Alwaz
JF-Expert Member
- Apr 29, 2010
- 7,122
- 10,829
Kwa wale wenye umri kama wa kwangu enzi hizo watakuwa na uzoefu wa majina ya miji ya kipalestina ambayo kwa sasa yote imezingirwa na makazi ya mayahudi wanaohamishwa kutoka mataifa mengine duniani kuja kuwabana wapalestina katika lengo la kuwamaliza.
Hayo maeneo yenye bluu iliyokoza ndiyo makazi ya kiyahudi. Unaweza ukashangaa kwanini yote yasiwe eneo moja na karibu na mpaka upande wa magharibi. Haya maeneo yanakuwa yamechaguliwa maalum na kuwekwa kwenye ramani. Yanakuwa ni yale yenye rutuba au vyanzo vya maji safi au miinuko kwa matumizi ya kijeshi. Kinachofuatia huwa ni muda tu kulingana na bajeti ya nchi.
Zamu ya eneo fulani ikifika wakazi wa eneo hilo hupewa notisi ya kuhama kwa visingizio mbali mbali. Kwa udhaifu walionao na kwa kujua nguvu ya Israel wapalestina wengi huvunja majumba yao na kukushanya baadhi ya vitu vyao na kutia kwenye masanduku.Wale wanaoduwaa hawajachukua uamuzi, siku ikifika mabuldoza hufika na kuvunja bila kuhoji. Baada ya muda mfupi unakuta maghorofa ya wakaazi wa kiyahudi yakiwa yamebadili sura ya eneo lote.
Wapalestina waliokosa makaazi hawajui pa kwenda pia hupewa jina la wakaazi na sio raia na huwa wanapigwa danadana huku na huko mpaka wengi hufa na wachache wanaoamua kuhama hurahisishiwa njia za kutoka nje ili wakawe wakimbizi.
Mbali na makazi ya kiyahudi vijiji vilivyobaki vya wapalestina huzingirwa na kutenganishwa kwa kuta ndefu na seng'enge kiasi kwamba wapalestina waliokuwa majirani inaweza kuwachukua siku nzima mtu kumfikia mwenzake kutokana na kulazimika kuvuka vizuizi vingi vya kijeshi.
Mbinu hizi ni za muda mrefu na zinapata kasi kila mwaka.Mwaka 1948 mpaka 1967 ilikuwa ni kitu kingine na kutoka 1967 mpaka ilipomegwa Gaza ni kitu kingine. Na kuanzia hapo mpaka muda huu ni mbinu hiyo ya kuwazunguka wapalestina ndani kwa ndani.
Mafanikio ya Israel katika kuwadhoofisha maadui zao zinaonekana zimezivutia nchi nyingi zenye raia waislamu kama vile China na India.
Hayo maeneo yenye bluu iliyokoza ndiyo makazi ya kiyahudi. Unaweza ukashangaa kwanini yote yasiwe eneo moja na karibu na mpaka upande wa magharibi. Haya maeneo yanakuwa yamechaguliwa maalum na kuwekwa kwenye ramani. Yanakuwa ni yale yenye rutuba au vyanzo vya maji safi au miinuko kwa matumizi ya kijeshi. Kinachofuatia huwa ni muda tu kulingana na bajeti ya nchi.
Zamu ya eneo fulani ikifika wakazi wa eneo hilo hupewa notisi ya kuhama kwa visingizio mbali mbali. Kwa udhaifu walionao na kwa kujua nguvu ya Israel wapalestina wengi huvunja majumba yao na kukushanya baadhi ya vitu vyao na kutia kwenye masanduku.Wale wanaoduwaa hawajachukua uamuzi, siku ikifika mabuldoza hufika na kuvunja bila kuhoji. Baada ya muda mfupi unakuta maghorofa ya wakaazi wa kiyahudi yakiwa yamebadili sura ya eneo lote.
Wapalestina waliokosa makaazi hawajui pa kwenda pia hupewa jina la wakaazi na sio raia na huwa wanapigwa danadana huku na huko mpaka wengi hufa na wachache wanaoamua kuhama hurahisishiwa njia za kutoka nje ili wakawe wakimbizi.
Mbali na makazi ya kiyahudi vijiji vilivyobaki vya wapalestina huzingirwa na kutenganishwa kwa kuta ndefu na seng'enge kiasi kwamba wapalestina waliokuwa majirani inaweza kuwachukua siku nzima mtu kumfikia mwenzake kutokana na kulazimika kuvuka vizuizi vingi vya kijeshi.
Mbinu hizi ni za muda mrefu na zinapata kasi kila mwaka.Mwaka 1948 mpaka 1967 ilikuwa ni kitu kingine na kutoka 1967 mpaka ilipomegwa Gaza ni kitu kingine. Na kuanzia hapo mpaka muda huu ni mbinu hiyo ya kuwazunguka wapalestina ndani kwa ndani.
Mafanikio ya Israel katika kuwadhoofisha maadui zao zinaonekana zimezivutia nchi nyingi zenye raia waislamu kama vile China na India.