On a Serious Note: Waziri wa Sheria anapokuwa hajui Katiba!

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,443
113,452
Kwa mlio na access,
Watch TBC sasa, Waziri wa Sheria na Katiba, Mhe. Selina Kombani yuko live hewani, akiutetea Muswada wa Kuunda Tume ya Kukusanya Maoni ya katiba mpya!.

Ameutetea kwa nguvu zake zote huo muswada jinsi ulivyo, ila pia amekubali, kuyapokeo maoni na mapendekezo yote yanayotolewa, ndio maana wametoa nafasi kwa wananchi kutoa maoni.

Update:
Wanabodi,

Leo ndio mara yangu ya kwanza kumuona Waziri wetu wa Sheria, Mhe. Selina Kombani akihojiwa live kwenye kipindi cha Jambo, kinachorushwa na TBC-1 asubuhi hii.

Alipokuwa akitetea mamlaka kubwa za rais kwenye utungaji wa katiba, Mhe. Kombani amesema, Tangu kutungwa kwa katiba ya Tanzania ya Mwaka 1977, Tanzania tumekuwa na katiba nyingine zaidi ya 5 ambazo zote process ndio hiyo hiyo kwa rais kuwa na mamlaka kubwa hivyo na zote zimesainiwa na rais, kitu ambacho sio kweli!.

Mhe. Kombani wakati akizungumzia katiba hizo tano, alimaanisha marekebisho zaidi ya matano ya katiba, yaliyofanywa kwenye katiba ya Tanzania ya Mwaka 1977, na sio katiba tano kama alivyoeleza Mhe. Waziri.

Usahihi ni kuwa Ile katiba ya Tanzania ya Mwaka 1977, ndio hiyo hiyo katiba iliyopo mpaka sasa, licha ya kufanyiwa marekebisho zaidi ya mara 5!. Marekebisho hayo hayabadilishi katiba na kuwa na katiba tano, katiba inabaki ni ile ile moja ya Mwaka 1977!.

Mhe. Kombani, hakuishia hapo, katika utetezi wake kwa mamlaka ya rais pale aliposema, katiba hizo zote 5!, zimesainiwa na rais, kitu ambacho pia sio kweli!. Katiba ya Tanzania ya Mwaka 1977, ilitokana na Bunge la Katiba 'Constituent Assembly' (Japo ni Bunge lile lile la chama kimoja lilijigeuza), ambalo ndilo liliipitisha katiba. Katiba ikishapitishwa na Bunge la Katiba, haisainiwi na rais, rais mwenyewe, anapata mamlaka toka kwenye katiba hiyo, ila kinachosainiwa na rais, ni yale marekebisho ya katiba!.

Hivyo mpaka ninapoandika hapa, Waziri wetu wa Sheria, anaamini yuko right kabisa kutoa mamlaka kubwa zile kwa rais katika marekebisho ya katiba, kwa vile anaamini kinachofanyika sasa, ni marekebisho mengine ya katiba ile ile ya Tanzania ya Mwaka 1977 na sio process ya Uundwaji wa katiba mpya!.

Waziri wa Sheria, anajua kuwa ni rais ndiye ameisaini Katiba ya Tanzania ya Mwaka 1977, kitu ambacho sio kweli!.

Japo sio kosa kubwa kwa mtu wa kawaida kuyaita marekebisho ya katiba kuwa ni katiba nyingine, lakini kwa Waziri wa Sheria, Live kwenye TV ya Taifa, kusema Tumekuwa na katiba 5 baada ya Katiba ya Tanzania ya Mwaka 1977, ni uthibitisho kuwa tunaye Waziri wa Sheria Asiyejua Katiba!.

Wasalaam.

Pasco.
 
Mhe Kombani, amekiri ni kweli rais amepewa madaraka makubwa sana kwenye muswada huo, lakini akasema madaraka hayo, yametokana na katiba yetu ya Tanzania ya mwaka 1977.
 
Mhe Kombani, amekiri ni kweli rais amepewa madaraka makubwa sana kwenye muswada huo, lakini akasema madaraka hayo, yametokana na katiba yetu ya Tanzania ya mwaka 1977.

