Ongezeko la uchumi wa China katika nusu ya kwanza ya mwaka 2021 laleta matumaini ya kufufuka kwa uchumi wa dunia

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,010
1,034
VCG111333310286.jpg

Takwimu zilizotolewa mwanzoni mwa wiki hii na Idara ya forodha ya China zinaonyesha kuwa, katika nusu ya kwanza ya mwaka huu hadi kufikia mwezi Mei, uchumi wa China uliendelea kupata ongezeko, ambapo uuzaji bidhaa kwa nchi za nje ulikuwa na ongezeko la asilimia 30.1, na uagizaji wa bidhaa ulikuwa na ongezeko la asilimia 25.9. Ongezeko hili si dogo, hasa ikizingatiwa kuwa hali ya uchumi duniani bado haijaondokana na hatua mbalimbali za vizuizi vya kupambana na janga la COVID-19.

Uchumi wa nchi nyingi za Afrika pia umeathiriwa vibaya na janga la COVID-19, kwa mfano katika eneo la Afrika Mashariki hadi sasa sekta ya utalii ambayo ni moja ya sekta zinazotoa ajira nyingi na kuziingizia mapato serikali, bado haijafufuka na watu wengi walioajiriwa kwenye sekta hiyo wana changamoto, na serikali zimepoteza mapato mengi.

Hata hivyo kutokana na kuchukua hatua kali za kupambana na COVID-19 ndani ya nchi, shughuli mbalimbali za kiuchumi na kijamii nchini China zinaendelea kurudi katika hali ya kawaida. Hali hii imekuwa ni ahueni kwa nchi nyingine ikiwa ni pamoja na nchi za Afrika. Kwa sasa katika miji mikubwa ya China, tunaweza kuona kuwa migahawa inayotumia kahawa kutoka nchi za Afrika, sasa inafanya kazi na kahawa kutoka nchi za Afrika inaingia kwenye soko la China. Na hivi karibuni pia shehena ya kwanza ya maharage ya Soya kutoka Tanzania iliingia kwenye soko la China. Hali hii ina manufaa makubwa kwa wakulima na hata wafanyabiashara wa mazao hayo wa nchi za Afrika.

Lakini tukumbuke pia kuwa hali ya usafiri kwa sasa duniani imekuwa ngumu, wafanyabiashara kutoka nchi za Afrika wanaotaka kuja kununua bidhaa zao kutoka China, au wale wanaotaka kuja kuuza bidhaa zao China hawawezi kufanya hivyo kwa urahisi kama zamani. Kwa sasa wafanyabiashara wa nchi za Afrika iwe ni wajasiriamali wadogo au wafanyabiashara wakubwa, wale wasio na uwezo wa kuja China kwa sasa, wanaweza kufanya biashara zao kupitia majukwaa mbalimbali ya internet kama Alibaba. Hali hii ni tofauti na nchi nyingine kama Ulaya na Marekani, ambazo kufanya biashara na Afrika kwa njia hii bado ni vigumu.

Vilevile tunatakiwa kukumbuka kuwa mauzo nje ya nchi si bidhaa pekee hata huduma pia ni sehemu ya mauzo. Hivi karibuni kumekuwa na habari kuwa kutokana na mazingira yenye changamoto kwenye sekta ya afya katika nchi nyingi za Afrika, idadi kubwa ya watu kutoka nchi za magharibi wamerudi kwenye nchi zao.

Wafanyakazi wachina wa makampuni ya ujenzi ya China yaliyoko katika nchi za Afrika, wameendelea kufanya kazi barani Afrika katika kipindi hiki cha janga la COVID-19, sambamba na wenyeji. Hivi karibuni waziri mkuu wa Ethiopia Bw. Abiy Ahmed amewapongeza wafanyakazi wa China kwa kukamilisha kiwanda cha sukari nchini humo, na nchini Kenya waziri wa usafirishaji, miundombinu, nyumba na maendeleo ya miji wa Kenya Bw. James Macharia, amesema ujenzi wa barabara ya Kenol-Sagana-Murua unatekelezwa na kampuni mbili za China unaendelea kwa kasi, na unatarajiwa kukamilika kabla ya tarehe iliyopangwa.

Kwa bahati mbaya janga la COVID-19 lilitokea wakati dunia inakabiliwa na “janga la kibiashara” yaani nchi mbalimbali duniani kuanza kuweka vizuizi vya kibiashara na kuwa na mwelekeo wa kujilinda kibiashara. Lakini China, tofauti na nchi hizo iliendelea kufungua milango yake kwa nchi nyingine. Mkurugenzi wa Shirika la Biashara Duniani (WTO) Bw. Roberto Azevedo aliwahi kusema China kuungana zaidi na nchi nyingine duniani, kuagiza zaidi bidhaa na kuuza zaidi bidhaa, kutaleta utulivu wa muda mrefu na maendeleo endelevu dunia. Kuongezeka kwa uagizaji na uuzaji wa bidhaa nje ya nchi kwa China, kunaonyesha mwelekeo huo.
 
Nilipoona bei ya mafuta imefika buku 2 nilijua kuwa Uchumi wa dunia ushatengemaa.
 
  • Kicheko
Reactions: BAK
Back
Top Bottom