Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,443
- 113,452
Kwa mlio na access,
Watch TBC sasa, Waziri wa Sheria na Katiba, Mhe. Selina Kombani yuko live hewani, akiutetea Muswada wa Kuunda Tume ya Kukusanya Maoni ya katiba mpya!.
Ameutetea kwa nguvu zake zote huo muswada jinsi ulivyo, ila pia amekubali, kuyapokeo maoni na mapendekezo yote yanayotolewa, ndio maana wametoa nafasi kwa wananchi kutoa maoni.
Update:
Wanabodi,
Leo ndio mara yangu ya kwanza kumuona Waziri wetu wa Sheria, Mhe. Selina Kombani akihojiwa live kwenye kipindi cha Jambo, kinachorushwa na TBC-1 asubuhi hii.
Alipokuwa akitetea mamlaka kubwa za rais kwenye utungaji wa katiba, Mhe. Kombani amesema, Tangu kutungwa kwa katiba ya Tanzania ya Mwaka 1977, Tanzania tumekuwa na katiba nyingine zaidi ya 5 ambazo zote process ndio hiyo hiyo kwa rais kuwa na mamlaka kubwa hivyo na zote zimesainiwa na rais, kitu ambacho sio kweli!.
Mhe. Kombani wakati akizungumzia katiba hizo tano, alimaanisha marekebisho zaidi ya matano ya katiba, yaliyofanywa kwenye katiba ya Tanzania ya Mwaka 1977, na sio katiba tano kama alivyoeleza Mhe. Waziri.
Usahihi ni kuwa Ile katiba ya Tanzania ya Mwaka 1977, ndio hiyo hiyo katiba iliyopo mpaka sasa, licha ya kufanyiwa marekebisho zaidi ya mara 5!. Marekebisho hayo hayabadilishi katiba na kuwa na katiba tano, katiba inabaki ni ile ile moja ya Mwaka 1977!.
Mhe. Kombani, hakuishia hapo, katika utetezi wake kwa mamlaka ya rais pale aliposema, katiba hizo zote 5!, zimesainiwa na rais, kitu ambacho pia sio kweli!. Katiba ya Tanzania ya Mwaka 1977, ilitokana na Bunge la Katiba 'Constituent Assembly' (Japo ni Bunge lile lile la chama kimoja lilijigeuza), ambalo ndilo liliipitisha katiba. Katiba ikishapitishwa na Bunge la Katiba, haisainiwi na rais, rais mwenyewe, anapata mamlaka toka kwenye katiba hiyo, ila kinachosainiwa na rais, ni yale marekebisho ya katiba!.
Hivyo mpaka ninapoandika hapa, Waziri wetu wa Sheria, anaamini yuko right kabisa kutoa mamlaka kubwa zile kwa rais katika marekebisho ya katiba, kwa vile anaamini kinachofanyika sasa, ni marekebisho mengine ya katiba ile ile ya Tanzania ya Mwaka 1977 na sio process ya Uundwaji wa katiba mpya!.
Waziri wa Sheria, anajua kuwa ni rais ndiye ameisaini Katiba ya Tanzania ya Mwaka 1977, kitu ambacho sio kweli!.
Japo sio kosa kubwa kwa mtu wa kawaida kuyaita marekebisho ya katiba kuwa ni katiba nyingine, lakini kwa Waziri wa Sheria, Live kwenye TV ya Taifa, kusema Tumekuwa na katiba 5 baada ya Katiba ya Tanzania ya Mwaka 1977, ni uthibitisho kuwa tunaye Waziri wa Sheria Asiyejua Katiba!.
Wasalaam.
Pasco.
Watch TBC sasa, Waziri wa Sheria na Katiba, Mhe. Selina Kombani yuko live hewani, akiutetea Muswada wa Kuunda Tume ya Kukusanya Maoni ya katiba mpya!.
Ameutetea kwa nguvu zake zote huo muswada jinsi ulivyo, ila pia amekubali, kuyapokeo maoni na mapendekezo yote yanayotolewa, ndio maana wametoa nafasi kwa wananchi kutoa maoni.
Update:
Wanabodi,
Leo ndio mara yangu ya kwanza kumuona Waziri wetu wa Sheria, Mhe. Selina Kombani akihojiwa live kwenye kipindi cha Jambo, kinachorushwa na TBC-1 asubuhi hii.
Alipokuwa akitetea mamlaka kubwa za rais kwenye utungaji wa katiba, Mhe. Kombani amesema, Tangu kutungwa kwa katiba ya Tanzania ya Mwaka 1977, Tanzania tumekuwa na katiba nyingine zaidi ya 5 ambazo zote process ndio hiyo hiyo kwa rais kuwa na mamlaka kubwa hivyo na zote zimesainiwa na rais, kitu ambacho sio kweli!.
Mhe. Kombani wakati akizungumzia katiba hizo tano, alimaanisha marekebisho zaidi ya matano ya katiba, yaliyofanywa kwenye katiba ya Tanzania ya Mwaka 1977, na sio katiba tano kama alivyoeleza Mhe. Waziri.
Usahihi ni kuwa Ile katiba ya Tanzania ya Mwaka 1977, ndio hiyo hiyo katiba iliyopo mpaka sasa, licha ya kufanyiwa marekebisho zaidi ya mara 5!. Marekebisho hayo hayabadilishi katiba na kuwa na katiba tano, katiba inabaki ni ile ile moja ya Mwaka 1977!.
Mhe. Kombani, hakuishia hapo, katika utetezi wake kwa mamlaka ya rais pale aliposema, katiba hizo zote 5!, zimesainiwa na rais, kitu ambacho pia sio kweli!. Katiba ya Tanzania ya Mwaka 1977, ilitokana na Bunge la Katiba 'Constituent Assembly' (Japo ni Bunge lile lile la chama kimoja lilijigeuza), ambalo ndilo liliipitisha katiba. Katiba ikishapitishwa na Bunge la Katiba, haisainiwi na rais, rais mwenyewe, anapata mamlaka toka kwenye katiba hiyo, ila kinachosainiwa na rais, ni yale marekebisho ya katiba!.
Hivyo mpaka ninapoandika hapa, Waziri wetu wa Sheria, anaamini yuko right kabisa kutoa mamlaka kubwa zile kwa rais katika marekebisho ya katiba, kwa vile anaamini kinachofanyika sasa, ni marekebisho mengine ya katiba ile ile ya Tanzania ya Mwaka 1977 na sio process ya Uundwaji wa katiba mpya!.
Waziri wa Sheria, anajua kuwa ni rais ndiye ameisaini Katiba ya Tanzania ya Mwaka 1977, kitu ambacho sio kweli!.
Japo sio kosa kubwa kwa mtu wa kawaida kuyaita marekebisho ya katiba kuwa ni katiba nyingine, lakini kwa Waziri wa Sheria, Live kwenye TV ya Taifa, kusema Tumekuwa na katiba 5 baada ya Katiba ya Tanzania ya Mwaka 1977, ni uthibitisho kuwa tunaye Waziri wa Sheria Asiyejua Katiba!.
Wasalaam.
Pasco.