee na kanakuwa kwa kasi kuliko hata ukuajia wa uchumi wa kitaifa wa 6%

Mwezi uliopita nilipanda basi la Aboud na kwa kuwa tulifika Morogoro saa moja jioni basi hilo lilifitikisha nakuturelemsha tulioelekea mjini pale ofisini kwao mjini karibu na stand. Niliteremka nikahitaji sehemu kupata dinner kabla sijapata sehemu ya kujiegesha, katika zunguka yangu kutafuta restaurant pale mtaa mmoja toka kwa Aboud Bus service nilikuta zimepangana guest nyingi na mabaa mengi tu hapo ni katikati ya jiji. Kwa utundu nikaamua nivute kiti kimoja niagieze soda, wakati nakunywa soda hiyo huku nikimwulizia kijana mmoja maelekezo ya restauranti yenye chakula kizuri walijipitisha pale wasichana kadhaa ambao walikuwa wamekaa meza nyingine. Kabla sijamaliza soda alisogea mmoja na kuvuta kiti kukaa karibu yangu, kisha ikaona mwingine anafuata. Nilichofanya ni kumaliza soda kwa mkupuo na kuondoka zangu nikiwaacha wakinisindikiza kwa kunikodolea macho.

Pale kuna biashara, na kabisa ukiona kujiuza kwa waziwazihivyo kwa vyo vyote kuna viashiria vya kuadhirika kwa HIV na hivyo ni biashara ya kuambukizana kwa kwenda mbele.

Jamani tuwe makini, so wote wenye mioyo inayofanana, wengine cha kujileta hakiachwi hivi hivi, wengine tunaona chema chajiuza na kibaya chajitembeza.

Saikolojia ya kutokuwa mtumwa wa ngono ni kutofikiria jambo hilo, na kupuuzi kwa nguvu zote hatimaye utashangaa ulivyoshinda vita hivi na kuwaonea huruma wenye bado kutumikia hali hiyo ya kuridhia misukumu ya silika na maungo bila kutumia bogo lao na utashi wao.
 
True that...rafik angu leo umetumia cm gan kuandika?maana umekua na mwandiko mbaya km haukusoma primary....haha

ah sie wengine tumesoma shule za kata bwana....kimeo leo kilikuwa hakijakaa sawa. mzima lakini wewe?
 
Back
Top Bottom