Ombi na Wito: Mwenye Ushahidi wa kuonyesha ya kuwa Dunia inazunguka atuwekee

Kisai

JF-Expert Member
Apr 6, 2018
27,878
27,987
Nimekaa nakuwaza na kuwazua, nikasema hivi, "Huwa tunaambiwa ya kuwa dunia inazunguka", lakini hatupewi ushahidi juu ya hilo, leo nikaona nije humu JF, huenda wadau wanao ushahidi juu ya hili.

Sambamba na hilo, nawanukulia maneno juu ya haya yasemwayo kuhusu kuzunguka kwa dunia.

Nanukuu :
Lincoln Barnett (1909-1979CE) wrote in his book: “The Universe and Dr. Einstein” (with a forward by Einstein himself), “... for we cannot feel our motion through space; nor has any physical experiment ever proved that the earth actually is in motion.”

Stephen Hawking wrote: “Although it is not uncommon for people to say that Copernicus proved Ptolemy wrong, that is not true... one can use either picture as a model of the universe, for our observations of the heavens can be explained by assuming either the earth or the sun to be at rest.”

Mwisho wa kunukuu.

Ahsanteni.
 
Mkuu unataka ushahidi gani? Kama ni calculations zipo nyingii unaweza kutafuta mwenyewe.. kama ni kwa kuona ndio unaona usiku na mchana.

Kama ni video hizo tafuta mwenyewe.
 
Kama huamini nenda mwenyewe angani kwenye earth's atmosphere ujifanye satellite ujipachike kwenye orbit uone kama unasonga au umesizi ukipata majibu uyalete JF
 
Ushahidi wa namna gani unaouhitaji?wa video ama picha?

Kishule shule ilikuwa tunaambiwa uwepo wa usiku na mchana ni matokeo ya dunia kuzunguka
Wowote tu ambao utakuwa wepesi kwako, na ukiulizwa maswali kutokana na ushahidi huo ujibu maswali hayo vizuri.
 
Mkuu unataka ushahidi gani? Kama ni calculations zipo nyingii unaweza kutafuta mwenyewe.. kama ni kwa kuona ndio unaona usiku na mchana.

Kama ni video hizo tafuta mwenyewe.
Calculations ni Uhalisia au sio uhalisia ? Unaweje kutumia Calculations kuthibitisha uhalisia wa dunia kuzunguka ? Usiniambie niangalie Calculatuons, sababu msingi wa Calculations unajulikana. Kama ushahidi huna sema huna.

Ahsante.
 
Calculations ni Uhalisia au sio uhalisia ? Unaweje kutumia Calculations kuthibitisha uhalisia wa dunia kuzunguka ? Usiniambie niangalie Calculatuons, sababu msingi wa Calculations unajulikana. Kama ushahidi huna sema huna.

Ahsante.
Calculations ni uhalisia!!.
Au unataka ushahidi gani?? Wa video? Au?
 
Calculations ni uhalisia!!.
Au unataka ushahidi gani?? Wa video? Au?
Weka Calculations inayo onyesha Dunia inazunguka, ukiona ndani ina "Assumptions" ujue hakuna uhalisia hapo.

Nakupa mfano wa uhalisia,yawezekana Uhalisi huujui, wewe kuzaliwa na kuwepo kwako huo ni Uhalisia.

Tuendelee .....
 
Una uhakika hujapewa ushaidi?.....ungesema haujaridhika na ushahidi ulipo
Sijapewa ushahidi, na ndio maana katika kupekua pekua kwangu, nikakutana na hizo kauli nilizo nukuu za wasomi manguli wa Sayansi, zikawa zimetilia nguvu kile nilichokiona ya kuwa hakuna ushahidi wa Kisayansi unaonyesha ya kuwa Dunia inazunguka, sasa kama wewe huo ushahidi unao tuwekee.
 
usiku na mchana :

Huu ni ushahidi namba moja unaoonesha kuwa dunia inazunguka, inazunguka yenyewe kwenye mhimili wake (rotation)

Majira ya mwaka:
Huu ni ushahidi namba mbili kuonesha kuwa dunia inazunguka, hapa inayozunguka jua (revolution), mzunguko mmoja ndio mwaka unakuwa umeisha inachukua siku 365 na nusu au 366,kutegemea na urefu wa mwaka (mwezi Februari)

Hivo ndivyo viashiria vikuu vinavyoonesha kuwa dunia inazunguka, japo kuna vingine vingi tu

uliza swali lingine

Ngonja nimalizie k-vant hapa
 
Sijapewa ushahidi, na ndio maana katika kupekua pekua kwangu, nikakutana na hizo kauli nilizo nukuu za wasomi manguli wa Sayansi, zikawa zimetilia nguvu kile nilichokiona ya kuwa hakuna ushahidi wa Kisayansi unaonyesha ya kuwa Dunia inazunguka, sasa kama wewe huo ushahidi unao tuwekee.
Nenda google chap au Youtube au tafuta Astronomy books.....ukikosa ushahidi huko kote usije kutegemea kuamini ushahidi utakao pata hapa JF
 
Wenzako wanafanya utafiti wa anga za mbali wewe usiyeweza kuruka hata mita 2 juu unatilia shaka sasa unataka watu hapa wakupe ushahidi gani natabiri utafungua thread inayosema watu wakupe ushahidi kama utakufa.Kama huamini vitu vilivyokuwa establish baada ya scientific research basi wewe uje utafiti wako
Naona umeshindwa kujibi hoja, unalalama tu.

Sasa wewe ulie ona hizo tafiti tuwekee ushahidi badala ya hizi porojo, hili jambo rahisi sana.

Siwezi kutaka ushahidi wa mimi kufa wala haitotokea sababu najua lazima nitakufa tu na huu ndio uhalisia, sasa ulitakiwa ujibu hoja yangu sio kuandika ujinga.

Ahsante.
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom