Sam Gidori
Senior Member
- Sep 7, 2020
- 165
- 414
Baada ya zaidi ya miaka 400, leo usiku sayari mbili kubwa zaidi katika mfumo wetu wa jua, sayari ya Mshtarii (Jupiter) na Zohali (Saturn) zinatarajiwa kuonekana katika umbo moja kutoka duniani.
Tukio hili linalotokea mara moja katika muda wa uhai wa mwanadamu linafanya sayari hizo mbili kuonekana kama 'nyota' moja. Mara ya mwisho tukio kama hilo kuonekana ilikuwa zaidi ya miaka 400 iliyopita, Julai 16 mwaka 1623.
Si kweli kwamba sayari hizo mbili zitaungana na kuwa kitu kimoja, kuna umbali wa zaidi ya kilomita 733,205 kati ya sayari hizo mbili, na umbali wa kilomita 886,440 kati ya dunia na sayari ya Zohali, ila sayari zote mbili zitakuwa katika mstari mmoja wa mwonekano kutoka duniani.
Sayari hizi mbili kubwa zinaonekana kwa urahisi kutoka duniani, na tukio hili linaweza kuonekana katika maeneo mengi duniani. Tafuta sehemu nzuri usiku wa leo utazame upande wa Kaskazini Magharibi uweze kuona tukio hili ambalo hautaweza kuliona tena katika maisha yako.