Kwahiyo hii ni "vicious circle"?

Nimesikia Mathias Chikawe BBC leo asubuhi anatetea pia muswada huu kwa "nguvu" zake zote!
 
Kwahiyo hii ni "vicious circle"?

Nimesikia Mathias Chikawe BBC leo asubuhi anatetea pia muswada huu kwa "nguvu" zake zote!

watetee kwa nguvu zote, hata kwa nguvu ya risasi.

all we need is Katiba. Katiba yetu, siyo yao.

vinginevyo patachimbika.

kama hawaamini, basi waendelee kucheza danadana na sheria mama ya vizazi vyetu.
 
These people really don't get IT! the are incapable of getting it, and they would never get it even if you were to hammer it with a six inches nail in their heads. It is not about them, it is not about cosmetic change; it is about the fact that the people want to exercise their sovereignty by writing a new constitution. I mean, what is so hard to understand in that?
 
Watanzania sasa wameamka na hawataki longo longo. nafikiri siku ya jana Tambwe hizi alijionea mwenyewe, kwa hiyo ngoja wapindishe tu, wataona mwisho wake. Hatukubali kwa nguzu zoteeeeeeeee
 
Kuna lawyer jana kaniboa sana STAR TV.......ati Marekani wana katiba ya miaka 250 na hawabadili katiba iweje sisi tubadili yetu yenye miaka 34 tu?
 
lakini pia kaelezea kuwa yale maeneo yaliyotajwa kama muungano, urais nk yanapaswa kutolewa maoni katika kuboresha tu na si kufifisha!
maoni kwamba muungano ufe hayatapokelewa
maoni kwamba uraisi ufe na tuweke usultani/ufalme pia hayatapokelewa

nafikiri hayajafafanuliwa vizuri kwenye mswada ule
 
Kuna lawyer jana kaniboa sana STAR TV.......ati Marekani wana katiba ya miaka 250 na hawabadili katiba iweje sisi tubadili yetu yenye miaka 34 tu?

Ni lawyer gani huyo anaboa kiasi hicho? Ni lazima awe zao la chuo cha kata kwani anachoongea ni upupu usio na mfano? Ni nani amemwambia ugomvi wetu ni umri wa katiba? Marekani hawabadili kwa kuwa yao iko valid kulingana na matakwa yao kama nchi? Sisi si copy ya Marekani kwamba wanachofanya wao ni lazima kiwe sahihi kwetu pia. Yetu haitufai kulingana na kilichomo kwenye sheria hiyo mama period. So kwake yeye kilichomo kwenye katiba yetu ni sahihi? Hivi wajinga kama hawa wanapataje audience kwenye hizi TV au ndio wametumwa? Inakera sana kwa kweli kwa the so called "msomi" kuongea utumbo kama huo on air.
 
Kuna lawyer jana kaniboa sana STAR TV.......ati Marekani wana katiba ya miaka 250 na hawabadili katiba iweje sisi tubadili yetu yenye miaka 34 tu?

Issue ni approach waliotumia wamarekani kupata katiba .....wao hawakuangalia katiba iwafae watu wa wakati wao tu bali walifikiria vizazi na vizazi. Sisi hapa watanzania naona walioko madarakani wana mkakati wa kuhakikisha katiba italinda maslahi yao badala ya kulinda maslahi ya watanzania wote. Kama katiba itajengwa kwa misingi mibovu si ajabu ikabadilishwa hata ndani ya muda mfupi.
 
Tambwe jana kaumbuka sana.....sijui atamwabia nini Baba yake Makamba

mkuu... hivi ccm wanafanya makusudi au ni nini...? hivi hakuna mtu mwingine anayeweza kuwakilisha ccm katika masuala muhimu ya taifa pasipo Tambwe Hiza .... huu ni mzaha na dharau katika kuleta maendeleo ya nchi yetu
 
Wanabodi,

Leo ndio mara yangu ya kwanza kumuona Waziri wetu wa Sheria, Mhe. Selina Kombani akihojiwa live kwenye kipindi cha Jambo, kinachorushwa na TBC-1 asubuhi hii.

