Fya-fyafya
Member
- May 2, 2019
- 43
- 125
Hapa Nchini kumekuwepo na wimbi kubwa la wizi wa pikipiki hasa pikipiki aina ya Boxer.
Tena baada ya uzuka kwa ugonjwa wa Kirona, ndo hali imekuwa mbaya. Watu (bodaboda) wengi wamekuwa wakilizwa mara kwa mara.
Kwa nini pikipiki aina za boxer ndo zimekuwa zikishambuliwa sana kuibiwa? Wengi wanasema kinachotafutwa pale ni injini yake tu. Inasemekana inatumika sana kama mita ya kuvutia na kumwagilizia maji kwenye visima au kilimo cha umwagiliaji. Ila kama ni kuuza kwa ajiri ya spea, wezi hao huziuza kwa bei ya kutupwa sana.
Siku hizi ukiwa na pikipiki mpyunaifanyia kazi basi inabidi uwe mwangalifu sana tena sana. Hasa uwe selective wa abiria wako.
Baada ya utangulizi huo sasa niende kwa maada husika :" Ona hapa aina mbili mpya za wizi wa pikipiki uloshamiri mijini" na hizo mbinu za wizi ni
1) Mhogo feki kwenye mguu.
Hapa inakuwa hivi. Jamaa anachukua mabox ama vitambaa na kujiviringishia pamba juu kwenye unyayo na vidole hadi usawa wa goti mithili ya mtu aliyevunjika mguu na kuwekewa mhogo.
Kisha anachukua gongo na kuzuga nalo mara nyingi wanategeshea maeneo ya hospitali. Anajifanya kama vile ameruhusiwa (discharge) kwenda nyumbani. Anaweza akawa na kijibegi mkononi au mgongoni.
Basi ana chunguza bodaboda mwenye pikipiki boxer mpya na kumwita ampeleke mahali hasa hasa nyumbani. Basi kwa shida sana atapanda piki piki kisha anaondoka.
Trick ya wizi
Mkiwa njiani, tadondosha kwa makusudi lile ngongo kisha kukuomba msimame. Basi kwa vyovyote vile kwa huruma bodaboda atasimamisha pikipiki na kwenda kwa mguu harakaharaka kumchukulia lile gongo. Hapo hapo ndo penye mistake. (One mistake one goal) Bodaboda akiwa anaenda kuchukuwa hongo ndipo Mwizi huyo hudandia Pikipiki na kuondoka nayo Nduki. Watoto wa mjini wanasema anamwachia manyoya huku akijisemea kwa dharau :" Pumbavu Shenzi!"
2) Makazi feki kwenye nyumba ya heri.
Hii nayo inakuwa hivi:
Tofauti na ya kwanza ambapo anakuwa mtu mmoja, hapa hawa mabwana (wezi) wanakuwa kidogo a team. Wanaweza kuwasiliana watatu ama wanne.
Mchezo unakuwa hivi.
Hawa jamaa wanatafuta nyumba yenye geti iliyoko sehemu tulivu sana. Na wanakuwa wanakuwa kuwa wakazi wa nyumba hiyo si wengi na wako bize na mambo yao ( watu wa serikali au wafanyabishara) na once wametoka hawarudi mapema na endapo wamerudi hawatoki tena mpaka kesho.
Basi, hawa mabwana wanajipanga hivi. Wawili ama watatu wanabaki wamejificha maeneo ya getini la hiyo nyumba kisha mmoja wao anaenda kijiwe chochote cha pikipiki na kusellecki (kuchagua) bodaboda mwenye pikipiki boxer mpya na kumwambia ampeleke nyumbani.
Basi bodaboda walivyo na haraka atakubali na kubagain naye bei na kumpakia na kwenda naye kama abiria. Wakiwa njiani, huyu bwana anakuwa anawasiliana na wenzake wale kuwa wanakuja nao wajiseti kisawasawa.
Kama tujuwavyo bodaboda huongozwa na abiria basi jamaa atampekeka mbaka getini kwenye ile nyumba ambayo wenzie wameshajipanga. Basi jamaa (wizi) atashuka na kumpa bodaboda hela kubwa inayohitaji Change let's say 10000 au 5000.
Basi huyu bodaboda akiwa kwenye harakati za kujisachi chenji mfukoni ndipo wale wezi wengine hujitokeza na kumkaba ama kumpiga sehemu mbaya mwilini (wao wanazijua) ambapo ukipigwa mara moja unalegea hata sauti haitoki. Basi wao hujisemea kwa zarau'' Bumbavu" na kuchukuwa pikipiki na kupakizana mshikaki na kuishia nayo.
Aina hii ya wizi hutokea muda wowote . Hasubuhi, mchana na hata jioni.
My take. Chonde chonde, madereva bodaboda kuweni makini sana. Yamkini wewe unaesoma post hii si bodaboda ila una ndugu au jamaa ambaye ni boda boda au kabisa wewe mwenyewe unamiliki Pikipiki na umemwajiri kijana anakuletea hesabu jioni, basi ni mwafaka wa kumpa semina ya wizi huu wa piki piki.
