Uchaguzi 2020 Ona alivyokiuka kiapo chake, hafai kuongezewa mitano tena

Mzalendo Uchwara

JF-Expert Member
Jan 26, 2020
3,633
11,475
Kwa lugha rahisi, kiapo ni ahadi rasmi, tena mbele ya ushahidi wa Mwenyezi Mungu juu ya matendo yako na tabia zako kuanzia siku hiyo ya kiapo.

Kwa ndugu zangu wakristo kama alivyo mheshimiwa JPM, kiapo kinaambatana na kushika biblia takatifu mkononi na hivyo basi kumfanya Mungu awe shahidi wa kiapo chako.

Msingi wa kiapo kwenye biblia ni kitabu cha hesabu 30:2, Mungu anasema hivi "Mtu akiweka nadhiri kwa Mwenyezi-Mungu au akiahidi kwa kiapo na kujifunga nafsi yake kwa ahadi, ni lazima atimize ahadi yake; ni lazima atekeleze yote yale aliyotamka kwa kauli yake".

Tukirejea kwa huyu mheshimiwa wetu, katika miaka mitano ya 'utawala' wake, tumeshuhudia akikiuka kiapo chake tena na tena, na hivyo kuthibitisha kuwa ni mtu asiye aminika na hafai kuwa kiongozi mkuu wa nchi.

Kiapo chake kilikua hivi:

"Mimi JPM, naapa nitakuwa mwaminifu kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na nitalinda na kuitetea Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kama ilivyowekwa kwa mujibu wa Sheria, ewe Mwenyezi MUNGU nisaidie."


"Mimi JPM naapa nitatenda kazi zangu za Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa uaminifu kwa kutimiza wajibu wa kazi hizo kwa bidii na moyo mkunjufu na nitawatendea haki watu wote kwa mujibu wa sheria, mila na desturi za Tanzania, bila woga, bila upendeleo, huba wala chuki. ewe mwenyezi MUNGU nisaidie."

"Mimi JPM naapa katika kutekeleza majukumu katika kutekeleza madaraka niliyopewa kwa mujibu wa KATIBA ya Umoja wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, nitatetea na kudumisha umoja wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa mujibu wa Katiba, ewe Mwenyezi MUNGU nisaidie."

Tuiache sehemu ya kwanza ya kiapo (japo kuna kila dalili amekua akiivunja pia)

Sehemu ya pili ya kiapo chake anaahidi kuwatumikia watanzania wote kwa moyo mkunjufu bila UPENDELEO, huba wala CHUKI. tena anaahidi kuwatendea HAKI!

Sasa ni mara ngapi katika kipindi cha miaka 5 tumesikia akizuia watu fulani wasibomolewe nyumba zao eti kwakua walimpigia kura yeye, na wakati huohuo akiagiza wengine ambao anaamini hawakumpigia kura wavunjiwe nyumba zao?

Au akiwananga, kuwazodoa, kuwatisha na kuwang'ong'a baadhi ya watanzania kuwa hawezi kuwaletea maendeleo eti kwakua walichagua mbunge wa chama tofauti na chama chake?? Hii ni chuki, ubaguzi na uvunjifu wa kiapo chake wa waziwazi.

Imefika kipindi kauli hizo za kibaguzi na zinazo onesha mwelekeo wa upendeleo zimeendelea kutolewa kwenye kampeni zake za kuomba nafasi tena, sote tulimsikia pale kawe akikiri dhambi hiyo mbaya ya upendeleo na ubaguzi.

Mbaya zaidi hata makamu wake naye ameanza kutoa kauli hizo za chuki na husda.

Matendo haya yanapelekea kuvunja sehemu ya tatu ya kiapo chake, ameahindi kudumisha umoja wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania, lakini sote ni mashahidi kuwa kwasasa nchi yetu imejaa chuki za kisiasa, na kuna viashiria vya ukabila na ukanda. Watanzania walio chama hiki wanawaona wa chama kile ni maadui na wasaliti! Wanatishia hata kuwaua waziwazi.

Watanzania tunastahili rais mkweli, mwenye kutambua wajibu wake ni kwa watanzania wote bila kujali dini, itikadi za kisiasa, kabila au rangi ya mtu. Rais atakaye tenda HAKI kwa wote, rais atakayeheshimu kiapo chake. Kwa uzoefu tulioupata ndani ya miaka mitano hii basi ni wazi kabisa kuwa ndugu JPM hawezi kuwa rais wa aina hiyo.
 
