Ongeza faida kwenye biashara yako kwa kumkwepa middle man

Nikupongeze kwa kuandika mambo mengi lakini ujaiumiza akili yako sana kuwaza nje ya bosi naona kesho unaweza ukaja hapa na uzi unaosema Walaji pia waache kununua vitu wadukani waende kwa manufacture
Fungua thread utueleze haya kwa kina mkuu,ukimaliza uni tag.
 
Nikupongeze kwa kuandika mambo mengi lakini ujaiumiza akili yako sana kuwaza nje ya bosi naona kesho unaweza ukaja hapa na uzi unaosema Walaji pia waache kununua vitu wadukani waende kwa manufacture
Anayefanikiwa kuvunja hiyo chain uliyosema ndie anayefanikiwa haraka, tafuta chein yako
Mfanyabiashara aliyekomaa hafungwi na procedures za darasani.


Stop being NORMAL mkuu
 
Nina siku sijakusoma Mkuu na Leo imebidi nikutafute nikakutana na Bandiko lako. Asante sana kwa somo hili kwangu nitaliita zuri Maana nimeliishi
Kaka wakati naanza Biashara yangu ya Chupi nilikwenda sokoni nikauziwa Kila dozen moja 36000/=, ilinilazimu Kukomaa na bei ya 5000/pc

Lakini baada ya kuizoea na kuyajua masoko bidhaa ileile nikaanza kuipata chini ya 36000 hapo ikanirahisishia namna ya kuuza maana napata Faida.

Haikutosha now natafuta huko wanakotoa wao ni wapi na wanafanyaje Nataka nifike huko hawa middle man wapo waendelee kuwepo ila ukipata namna ya kumkimbia mkimbie haraka sana.

Hata huko China middle man wapo wengi nataka kuwakwepa pia. NASHUKURU MUNGU Kwa mtaji huu mdogo now naweza kuagiza Mzigo China unakuja namuomba Mungu mwaka huu ukiisha mwakani NAKWENDA MWENYEWE CHINA
Tuungane mkuu ukiwa tyr mi mwenywe ndo ndoto zangu.
 
Maisha ya biashara na ujasiriamali kila unapoamka inapaswa upashe akili moto kuongeza ile 500 uliyoipata jana leo upate 1000 na kesho kutwa upate 1500 Hiyo ndio inatwa biashara na ujasiriamali.

Leo nataka kuandika kitu kidogo chakufungulia mwaka kuamsha waliolala,na jambo lingine leo nataka zaidi kuongea na wale wanaolalamika hawaoni faida katika biashara wanazofanya ijapokua wana wateja na biashara inaenda hata mtu ukienda kazini kwake kweli unaona kbsa huyu mtu anauza anapata pesa lakini yeye kiuhalisia moyoni mwake jioni anajua fika kbsa sipati kitu cha maana.

WATU wa namna hii mpo,najua upo sehemu unajifkiria kuacha hiyo bishara ujaribu biashara nyingine labda utatoboa,ila leo nataka tuongee kitu flani kisha ntaomba mkijaribu kwa vitendo,msipoona matunda yake basi nawaruhusu kufunga au kubadilisha biashara mnayofanya ila kwasasa naomba usifunge biashara au kubadilisha biashara,soma hii thread taratbu uielewe kisha ingia nayo kwenye vitendo.

Middle Man/Mtu wa katikati/Dalali
Huyu n yule mtu anaewasiliana moja kwa moja na mzalisha bidhaa anainunua kisha na yeye ndio anakuja kukuuzia wewe mfanyabiashara,najua n mara nyingi tunaenda masokoni/madukani kununua vitu mbali mbali vya biashara yetu wale wanaotuuzia vile vitu huko masokoni/madukani ndio hawa leo nataka tuwaongelee hawa ndio ma middle man wenyewe.

Yawezekana unauza sana halafu hujui hela inaenda wapi,unafanya biashara sana ila huoni ukpga hatua mbele shida sio biashara yako ila shida na mchawi anaekuvuta shati usiende mbele ni huyu middle man wala hujalogwa.

