Ondoa matarajio makubwa kutoka kwa watu, yatakuumiza sana

boniuso

JF-Expert Member
Mar 13, 2013
675
839
KINACHO KUVUNJA MOYO SIO UBAYA WA TABIA ZA WATU BALI MATARAJIO YAKO KWAO

Kama usielewa asili ya tabia za binadamu utapata wakati mgumu sana kuwaelewa na kuishi nao

Alisema Marcus Aurelius miaka takribani 2000 iliyopita "Unayo nguvu ya kudhibiti akili yako tu sio watu au matukio kutoka nje yako"

Kwa sababu watu wengi hawajui hilo ndio sababu ya mateso yao ya kihisia kila siku

Ni ukweli usiopingika kuwa hakuna binadamu aliyekamilika na huwezi kuwa mkamilifu hivyo unatakiwa kuishi na watu vile walivyo sio vile unataka wewe

Binadamu huongozwa na hisia kwa kila maamuzi anayofanya hivyo akiwa na hisia za furaha atakusifia sana na akiwa na hasira atakulaumu sana hivyo sio matendo yako yenye kuamua kauli zao bali hisia zao kwa wakati huo

Chochote ambacho utasema au kufanya watu hawakipokei kwa uwiano sawa kwa sababu kila mtu anapitia maumivu tofauti na hisia tofauti

Mtu akiwa na hasira akili huwa inazima (brain shutdown) hivyo chochote utasema kwa ukali hakuelewi hivyo ukiendelea kumfokea ndio utafanya awe jeuri sana kuliko mwanzo

Kwa kawaida akili huwa inafanya kazi mtu akiwa na utulivu wa akili na sio kwenye stress

Hivyo unapokuwa na hasira huwezi kumuelewa mtu kwa chochote atasema na unaeongea nae akiwa na hasira hawezi kukuelewa hivyo inakuwa sawa na ubishi wa viziwi

Mtu aliyepita maumivu makali sana kama kubakwa,kuteswa, kubaguliwa, kupata ajali ikafanya apate ulemavu wa kudumu,kufanyiwa unajisi labda kubakwa na baba yake mzazi au ndugu wa karibu,mtu mwenye kupitia mahusiano yasiyodumu, mtu mwenye kupitia kipindi kigumu sana kiifedha, endapo utasimulia hadithi ya kuhuzunisha utaona analia sana au kuhuzunika sana unaweza kudhani hadithi yako ndio inafanya atoe machozi kumbe anakumbuka maumivu alipitia zamani au maumivu anayopitia kwa wakati huo

Ndio sababu mnaweza kwenda. Sehemu labda kwenye vituo vya watoto yatima kisha ukaona mwenzio anatokwa machozi kwa kuwaona yatima huku mwingine haonekani kuhuzunika kwa chochote

Kumbe mwenzio analia kwa uchungu kwa sababu alipitia maumivu utotoni hivyo ameona mtu ambaye anapitia maumivu kama yake

Watu wakiwa wamechanganyikiwa huwa hawaelewi chochote hivyo hata ukiwapa ushauri hawaoni uzuri wa ushauri bali wanaona giza kwa sababu ya maumivu wanayopitia

Kinachotokea katika maisha yako sio tatizo ila tafsiri unayoweka ndio inaweza kuwa tatizo au suluhu ya matatizo.

Maisha huleta 10% ya furaha yetu au huzuni yetu kisha kile watu huwa wanafikiria ndio huamua 90% ya furaha au huzuni

Mnaweza kutukanwa mkiwa kwenye kikao watu wengi tu lakini kuna baadhi watakuja juu sana kumshambulia alietukana na wengine utaona wapo kimya

Mfano kwenye whatsap group mtu anaweza kutuma link au video ambayo haiendani na maudhui ya group lakini kuna member wengi wa group baadhi watamtukana alietuma link na wengine watakaa kimya na wengine wanaweza kumjibu kwa ustaarabu tu

Tatizo sio kile kimetokea bali tasfiri yako unayoweka ndio huamua hisia zako wakati huo

