Ombi Maalum kwa Watanzania mlio nje ya Nchi:Tanzania Inakuhitaji

Mlalahoi

JF-Expert Member
Aug 31, 2006
2,182
883
Kwanza naomba kutamka mapema kuwa haya ni mawazo yangu binafsi. Yanaweza kuwa sio sahihi lakini bado yanabaki kuwa mawazo, na something is better than nothing.Kama ni ya kipuuzi,achana nayo.Kama ni ya muhimu,fanyia kazi tafadhali.

Nimefanya utafiti japo (sio wa kutosha sana) kuhusu nafasi ya raia walio nje ya nchi kuchangia mabadiliko katika nchi yao ya asili. Miongoni mwa tabia zinazoathiri mchango wa raia hao ni ukweli kwamba japo kuwa nje ya nchi, kwa kiasi flani, kunasaidia kuongezeka kwa awareness ya uraia (hasa kutokana na taratibu mbalimbali huko ugenini ambapo from time to time tunajikuta tukijaza forms moja au nyingine zinazotutaka kutaja uraia wetu, hence kutukumbusha tunatoka wapi originally) kikwazo kikubwa ni matarajio ya wale walio karibu nasi (familia, ndugu, jamaa na marafiki) huko nyumbani hasa kwenye suala la misaada. Kwa kifupi, tunajikuta tukikabiliwa na majukumu makubwa (real or imagined) ya kibinafsi (in the sense ya hao walio karibu nasi) kuliko ya umma au jamii nzima.

However,ukaribu huo na walio karibu nasi unaweza pia kuwa manufaa kwa maana ya kwamba msemaji mkuu wa umma ni watawala wetu ambao kama tunavyofahamu wanapenda kutoa takwimu za kupendeza hata pale zinapokinzana na hali halisi.Na hilo ni miongoni mwa matatizo ya “jumuiya” au “umoja”: kuzungumzia ujumla badala ya upekee.Wawakilishi au viongozi wa umoja hulazimika kujumuisha yale yanayowahusu wanaounda jumuiya au kundi husika, na hivyo kuficha (kwa kukusudia au kwa ulazima) yanayomgusa mtu moja mmoja au vikundi vidogo vinavyounda umoja huo.

Ukaribu huo unaweza kutusaidia kufahamu yanayofichika kwenye taarifa zinazohusu “umoja” (kwa maana ya jamii nzima) kwa sababu umoja huo hutokana na wingi au ujumla wa aina hii: mtu mmoja mmoja---kikundi---vikundi---umoja.Kwa lugha nyepesi: mimi/wewe/yeye---familia/marafiki/ndugu/jamaa---ukoo/kijiwe,nk--- kabila,nk---taifa.Ni dhahiri basi ukaribu wetu na hao walio karibu yetu unatuwezesha kabisa kufahamu yanayowasibu kwa ujumla wao.Kinachokosekana,so far, ni networking katika hiyo unit ya kwanza, yaani mimi,wewe,yeye,nk.Laiti ingekuwa hivi: taifa---vikundi---kikundi---mimi,wewe,yeye---SISI (kwa maana ya muungano wa unit ya kwanza) then tunaweza kabisa kupata kitu kama SISI---TAIFA au TAIFA---SISI.

Naamini logic yangu imeeleweka.Hata hivyo, logic hiyo ina-neglect factors flaniflani kwa mfano watu wasio na connection na nyumbani (kwa maamuzi yao binafsi au mazingira waliyomo),wale ambao majukumu au utashi wao hauwaruhusu kuwa na mtazamo tofauti na watawala (yaani wao---taifa,au vice versa),nk.

Sasa tuelekeze macho yetu kwenye unit ya kwanza, yaani mimi, wewe, yeye na hatimaye umoja wetu (sisi, ninyi, wao).Bila kupoteza muda, naomba kuwasilisha ombi kwenu tuanze jitihada za kuleta mabadiliko huko nyumbani.

Natambua vikwazo vilivyo mbele yetu, lakini kila safari ina vikwazo vyake.Kinachohitajika ni determination na resilience.Tukiamini katika mission yetu, then tunaweza kufanikiwa. Safari ya kuelekea kwenye mafanikio inaanza na imani kwamba dhumuni la safari hiyo ni jema, tunajua tunakoelekea na tuna dhamira thabiti ya kufika huko.

