pinno
JF-Expert Member
- Jan 17, 2013
- 1,213
- 1,228
Wakuu
Nakumbuka wakati waziri wa Fedha, Dr Mpango anasoma bajeti, kipengele kilichoshangiliwa sana kuliko vyote ni habari ya kufutwa kwa kodi ya motorvehicle
Wabunge hasa wa CCM walishangilia sana bila kuangalia kwamba hiyo kodi imewekwa kwenye mafuta na kwamba pengine ikawa na madhara makubwa sana.
Walishangilia zaidi baada ya serikali kutamka kuwa inafuta madeni yote yatokanayo na kodi hiyo sumbufu.
Wapinzani wao walipinga wazi wazi, huku wakisema serikali imekosea
Kwa kuwa kodi hii ilikuwa ni kero kwa watu wengi, wakiwemo watu walio wahi kuuza vyombo vyao vya moto pasipo kubadilisha umiliki ,watu ambao vyombo vyao vya moto vimechakaa na havitumiki tena, wote hao walitakiwa kulipa TRA malimbikizo ya kodi hiyo ambayo kwa wengi wao yalionekana kuwa ni mzigo mkubwa, na kuna baadhi mali zao zilishaanza kukamatwa na TRA
Je:Wapinzan kwenye bajeti yao ya kivuli wametoa msimamo gani juu ya hili?
Nataman wawe wameunga mkono kufutwa ,ila wawe wamepinga kuwekwa kwenye mafuta ,na wawe wametoa suluhisho makini zaidi ,la kitaalamu zaidi,ambalo litatoa suluhisho bora zaidi.
Ila kama wameishia tu kulalamika bila kutoa wazo Mbadala lolote then nathubutu kusema haina maana ya kuwa na bajeti kivuli wala kuwa na hao wapinzani labda kama tunataka tuwe na watu ambao katiba inawatambua kuwa ni wapingaji wa kila kitu.
Na kama wamekaa kimnya ,yaani hawajasema chochote juu ya hili ,basi watakuwa ni wapuuzi kwa sababu watakuwa wamepuuzia kero ya wananchi juu ya kodi iliyo kuwa sumbufu, lakin pia watakuwa wamejionesha namna ambavyo wao ni mabingwa wa kulalamika lalamika tu bila kutoa ufumbuzi mbadala wa kero za wananchi,kwa sababu wamepiga kelele sana juu ya kuwekwa kwenye mafuta, hivyo tunategemea waioneshe serikali mahali sahihi pa kuiweka.
Mwenye update ya kile walichosema naomba anijuze tafadhali.
Nakumbuka wakati waziri wa Fedha, Dr Mpango anasoma bajeti, kipengele kilichoshangiliwa sana kuliko vyote ni habari ya kufutwa kwa kodi ya motorvehicle
Wabunge hasa wa CCM walishangilia sana bila kuangalia kwamba hiyo kodi imewekwa kwenye mafuta na kwamba pengine ikawa na madhara makubwa sana.
Walishangilia zaidi baada ya serikali kutamka kuwa inafuta madeni yote yatokanayo na kodi hiyo sumbufu.
Wapinzani wao walipinga wazi wazi, huku wakisema serikali imekosea
Kwa kuwa kodi hii ilikuwa ni kero kwa watu wengi, wakiwemo watu walio wahi kuuza vyombo vyao vya moto pasipo kubadilisha umiliki ,watu ambao vyombo vyao vya moto vimechakaa na havitumiki tena, wote hao walitakiwa kulipa TRA malimbikizo ya kodi hiyo ambayo kwa wengi wao yalionekana kuwa ni mzigo mkubwa, na kuna baadhi mali zao zilishaanza kukamatwa na TRA
Je:Wapinzan kwenye bajeti yao ya kivuli wametoa msimamo gani juu ya hili?
Nataman wawe wameunga mkono kufutwa ,ila wawe wamepinga kuwekwa kwenye mafuta ,na wawe wametoa suluhisho makini zaidi ,la kitaalamu zaidi,ambalo litatoa suluhisho bora zaidi.
Ila kama wameishia tu kulalamika bila kutoa wazo Mbadala lolote then nathubutu kusema haina maana ya kuwa na bajeti kivuli wala kuwa na hao wapinzani labda kama tunataka tuwe na watu ambao katiba inawatambua kuwa ni wapingaji wa kila kitu.
Na kama wamekaa kimnya ,yaani hawajasema chochote juu ya hili ,basi watakuwa ni wapuuzi kwa sababu watakuwa wamepuuzia kero ya wananchi juu ya kodi iliyo kuwa sumbufu, lakin pia watakuwa wamejionesha namna ambavyo wao ni mabingwa wa kulalamika lalamika tu bila kutoa ufumbuzi mbadala wa kero za wananchi,kwa sababu wamepiga kelele sana juu ya kuwekwa kwenye mafuta, hivyo tunategemea waioneshe serikali mahali sahihi pa kuiweka.
Mwenye update ya kile walichosema naomba anijuze tafadhali.