Ukiamua kuangalia mabaya kwa watu utakuta mabaya mengi sana na utawachukia watu na ukitazama mazuri yao utawapenda

Ukiona mtu anakupenda anakuwa ametazama mazuri yako na endapo atatazama mabaya yako atakuwa adui yako

Na ukiona mtu anakuchukia anakuwa ametazama mabaya yako na endapo akitazama mazuri yako atakupenda

Hakuna binadamu mwenye mazuri tu au mabaya tu

Kwa vyovyote utafanya kuna mtu atapenda na kuna mtu atachukia kwa sababu kila mmoja huamua kuchagua upande wa kutazama kwa kila tukio

Ukitazama ubaya utapata hasira na ukitazama uzuri utakuwa na furaha ila watu wengi zaidi ya 80% ya watu duniani hutazama mabaya kwa kila jambo na kwa kila mtu ndio sababu maadui zako ni wengi kuliko marafiki wa kweli

Humpendi kila mtu hivyo huwezi kupendwa na kila mtu

Ili umchukie mtu tazama mabaya yake kwenye tabia na kasoro zake za maumbile lazima utamchukia

Ili ujichukie tazama kasoro zako za maumbile na matatizo yako unayopitia kwa sasa au makusa yako ya zamani

Ukianza kumsema mtu kwa mabaya yake lazima utamchukia na unaemchukia akipata pesa kukuzidi au cheo kikubwa au kuwa maarufu wewe ndio utateseka sio yeye

Utateseka kwa sababu utakuwa unapata hasira kwa mafanikio yake

Watu wanakuvunja moyo sio kwa sababu ya ubaya wa tabia zao bali matarajio yako kwao

Ondoa matarajio kwa watu kisha kubali chochote watafanya kisha angalia wapi unaweza kubadilisha na ikiwa huwezi kubadilisha acha tatizo kama lilivyo

Kama utaondoa matarajio utakuwa umejipa jukumu la kuwa problem solver na ukiwa na matarajio unakuwa unajizuia kufikiria njia mbadala endapo matarajio yako hayatatimia

Ondoa matarajio kisha wekeza nguvu kwa kile kipo ndani ya uwezo wako

Kusubiri .mtu mwengine abadilike tabia ili wewe uwe na furaha huko ni kuchanganyikiwa

Utazidi kupata hasira kama unataka mtu awe vile unataka wewe badala ya kumuacha awe vile alivyo kisha jifunze kuishi naye vile alivyo

Mvua ikinyesha na wewe umeanika nguo huwa unazitoa kwenye mvua ili hali ikiwa nzuri uanike upya kwanini ukipata matatizo hukubali kubadilika kuendana na mabadiliko?

Ukipata hasira kwa sababu mvua inanyesha ni kujitesa bure kwanza hasira haiwezi kukusaidia chochote wala haiwezi kuzuia mvua kunyesha

Ukipata matatizo kisha ukapata hasira ni wewe unateseka sio matatizo yako na vilevile hasira zako haziondoi tatizo unalopitia

Tabasamu kwa sababu haumiliki matatizo yote ya ulimwengu

Kupata kitabu cha
1.FIKRA ZAKO FURAHA YAKO (softcopy)
2TIBA YA MSONGO WA MAWAZO (hardcopy & softcopy)
3.BADILI FIKRA ZAKO BADILI MAISHA YAKO (hardcopy & Softcopy)
4.MALEZI YA UBONGO KISAYANSI( hardcopy & softcopy)
5.TABIA ZA WATU WALIOFANIKIWA (Hardcopy & softcopy)

6 MISINGI 10 YA FURAHA SIKU ZOTE (hardcopy &softcopy)

+255766862579
+255622414991

Imeandikwa na Psychologist
Said Kasege
Temeke, Dar es salaam
 
Binadamu anaongozwa na hisia?

Sio kweli binadamu anaongozwa na akili then inafuata hisia, msimamo, imani kwahiyo akili ndo inaweza Ku control hivyo vingine

Anayeongozwa na hisia ni n'gombe na viumbe wengine.
 
