Ombi la Lema kwa Zitto na kauli ya Werema - Unganisha dots...

Bonge la bandiko mkuu, naamini vijana wote tuliotimamu tumekuelewa na tupo bega kwa bega na ZZK japo naamini bado wapo wengi tu waliolishwa unga wa ndele wasioweza kufikiri nje ya box, wapo vijana wa ndiyo mheshimiwa, ndiyo mzee, wapo vijana waliojaa udini, ukanda na ukabila n.k ambao wana viburi vya asili katika uelewa! lakini usijali tupo wengi tu tunaomwamini ZZK na tupo naye hadi tone la mwisho!
 
haahaaaahvmnamsukumia lawama Lems kwa failures za Zitto.
mwambieni Zitto ataje aache ngonjera

Kutaja majina kutaja majina!!! what is that? unafikiri hio ndio suluhisho la tatizo hilo? Babu Dr. Slaa alitaja majina ya EPA llakini mpaka sasa hakuna jipya! Suluhu hapa ni kuibana serikali pesa zirudi na walio husika wachukuliwe hatua kali za kisheria.

Au mwagopa lile jumba la kifahari la uarabuni la yule Disco Jocker (Dj) litapigwa mnada!
 
umemshambulia zaidi LEMA na kumpamba sana ZITTO , kuna kitu usichokijua , ni kwamba katika dunia hii hatuishi kwa mafumbo ! Kama Zito alikuwa na majina anayahifadhi kwa manufaa ya nani ?
 
Dizaini kuna ubabaishaji hivi siasa yetu bado tu haikomai jmn au viongozi wetu wananyota za wafu???!!. Acheni ulimbukeni watz tunachoka tumezaliwa masikini but hata kufa tufe tukiwa masikini!!!!!!.
 
Mwambie kwanza Mbowe atoe hadharani mkanda wa bomu la Soweto ambao alisema kuwa anao. Hakika Nyani haoni kundule

Angalau mbowe aliweka wazi terms ambazo alitaka zifuatwe ili aweze kuweka huo mkanda hadharani,bahati mbaya vigezo na masharti havikuzingatiwa,japo wengi wetu bado tunasubiri kwa hamu kuujua undani wake,sasa zitto naye angeweka terms&condition halafu zisizingatiwe hapo angeeleweka,ila hii ninayo ninayo without any stipulation is idiocy period.
 
... kila mwenye akili anajua kuwa ZZK anayo majina tena sio majina tu bali pamoja na account details za walioficha fedha uswisi na kwingineko. ila kutokana na nguvu kubwa ya kifisadi iliyo nyuma ya wamiliki hawa wa mabilioni, ZZK hayuko tayari kuwasilisha chochote au kwa mtu yeyote ushahidi alionao kuhusu sakata husika. ushahidi alionao ndio uliobeba FUNGUO YA USALAMA WA MAISHA YAKE NA NAFASI YAKE KISIASA. endapo ataukabidhi, ni wazi utateketezwa na maisha yake yatakuwa hatarini. ...
Mkuu, sasa kama ZZK anaona ni HERI kulinda usalama wa maisha yake na nafasi yake kisiasa KULIKO kurahisisha mchakato wa kuyachunguza mabilioni ya Uswisi kwa kutoa details za walioficha, basi aendelee kukaa kimya na mjadala ufungwe kwa upande wake au aiachie Kamati Maalum ya Bunge iendelee kimya kimya na kazi ya uchunguzi, na sio kuibuka kila baada ya muda fulani na kusema serikali haina nia ya kufuatilia. Unaambiwa taja majina tupate urahisi, hautaki. Basi kaa kimya usubiri tuchunguze wenyewe, hautaki. Leta majina tutaje sisi, hautaki! Sasa ikiitwa ngonjera hapo kuna kosa gani?
 
I am confused for what is happening now!!!!!
but my confussion will never lead me astray and miss my point. I WILL SATAND BY HIM(ZZK) no matter what.
Nilitaka kukuhukumu kwa pumba ulizotandaza,

lakini baada ya kusoma hiyo sentensi imebidi nikusamehe bure najua siyo akili zako.
 
Hivi kwa nini hii list nzito ni ya Zito pekee na isiwe ya chama kama list of shame?????!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
...ndo maana tunapiga chini wasaliti wanaojenga majina badala ya kujenga philosophy ya ukombozi ktk chama,watu hawa wako tayari kufanya lolote hata kuua chama ili kukuza majina yao...!
 
duuuh maelezo marefu pumba tupu.

you can fool some people at one time but you cant fool all the people all the time, at least wahenga walikwishasema hayana mkashindwa kutambua hili, chukua na wewe kama hii tahadhari itakusaidiana wewe maishani mwako.

Eti mnakusabya ushahidi! subiri siku ushahidi ukikamilika ndio ukuje huku na ushahidi wako, tutapima kwa hoja na uzito wake, but for now hii ni empty set mkuu.

Eti tuunganishe doti wakati doti zenyewe za kuunganisha hazipo in ur favor. Watanzania washaunganisha doti na kufikia conclusion kwamba hapa hamna kitu, ni utukufu binafsi na ego isiyo na faida. We jamaa vp?

