Nicholaus Kilunga
JF-Expert Member
- Feb 15, 2014
- 1,188
- 567
OMBI
Ili kunogesha na kutia nguvu zaidi katika mapambano na vita dhidi ya rushwa kubwa na ndogo,ufisadi na uhujumu uchumi,vita ambayo ameonekana mh rais Magufuli anaipigana na ili aweze kuishinda inabidi mh rais awe na maaskari hodari na wenye weredi wa kupambana katika vita hii ngumu na ya muda mrefu,namshauri mambo makubwa yafuatayo
1:Mosi aache kuwaona wapinzani kama maadui zake na maadui wa nchi,ama kuwaona si wazalendo kwa kuamini kila anaemkosoa ni sehemu ya wezi.
2:Asione aibu kuwaita na kukaa nao meza moja na kupokea hoja zao za msingi,kwa maana meza humaliza jambo gumu,kama ameweza kukubali kukaa meza moja na watu tunaowatuhumu kutuibia madini miaka dahali nafikiri hili halitamshinda kama anadhamira ya kweli.
3:Akubali na kuruhusu mijadala ya kumkosoa yeye kama rais,akubali serikali yake ikosolewe na chama chake pia,kuanzia ndani ya bunge,nje ya bunge na kwenye vyombo vya habari na mitandao ya kijamii,ili mradi ukosoaji uwe wa staha,lugha isiyouzi na ukweli na heshima.
4:Kuanzia sasa awe anatoa hotuba za kuliunganisha taifa zaidi,na aepuke kuongea ama kusema jambo lolote litakalotafsiriwa kama kutugawa watanzania,mfano kusema kushirikiana na wapinzani nk,aunganishe taifa zaidi ili aweze kuungwa mkono na watu wote wenye itikadi na mitazamo tofauti ili kuijenga nchi kizalendo.
5:Mwisho ila sio kwa umuhimu,nimwombe sasa mh rais amteue David Kafulila kuwa mbunge katika bunge la jamhuri TZ,kama hilo linawezekana,kwani nafahamu bado anazo nafasi 2,huyu ni kiungo muhimu sana katika vita hii,kama ingekuwa jeshini mstari wa mbele kule vitani tungemwita runer(wale askari maalumu wanaotumwaga kusafisha eneo na kumchokoza adui ili ajulikane yupo wapi na jeshi zima baadae limshambulie)kwa kauli ya David Kafulila mwenyewe rais Magufuli wakati huo alikuwa ni miongoni mwa mawaziri 5 waliomtia moyo Kafulila ili aendelee kupambana kwa kumwambia escrow ni dili na akomae mpaka mwisho,
mh rais uwezo wa Kafulila katika kujenga hoja unaufahamu,uzalendo wake sio wa kutilia shaka,maana asingekuwa mzalendo haswaa sakata la escrow lisingemwacha salama,maana walijaribu mara kazaa kumuhonga na waliposhindwa walimtishia maisha,hivyo mh watanzania tunamuhitaji zaidi mh Kafulila bungeni ili aende kuliamsha dude,na unafahamu ni kwa namna gani Kafulila alifanyiwa figisu ili asirudi bungeni,na hata alipojaribu kwenda mahakamani,wote tunajua yaliyotokea,na watuhumiwa wa escrow walikuwa nyuma kuhakikisha harudi bungeni kama kumkomoa kwa lugha yao wao walisema walipokea maagizo ya "kumfix"
Ili kunogesha na kutia nguvu zaidi katika mapambano na vita dhidi ya rushwa kubwa na ndogo,ufisadi na uhujumu uchumi,vita ambayo ameonekana mh rais Magufuli anaipigana na ili aweze kuishinda inabidi mh rais awe na maaskari hodari na wenye weredi wa kupambana katika vita hii ngumu na ya muda mrefu,namshauri mambo makubwa yafuatayo
1:Mosi aache kuwaona wapinzani kama maadui zake na maadui wa nchi,ama kuwaona si wazalendo kwa kuamini kila anaemkosoa ni sehemu ya wezi.
2:Asione aibu kuwaita na kukaa nao meza moja na kupokea hoja zao za msingi,kwa maana meza humaliza jambo gumu,kama ameweza kukubali kukaa meza moja na watu tunaowatuhumu kutuibia madini miaka dahali nafikiri hili halitamshinda kama anadhamira ya kweli.
3:Akubali na kuruhusu mijadala ya kumkosoa yeye kama rais,akubali serikali yake ikosolewe na chama chake pia,kuanzia ndani ya bunge,nje ya bunge na kwenye vyombo vya habari na mitandao ya kijamii,ili mradi ukosoaji uwe wa staha,lugha isiyouzi na ukweli na heshima.
4:Kuanzia sasa awe anatoa hotuba za kuliunganisha taifa zaidi,na aepuke kuongea ama kusema jambo lolote litakalotafsiriwa kama kutugawa watanzania,mfano kusema kushirikiana na wapinzani nk,aunganishe taifa zaidi ili aweze kuungwa mkono na watu wote wenye itikadi na mitazamo tofauti ili kuijenga nchi kizalendo.
5:Mwisho ila sio kwa umuhimu,nimwombe sasa mh rais amteue David Kafulila kuwa mbunge katika bunge la jamhuri TZ,kama hilo linawezekana,kwani nafahamu bado anazo nafasi 2,huyu ni kiungo muhimu sana katika vita hii,kama ingekuwa jeshini mstari wa mbele kule vitani tungemwita runer(wale askari maalumu wanaotumwaga kusafisha eneo na kumchokoza adui ili ajulikane yupo wapi na jeshi zima baadae limshambulie)kwa kauli ya David Kafulila mwenyewe rais Magufuli wakati huo alikuwa ni miongoni mwa mawaziri 5 waliomtia moyo Kafulila ili aendelee kupambana kwa kumwambia escrow ni dili na akomae mpaka mwisho,
mh rais uwezo wa Kafulila katika kujenga hoja unaufahamu,uzalendo wake sio wa kutilia shaka,maana asingekuwa mzalendo haswaa sakata la escrow lisingemwacha salama,maana walijaribu mara kazaa kumuhonga na waliposhindwa walimtishia maisha,hivyo mh watanzania tunamuhitaji zaidi mh Kafulila bungeni ili aende kuliamsha dude,na unafahamu ni kwa namna gani Kafulila alifanyiwa figisu ili asirudi bungeni,na hata alipojaribu kwenda mahakamani,wote tunajua yaliyotokea,na watuhumiwa wa escrow walikuwa nyuma kuhakikisha harudi bungeni kama kumkomoa kwa lugha yao wao walisema walipokea maagizo ya "kumfix"