Mag3
Platinum Member
- May 31, 2008
- 13,064
- 22,757
Bado nakumbuka yaliyotokea kwa jirani zetu Kenya ambako tamko la aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi, Bwana Samuel Kiviutu, lilivyoweza kuigeuza nchi jirani, Kenya, kuwa uwanja wa mapambano na vita. Matokeo ya Uchaguzi Mkuu mwaka 2008 yaliyotangazwa na kumpa ushindi incumbent, Raisi Mwai Kibaki, yalisababisha umwagaji mkubwa wa damu ambao karibu usambaratishe nchi hiyo. Ni juhudi tu za ziada za mataifa na wadau mbali mbali zilizowezesha hali angalau ya amani kurejeshwa tena na kuzuia mauaji zaidi.
Hali kama hii pia tuliishuhudia Tanzania Visiwani ambapo kwa mara ya kwanza kabisa Watanzania walijikuta wakiwa wakimbizi nchi za jirani kama Kenya na kwingineko. Kama ilivyotokea huko Kenya, ni matokeo ya Uchaguzi Mkuu Visiwani yaliyotangazwa na kumpa ushindi incumbent, Salmin Amour, huku ushindi wake ukiwa umegubikwa na mashaka kibao. Tulishuhudia wananchi kadhaa wakiuawa na wana usalama ambao kimsingi walitakiwa kuwalinda lakini Raisi Benjamin Mkapa akaamua vinginevyo.
Mheshimiwa Jaji Lewis Makame, kosa si kosa ila kurudia kosa na ninakuomba usije ukawa Sameli Kiviutu wetu wa Tanzania. Dalili zote zaonyesha kuwa uchaguzi wa mwaka huu utakuwa tofauti kidogo na wananchi wameamua kuwa hawako tayari kuendelea kuwabeba viongozi wasio na uwezo. Nakuomba uweke historia kwa mara ya kwanza kuendesha uchaguzi wa haki kuanzia matayarisho ya awali hadi siku matokeo yanatangazwa. Kama ni kujifunza naamini umejifunza na, for heavens sake, Kofi Anan hatakiwi hapa - tafadhali usiliangushe taifa, ni ombi tu.
Hali kama hii pia tuliishuhudia Tanzania Visiwani ambapo kwa mara ya kwanza kabisa Watanzania walijikuta wakiwa wakimbizi nchi za jirani kama Kenya na kwingineko. Kama ilivyotokea huko Kenya, ni matokeo ya Uchaguzi Mkuu Visiwani yaliyotangazwa na kumpa ushindi incumbent, Salmin Amour, huku ushindi wake ukiwa umegubikwa na mashaka kibao. Tulishuhudia wananchi kadhaa wakiuawa na wana usalama ambao kimsingi walitakiwa kuwalinda lakini Raisi Benjamin Mkapa akaamua vinginevyo.
Mheshimiwa Jaji Lewis Makame, kosa si kosa ila kurudia kosa na ninakuomba usije ukawa Sameli Kiviutu wetu wa Tanzania. Dalili zote zaonyesha kuwa uchaguzi wa mwaka huu utakuwa tofauti kidogo na wananchi wameamua kuwa hawako tayari kuendelea kuwabeba viongozi wasio na uwezo. Nakuomba uweke historia kwa mara ya kwanza kuendesha uchaguzi wa haki kuanzia matayarisho ya awali hadi siku matokeo yanatangazwa. Kama ni kujifunza naamini umejifunza na, for heavens sake, Kofi Anan hatakiwi hapa - tafadhali usiliangushe taifa, ni ombi tu.