Binadamu anaongozwa na hisia?

Sio kweli binadamu anaongozwa na akili then inafuata hisia, msimamo, imani kwahiyo akili ndo inaweza Ku control hivyo vingine

Anayeongozwa na hisia ni n'gombe na viumbe wengine.
Kwani shiida ipo wapi mkuu, ukiwa na furaha au hasira unaambiwa hutakiwi kufanya maamuzi kwan asilimia nyingi yatategemea hisia ulizonazo kwa muda huo. Hivyo nikujuze kuwa hisia zina nafasi kubwa sana katika maisha yako ya kila siku.
 
Kwani shiida ipo wapi mkuu, ukiwa na furaha au hasira unaambiwa hutakiwi kufanya maamuzi kwan asilimia nyingi yatategemea hisia ulizonazo kwa muda huo. Hivyo nikujuze kuwa hisia zina nafasi kubwa sana katika maisha yako ya kila siku.
Sijakataa na tena hisia zina nguvu sana lakini zinaongozwa na akili
 
Kwani shiida ipo wapi mkuu, ukiwa na furaha au hasira unaambiwa hutakiwi kufanya maamuzi kwan asilimia nyingi yatategemea hisia ulizonazo kwa muda huo. Hivyo nikujuze kuwa hisia zina nafasi kubwa sana katika maisha yako ya kila siku.
Jibu zuri
 
KINACHO KUVUNJA MOYO SIO UBAYA WA TABIA ZA WATU BALI MATARAJIO YAKO KWAO

Kama usielewa asili ya tabia za binadamu utapata wakati mgumu sana kuwaelewa na kuishi nao

Alisema Marcus Aurelius miaka takribani 2000 iliyopita "Unayo nguvu ya kudhibiti akili yako tu sio watu au matukio kutoka nje yako"

Kwa sababu watu wengi hawajui hilo ndio sababu ya mateso yao ya kihisia kila siku

Ni ukweli usiopingika kuwa hakuna binadamu aliyekamilika na huwezi kuwa mkamilifu hivyo unatakiwa kuishi na watu vile walivyo sio vile unataka wewe

Binadamu huongozwa na hisia kwa kila maamuzi anayofanya hivyo akiwa na hisia za furaha atakusifia sana na akiwa na hasira atakulaumu sana hivyo sio matendo yako yenye kuamua kauli zao bali hisia zao kwa wakati huo

Chochote ambacho utasema au kufanya watu hawakipokei kwa uwiano sawa kwa sababu kila mtu anapitia maumivu tofauti na hisia tofauti

Mtu akiwa na hasira akili huwa inazima (brain shutdown) hivyo chochote utasema kwa ukali hakuelewi hivyo ukiendelea kumfokea ndio utafanya awe jeuri sana kuliko mwanzo

Kwa kawaida akili huwa inafanya kazi mtu akiwa na utulivu wa akili na sio kwenye stress

Hivyo unapokuwa na hasira huwezi kumuelewa mtu kwa chochote atasema na unaeongea nae akiwa na hasira hawezi kukuelewa hivyo inakuwa sawa na ubishi wa viziwi

Mtu aliyepita maumivu makali sana kama kubakwa,kuteswa, kubaguliwa, kupata ajali ikafanya apate ulemavu wa kudumu,kufanyiwa unajisi labda kubakwa na baba yake mzazi au ndugu wa karibu,mtu mwenye kupitia mahusiano yasiyodumu, mtu mwenye kupitia kipindi kigumu sana kiifedha, endapo utasimulia hadithi ya kuhuzunisha utaona analia sana au kuhuzunika sana unaweza kudhani hadithi yako ndio inafanya atoe machozi kumbe anakumbuka maumivu alipitia zamani au maumivu anayopitia kwa wakati huo

Ndio sababu mnaweza kwenda. Sehemu labda kwenye vituo vya watoto yatima kisha ukaona mwenzio anatokwa machozi kwa kuwaona yatima huku mwingine haonekani kuhuzunika kwa chochote