Alipokuwa akitetea mamlaka kubwa za rais kwenye utungaji wa katiba, Mhe. Kombani amesema, Tangu kutungwa kwa katiba ya Tanzania ya Mwaka 1977, Tanzania tumekuwa na katiba nyingine5 ambazo zote process ndio hiyo hiyo kwa rais kuwa na mamlaka kubwa hivyo na zote zimesainiwa na rais, kitu ambacho sio kweli.

Mhe. Kombani wakati akizungunzia katiba hizo tano, alimaanisha marekebisho ya matano ya katiba, yaliyofanywa kwenye katiba ya Tanzania ya Mwaka 1977, na sio katiba tano kama alivyoeleza Mhe. Waziri.

Usahihi ni kuwa Ile katiba ya Tanzania ya Mwaka 1977, ndio hiyo katiba katiba iliyopo mpaka sasa, licha ya kufanyiwa marekebisho mara 5, marekebisho hayo hayabadilishi katiba na kuwa na katiba tano, katiba inabaki ni ile ile moja ya Mwaka 1977!.

Mhe. Kombani, hakuishia hapo, katika utetezi wake kwa mamlaka ya rais pale aliposema, katiba hizo zote 5, zimesainiwa na rais, kitu ambacho pia sio kweli. Katiba ya Tanzania ya Mwaka 1977, ilitokana na Bunge la Katiba 'Constituent Assembly' (Japo ni Bunge lile lile la chama kimoja lilijigeuza), ambalo ndilo liliipitisha katiba. Katiba ikishapitishwa na Bunge la Katiba, haisainiwi na rais, rais mwenyewe, anapata mamlaka toka kwenye katiba hiyo, ila kinachosainiwa na rais, ni yale marekebisho ya katiba.

Hivyo mpaka ninapoandika hapa, Waziri wetu wa Sheria, anaamini yuko right kabisa kutoa mamlaka kubwa zile kwa rais katika marekebisho ya katiba, kwa vile anaamini kinachofanyika sasa, ni marekebisho mengine ya katiba ile ile ya Tanzania ya Mwaka 1977 na sio process ya Uuundwaji wa katiba mpya.

Waziri wa Sheria, anajua kuwa ni rais ndiye ameisaini Katiba ya Tanzania ya Mwaka 1977, kitu ambacho sio kweli.

Japo sio kosa kubwa kwa mtu wa kawaida kuyaita marekebisho ya katiba kuwa ni katiba nyingine, lakini kwa Waziri wa Sheria, Live kwenye TV ya Taifa, kusema Tumekuwa na katiba 5 baada ya Katiba ya Tanzania ya Mwaka 1977, ni uthibitisho kuwa tunaye Waziri wa Sheria Asiyejua Katiba.

Wasalaam.

Pasco.

NB.(Somo la Katiba, ndio somo la kwanza kwa mwanafunzi wa mwaka wa kwanza wa sheria, anapufundishwa 'What is Law?').
 
Hahahahhaaaaaaaa.
Mama selina rudi jimbon ukalime mpungaaaa,eeeeeh hayo mambo ya sheria ni KIZUNGUMKUT
 
yaani acha tuu...hata Robert Manumba aliulizwa kwamba katiba ya tanzania inasemaje kuhusu madaraka ya jeshi la polisi ..akajibu kuwa yeye sio mtaalam wa katiba .... najiuliza katiba hii nani anatakiwa aijue...?
 
These people really don't get IT! the are incapable of getting it, and they would never get it even if you were to hammer it with a six inches nail in their heads. It is not about them, it is not about cosmetic change; it is about the fact that the people want to exercise their sovereignty by writing a new constitution. I mean, what is so hard to understand in that?[/QUOTE]

Asante Mwanakijiji kwa hoja na swali la kutafakari. Naomba kuufananisha ugumu wa watawala wetu kuelewa na uhusiano wa baba na binti:

Siku zote baba mwenye binti mpole na mtulivu huwa haamini kuwa binti huyo amekuwa hata pamoja na kuwa anajua amevunja ungo. Nimeshuhudia wababa hao wakishtuka wanapoambiwa binti yake anataka kuolewa. Huwa wanakuwa wagumu sana.