Mkakati ninaopendekeza hapa ni huu: anza kuchunguza namna gani unaweza kuwasiliana na “mamlaka husika” hapo ulipo. Kwa vile mie niko UK, mfano wa “mamlaka husika” unaweza kuwa Mbunge, vikundi vya kijamii vinavyohusika na masuala ya ustawi wa jamii (hususan kwa nchi za Afrika, au Tanzania in specific) na hata vyombo vya habari. Kwa wenzetu wa Marekani, nadhani kuna watu kama maseneta, members of the house of representantives, advocacy groups, nk.

Baada ya kubaini ni watu au taasisi gani zinazoweza kusikiliza ajenda yako, then anza mawasiliano nao.Waeleze kwamba tunahitaji msaada wao.Kwamba, serikali zao na taasisi zao nyingine ni miongoni mwa wafadhili “wetu”.Tunawashukuru kwa hilo. Hata hivyo, tunawaomba wafahamu our version of hali halisi ya Tanzania hivi sasa.

Kuongeza uzito (na pengine kuwa-convince kwamba cause yetu inaweza kuwa na manufaa kwao pia) wajulishe kwamba tunafahamu kuwa mingi ya misaada wanayotupatia inatokana na fedha za walipa kodi wao. Kwamba wanajinyima kwa ajili “yetu”.Kwahiyo basi tunategemea wangependa kuona misaada hiyo ikitumika kulingana na matarajio yao.

Ufumbuzi sio wao kushinikiza kusitishwa kwa misaada. Hilo litawaumiza walalahoi wasio na hati huko nyumbani.Cha kuwaomba ni kuwabana watawala wetu.Na hapa ni muhimu kuwa very specific: kutoa mifano hai ya namna gani misaada ya wafadhili na wahisani imekuwa msingi wa kiburi cha watawala wetu (rejea kauli ya Dkt Makongoro Mahanga kwamba laiti wafadhili wangekuwa hawaridhishwi na performance ya serikali, wasingependelea kutupatia misaada).Naamini pia kuwa kuna mifano hai huko vijijini, wilayani, mikoani na taifani kwa ujumla.

Mifano mingine ni namna ufisadi unavyotafuna fedha za umma (ambazo zingeweza kupunguza kiwango cha misaada tunayohitaji kutoka kwa wafadhili), ukiukwaji wa haki za binadamu sambamba na uminywaji wa uhuru wa kujieleza, nk.
Kwa leo, nadhani haya “machache” yanatosha.Mwenye kuamini katika ninachoamini, tunaweza kuwasiliana japo ningependelea zaidi iwapo tungepunguza maneno na badala yake tuelekeze nguvu kwenye vitendo.
 
Last edited:
Kwanza naomba kutamka mapema kuwa haya ni mawazo yangu binafsi. Yanaweza kuwa sio sahihi lakini bado yanabaki kuwa mawazo, na something is better than nothing.Kama ni ya kipuuzi,achana nayo.Kama ni ya muhimu,fanyia kazi tafadhali.

Nimefanya utafiti japo (sio wa kutosha sana) kuhusu nafasi ya raia walio nje ya nchi kuchangia mabadiliko katika nchi yao ya asili. Miongoni mwa tabia zinazoathiri mchango wa raia hao ni ukweli kwamba japo kuwa nje ya nchi, kwa kiasi flani, kunasaidia kuongezeka kwa awareness ya uraia (hasa kutokana na taratibu mbalimbali huko ugenini ambapo from time to time tunajikuta tukijaza forms moja au nyingine zinazotutaka kutaja uraia wetu, hence kutukumbusha tunatoka wapi originally) kikwazo kikubwa ni matarajio ya wale walio karibu nasi (familia, ndugu, jamaa na marafiki) huko nyumbani hasa kwenye suala la misaada. Kwa kifupi, tunajikuta tukikabiliwa na majukumu makubwa (real or imagined) ya kibinafsi (in the sense ya hao walio karibu nasi) kuliko ya umma au jamii nzima.

However,ukaribu huo na walio karibu nasi unaweza pia kuwa manufaa kwa maana ya kwamba msemaji mkuu wa umma ni watawala wetu ambao kama tunavyofahamu wanapenda kutoa takwimu za kupendeza hata pale zinapokinzana na hali halisi.Na hilo ni miongoni mwa matatizo ya “jumuiya” au “umoja”: kuzungumzia ujumla badala ya upekee.Wawakilishi au viongozi wa umoja hulazimika kujumuisha yale yanayowahusu wanaounda jumuiya au kundi husika, na hivyo kuficha (kwa kukusudia au kwa ulazima) yanayomgusa mtu moja mmoja au vikundi vidogo vinavyounda umoja huo.

Ukaribu huo unaweza kutusaidia kufahamu yanayofichika kwenye taarifa zinazohusu “umoja” (kwa maana ya jamii nzima) kwa sababu umoja huo hutokana na wingi au ujumla wa aina hii: mtu mmoja mmoja > kikundi > vikundi > umoja.Kwa lugha nyepesi: mimi/wewe/yeye > familia/marafiki/ndugu/jamaa> ukoo/kijiwe,nk > kabila,nk> taifa.Ni dhahiri basi ukaribu wetu na hao walio karibu yetu unatuwezesha kabisa kufahamu yanayowasibu kwa ujumla wao.Kinachokosekana,so far, ni networking katika hiyo unit ya kwanza, yaani mimi,wewe,yeye,nk.Laiti ingekuwa hivi: taifa > vikundi > kikundi > mimi,wewe,yeye > SISI (kwa maana ya muungano wa unit ya kwanza) then tunaweza kabisa kupata kitu kama SISI > TAIFA au TAIFA > SISI.

Naamini logic yangu imeeleweka.Hata hivyo, logic hiyo ina-neglect factors flaniflani kwa mfano watu wasio na connection na nyumbani (kwa maamuzi yao binafsi au mazingira waliyomo),wale ambao majukumu au utashi wao hauwaruhusu kuwa na mtazamo tofauti na watawala (yaani wao>taifa,au vice versa),nk.

Sasa tuelekeze macho yetu kwenye unit ya kwanza, yaani mimi, wewe, yeye na hatimaye umoja wetu (sisi, ninyi, wao).Bila kupoteza muda, naomba kuwasilisha ombi kwenu tuanze jitihada za kuleta mabadiliko huko nyumbani.

Natambua vikwazo vilivyo mbele yetu, lakini kila safari ina vikwazo vyake.Kinachohitajika ni determination na resilience.Tukiamini katika mission yetu, then tunaweza kufanikiwa. Safari ya kuelekea kwenye mafanikio inaanza na imani kwamba dhumuni la safari hiyo ni jema, tunajua tunakoelekea na tuna dhamira thabiti ya kufika huko.

Mkakati ninaopendekeza hapa ni huu: anza kuchunguza namna gani unaweza kuwasiliana na “mamlaka husika” hapo ulipo. Kwa vile mie niko UK, mfano wa “mamlaka husika” unaweza kuwa Mbunge, vikundi vya kijamii vinavyohusika na masuala ya ustawi wa jamii (hususan kwa nchi za Afrika, au Tanzania in specific) na hata vyombo vya habari. Kwa wenzetu wa Marekani, nadhani kuna watu kama maseneta, members of the house of representantives, advocacy groups, nk.

Baada ya kubaini ni watu au taasisi gani zinazoweza kusikiliza ajenda yako, then anza mawasiliano nao.Waeleze kwamba tunahitaji msaada wao.Kwamba, serikali zao na taasisi zao nyingine ni miongoni mwa wafadhili “wetu”.Tunawashukuru kwa hilo. Hata hivyo, tunawaomba wafahamu our version of hali halisi ya Tanzania hivi sasa.

Kuongeza uzito (na pengine kuwa-convince kwamba cause yetu inaweza kuwa na manufaa kwao pia) wajulishe kwamba tunafahamu kuwa mingi ya misaada wanayotupatia inatokana na fedha za walipa kodi wao. Kwamba wanajinyima kwa ajili “yetu”.Kwahiyo basi tunategemea wangependa kuona misaada hiyo ikitumika kulingana na matarajio yao.

Ufumbuzi sio wao kushinikiza kusitishwa kwa misaada. Hilo litawaumiza walalahoi wasio na hati huko nyumbani.Cha kuwaomba ni kuwabana watawala wetu.Na hapa ni muhimu kuwa very specific: kutoa mifano hai ya namna gani misaada ya wafadhili na wahisani imekuwa msingi wa kiburi cha watawala wetu (rejea kauli ya Dkt Makongoro Mahanga kwamba laiti wafadhili wangekuwa hawaridhishwi na performance ya serikali, wasingependelea kutupatia misaada).Naamini pia kuwa kuna mifano hai huko vijijini, wilayani, mikoani na taifani kwa ujumla.