Kumbe mwenzio analia kwa uchungu kwa sababu alipitia maumivu utotoni hivyo ameona mtu ambaye anapitia maumivu kama yake

Watu wakiwa wamechanganyikiwa huwa hawaelewi chochote hivyo hata ukiwapa ushauri hawaoni uzuri wa ushauri bali wanaona giza kwa sababu ya maumivu wanayopitia

Kinachotokea katika maisha yako sio tatizo ila tafsiri unayoweka ndio inaweza kuwa tatizo au suluhu ya matatizo.

Maisha huleta 10% ya furaha yetu au huzuni yetu kisha kile watu huwa wanafikiria ndio huamua 90% ya furaha au huzuni

Mnaweza kutukanwa mkiwa kwenye kikao watu wengi tu lakini kuna baadhi watakuja juu sana kumshambulia alietukana na wengine utaona wapo kimya

Mfano kwenye whatsap group mtu anaweza kutuma link au video ambayo haiendani na maudhui ya group lakini kuna member wengi wa group baadhi watamtukana alietuma link na wengine watakaa kimya na wengine wanaweza kumjibu kwa ustaarabu tu

Tatizo sio kile kimetokea bali tasfiri yako unayoweka ndio huamua hisia zako wakati huo

Ukiamua kuangalia mabaya kwa watu utakuta mabaya mengi sana na utawachukia watu na ukitazama mazuri yao utawapenda

Ukiona mtu anakupenda anakuwa ametazama mazuri yako na endapo atatazama mabaya yako atakuwa adui yako

Na ukiona mtu anakuchukia anakuwa ametazama mabaya yako na endapo akitazama mazuri yako atakupenda

Hakuna binadamu mwenye mazuri tu au mabaya tu

Kwa vyovyote utafanya kuna mtu atapenda na kuna mtu atachukia kwa sababu kila mmoja huamua kuchagua upande wa kutazama kwa kila tukio

Ukitazama ubaya utapata hasira na ukitazama uzuri utakuwa na furaha ila watu wengi zaidi ya 80% ya watu duniani hutazama mabaya kwa kila jambo na kwa kila mtu ndio sababu maadui zako ni wengi kuliko marafiki wa kweli

Humpendi kila mtu hivyo huwezi kupendwa na kila mtu

Ili umchukie mtu tazama mabaya yake kwenye tabia na kasoro zake za maumbile lazima utamchukia

Ili ujichukie tazama kasoro zako za maumbile na matatizo yako unayopitia kwa sasa au makusa yako ya zamani

Ukianza kumsema mtu kwa mabaya yake lazima utamchukia na unaemchukia akipata pesa kukuzidi au cheo kikubwa au kuwa maarufu wewe ndio utateseka sio yeye

Utateseka kwa sababu utakuwa unapata hasira kwa mafanikio yake

Watu wanakuvunja moyo sio kwa sababu ya ubaya wa tabia zao bali matarajio yako kwao

Ondoa matarajio kwa watu kisha kubali chochote watafanya kisha angalia wapi unaweza kubadilisha na ikiwa huwezi kubadilisha acha tatizo kama lilivyo

Kama utaondoa matarajio utakuwa umejipa jukumu la kuwa problem solver na ukiwa na matarajio unakuwa unajizuia kufikiria njia mbadala endapo matarajio yako hayatatimia

Ondoa matarajio kisha wekeza nguvu kwa kile kipo ndani ya uwezo wako

Kusubiri .mtu mwengine abadilike tabia ili wewe uwe na furaha huko ni kuchanganyikiwa

Utazidi kupata hasira kama unataka mtu awe vile unataka wewe badala ya kumuacha awe vile alivyo kisha jifunze kuishi naye vile alivyo

Mvua ikinyesha na wewe umeanika nguo huwa unazitoa kwenye mvua ili hali ikiwa nzuri uanike upya kwanini ukipata matatizo hukubali kubadilika kuendana na mabadiliko?

