Ongezeko la MB.......!!!!!!!!

Phlagiey

JF-Expert Member
Oct 26, 2013
3,487
1,651
Habari zenu wakuu kunajambo linanitatanisha sana kwa hizi siku za hapa karibuni,kipindi cha nyuma kidogo nakumbuka wakati nikidownload mp4 kutoka You tube wimbo unakuta una mb labda 12, 15 na kushuka chini, nitofauti na siku hizi uleule wimbo ulio kuwa uki download kwa mb 12 sasa hivi unaupata kwa mb 51.

Nimesha jaribu kujiuliza kwa kweli nimekosa jibu la moja kwa moja sijui kuna nini kinacho endelea, labda kama na wewe unakutana na jambo hili au ni kwangu tu tena sio kwenye computer tu, hata kama nikitumua simu bado janga ni hilo hilo leo nimeamua kuvunja ukimia na kulejea hapa jukwaani tujaribu kupeana mawazo kama kunalolote ambalo nitakuwa sirifahamu.

Ebu tuambizane hapa...................!!!!!!!!!!!!
 
naomba nichomekee ombi langu hapa wakuu,natumia galaxy S3 ila siku za hivi karibuni imegoma kabisa kuplay video,iwe za online kama youtube au zile ninazo download,tatizo laweza kuwa nini wakuu?
 
Huwa na download mp 4 mkuu.


Mp4 pia inategemea ubora wa picha na sauti so utakuta kuna MP4 144P,240P,360P,420P,720P,1080P kadri unavyopanda. Kutoka 144 kwenda 1080 ndivyo ukubwa wa Mbs unapanda
 
Amini ni nacho kuambia mkuu me huwa nadownload sana nyimbo ndo maana hili nikaligundua na sitanii

Check na ubora wa unachodownload kaka/dada maana uenda kideo ni hicho hicho kimoja but umedownload kwa pixel tofauti
 
Mp4 pia inategemea ubora wa picha na sauti so utakuta kuna MP4 144P,240P,360P,420P,720P,1080P kadri unavyopanda. Kutoka 144 kwenda 1080 ndivyo ukubwa wa Mbs unapanda
Kwa hivyo me unaniweka kwenye kundi gani la kudownload mpaka napakuwa mzigo kwa mb nyingi.
 
kaka youtube wanaudhi sana siku hizi.

zamani ilikua by default wanaeka video ya quality ya 360p na inakua mp4.

siku hizi wanaaangalia speed yako halafu wanaeka video kulingana na speed. na wewe inaonesha speed yako ipo njema wameongeza hapo imekua 480p.

system hii inaboa zaidi unapokua na bandwitch kidogo maana mara moja bundle inaisha
 
kaka youtube wanaudhi sana siku hizi.

zamani ilikua by default wanaeka video ya quality ya 360p na inakua mp4.

siku hizi wanaaangalia speed yako halafu wanaeka video kulingana na speed. na wewe inaonesha speed yako ipo njema wameongeza hapo imekua 480p.

system hii inaboa zaidi unapokua na bandwitch kidogo maana mara moja bundle inaisha

Kama ulikuwepo vile yani hata nyimbo 5 kuzi kamilisha umesha labwa vya kutosha.
 
Mp4 pia inategemea ubora wa picha na sauti so utakuta kuna MP4 144P,240P,360P,420P,720P,1080P kadri unavyopanda. Kutoka 144 kwenda 1080 ndivyo ukubwa wa Mbs unapanda

Siku hizi wana-upload HD kuanzia 720dpi hadi 1080dpi,vevo wanajitahidi sana video zao hata ya 360dpi inaiondoa ya 720dpi HD za kibongo kwa quality.
 
Kuna option ya kuchagua quality unayotaka ku play au ku download ktk yt player yao. Na sasa zipo video za 4k kwa wale wa ultra HD ka video cha dak 7 kanafika hadi 500mb
 
Tumia line ya vodacom na ikifika saa nne usiku jiunge na wajanja night offer kwa sh 500 tu unadownload utakavyo wewe mpaka saa 12 asubuh, speed ya pc yako ndiyo limit

.
Sidhani kama sielewi biology
.
ila kwa ninavyojua
.
THE GROWTH ACTIVITIES TAKES PLACE DURING THE NIGHT TIME WHEN AN ORGANISM SLEEP
.
.
 
Umeridhika kwavile kasema mkwawa?
Hivi alichokueleza mkwawa si ni kile kile tu nilichokueleza pale juu

Hapa sio kihivyo yeroo ujue nakosa uhuru wa kudownload inaonekana kama nawafaidisha wao
 
Back
Top Bottom