Mifano mingine ni namna ufisadi unavyotafuna fedha za umma (ambazo zingeweza kupunguza kiwango cha misaada tunayohitaji kutoka kwa wafadhili), ukiukwaji wa haki za binadamu sambamba na uminywaji wa uhuru wa kujieleza, nk.
Kwa leo, nadhani haya “machache” yanatosha.Mwenye kuamini katika ninachoamini, tunaweza kuwasiliana japo ningependelea zaidi iwapo tungepunguza maneno na badala yake tuelekeze nguvu kwenye vitendo.

Mawazo mazuri, watz UK wengi wako busy kufungua matawi ya CCM, wanaridhishwa na ufisadi na uporaji unaoendelea. Awareness uliyoiongelea kwa wengi ni ndoto, wameona utawala wenye kuwajibika katika nchi nyingine bado wanachoweza ni kuvaa magwanda ya kijani na kujitangaza ni wakereketwa. Kama wote tungekuwa na uchungu wa kweli wa nchi hii, hawa watawala wasingekuwa na amani ya kutuibia, na kututukana.
 
Mawazo mazuri, watz UK wengi wako busy kufungua matawi ya CCM, wanaridhishwa na ufisadi na uporaji unaoendelea. Awareness uliyoiongelea kwa wengi ni ndoto, wameona utawala wenye kuwajibika katika nchi nyingine bado wanachoweza ni kuvaa magwanda ya kijani na kujitangaza ni wakereketwa. Kama wote tungekuwa na uchungu wa kweli wa nchi hii, hawa watawala wasingekuwa na amani ya kutuibia, na kututukana.
Nakubaliana nawe Mpiga Filimbi.Ila hata baadhi ya ndoto huweza kuwa reality,hususan zile ambazo tunaziota tukiwa macho.Yaani,kwa mfano kuwa na ndoto ya kutaka kuwa na taaluma flani....inaweza kabisa,penye nia na resource,kuwa reality.
 
Mlalahoi,
Concern yako ni sahihi.....however, umejiuliza kwanini wao wanaendelea kutoa misaada na huku wakijua fika kuwa misaada wanayotoa inafisadiwa!!
 
Mlalahoi,
.....however, umejiuliza kwanini wao wanendelea kutoa misaada na huku wakijua fika kuwa inafisadiwa!!
Japo sina uhakika wa asilimia 100 ila naamini kuna connection kati ya hawa watawala wa nchi wafadhili na hao wetu tunaowapigia kelele.Ni kwa mtazamo huo ndio maana nachojaribu ku-encourage ni advocacy kupitia wawakilishi wa watu ktk nchi wafadhili na sio viongozi wa nchi as such.Unajua,kwa uzoefu wangu mdogo,serikali za nchi wafadhili zinapokea taarifa kutoka kwa nchi masikini na kuziamini on the face value.Wabunge au advocacy group nyingine wanaweza kuzihoji (au hata kuweka shinikizo) zinazoweza kupelekea certain legislations.Ni safari ndefu,na matokeo yake yanaweza yasionekane hivi karibuni....lakini cha muhimu ni kuonekana kwa matokeo hayo.
 
Mawazo mazuri, watz UK wengi wako busy kufungua matawi ya CCM, wanaridhishwa na ufisadi na uporaji unaoendelea. Awareness uliyoiongelea kwa wengi ni ndoto, wameona utawala wenye kuwajibika katika nchi nyingine bado wanachoweza ni kuvaa magwanda ya kijani na kujitangaza ni wakereketwa. Kama wote tungekuwa na uchungu wa kweli wa nchi hii, hawa watawala wasingekuwa na amani ya kutuibia, na kututukana.


Mkuu Mpiga Filimbi,

Una maana hao wanaofungua matawi ya CCM ndio wanakufanya wewe usiweze kufanya anachopendekeza Mlalahoi hapa??

Nina imani una upeo mkubwa zaidi ya kutafuta visingizio rahisi rahisi kama hivi.
 
Malalahoi

Hili ni wazo zuri. Mimi naomba nichangie katika kona tofauti.