Unapotaka kuona faida ya ujasiriamali/biashara yako jitahidi kufa na kupona,afe kipa afe beki,kwa jasho na damu fanya kila unaloweza kumkwepa middle man ndipo utakapoona faida ya ujasiriamali na biashara yako. Nitatolea mifano ya biashara kadhaa ili nieleweke nin hasa naongelea leo.

KUUZA MKAA
Kuna mtu yupo mahali anafanya biashara ya kuuza mkaa kwa watu wa mtaani kwake,ukimuuliza mka ananunua wapi yeye atakwambia Pale mbeleeee kuna mama anauza mkaa kwa jumla,unapoenda kununua mkaa kwa yule mtu kumbuka yeye hachomi miti wala hatengenezi mkaa kwa maana hiyo na yeye ananunua kisha anakuja kukuuzia wewe, Gunia analonunua 50,000 yeye anakuja kukupga 150,000,sasa wewe muuza mkaa kwanini usimruke huyu mtu ukaenda tafuta mkaa huko porini kwa watengeneza mkaa wenyewe, unafkiri hautopata?

Ukifanikiwa kwende porini mwenyewe gunia utalichukua kwa 50k na utakuja kupata faida mara mbili ya ile uliyokua ukipata mwanzo,inawezekana amua tu kuacha uvivu na uinuke hapo ulipo ukatafute mwenzako anapata wapi huo mkaa.

KUUZA CHIPSI
Kuna mtu huu mwaka wa 5 anafanya biashara ya chipsi lakini maendeleo n 1+1-2 analalamika kalogwa,muulize unanunua wapi viazi anakwambia ananunua mabibo sokoni au soko kuu,gunia linauzwa sokoni 100,000 tena hapo limeshapunguzwa punguzwa ndipo mnauziwa laki,wakati ujazo wagunia hilo la laki yawe magunia matatu ndio gunia 1 kwa mkulima shambani na shambani gunia mkulima anauza 80,000, lakini kutokana na uvivu wetu wakusubiri mpaka tuletewe sokoni ndio tufate viazi tunaenda nunua mtoto wa gunia kwa 100,000,hivi unategemea faida utaipatia au iona wapi?

Uwezo wa kwenda shambani unao kama unaweza fata gunia sokoni unashndwa nn kufata gunia kwa mkulima wa viazi shambani,ila upo unasubiri Middle man akuletee,sawa kaaa hapo subiri uletewe utalikuta sokoni.

BIASHARA YA GENGE
Mtu ananunua karoti sokoni,hoho sokoni hajiulizi hizi hoho/karoti zinatoka wapi,kwann mimi nisizifate huko zinakotoka? anasubiri karoti auziwe moja 300 wakati akienda shambani mkulima anamuuzia Ndoo ya lita kumi sh.3000,hivi ndoo ya lita kumi mpaka ijae ina karoti ngapi ndani? Lakini yeye anasubri aletewe pale soko kuu akanunue 500 aje atupge mtaani karoti sh 700 atuambie karoti saivi ni BEI kumbe n uzembe wake na uvivu wake. Ukigusa Limao gengeni saivi unaweza ambiwa ni buku ila muulize huyo muuza genge katoa wapi hilo limao atakwambia soko kuu.

BIASHARA YA GESI na VIFAA VYAKE
Upo ofisini unauza gesi zikikuishia unavuta simu unapga unaletewa na kampuni hadi mlangoni,hivi umeshawahi jiliza what if nikifata mwenyewe hizi gesi ntauziwa kiasi gani? niwambie tu wauza gesi fateni gesi wenyewe huko zinapojazwa,Mtanishukuru badae kwa bei mtakayoikuta.

Unauza burner/Stand/Regulator/Pipe hivi vifaa umewahi kujua vinatengenezewa wapi? jiulize kisha vifate kutoka kwa mtengenezaji mkwepe middle man yule unaempgia simu akuletee vifaa kila vikiisha utaona bei utayoikuta.

MAMA NTILIE
Tukiachana na hawa wanaokopa vitu kwa mangi then wanalipa jioni,nawaongelea nyie mnaonunua mchele kwa cash mnauziwa kilo ya mchele 2500 hivi umeshaenda kahama huko au magugu au mbeye mchele unakotoka ukajua bei ya huo mchele unaouziwa kilo 2500,ni kwamba hiyo bei unapigwa mruke huyo middle man uone matunda ya ujasiriamali wako.