Tena baada ya uzuka kwa ugonjwa wa Kirona, ndo hali imekuwa mbaya. Watu (bodaboda) wengi wamekuwa wakilizwa mara kwa mara.
Kwa nini pikipiki aina za boxer ndo zimekuwa zikishambuliwa sana kuibiwa? Wengi wanasema kinachotafutwa pale ni injini yake tu. Inasemekana inatumika sana kama mita ya kuvutia na kumwagilizia maji kwenye visima au kilimo cha umwagiliaji. Ila kama ni kuuza kwa ajiri ya spea, wezi hao huziuza kwa bei ya kutupwa sana.
Siku hizi ukiwa na pikipiki mpyunaifanyia kazi basi inabidi uwe mwangalifu sana tena sana. Hasa uwe selective wa abiria wako.
Baada ya utangulizi huo sasa niende kwa maada husika :" Ona hapa aina mbili mpya za wizi wa pikipiki uloshamiri mijini" na hizo mbinu za wizi ni
1) Mhogo feki kwenye mguu.
Hapa inakuwa hivi. Jamaa anachukua mabox ama vitambaa na kujiviringishia pamba juu kwenye unyayo na vidole hadi usawa wa goti mithili ya mtu aliyevunjika mguu na kuwekewa mhogo.
Kisha anachukua gongo na kuzuga nalo mara nyingi wanategeshea maeneo ya hospitali. Anajifanya kama vile ameruhusiwa (discharge) kwenda nyumbani. Anaweza akawa na kijibegi mkononi au mgongoni.
Basi ana chunguza bodaboda mwenye pikipiki boxer mpya na kumwita ampeleke mahali hasa hasa nyumbani. Basi kwa shida sana atapanda piki piki kisha anaondoka.
Trick ya wizi
Mkiwa njiani, tadondosha kwa makusudi lile ngongo kisha kukuomba msimame. Basi kwa vyovyote vile kwa huruma bodaboda atasimamisha pikipiki na kwenda kwa mguu harakaharaka kumchukulia lile gongo. Hapo hapo ndo penye mistake. (One mistake one goal) Bodaboda akiwa anaenda kuchukuwa hongo ndipo Mwizi huyo hudandia Pikipiki na kuondoka nayo Nduki. Watoto wa mjini wanasema anamwachia manyoya huku akijisemea kwa dharau :" Pumbavu Shenzi!"
2) Makazi feki kwenye nyumba ya heri.
Hii nayo inakuwa hivi:
Tofauti na ya kwanza ambapo anakuwa mtu mmoja, hapa hawa mabwana (wezi) wanakuwa kidogo a team. Wanaweza kuwasiliana watatu ama wanne.
Mchezo unakuwa hivi.
Hawa jamaa wanatafuta nyumba yenye geti iliyoko sehemu tulivu sana. Na wanakuwa wanakuwa kuwa wakazi wa nyumba hiyo si wengi na wako bize na mambo yao ( watu wa serikali au wafanyabishara) na once wametoka hawarudi mapema na endapo wamerudi hawatoki tena mpaka kesho.
Basi, hawa mabwana wanajipanga hivi. Wawili ama watatu wanabaki wamejificha maeneo ya getini la hiyo nyumba kisha mmoja wao anaenda kijiwe chochote cha pikipiki na kusellecki (kuchagua) bodaboda mwenye pikipiki boxer mpya na kumwambia ampeleke nyumbani.
Basi bodaboda walivyo na haraka atakubali na kubagain naye bei na kumpakia na kwenda naye kama abiria. Wakiwa njiani, huyu bwana anakuwa anawasiliana na wenzake wale kuwa wanakuja nao wajiseti kisawasawa.
Kama tujuwavyo bodaboda huongozwa na abiria basi jamaa atampekeka mbaka getini kwenye ile nyumba ambayo wenzie wameshajipanga. Basi jamaa (wizi) atashuka na kumpa bodaboda hela kubwa inayohitaji Change let's say 10000 au 5000.
Basi huyu bodaboda akiwa kwenye harakati za kujisachi chenji mfukoni ndipo wale wezi wengine hujitokeza na kumkaba ama kumpiga sehemu mbaya mwilini (wao wanazijua) ambapo ukipigwa mara moja unalegea hata sauti haitoki. Basi wao hujisemea kwa zarau'' Bumbavu" na kuchukuwa pikipiki na kupakizana mshikaki na kuishia nayo.
Aina hii ya wizi hutokea muda wowote . Hasubuhi, mchana na hata jioni.
My take. Chonde chonde, madereva bodaboda kuweni makini sana. Yamkini wewe unaesoma post hii si bodaboda ila una ndugu au jamaa ambaye ni boda boda au kabisa wewe mwenyewe unamiliki Pikipiki na umemwajiri kijana anakuletea hesabu jioni, basi ni mwafaka wa kumpa semina ya wizi huu wa piki piki.