Moja: Hawa wafadhili kabla hawajatoa misaada huwa wana vigezo ambavyo Tanzania ni lazima ikamilishe ndipo wapewe misaada. Serikali ya Tanzania inatumia kila mbinu kuhakikisha vigezo hivyo vinakamilishwa au angalau wafadhili "wanaamini" kuwa vigezo vimekamilishwa kwa kadri walivyotaka. Ni njia zipi zitatumika kutengeneza ushahidi kwamba hela kiasi kadhaa kilichotolewa na Serikali ya UK/ Germany etc hakijafanya kile kilichotakiwa kufanyika (on the ground). Upande mmoja utakuwa kwenye vita na serikali ya Tanzania na upande mwingine utakuwa na kazi ya kuthibitisha tuhuma au hofu yako.

Pili: Kwa jinsi ninavyoona mimi; Fedha nyingi za wafadhili hazitolewi kwa ajili ya vitu ambavyo ni substancial kama dawati, hospitali n.k Fedha nyingi zinakwenda kwenye vitu kama kampeni dhidi ya ukwimwi, mafunzo ya utawala bora, elimu ya demokrasia n.k Matumizi kama haya ni vigumu mno kuyngea hoja kuwa fedha zimetumika vibaya au hazikwenda kabisa zilikokusudiwa.

Ni hayo tu kwa leo mkuu otherwise, wazo zuri indeed.
 
Malalahoi

Hili ni wazo zuri. Mimi naomba nichangie katika kona tofauti.

Moja: Hawa wafadhili kabla hawajatoa misaada huwa wana vigezo ambavyo Tanzania ni lazima ikamilishe ndipo wapewe misaada. Serikali ya Tanzania inatumia kila mbinu kuhakikisha vigezo hivyo vinakamilishwa au angalau wafadhili "wanaamini" kuwa vigezo vimekamilishwa kwa kadri walivyotaka. Ni njia zipi zitatumika kutengeneza ushahidi kwamba hela kiasi kadhaa kilichotolewa na Serikali ya UK/ Germany etc hakijafanya kile kilichotakiwa kufanyika (on the ground). Upande mmoja utakuwa kwenye vita na serikali ya Tanzania na upande mwingine utakuwa na kazi ya kuthibitisha tuhuma au hofu yako.

Pili: Kwa jinsi ninavyoona mimi; Fedha nyingi za wafadhili hazitolewi kwa ajili ya vitu ambavyo ni substancial kama dawati, hospitali n.k Fedha nyingi zinakwenda kwenye vitu kama kampeni dhidi ya ukwimwi, mafunzo ya utawala bora, elimu ya demokrasia n.k Matumizi kama haya ni vigumu mno kuyngea hoja kuwa fedha zimetumika vibaya au hazikwenda kabisa zilikokusudiwa.

Ni hayo tu kwa leo mkuu otherwise, wazo zuri indeed.

Naafikiana nawe mkuu.

Ila pasipo kwenda mbali na kutafuta solid eveidence,ripoti ya juzijuzi ya CAG inaweza kuonyesha ni namna ufisadi ulivyo at work nchini.Fedha za wahisani kwenye miradi kama ya ukimwi,utawala bora,nk zina ugumu wake kuzi-trace lakini CAG,as afisa aliyetueliwa na serikali yenyewe (mithili ya internal auditor amebainisha ufisadi mpaka Ikulu,document hiyo inaweza kuwa mahala mwafaka pa kuanzia harakati hizi.

Advantage ya mafisadi serikalini ni kwamba hakuna external mechanism ya ku-prove kuwa taarifa wanazowasilisha kwa wahisani zimefanyiwa usanii.Sasa strategy hii nayo-propose inaweza kutengeneza kitu kama hicho (si kwa lengo la kuwasaidia nchi wahisani as such bali kuwasukuma wafanye kitu flani).
 
Ndugu yangu Mlalahoi,

Kwanza ningependa kujua where are you located... Inaonesha ni kama uko UK vile... Kama ni kweli, ningependa kujua ni lini ilikua mara yako ya mwisho kwenda/kuja nyumbani Tanzania...