Lema kasema yeye yupo tayari kutaja hayo majina, apewe kama yeye zitto anaogopa kutaja, its as simple as that....

kifupi tumechoka na ngojera hizi, hii singo kwisha habari yake na ZZK pia is gone loooong time
 
Nitamwomba Mh Lema amwombe Rais Kikwete majina ya wafanya biashara wa madawa ya kulevya
Mkuu, Lema anafanya siasa nyepesi. Anaangaliwa wapi penye mwanya. Hawezi kuthubuti kwenye suala la madawa ya kulevya kwani anajua wale watu ni kuua tu kama utawafuata. Uzuri wa mafisadi i kuwa wakikuona ni chadomo, wanakukatia mkwanja tu wa maana na hapo unabaki mpole. Utaanza kuimba wimbo wao na hutathubutu kuwataja tena. Ndivyo lema alivyonunuliwa na mafisadi. Tena ukiongeza lile sakata la kushikilia meza huku ameinama na wengine wamesimama nyuma yake, hapo utamuona Lema amekuwa mpoleeeee.
 
Hawa watu "wazito" ambao ZZK "anawaogopa" ni wakubwa kiasi gani kushinda wale waliowahi kutajwa pale Mwembeyanga na CDM?

SMU uko sahihi sana. Maana pale mwembeyanga Dr Slaa kwa ujasiri mkubwa aliwataja bila HOFU wala WOGA na hatimaye ilipelekea waziri mkuu wa kipindi kile Mh Edward Lowassa kujiuzulu. So Zitto kama wewe ni jasiri na una ukweli wowote kuhusiana na swala hili basi funguka tukuone.
 
  • Thanks
Reactions: SMU
Kwahiyo Zito ameogopa kuitaja hiyo list kwakuwa na Ndesamburo yupo. Unajitia aibu ndugu yangu kumtetea Zito.

Watanzania bado wanaukumbuka
ufisadi wa rada na orodha ya
waliotuhumiwa kupatiwa mgawo
kupitia akaunti zao zilizopo visiwa
vya Jersey, akiwepo Mh. Chenge na
Dr. I Rashidi. Hata kama mahakama haikuthibisha uhusika wao bado
hawakukana kuwa na akaunti
kwenye visiwa hivyo. Labda tujiulize; Je hizo akaunti zilifunguliwa kwa mujibu wa sheria zetu? Je hivyo vijisenti /mabilioni yaliyoingizwa humo yalitokana na kipato halali kinachotambuliwa na
tume ya maadili?

Hata mtandao wa waandishi wa habari ulimwenguni unaofuatilia
mambo haya umeshaanza kutoa
majina ya watanzania wenye
mabilioni Uswisi akiwepo Yusuf
Manji. Lakini mwenye jukumu la kuchunguza kama fedha hizo
zilipatikana kihalali au la, si ZZK bali
ni tume/serikali. Mbona hatujiulizi ni kwa nini Zitto alishindwa kuwataja hata hawa.? Kwani hawajui? Na hao wanaotaka orodha ili wawataje, mbona wanashindwa
kuwataja hata hawa?

Labda wataalamu wa sheria watujuze legal implication
kwa Zitto kusema kuwa anawajua
watanzania walioficha hizo fedha nje ya nchi (tena chini ya kiapo bila kinga yoyote ya kibunge) katika mazingira haya ambapo hata serikali haitaki kuridhia mkataba wa kubadilishana taarifa, achilia mbali kuwapeleka mahakamani watuhumiwa wakubwa wa ufisadi?

Sasa kulikuwa kuna haja gani ya
kuunda hiyo tume kama serikali
ilikuwa inategemea ushahidi wa
kiapo cha Mtanzania mmoja (ZZK)?
Tume inapaswa kuacha siasa bali
ifanye kazi yake (uchunguzi)
 
Jibu hoja kwa mifano hai na sio kuleta porojo za uhafidhina na propaganda zenu za kipumbavu zisizo na masilahi ya taifa wala kwa next generation.


Mkuu Abdillah, mbona unakimbizana na mwehu??huoni watu walishaacha kuangaika na uyo leasbian...achana naye uyo mkuu atakusumbua akili bure....
 
Mkuu, sasa kama ZZK anaona ni HERI kulinda usalama wa maisha yake na nafasi yake kisiasa KULIKO kurahisisha mchakato wa kuyachunguza mabilioni ya Uswisi kwa kutoa details za walioficha, basi aendelee kukaa kimya na mjadala ufungwe kwa upande wake au aiachie Kamati Maalum ya Bunge iendelee kimya kimya na kazi ya uchunguzi, na sio kuibuka kila baada ya muda fulani na kusema serikali haina nia ya kufuatilia. Unaambiwa taja majina tupate urahisi, hautaki. Basi kaa kimya usubiri tuchunguze wenyewe, hautaki. Leta majina tutaje sisi, hautaki! Sasa ikiitwa ngonjera hapo kuna kosa gani?

kama serikali ina nia kwanini isisaini mkataba wa kubadilishana taarifa??
 
Back
Top Bottom