OMBI MAALUM: Je unamfahamu Anayedaiwa Kubakwa na Makamba?

Status
Not open for further replies.
[Mie namjua, sasa hivi ni waziri katika serikali ya Kikwete ]

LUTALA: kama unamjua si umtaje kwa jina?hofu yako ni niini?
 
au ndo alibaka akampa mimba huyo mama wa watu ndo maana kwenye kuta kibao hapa dar zimeandikwa kwa maandishi makubwa " Makamba anataka kumuua mama yangu" je ndo chanzo?? ili apoteze ushahidi??
 
kaka hiyo ni ngumu, ukianza hayo itakuwa taabu sana, kwanza miaka mingi imepita na si ajabu anaweza kuwa ameshaolewa, na ana mume hivyo ukianzisha hayo mume anaweza kumuacha, kama wale akina mama wa congo wanaobakwa kisha wanaachwa na waume zao, Hayo si mazuri kuyajadili ukizingatia aliyerusha mawe hagombei nafasi yoyote.

Hatuwezi kufika mbali tuki hendekeza kujadiliana udaku, lets focus october 31,Watu kibao wana kashifa nyingi tu, udaku wa kila mtu hata asiye kiongozi ukiwekwa hadharani tutabaki midomo wazi. na kama huamini au hujijui ulivyo au ulichokwisha wahi kufanya Gombea uongozi ngazi yoyote utajijua.

Hayo tuyaache tuangalia ujenzi wa nchi yetu na tukemee wasio na huruma kutafuna nchi yetu huku raia wengi wakibaki na umasikini wa kutupwa.

Mi Naomba siku zote atakayeingia madarakani, afumbe macho asionee huruma wale wote wanaofanya makosa, ukifanya kosa ukasamehewa ndo kosa huwezi kuwa makini hata siku moja. MI naona rais akiwa serious na watendaji watakuwa serious, upotevu wa rasimali za nchi chanzo chake kinajulikana kudhibiti ni rahisi.

Nampongeza sana tenga rais wa TFF kwa hatua alizomchukulia Kaijage kwa swala la nyimbo zataifa, Taasisi zote zikiwa serious tutafika tunakoenda.

Jamani hamjawahi kusikia habari za CHINA, ukichemka inakula kwako hata ukihisiwa tu, na ndo maana wachina wako makini.

Pia DEpartment ya CHEMISTRY pale UDSM ile ni mfano wa kuigwa, wale jamaa wanaosimamia Practical hasa kule juu kwenye practical za phyisical chemistry nawapenda wako serious kupita maelezo nchi nzima ingetenda kazi kama wale tungefika mbali wanafaa na hawababaishi.

Tusichumie TUMBO na familia zetu, tufikilie na huko mbeleni, Hivi unadhani nchi za ulaya maendeleo yake unadhani yalikuwa ya muda mfupi?
 
hii labda inaweza kukusaidia mtafuta hii habari kwa kuanzia, mtafute kiongozi wa upinzani huko morogoro mjini alipokuwa anafanya
kazi makamba, yeye itakuwa rahisi kupata info kutoka kwa waalimu wa shule za misingi hapo morogoro mjini na hasa ukizingatia kuwa
waalimu wengi wako against CCM kwahiyo inaweza kuwa rahisi kupata hizo info.
 
Makamba ni darasa la saba kwa elimu, kwa hiyo labda apewe onyo kwanza. Akiendelea ndio tumfanyie kazi. Ila kwa sasa mi nadhani kuanzia shule aliyokuwa anafundisha ndio jibu au mwelekeo utapatikana.
 
wakuu mmesahau kitu kimoja; ikumbukwe mabinti waliotumuliwa kwa mujibu wa wakubwa wetu ni 'kwa kujitakia.' sasa huenda huko kubakwa ni katika maana ya kisheria ya u-18 lakini wakati huo huo kumbe alitaka mwenyewe na huenda kwa sasa huyo tunayemtafuta humu ndiye...
 
Nampongeza sana tenga rais wa TFF kwa hatua alizomchukulia Kaijage kwa swala la nyimbo zataifa...................
Kaka unaweza kutafuta details zaidi za kaijage na Tenga kwenye hilo sakata la nyimbo za taifa? Usije ukawa umeingiwa na kale kaugonjwa kanakoitwa magazetizm, ambapo kila habari ya gazeti unaibeba tu bila kufanya uchunguzi. Anyways, niko tayari kukosolewa lakini as far as I know ni kuwa SIASA zimetawala "inshu" nzima ya Kaijage maana hata mkataba ulikuwa umeshaeksipaya by the time ana"haribu" mbele ya MKWERE
 
OMBI MAALUM: Je unamfahamu Anayedaiwa Kubakwa na Makamba?


Wenye busara zao wanatuusia kuwa pindi ukiwa unaishi kwenye nyumba ya vioo then sio wazo jema ku-entertain kurusha mawe.Mantiki ya msemo huo ni kwamba kama una ishu zenye utata katika maisha yako then sio wazo jema kuanza kushupalia ishu za watu wengi lest flani akakugeuzia kibao.


Lakini usemi huo umeonekana hauna maana kwa Katibu Mkuu wa CCM,Yusuph Makamba,ambaye kwa siku kadhaa sasa ameamua "kuvalia njuga maisha binafsi ya Dokta Wilbroad Slaa" na kuligeuza suala la ndoa ya mgombea huyo wa Chadema kuwa ajenda ya uchaguzi.


Pengine ni dharau au ujinga,Makamba alijisahau kuwa wakati anamnyooshea kidole Dkt Slaa,yeye mwenyewe (Makamba) alikuwa na doa linaloweza kabisa kumpeleka jela.Kwa mujibu wa taarifa zilizozagaa mtandaoni,Makamba anatuhumiwa kumbaka mwanafunzi wakati akiwa mwalimu mkuu wa shule moja na hatimaye kufukuzwa ualimu.


Hizi ni tuhuma nzito sana kwani licha ya kumtia doa Makamba kama mwanasiasa,ni suala linaloweza kumpeleka jela endapo victim wake atajitokeza hadharani,na kupatiwa msaada wa kisheria.Lakini tukiweka ishu za kisiasa kando,hapa kuna suala la binti asiye na hatia ambaye inadaiwa alibakwa na mtu aliyekabidhiwa dhamana ya kumpatia elimu na mwongozo katika maisha yake,mwalimu wake,lakini akaishi kubakwa.


Blogu hii inatoa ombi maalum kwa yeyote yule anayeweza kuipatia taarifa za uhakika kuhusu binti huyo anayedaiwa kubakwa na Makamba.Lengo si kumkomoa mtuhumiwa bali kuhakikisha sheria inachukua mkondo wake as well as kutoa reminder kwa watu wengine wanaotumia vibaya dhamana walizokabidhiwa,iwe mashuleni,makazini au hata katika ngazi ya familia.


Je unamfahamu binti anayedaiwa kubakwa na Makamba?Kama jibu ni ndiyo basi tafadhali sana tuwasiliane kwa barua pepe kwa anuani hii epgc2@yahoo.co.uk.

source: KULIKONI UGHAIBUNI

umbeya mtupu BEBENI MABOXI........BLA BLAH NYINGIIIII
 
Ni Kweli kuwa makamba aliwahi kumpa mimba mwanafunzi huko tabora ... yeye na moses mnauye walikuwa wanapenda sana wanafunzi hasa wa primary...
 
umbeya mtupu BEBENI MABOXI........BLA BLAH NYINGIIIII

ha ha ha ha!
Kama kweli vile.
Waliowaua watu arusha kwenye maandamano si wanawajua! Hebu waanze na hao.

Mnavyovijua hamvisolve mna kazi ya kuhaha na vya uvunguni.
 
Status
Not open for further replies.
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom