Ombi Maalum na Wito kwa Wataalamu Wetu Tanzania

JF Member

JF-Expert Member
Dec 14, 2014
7,385
9,651
Kwanza nitangulize pongezi zangu kwa wataalam wetu. Hapa namaanisha Walimu, Madaktari, Wanasheria, Wahasibu n.k
Kumekuwa na kasumba za uvivu na kutotekeleza majukumu yetu kama inavyotakiwa. Kiukweli naweza nikaona sasa Trump alikuwa sahihi alipo sema Waafrika ni wazembe, wapenda starehe na ngono.
Watu hatutekelezi majukumu yetu na hata tunapo wajibishwa tunaona kama tumeonewa, Ebu jiulize.
Mfano. 1. Wewe ni mwalimu haufundishi vipindi ulivyo pangiwa unataka ufanywe nini, unahitaji serikali ikufanyie nini?
2. Wewe ni Daktari hutibu wagonjwa wala huoneshi moyo wa kuwasaidia, badala yake unakuja kazini kupiga story na siasa. unataka ufanywe nini?
Achia mbali masirahi ya wafanya kazi ambayo yanaweza yasitoshe. Hapa serikali inapaswa pia iangalie.
Ila kama watalam wetu hawatakuwa makini basi tutapoteza mapato na nguvu kazi-watu katika taifa hili na hatimaye taifa litaangamia. Maendeleo huletwa na wataalamu wote hivo tushikamane ili tulisukume grudumu la Tanzania yetu.
Pamoja tutajenga Taifa. Tusisubiri kutumbuliwa. Tujitume.
 
Back
Top Bottom