Mfano huu unaweza usiwe linganifu sana hata hivyo unawasilisha ujumbe ninaotaka kusema.

Watz siku zote wamekuwa watulivu sana wakiimba wimbo wa zidumu fikra za baba. Watawala wetu wanashangaa ni nini kimetokea hata watz (mabinti watulivu na wapole) wanaleta uasi huu? Ni lini baba amekosa fikra? Hivyo ndivyo watawala wetu wanachoshangaa.
Watawala wetu wanapaswa kujua kuwa hiyo pekee ni sababu tosha ya kuandika katiba mpya: Kwamba Watz wa miaka ya 70, 80, na 80 sio hao wa sasa. Mambo yamebadilika sana na ndio maana inahitajika katiba mpya.
 
Wanabodi,

Leo ndio mara yangu ya kwanza kumuona Waziri wetu wa Sheria, Mhe. Selina Kombani akihojiwa live kwenye kipindi cha Jambo, kinachorushwa na TBC-1 asubuhi hii.

Alipokuwa akitetea mamlaka kubwa za rais kwenye utungaji wa katiba, Mhe. Kombani amesema, Tangu kutungwa kwa katiba ya Tanzania ya Mwaka 1977, Tanzania tumekuwa na katiba nyingine5 ambazo zote process ndio hiyo hiyo kwa rais kuwa na mamlaka kubwa hivyo na zote zimesainiwa na rais, kitu ambacho sio kweli.

Mhe. Kombani wakati akizungunzia katiba hizo tano, alimaanisha marekebisho ya matano ya katiba, yaliyofanywa kwenye katiba ya Tanzania ya Mwaka 1977, na sio katiba tano kama alivyoeleza Mhe. Waziri.

Usahihi ni kuwa Ile katiba ya Tanzania ya Mwaka 1977, ndio hiyo katiba katiba iliyopo mpaka sasa, licha ya kufanyiwa marekebisho mara 5, marekebisho hayo hayabadilishi katiba na kuwa na katiba tano, katiba inabaki ni ile ile moja ya Mwaka 1977!.

Mhe. Kombani, hakuishia hapo, katika utetezi wake kwa mamlaka ya rais pale aliposema, katiba hizo zote 5, zimesainiwa na rais, kitu ambacho pia sio kweli. Katiba ya Tanzania ya Mwaka 1977, ilitokana na Bunge la Katiba 'Constituent Assembly' (Japo ni Bunge lile lile la chama kimoja lilijigeuza), ambalo ndilo liliipitisha katiba. Katiba ikishapitishwa na Bunge la Katiba, haisainiwi na rais, rais mwenyewe, anapata mamlaka toka kwenye katiba hiyo, ila kinachosainiwa na rais, ni yale marekebisho ya katiba.

Hivyo mpaka ninapoandika hapa, Waziri wetu wa Sheria, anaamini yuko right kabisa kutoa mamlaka kubwa zile kwa rais katika marekebisho ya katiba, kwa vile anaamini kinachofanyika sasa, ni marekebisho mengine ya katiba ile ile ya Tanzania ya Mwaka 1977 na sio process ya Uuundwaji wa katiba mpya.

Waziri wa Sheria, anajua kuwa ni rais ndiye ameisaini Katiba ya Tanzania ya Mwaka 1977, kitu ambacho sio kweli.

Japo sio kosa kubwa kwa mtu wa kawaida kuyaita marekebisho ya katiba kuwa ni katiba nyingine, lakini kwa Waziri wa Sheria, Live kwenye TV ya Taifa, kusema Tumekuwa na katiba 5 baada ya Katiba ya Tanzania ya Mwaka 1977, ni uthibitisho kuwa tunaye Waziri wa Sheria Asiyejua Katiba.

Wasalaam.

Pasco.

NB.(Somo la Katiba, ndio somo la kwanza kwa mwanafunzi wa mwaka wa kwanza wa sheria, anapufundishwa 'What is Law?').

samehe baba samehe. ndiyo mawaziri wachapakazi na waadilifu tulioahidiwa na m*k*w*e*r*e

huyu mama si ndiyo yule alisema serikali haina pesa?
 
Back
Top Bottom