Nafikiri una idea nzuri sana.. ILA nasikitika kukueleza kwamba hizo ideas zako hazitekelezeki. Ask yourself why Danganyika yetu mpaka leo ni masikini wa kutupwa. Ask yourself why pamoja na data zote zinazoshindiliwa kwa the so called "viongozi" why hawazi-implement hata kama izo data zimetafunwa na kuwekwa mezani kabisa kama vile
1. KIWIRA - Mkapa,
2. IPTL - Waziri wa energy waliyekuwepo madarakani wakati IPTL wanaingia nchini,
3. LISTI YA WAUZA UNGA - ambayo mwenye nchi alitueleza ameshapatiwa ila mpaka sasa hatujasikia akiizungumzia
4. Maprofesa, mawaziri, madirectors na viongozi wengine wenye vyeti kutoka kwenye the so called "diploma mills" - ambayo huhitaji dakika mbili ku-search info online kustukia kua vyuo walivyosomea ni feki
5. Kashfa za serikali iliyomo madarakani kwa sasa kuhusiana na pesa zilizowaingiza madarakani thru uchaguzi mkuuwa 2005
6. etcetera etcetera...

Hivyo basi, nafikiri ndugu yangu, ingawa ideas zako ni nzuri, mi nakushauri ufikirie mara mbili (think twice) kabla ya ku-implement hizo ideologies ulizozisema maana nina uhakika itakuwa ni "a waste of your precious time" na unaweza ukaja juta baadaye why uliamua kutekeleza ideas nzuri kwa "kadamnasi" isiyo tayari ku-accept good ideas. I guess unafahamu kwamba asilimia kubwa ya viongozi wetu wamekaa mkao wa kula... Usipoteze mda wako mwingi kufikiria mambo mazuri ambayo nina uhakika (ingawa sikukaziti tamaa) kwamba nobody in bongo administration will be sincere to implement them..

Those were my two cents mkuu
 
Ndugu yangu Mlalahoi,

Kwanza ningependa kujua where are you located... Inaonesha ni kama uko UK vile... Kama ni kweli, ningependa kujua ni lini ilikua mara yako ya mwisho kwenda/kuja nyumbani Tanzania...

Nafikiri una idea nzuri sana.. ILA nasikitika kukueleza kwamba hizo ideas zako hazitekelezeki. Ask yourself why Danganyika yetu mpaka leo ni masikini wa kutupwa. Ask yourself why pamoja na data zote zinazoshindiliwa kwa the so called "viongozi" why hawazi-implement hata kama izo data zimetafunwa na kuwekwa mezani kabisa kama vile
1. KIWIRA - Mkapa,
2. IPTL - Waziri wa energy waliyekuwepo madarakani wakati IPTL wanaingia nchini,
3. LISTI YA WAUZA UNGA - ambayo mwenye nchi alitueleza ameshapatiwa ila mpaka sasa hatujasikia akiizungumzia
4. Maprofesa, mawaziri, madirectors na viongozi wengine wenye vyeti kutoka kwenye the so called "diploma mills" - ambayo huhitaji dakika mbili ku-search info online kustukia kua vyuo walivyosomea ni feki
5. Kashfa za serikali iliyomo madarakani kwa sasa kuhusiana na pesa zilizowaingiza madarakani thru uchaguzi mkuuwa 2005
6. etcetera etcetera...

Hivyo basi, nafikiri ndugu yangu, ingawa ideas zako ni nzuri, mi nakushauri ufikirie mara mbili (think twice) kabla ya ku-implement hizo ideologies ulizozisema maana nina uhakika itakuwa ni "a waste of your precious time" na unaweza ukaja juta baadaye why uliamua kutekeleza ideas nzuri kwa "kadamnasi" isiyo tayari ku-accept good ideas. I guess unafahamu kwamba asilimia kubwa ya viongozi wetu wamekaa mkao wa kula... Usipoteze mda wako mwingi kufikiria mambo mazuri ambayo nina uhakika (ingawa sikukaziti tamaa) kwamba nobody in bongo administration will be sincere to implement them..

Those were my two cents mkuu

Asante Mkuu kwa mchango wako,

Pamoja na kuafikiana na ushauri wako lakini najipa matumaini kwamba ili tufike mahala flani inabidi flani na flani wajitoe mhanga.Ni wazi watawala wetu hawapendi kusikia habari kiama hizi kwa vile zinahatarisha ufisadi wao.Ni wazi pia watahangaika kadri wawezavyo kudhibiti harakati za aina hii.

