Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 269,606
- 696,720
Kila jambo huwa na asili... Yaani chanzo.. Hata mtu asili yake ni manii.
Kosa moja kubwa kabisa tulilolifanya hapo nyuma wakati wa Benjamin Mkapa ni kuipa taaluma kisogo na kuipa SIASA thamani kubwa kuliko uhalisia wake
Jambo hilo halikuwahi kurekebishwa na yeyote yule bali ndio kwanza lilizidi kupaliliwa na kuwekewa mbolea.... Matokeo yake ni haya sasa.
Tuko kwenye kilele cha Kuisigina taaluma, kuihujumu na kuifanya si lolote si chochote mbele ya mwanasiasa aliyefeli masomo yote darasani mpaka lile la lugha yake mwenyewe
Minofu na vinono vya SIASA kipandio chake ni cheo cha ubunge. Nafasi ya kuchaguliwa na wananchi yenye uhakika wa kula mema ya nchi kwa kipindi cha miaka mitano bila shida kabisa
Pale unapofanikiwa tu kuipata nafasi hii adhimu ya utumishi uliotukuka basi hapo hapo jina lako linabadilika na kuitwa MHESHIMIWA. Hapa utajihakikishia kibunda cha million kumi tasilimu kila mwezi kwa kazi unayofanya kwa starehe mno. Na baada ya miaka mitano unaondoka na kiinua mgongo cha milioni mia mbili.
Hapo ni ukiwa na kipandio cha ubunge tuu.. Ulibahatika kuukwaa uwaziri ama unaibu wake.. Pepo yako ni hapa hapa duniani
Huko kwenye ubunge kuna fursa na marupurupu ya kila aina tofauti kabisa na kwenye utumishi mwingine wenye suluba na changamoto za kila aina..
Leo hii ubunge sio utumishi wa wananchi tena.. Leo hii ubunge sio kazi ya mkulima na mfanyakazi wa kawaida
Leo hii ubunge ni nafasi ghali, ngumu kupata na ya watu wenye maisha yao... Yaani mambo safi... Kama
Wakurugenzi mbalimbali
Wakuu wa mikoa
Wakuu wa wilaya
Wafanyabiashara wakubwa
Wasanii wakubwa
Watu maarufu nknk
Yaani kupata Ubungo sasa hivi ni lazima uwe fulani kwenye jamii la sivyo utabaki kuwa mpenzi msindikizaji tuu
Wimbi la wakuu wa mikoa na wilaya pamoja na wakurugenzi kukimbilia ubunge ni kwamba hawana uhakika na kesho yao kwenye nafasi zao.. Lolote muda wowote linaweza kutokea kama aliyekuteua akichafukwa... Ila wanajua kwa hakika kwenye ubunge ni mkataba.. Tena wa miaka mitano
Inashangaza mno kuwa hata wasanii mbalimbali wanaacha kukuza vipaji na vipawa vyao wanakimbilia kuwa wabunge.. Wanashindwa kabisa kujua kuwa ndani ya miaka mitano wakitumikia vema vipaji vyao wanaweza kumake kuliko hata hao wabunge
Nao wamekumbwa na ubinafsi ule wa wengine wasioridhika na walichonacho... Hivi mtu kama Kimei anataka ubunge wa nini? Kwanini asiwaachie damu changa ioneshe uwezo wao? Mzee Wasira bado anataka ubunge... Dah.
Hakika tuna ombwe kubwa la uongozi.. Sasa hivi hata wanataaluma wanaachana na taaluma zao na kukimbilia ubunge
Je tutafika?
Kosa moja kubwa kabisa tulilolifanya hapo nyuma wakati wa Benjamin Mkapa ni kuipa taaluma kisogo na kuipa SIASA thamani kubwa kuliko uhalisia wake
Jambo hilo halikuwahi kurekebishwa na yeyote yule bali ndio kwanza lilizidi kupaliliwa na kuwekewa mbolea.... Matokeo yake ni haya sasa.
Tuko kwenye kilele cha Kuisigina taaluma, kuihujumu na kuifanya si lolote si chochote mbele ya mwanasiasa aliyefeli masomo yote darasani mpaka lile la lugha yake mwenyewe
Minofu na vinono vya SIASA kipandio chake ni cheo cha ubunge. Nafasi ya kuchaguliwa na wananchi yenye uhakika wa kula mema ya nchi kwa kipindi cha miaka mitano bila shida kabisa
Pale unapofanikiwa tu kuipata nafasi hii adhimu ya utumishi uliotukuka basi hapo hapo jina lako linabadilika na kuitwa MHESHIMIWA. Hapa utajihakikishia kibunda cha million kumi tasilimu kila mwezi kwa kazi unayofanya kwa starehe mno. Na baada ya miaka mitano unaondoka na kiinua mgongo cha milioni mia mbili.
Hapo ni ukiwa na kipandio cha ubunge tuu.. Ulibahatika kuukwaa uwaziri ama unaibu wake.. Pepo yako ni hapa hapa duniani
Huko kwenye ubunge kuna fursa na marupurupu ya kila aina tofauti kabisa na kwenye utumishi mwingine wenye suluba na changamoto za kila aina..
Leo hii ubunge sio utumishi wa wananchi tena.. Leo hii ubunge sio kazi ya mkulima na mfanyakazi wa kawaida
Leo hii ubunge ni nafasi ghali, ngumu kupata na ya watu wenye maisha yao... Yaani mambo safi... Kama
Wakurugenzi mbalimbali
Wakuu wa mikoa
Wakuu wa wilaya
Wafanyabiashara wakubwa
Wasanii wakubwa
Watu maarufu nknk
Yaani kupata Ubungo sasa hivi ni lazima uwe fulani kwenye jamii la sivyo utabaki kuwa mpenzi msindikizaji tuu
Wimbi la wakuu wa mikoa na wilaya pamoja na wakurugenzi kukimbilia ubunge ni kwamba hawana uhakika na kesho yao kwenye nafasi zao.. Lolote muda wowote linaweza kutokea kama aliyekuteua akichafukwa... Ila wanajua kwa hakika kwenye ubunge ni mkataba.. Tena wa miaka mitano
Inashangaza mno kuwa hata wasanii mbalimbali wanaacha kukuza vipaji na vipawa vyao wanakimbilia kuwa wabunge.. Wanashindwa kabisa kujua kuwa ndani ya miaka mitano wakitumikia vema vipaji vyao wanaweza kumake kuliko hata hao wabunge
Nao wamekumbwa na ubinafsi ule wa wengine wasioridhika na walichonacho... Hivi mtu kama Kimei anataka ubunge wa nini? Kwanini asiwaachie damu changa ioneshe uwezo wao? Mzee Wasira bado anataka ubunge... Dah.
Hakika tuna ombwe kubwa la uongozi.. Sasa hivi hata wanataaluma wanaachana na taaluma zao na kukimbilia ubunge
Je tutafika?