Kwa lugha rahisi, kiapo ni ahadi rasmi, tena mbele ya ushahidi wa Mwenyezi Mungu juu ya matendo yako na tabia zako kuanzia siku hiyo ya kiapo.

Kwa ndugu zangu wakristo kama alivyo mheshimiwa JPM, kiapo kinaambatana na kushika biblia takatifu mkononi na hivyo basi kumfanya Mungu awe shahidi wa kiapo chako.

Msingi wa kiapo kwenye biblia ni kitabu cha hesabu 30:2, Mungu anasema hivi "Mtu akiweka nadhiri kwa Mwenyezi-Mungu au akiahidi kwa kiapo na kujifunga nafsi yake kwa ahadi, ni lazima atimize ahadi yake; ni lazima atekeleze yote yale aliyotamka kwa kauli yake".

Tukirejea kwa huyu mheshimiwa wetu, katika miaka mitano ya 'utawala' wake, tumeshuhudia akikiuka kiapo chake tena na tena, na hivyo kuthibitisha kuwa ni mtu asiye aminika na hafai kuwa kiongozi mkuu wa nchi.

Kiapo chake kilikua hivi:

"Mimi JPM, naapa nitakuwa mwaminifu kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na nitalinda na kuitetea Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kama ilivyowekwa kwa mujibu wa Sheria, ewe Mwenyezi MUNGU nisaidie."


"Mimi JPM naapa nitatenda kazi zangu za Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa uaminifu kwa kutimiza wajibu wa kazi hizo kwa bidii na moyo mkunjufu na nitawatendea haki watu wote kwa mujibu wa sheria, mila na desturi za Tanzania, bila woga, bila upendeleo, huba wala chuki. ewe mwenyezi MUNGU nisaidie."

"Mimi JPM naapa katika kutekeleza majukumu katika kutekeleza madaraka niliyopewa kwa mujibu wa KATIBA ya Umoja wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, nitatetea na kudumisha umoja wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa mujibu wa Katiba, ewe Mwenyezi MUNGU nisaidie."

Tuiache sehemu ya kwanza ya kiapo (japo kuna kila dalili amekua akiivunja pia)

Sehemu ya pili ya kiapo chake anaahidi kuwatumikia watanzania wote kwa moyo mkunjufu bila UPENDELEO, huba wala CHUKI. tena anaahidi kuwatendea HAKI!

Sasa ni mara ngapi katika kipindi cha miaka 5 tumesikia akizuia watu fulani wasibomolewe nyumba zao eti kwakua walimpigia kura yeye, na wakati huohuo akiagiza wengine ambao anaamini hawakumpigia kura wavunjiwe nyumba zao?

Au akiwananga, kuwazodoa, kuwatisha na kuwang'ong'a baadhi ya watanzania kuwa hawezi kuwaletea maendeleo eti kwakua walichagua mbunge wa chama tofauti na chama chake?? Hii ni chuki, ubaguzi na uvunjifu wa kiapo chake wa waziwazi.

Imefika kipindi kauli hizo za kibaguzi na zinazo onesha mwelekeo wa upendeleo zimeendelea kutolewa kwenye kampeni zake za kuomba nafasi tena, sote tulimsikia pale kawe akikiri dhambi hiyo mbaya ya upendeleo na ubaguzi.

Mbaya zaidi hata makamu wake naye ameanza kutoa kauli hizo za chuki na husda.

Matendo haya yanapelekea kuvunja sehemu ya tatu ya kiapo chake, ameahindi kudumisha umoja wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania, lakini sote ni mashahidi kuwa kwasasa nchi yetu imejaa chuki za kisiasa, na kuna viashiria vya ukabila na ukanda. Watanzania walio chama hiki wanawaona wa wanawaona wa chama kile ni maadai na wasaliti! Wanatishia hata kuwaua waziwazi.

Watanzania tunastahili rais mkweli, mwenye kutambua wajibu wake ni kwa watanzania wote bila kujali dini, itikadi za kisiasa, kabila au rangi ya mtu. Rais atakaye tenda HAKI kwa wote, rais atakayeheshimu kiapo chake. Kwa uzoefu tulioupata ndani ya miaka mitano hii basi ni wazi kabisa kuwa ndugu JPM hawezi kuwa rais wa aina hiyo.
Piga chini 28/10 nampa lisu kura yangu
 
Hivi mtu na akili zako timamu kabisa yani. Unaamka asubuhi unachukua kitambulisho chako cha kupiga kura unaenda kujipanga foleni kituo cha kupiga kura then kura yako unampa Magufuli!


...si bora ukalala tu kuliko kupoteza muda wako ambao utaujutia ndani ya siku 100 magufuli akiapishwa kuwa rais tena!
 
Kwa lugha rahisi, kiapo ni ahadi rasmi, tena mbele ya ushahidi wa Mwenyezi Mungu juu ya matendo yako na tabia zako kuanzia siku hiyo ya kiapo.

Kwa ndugu zangu wakristo kama alivyo mheshimiwa JPM, kiapo kinaambatana na kushika biblia takatifu mkononi na hivyo basi kumfanya Mungu awe shahidi wa kiapo chako.

Msingi wa kiapo kwenye biblia ni kitabu cha hesabu 30:2, Mungu anasema hivi "Mtu akiweka nadhiri kwa Mwenyezi-Mungu au akiahidi kwa kiapo na kujifunga nafsi yake kwa ahadi, ni lazima atimize ahadi yake; ni lazima atekeleze yote yale aliyotamka kwa kauli yake".

Tukirejea kwa huyu mheshimiwa wetu, katika miaka mitano ya 'utawala' wake, tumeshuhudia akikiuka kiapo chake tena na tena, na hivyo kuthibitisha kuwa ni mtu asiye aminika na hafai kuwa kiongozi mkuu wa nchi.

Kiapo chake kilikua hivi:

"Mimi JPM, naapa nitakuwa mwaminifu kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na nitalinda na kuitetea Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kama ilivyowekwa kwa mujibu wa Sheria, ewe Mwenyezi MUNGU nisaidie."


"Mimi JPM naapa nitatenda kazi zangu za Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa uaminifu kwa kutimiza wajibu wa kazi hizo kwa bidii na moyo mkunjufu na nitawatendea haki watu wote kwa mujibu wa sheria, mila na desturi za Tanzania, bila woga, bila upendeleo, huba wala chuki. ewe mwenyezi MUNGU nisaidie."

"Mimi JPM naapa katika kutekeleza majukumu katika kutekeleza madaraka niliyopewa kwa mujibu wa KATIBA ya Umoja wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, nitatetea na kudumisha umoja wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa mujibu wa Katiba, ewe Mwenyezi MUNGU nisaidie."

Tuiache sehemu ya kwanza ya kiapo (japo kuna kila dalili amekua akiivunja pia)

Sehemu ya pili ya kiapo chake anaahidi kuwatumikia watanzania wote kwa moyo mkunjufu bila UPENDELEO, huba wala CHUKI. tena anaahidi kuwatendea HAKI!

Sasa ni mara ngapi katika kipindi cha miaka 5 tumesikia akizuia watu fulani wasibomolewe nyumba zao eti kwakua walimpigia kura yeye, na wakati huohuo akiagiza wengine ambao anaamini hawakumpigia kura wavunjiwe nyumba zao?

Au akiwananga, kuwazodoa, kuwatisha na kuwang'ong'a baadhi ya watanzania kuwa hawezi kuwaletea maendeleo eti kwakua walichagua mbunge wa chama tofauti na chama chake?? Hii ni chuki, ubaguzi na uvunjifu wa kiapo chake wa waziwazi.

Imefika kipindi kauli hizo za kibaguzi na zinazo onesha mwelekeo wa upendeleo zimeendelea kutolewa kwenye kampeni zake za kuomba nafasi tena, sote tulimsikia pale kawe akikiri dhambi hiyo mbaya ya upendeleo na ubaguzi.

Mbaya zaidi hata makamu wake naye ameanza kutoa kauli hizo za chuki na husda.

Matendo haya yanapelekea kuvunja sehemu ya tatu ya kiapo chake, ameahindi kudumisha umoja wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania, lakini sote ni mashahidi kuwa kwasasa nchi yetu imejaa chuki za kisiasa, na kuna viashiria vya ukabila na ukanda. Watanzania walio chama hiki wanawaona wa wanawaona wa chama kile ni maadai na wasaliti! Wanatishia hata kuwaua waziwazi.

Watanzania tunastahili rais mkweli, mwenye kutambua wajibu wake ni kwa watanzania wote bila kujali dini, itikadi za kisiasa, kabila au rangi ya mtu. Rais atakaye tenda HAKI kwa wote, rais atakayeheshimu kiapo chake. Kwa uzoefu tulioupata ndani ya miaka mitano hii basi ni wazi kabisa kuwa ndugu JPM hawezi kuwa rais wa aina hiyo.
Ndio amesha kuwa kama hutaki mlete babako awe raisi .mpuuzi wewe
 
32 Reactions
Reply
Back
Top Bottom