Kama nilivyojaribu kueleza hapo awali,TUKIAMUA INAWEZEKANA.It all starts with MIMI,WEWE na YEYE (au SISI) kisha inasambaa taratibu.
 
mimi wallhi billahi wa tallahi sitarudi Tanzania mpaka chama cha Mafisadi (CCM) kitakapoondoka madarakani niradhi nife hukuhuku niliko loooo
 
Mawazo mazuri, watz UK wengi wako busy kufungua matawi ya CCM, wanaridhishwa na ufisadi na uporaji unaoendelea. Awareness uliyoiongelea kwa wengi ni ndoto, wameona utawala wenye kuwajibika katika nchi nyingine bado wanachoweza ni kuvaa magwanda ya kijani na kujitangaza ni wakereketwa. Kama wote tungekuwa na uchungu wa kweli wa nchi hii, hawa watawala wasingekuwa na amani ya kutuibia, na kututukana.

MpingaFilimbi,

Watanzania wengi walioko UK wako busy wakifanya kazi zao na kujipatia vipato vyao vya halali. Ukifuatilia majina ya watanzania wanaofungua hayo matawi ya CCM, utagundua kuwa ni baadhi tu ya watanzania ndio wako busy kufungua matawi ya ccm UK - Niko tayari kusahihishwa kwenye hili.
 
Naunga hoja ya YEBO YEBO kuwa wafadhili wengi wamekuwa wakitoa misaada kwenye shughuli ambazo wao huita 'capacity building' or soft skills. Na inakuwa vigumu hasa kujua matokeo ya shughuli hizi! Na kwa kiasi kikubwa utaona NGO nyingi tu zinaongezeka kama njugu na zote zina deal na 'capacity building' na huku ndiko ufisadi hupo!
 
mimi wallhi billahi wa tallahi sitarudi Tanzania mpaka chama cha Mafisadi (CCM) kitakapoondoka madarakani niradhi nife hukuhuku niliko loooo

Wenye mawazo kama yako wako wengi sana, na idadi ya Wataalamu wa Kitanzania wanaokwenda nje kila mwaka inazidi kuongezeka kutokana na kutothaminiwa kwao, mishahara duni, ili kufanikiwa inabidi uwe na kimungu mtu au vimungu mtu uvisifiesifie na kuvipa rushwa ili vikupe promotion, vitendea kazi duni n.k. Haya yote yanasababishwa na chama cha mafisadi ambacho kimeweka mbele maslahi ya mafisadi badala ya yale ya nchi..
 
Wenye mawazo kama yako wako wengi sana, na idadi ya Wataalamu wa Kitanzania wanaokwenda nje kila mwaka inazidi kuongezeka kutokana na kutothaminiwa kwao, mishahara duni, ili kufanikiwa inabidi uwe na kimungu mtu au vimungu mtu uvisifiesifie na kuvipa rushwa ili vikupe promotion, vitendea kazi duni n.k. Haya yote yanasababishwa na chama cha mafisadi ambacho kimeweka mbele maslahi ya mafisadi badala ya yale ya nchi..

Son:

Ina maana ungekuwa na kimungu mtu, ungebaki bongo?
 
Son:

Ina maana ungekuwa na kimungu mtu, ungebaki bongo?

Grandson,

NO WAY! Vimungu mtu hutaka kukudhalilisha wakati mwingine usipokuwa mwangalifu. Nchi za watu makaratasi yako tu na jinsi unavyojituma ndio silaha yako huhitaji kimungu mtu wala fisadi akupigie debe. Kama unajali kazi yako na utendaji wako ni superb basi jamaa wanakuthamini na matunda yake utayaona. Siyo bongo, ntimanyongo kibao.
 
Wazo zuri lakini linahitaji kuwa tayari kupambana na utawala dhalimu. Hili linahitaji nguvu kutumika na si longo longo kwani 'watawala' wetu hawaelewi maana ya demokrasia. Kwao demokrasia ni wao kutawala milele hata kama umma hauwaungi mkono. Kuna haja ya kutumia nguvu kuondokana na zahama hii.
 
Wazo zuri lakini linahitaji kuwa tayari kupambana na utawala dhalimu. Hili linahitaji nguvu kutumika na si longo longo kwani 'watawala' wetu hawaelewi maana ya demokrasia. Kwao demokrasia ni wao kutawala milele hata kama umma hauwaungi mkono. Kuna haja ya kutumia nguvu kuondokana na zahama hii.
Agreeing with you,Mukuru.
Cha muhimu ni kuwa je proposal hii inawezekana?I am 100% sure it is (possible).Kuwa nje ya Tanzania kunatoa privilege ya kuepuka "michezo michafu" ya CCM na serikali yake kunyamazisha kila wazo linalotishia kukomesha political capital yake ya ufisadi.

Yes we can!
 
Back
Top Bottom