Ukipata hasira kwa sababu mvua inanyesha ni kujitesa bure kwanza hasira haiwezi kukusaidia chochote wala haiwezi kuzuia mvua kunyesha

Ukipata matatizo kisha ukapata hasira ni wewe unateseka sio matatizo yako na vilevile hasira zako haziondoi tatizo unalopitia

Tabasamu kwa sababu haumiliki matatizo yote ya ulimwengu

Kupata kitabu cha
1.FIKRA ZAKO FURAHA YAKO (softcopy)
2TIBA YA MSONGO WA MAWAZO (hardcopy & softcopy)
3.BADILI FIKRA ZAKO BADILI MAISHA YAKO (hardcopy & Softcopy)
4.MALEZI YA UBONGO KISAYANSI( hardcopy & softcopy)
5.TABIA ZA WATU WALIOFANIKIWA (Hardcopy & softcopy)

6 MISINGI 10 YA FURAHA SIKU ZOTE (hardcopy &softcopy)

+255766862579
+255622414991

Imeandikwa na Psychologist
Said Kasege
Temeke, Dar es salaam
Ahsante sana kwa elimu nzuri na mchanganuo mzuri wa falsafa ya Stoicism.

Dunia nowdays imebadilika nakuwa kijiji kutokana na World Wide web na kusababisha msululu wa taarifa kutoka pande zote za dunia. Ambazo kwa namna moja au nyingine pia uchangia mwanadamu kudevelop tabia ambayo hakuwa nayo hapo nyuma na kuishi maisha ambayo sio ya hadhi yake (Fake Life).
Na kuwa na matarajio makubwa zaidi ya uwezo wake kwa sababu tu aliona fulani na fulani mtandaoni.

Pia uchangia mtu kukosa furaha kwa sababu ya kuwa na greedy na vitu ambavyo vipo juu ya uwezo wake.
 
'Kusubiri .mtu mwengine abadilike tabia ili wewe uwe na furaha huko ni kuchanganyikiwa'
Kwenye maisha usitegemee watu kubalika au kuwabadilisha, mabadiliko unawez kufanya wew yaani wew mdio ubadilike kuendana na tabia za watu au usibadilike na usiumizwe na tabia za watu.
 
Kwanini walimu hulazimisha wanafunzi wawe na uelewa Kama wao walivyo ilihali kila binadamu ameumbwa na uelewa wake tofauti
Na kama ukifuatilia vizuri basi utaona walimu hao uishia kuwachapa wanafunzi na kuwapa adhabu bila mafanikio, mwisho utasikia mwalimu ana case ya kujeruhi nk.

Huwa sielewi shiida nin maana walimu wote hufundishwa somo la ualimu na wanasoma saikolojia ya elimu.
 
Ahsante sana kwa elimu nzuri na mchanganuo mzuri wa falsafa ya Stoicism.

Dunia nowdays imebadilika nakuwa kijiji kutokana na World Wide web na kusababisha msululu wa taarifa kutoka pande zote za dunia. Ambazo kwa namna moja au nyingine pia uchangia mwanadamu kudevelop tabia ambayo hakuwa nayo hapo nyuma na kuishi maisha ambayo sio ya hadhi yake (Fake Life).
Na kuwa na matarajio makubwa zaidi ya uwezo wake kwa sababu tu aliona fulani na fulani mtandaoni.

Pia uchangia mtu kukosa furaha kwa sababu ya kuwa na greedy na vitu ambavyo vipo juu ya uwezo wake.
Kweli kabisa mkuu, kuna mambo mengi sana tunaweza takiwa kujifunza kila uchwao. Ili jamii iweze kubadilika ni ngumu sana maana jamii huwa inaathiriwa na mambo mengi sana. Mfano tamaduni, familia zao, dini nk.

Hivyo huwa tunajaribu kuandika yale yanayoweza eleweka kwa wakati huo tu. Ndiomana utaona watu wanamaswali mengin mno.
 
Back
Top Bottom