mapambanodaima
Senior Member
- Oct 22, 2012
- 108
- 15
Nimepata taarifa ambazo sina uhakika nazo kuwa Dr. Slaa na timu yake watakuwa na mkutano katika kijiji cha Kyengege katika tarafa ya Kinampanda wilaya ya Iramba. kama ndivyo naomba sana ziara hii isipite bila kupitia eneo la Kinampanda ambapo kuna wafuasi wengi wanahitaji kupata matumaini mapya kwa chama chao pendwa CDM. hili ni ombi langu kwakuwa nami ni mwanachama hai na pia kwa eneo la Kyengege kuna distance kidogo ambayo itawafanya wanaopenda kumsikiliza Dr. washindwe kuhudhuria. Pia niuombe uongozi wa Wilaya wa Chadema Iramba wajitahidi kupanga ziara eneo la kinampanda ambalo lina wasomi wengi na ambao wanaweza kuwa kitovu cha mabadiliko.Niwatakie maandalizi mema tutakuwa pamoja katika kuimarisha chama.