Tuache uvivu ndugu zangu tusisubiri kuletewa kisha ndio tukanunue,wanaofata mizigo china sio kwamba wao n maboss sana au wanapenda sifa hao wote wameshaona madhara ya middle man,kama unafanya biashara yoyote usipende mambo ya Free delivery sijui toa oda tunakuletea usipende hizo ofa ndio zinapunguza faida yako na mwisho unaona hupati faida kumbe unapata,Middle man ndio anaekufanya wewe ujione kama hela yako inapotea hujui inakoenda.

Kabla hujafunga au kubadlisha biashara unayofanya hebu mkwepe middle man halafu fata mzigo production center halafu tuone kama ndani ya mwezi huu mawazo ya kufunga hyo biashara kama yataendelea kuwepo.

Faida ya mauzo yako inapotezwa na huyo middle man ndie anaekupa loss wala sio kwamba una matumizi makubwa au nni TUACHE UVIVU vyakuletewa vina gharama.

Heri ya Mwaka Mpya.
Naomba kujuzwa chimbo LA vitu vya urembo wa kike, kama vile hereni na mikufu, kwa bei rafiki zaidi, ukiachana na pale mtaa wa mchikichini, naomba kujua chimbo lingine kwenye bei nafuu zaidi
 
Kokudo ni 1 ya watu wachache sana wanaoelewa masomo ninayo yatoa,yani kama ni mwanafunzi niaejivunia darasani hata nikifundisha kitu wengine waseme hawajaelewa ntawambia wote ambao hawajaelewa wamfate "kokudo" awaeleweshe.

sina shaka na utendaji wako,sina mashaka na wewe ktk biashara,nakuona mbali sana sana kuliko unavyoweza kufikir kuna vitu nasoma unapokua unachangia thread zangu napata majibu "yes huyu kweli ni msaka pesa ninaemtaka".

Endeleza hiyo spirit usipoe hata kidogo, acha hawa wasiojua Middle Man anawaumiza kwa kiasi gani waendeleee kulia biashara mbaya biashara mbovu,waache wao walie muda wakijitambua walipokua wanakosea itakua too late.

kuna watu utajiri wataushika wakiwa na 40's au 50's mimi nawaangalia tu wanavyo complicate mambo ktk thread ninazozitoa,waache wafanye biashara wasijiongeze.Sitochoka andika Thread zakuinua wengine na kuwasaidia wengine,ndio malengo yangu Kila mtu afaidike na uwepo wangu duniani,wanao ona naandika vitu haviwezekani nakaaga kimyaa natulia.

Kokudo Big Up,usichoke kujifunza kila iitwapo leo biashara ina mbinu tofauti tofauti ji update kila unapopata nafasi either kwa kusoma au kupga story na wafanyabiashara waliokuzidi wewe siku 1 utakua Mafia ktk dunia ya ujasiriamali na Biashara kwa ujumla wake.
Haka kaujumbe hua natamani nikafanyie lamination 😋
 
Screenshot_20210727-120248.png
 
Duuuh... mkuu biashara inaenda stage kwa stage sio kama unavyotaka wewe hvyo.

Kwenye biashara kuna makundi makuu kama manner hv.
1" mzalishaji (producer/manufacturer)

2" msambazaji/mnunuaji wa jumla kutoka kwa mzalishaji (wholesaler/supplier)

3" mnunuaji wa jumla kutoka kwa msambazaji anajulikana kama mchuuzi/mmachinga (retailer)

4" mnunuzi wa mwisho/ mtumiaji (final consumer)

Sasa apo wewe retailer kwenda moja kwa moja kwa manufacturer kununua mzigo si kazi rahisi coz kuna vigezo inabidi uwe navyo either uwe na sifa za kuwa wholesaler.

NB:- mtaji wako na maarifa yako ndo yatakuweka katka kundi fulani.
Umejibu kisomi mzee, heko

Sent from my Moto C using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom