on your own opinion; Who is the best Marketing manager in Tanzania?

Lucas

JF-Expert Member
Dec 3, 2011
2,457
1,108
On my own side i refer Kelvin Twisa and Ephraim Mafuru.

These two guys they played well in communication industry whereby Twisa is mainly based on Youths as major targeted customers while Mafuru always based on product differentiaon.

for me these two guys they have done well in the industry, who are your favorite Marketing personels in Tanzania?
 
huyo twisa na mafuru ndo akina nani..marketing managers kwenye nin?
 
Thread zingine ni noma, Huwezi linganisha Marketing manager kwenye industrt tofauti, ni kama mtu aje hapa aulize kati ya Kampuni ya Kutengeneza Ndege ya AirBus na kampuni ya SONY ni ipi inauza sana, havi ni vitu viwili tofauti,

Na hata kwa mameneja ni bora ukawalinganisha wa the same Industry kama ni Mabenk basi mabenk tu, kama ni mwasilinan iwe ni mawasilino tu, sasa kuja hapa na kutaka kujua ni nani mzuri inakuwa vigumu sana, make Industry ni tofauti na Aproach zao ni tofauti.
 
Kwa. Vigezo vp ?
Kutoa misaada na kuoneka katika luninga ukitoa dakika moja kwa. Sh 60 sidhani hiyo ni marketing
 
Kwa kuwa wanaonekana kwenye TV kila mara au ni vigezo gani unatumia. Kwangu mimi hawa ni mapropaganda wazuri. Nafikiri kabla ya kusema flani ni mzuri au la ni lazima kuwa na vigezo. Hebu weka vigezo vya marketing manager mzuri kwanza
 
  • Thanks
Reactions: DSN
Naona ulitaka kuwapaisha na si kutafuta hicho unachokitafuta!! kama ni nani is who's in town corporate talk basi dhahiri umeshawataja!!!Kama wadau wengine walivuokwisha sema kuna vigezo. Japo waweza kuwaweka kwenye mizania moja lakini ukizingatia soko la bidhaa husika.

Mpaka sasa wataalamu wa masoko Tanzania ni taaluma ambayo bado inaonekana kama ipo ipo tu, lakini kwa ujumla wake ndiyo taaluma inayosababisha walaji waamue kununua ama kutokunua bidhaa ama huduma husika kwa mujibu wa mapokeo yaliyotengenezwa na wanataaluma hiyo.

Mimi binafsi zamani nilijua Afisa masoko ni mfanyakazi wa umma, kama vile mashirika ya umma kama BIMA, RTC, Vyama vya ushirika na ofsi za biashara za wilaya.Na utendaji wao wa zama zile hakika ulikuwa ni ule tusiona leo!!Zaidi kama ulikuwa unafahamiana na mmoja wapo basi utasikia ameenda ulaya, lakini utendaji wa hapa ndani zaidi ya kumuona afisa bishara na masoko akijaza form za biashara hakuna jingine.

Ujio wa Private companiesa na Corporate companies kama mobile phone network provide, Beer Industries, Soda umeleta aina mpya ya kizazi kilichosoma biashara na hasa kwa Tanzania zao kubwa la marketing ukiacha elimu ya Nje ni chuo cha biashara cha CBE.Japo vyuo kama Mzumbe na UDSM nao kupitia mifumo yao wana wanataaluma wa fani hiyo lakini wengi kwa mfano UDSM wanatokana na Bcom na Mzumbe wao ndio wameanzisha kwa sasa Degree ya Marketing.

Kwa watanzania walio wengi hawajui umuhimu wa fani hii ya masoko na hivyo hata mwenendo mzima wa taaluma hii kwa Tanzania bado haujapata kizazi cha kuifanya watanzania waifahamu Taaluma hii kwa mapana yake.Watanzania hawajui kuwa haya mabango, wanayoyaona mabarabarani, matangazo wanayosikia kwenye radio au television , ni kazi iliyobuniwa na kutengenezwa na taaluma hiyo.Watanzania walio wengi hawana ufahamu japo kuwa mpaka anavutika kununua kitu ni kazi ya mtu wa masoko
 
Sioni m2 mimi awe imani kajula, mafuru, au twissa mbwembwe 2 na wizi ndo vimewatawala.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom