Habari wana JF,
Binafsi sijawahi kuwa Mwanachama wa CCM na ni ukweli usipingika kwa Hiki Chama kutoka madarakani itakuwa Ngumu sana sana kuliko tunavyofikiri
Sasa hivi kwa hali ilivyo sio rafiki sana kama ilivyo kwa tawala zilizopita za CCM pesa zetu zinapotea sana na raslimali zetu zinapotea. Yaani kikubwa tunachofurahia sasa ni Uhuru wa kijamii huku mambo mengine yakiwa magumu sana
Kibaya zaidi ni kwamba wananchi wa chini ndio tunakamuliwa sana kupitia Kodi, Tozo pamoja na kupanda kwa Ugumu wa Maisha .
Kwa kifupi inaumiza sana kuhimizwa kutoa kodi na Tozo kisha mtu au kikundi cha Watu kujinufaisha pesa zetu .
OMBI LANGU:- Muonee huruma wananchi na Nchi kwa ujumla kwa kukubali kuachia Madaraka au Kwa maslahi mapana ya Taifa mbadilike na kuwa wazalendo mtuletee viongozi waadilifu na wachapakazi sio hawa wasio na mchango kwa Taifa zaidi kutafuta umaarufu wa kisiasa na kujinufaisha Wao .
Ntashukuru kama Ombi langu litachukuliwa kwa Mtazamo Chanya Maana mmetawala kwa Muda mrefu Sana hatuoni matunda yanayoendana na raslimali tulizo nazo .
Binafsi sijawahi kuwa Mwanachama wa CCM na ni ukweli usipingika kwa Hiki Chama kutoka madarakani itakuwa Ngumu sana sana kuliko tunavyofikiri
Sasa hivi kwa hali ilivyo sio rafiki sana kama ilivyo kwa tawala zilizopita za CCM pesa zetu zinapotea sana na raslimali zetu zinapotea. Yaani kikubwa tunachofurahia sasa ni Uhuru wa kijamii huku mambo mengine yakiwa magumu sana
Kibaya zaidi ni kwamba wananchi wa chini ndio tunakamuliwa sana kupitia Kodi, Tozo pamoja na kupanda kwa Ugumu wa Maisha .
Kwa kifupi inaumiza sana kuhimizwa kutoa kodi na Tozo kisha mtu au kikundi cha Watu kujinufaisha pesa zetu .
OMBI LANGU:- Muonee huruma wananchi na Nchi kwa ujumla kwa kukubali kuachia Madaraka au Kwa maslahi mapana ya Taifa mbadilike na kuwa wazalendo mtuletee viongozi waadilifu na wachapakazi sio hawa wasio na mchango kwa Taifa zaidi kutafuta umaarufu wa kisiasa na kujinufaisha Wao .
Ntashukuru kama Ombi langu litachukuliwa kwa Mtazamo Chanya Maana mmetawala kwa Muda mrefu Sana hatuoni matunda yanayoendana na raslimali tulizo nazo .