Mwafrika wa Kike
JF-Expert Member
- Jul 5, 2007
- 5,185
- 56
Mheshimiwa Jakaya Kikwete,
Hongera sana kwa kuteuliwa kuwa kiongozi wa muungano wa Afrika kwa kipindi kijacho. Hongera pia kwa kufanikisha upatikanaji wa amani kwa majirani zetu Kenya. Hongera pia kwa kumualika raisi wa Marekani George Bush kutembelea Tanzania. Hongera pia kwa net za mbu ambazo Bush ametoa kwa watanzania. Hongera pia kwa kumtoa Mramba kwenye Baraza lako la mawaziri.
Pamoja na hongera na sifa zote hizi, pamoja na email zangu zote zilizopita ambazo nimekuwa nakuandikia (ingawa nimekuwa sipati majibu toka kwako au kwa wasaidizi wako), nimeamua kukuandikia hii email nyingine ambayo pia nitaiweka kwenye mtandao mtukufu wa JF (kama ushahidi) kama ombi maalumu kwako kushughulikia hili suala la bei ya umeme.
Mheshimiwa Kikwete, inawezekana kuwa huna taarifa ya hili ila ni kweli kuwa bei ya umeme imekuwa juu sana kiasi kwamba hali ya maisha ya watu inazidi kuharibika na kuelekea kwenye matatizo makubwa kifedha. Bei ya umeme kwa wastani kwa wengi wa wakazi wa Dar es salaam ni zaidi ya asilimia 50 ya kipato chao cha mwezi. Hii ni hatari sana hasa inapowafikisha wananchi kwenye mjadala wa kuamua kama wanunue chakula au walipie gharama za umeme.
Baadhi ya washauri wako wa uchumi wamesingizia sera za soko huria kama kigezo cha kutoingilia kati suala la umeme, na bei ya mafuta, sementi, usafiri nk. Naomba nikuhakikishie (kama kweli hukujua hili) kuwa hata hapa Marekani, rafiki yako Joji imebidi aingilie kati suala la mortgages baada ya kuona kuwa uchumi wa nchi unaporomoka na mabenki yanafilisika. Kuna wakati ambao inabidi serikali iingilie kati biashara binafsi ili kunusuru maisha ya wananchi wake wa kawaida.
Safari yangu niliyofanya Tanzania mwezi december, niligundua kuwa hata dawa ya mswaki ni ghali Tanzania ambako bei ya kufanya kazi ni rahisi kuliko marekani (dola 6 vs dola 2). Sitakuuliza kuwa uingilie kati ili kushusha bei ya dawa ya mswaki au dawa ya sementi, mafuta, usafiri nk. Lakini mheshimiwa Raisi, kwa vile bado uzalishaji na usambazaji wa umeme uko chini ya serikali, ni vizuri ukaingilia kati na kuwaokoa wananchi wako na hii dhahama.
Bado sijui kwa nini serikali inayalipa makampuni ya IPTL, Kiwira, Richmond na Dowans, Songas, nk mapesa yote haya kuzalisha umeme na bado unakuwa ghali hivi (kuna taarifa kuwa haya yote yanalipwa wakati hayazalishi chochote). Naomba pia nikukumbushe kuwa rafiki ya Joji na serikali yake wanakatisha mikataba ya makampuni mbalimbali na serikali (mfano boeing na contract yake ya kutengeneza ndege za kijeshi nk) kila mara inapogundulika matatizo katika mikataba na utekelezaji wake.
Chondechonde Kikwete, najua kuna mengi huwezi kufanya lakini hili la umeme ni muhimu sana kwa maslahi ya watanzania wengi.
Asante sana!
Hongera sana kwa kuteuliwa kuwa kiongozi wa muungano wa Afrika kwa kipindi kijacho. Hongera pia kwa kufanikisha upatikanaji wa amani kwa majirani zetu Kenya. Hongera pia kwa kumualika raisi wa Marekani George Bush kutembelea Tanzania. Hongera pia kwa net za mbu ambazo Bush ametoa kwa watanzania. Hongera pia kwa kumtoa Mramba kwenye Baraza lako la mawaziri.
Pamoja na hongera na sifa zote hizi, pamoja na email zangu zote zilizopita ambazo nimekuwa nakuandikia (ingawa nimekuwa sipati majibu toka kwako au kwa wasaidizi wako), nimeamua kukuandikia hii email nyingine ambayo pia nitaiweka kwenye mtandao mtukufu wa JF (kama ushahidi) kama ombi maalumu kwako kushughulikia hili suala la bei ya umeme.
Mheshimiwa Kikwete, inawezekana kuwa huna taarifa ya hili ila ni kweli kuwa bei ya umeme imekuwa juu sana kiasi kwamba hali ya maisha ya watu inazidi kuharibika na kuelekea kwenye matatizo makubwa kifedha. Bei ya umeme kwa wastani kwa wengi wa wakazi wa Dar es salaam ni zaidi ya asilimia 50 ya kipato chao cha mwezi. Hii ni hatari sana hasa inapowafikisha wananchi kwenye mjadala wa kuamua kama wanunue chakula au walipie gharama za umeme.
Baadhi ya washauri wako wa uchumi wamesingizia sera za soko huria kama kigezo cha kutoingilia kati suala la umeme, na bei ya mafuta, sementi, usafiri nk. Naomba nikuhakikishie (kama kweli hukujua hili) kuwa hata hapa Marekani, rafiki yako Joji imebidi aingilie kati suala la mortgages baada ya kuona kuwa uchumi wa nchi unaporomoka na mabenki yanafilisika. Kuna wakati ambao inabidi serikali iingilie kati biashara binafsi ili kunusuru maisha ya wananchi wake wa kawaida.
Safari yangu niliyofanya Tanzania mwezi december, niligundua kuwa hata dawa ya mswaki ni ghali Tanzania ambako bei ya kufanya kazi ni rahisi kuliko marekani (dola 6 vs dola 2). Sitakuuliza kuwa uingilie kati ili kushusha bei ya dawa ya mswaki au dawa ya sementi, mafuta, usafiri nk. Lakini mheshimiwa Raisi, kwa vile bado uzalishaji na usambazaji wa umeme uko chini ya serikali, ni vizuri ukaingilia kati na kuwaokoa wananchi wako na hii dhahama.
Bado sijui kwa nini serikali inayalipa makampuni ya IPTL, Kiwira, Richmond na Dowans, Songas, nk mapesa yote haya kuzalisha umeme na bado unakuwa ghali hivi (kuna taarifa kuwa haya yote yanalipwa wakati hayazalishi chochote). Naomba pia nikukumbushe kuwa rafiki ya Joji na serikali yake wanakatisha mikataba ya makampuni mbalimbali na serikali (mfano boeing na contract yake ya kutengeneza ndege za kijeshi nk) kila mara inapogundulika matatizo katika mikataba na utekelezaji wake.
Chondechonde Kikwete, najua kuna mengi huwezi kufanya lakini hili la umeme ni muhimu sana kwa maslahi ya watanzania wengi.
Asante sana!