Ombi la Lema kwa Zitto na kauli ya Werema - Unganisha dots...

notradamme

JF-Expert Member
Nov 2, 2010
2,009
452
wanaoifahamu vizuri historia ya IZRAEL, watakuwa wameshawahi kusikia jina la kikundi kimoja cha wapiganaji wa msituni kilichojulikana kama IRGUN. kundi hili liliamua kujitoa kutoka CENTRAL COMMANDING POINT ya jeshi la izrael wakati huo baada ya kuona jeshi la izrael linaendekeza siasa wakati muda wa siasa haukuwepo(kumbuka Hitler alikuwa anaendesha Holocaust dhidi ya wayahudi na wayahudi walikuwa hawana pa kukimbilia zaidi ya palestine). IRGUN CHINI YA KAMANDA WARDE WINGATE waliamua kupigana dhidi ya yeyote aliye kinyume na ZIONISM hata kama alikuwa alikuwa myahudi mwenzao. kundi hili ndilo kundi la kwanza katika historia ya dunia kutumia mabomu ya kujitoa muhanga(suicide bombers) na shambulizi lao la kwanza lilikuwa ni dhidi ya BRITISH POLICE HEAD QUARTERS katika mji wa JAFFA. katika malengo yao waliamini na kuona kwamba SIASA NA WANASIASA ni kikwazo cha kufikia malengo yoyote.
utangulizi wangu hapo juu unatokana na jinsi ninavyoyaangalia masuala ya kisiasa hapa nchini na jinsi siasa zetu zinavyojidhihirisha kuwa ni aina nyingine ya usanii na MAIGIZO yasiyomithilika.kibaya zaidi ni kwamba SIASA ZA SASA ZIME-CENTRALIZED kwa mtu mmmoja tu naye ni ZZK.
Last week niliandika humu kwamba ''kuna tuhuma/tetesi tunazifanyia kazi ya kukusanya ushahidi na pindi ushahidi utakapopatikana tutauweka hadharani kwa kila mtu kuona na kusikia. tuhuma zenyewe ni kwamba""" MAFISADI KUTOKA SERIKALINI NA CCM WAMEUNGANISHA NGUVU NA WENZAO WA CHADEMA KUHAKIKISHA ZZK ANAANGAMIA IWE NI KISIASA AU HATA KIMWILI NA ROHO''''
huu ni mkakati ambao hauko kichama, bali ni watu fulani na makundi yao yenye nguvu ndani ya serikali na hivyo vyama viwili dhidi ya ZZK huku yakijaribu(na wanaelekea kufaulu) kuwaaminisha watu kuwa kinachoendelea ni siasa na hivyo basi utatuzi wake unatakiwa uwe wa kisiasa.
kwa wao(mafisadi ) , ZZK ni kikwazo katika mikakati yao, malengo yao na hata dhamira zao. kwao wao, huyu mtu hana bei na kwamba hanunuliki na msimamo wake pamoja na weledi na uwezo wake kiakili ni tishio la maharamia ndani ya chama chake na na wale maharamia walioko CCM na serikalini. ili kumdhibiti wameamua kutengeza JOINT FORCE ili awe anashambuliwa toka kila pembe. na hapa ndipo tunapoweza kuunganisha dots za kile kinachoendelea bungeni KUPITIA OMBI LA LEMA NA KAULI YA WEREMA...
kwa mcho na masikio yangu nimemuona na kumsikia lema akiliita swala zima la FEDHA ZILIZOFICHWA USWIS KAMA NGONJERA!!!!!! na akamuomba ZZK kama anaogopa kuyataja hayo majina basi ampe yeye LEMA ayataje na kwa hili yeye(lema) hahitaji ulinzi wowote...''''''' JE AMESHAHAKIKISHIWA ULINZI NA WAHUSIKA HIVYO KUWA NA UHAKIKA NA USALAMA WAKE!!!!????"""" baada ya majigambo na porojo za kihalifu za LEMA, mwanasheria mkuu wa serikali naye alisimama na kusema kwamba eti ZZK ameapa kwamba hana jina hata moja la wamiliki wa fedha uswisi.

kwangu mimi, huu ni unabii unaothibitisha ile dhana tunayoifanyia kazi ya MAFISADI UNITED AGAINST ZZK.
mimi najua,lema anajua,werema anajua na kila mwenye akili anajua kuwa ZZK anayo majina tena sio majina tu bali pamoja na account details za walioficha fedha uswisi na kwingineko. ila kutokana na nguvu kubwa ya kifisadi iliyo nyuma ya wamiliki hawa wa mabilioni, ZZK hayuko tayari kuwasilisha chochote au kwa mtu yeyote ushahidi alionao kuhusu sakata husika. ushahidi alionao ndio uliobeba FUNGUO YA USALAMA WA MAISHA YAKE NA NAFASI YAKE KISIASA. endapo ataukabidhi, ni wazi utateketezwa na maisha yake yatakuwa hatarini. werema anasema kuhusu swala la kupeleka ZZK mahakamani, lakini nina hakika huko ndiko haswaa ambako ZZK anapataka . kupitia mahakama ndiko ambako ushahidi atakuwa tayari kuutoa na si vinginevyo. na kwa hilo basi, niwahakikishie kwamba sio serikali wala WEREMA atakayethubutu kwenda mahakamani.
G.LEMA KAMA TUNAVYOMJUA NI MTUMWA WA MBOWE... na namchukulia kama adui namba moja wa ZZK kutokana na matendo na kauli zake kwa muda mrefu sasa. haihitaji kipaji cha ujasusi kuweza kung'amua kuwa ombi lake la jana kwenda kwa ZZK pale bungeni lilikuwa limeficha dhamira OVU dhidi ya ZZK. anadhani ZZK ameshindwa(au labda anadanganya kuwa nayo) kuyataja majina ya walioficha fedha uswis. ni wazi JOINT FORCE imemtuma akalitumie bunge kumuomba ZZK ampe yeye majina ili ayataje na kama ZZK akikataa basi ieleweke kuwa ZZK ni muongo na mfitini. kwa kuahidiwa ulinzi wa kutosha au huenda na fedha vilevile, G.LEMA akasimama bungeni kumuomba ZZK ampe yeye hayo majina ayatangaze na yeye hahitaji ulinzi wowote(baada ya kuhakikishiwa ulinzi na wahusika).
tatizo hakuna kinachofikiriwa na wanasiasa wetu zaidi ya uchaguzi 2015. wanafanya mambo utadhani 2015 ndio mwisho wa taifa letu na baada ya hapo halitakuwepo tena. wanaunda mitandao ya siri dhidi ya wazalendo wa kweli na kuwaandama kutaka kuwaangamiza.
hivi ni nani anayebisha kuhusu uwepo wa akaunti za siri za baadhi ya watanzania huko ughaibuni!!!! habari hizi zilikuwepo tangu enzi ya utawala wa mwalimu nyerere ila leo tunaziona KAMPENI zimeshaanza za kutaka kutuaminisha tofauti. hivi ni nani kati yetu anayependa kujisomea asiyejua jinsi YULE MWANADADA WA KI-NIGERIA alivyotishiwa maisha na jinsi kazi ya kuyarudisha mabilioni ya dola zilizofichwa na wanasiasa wa nigeria ilivyokuwa ngumu!!!
kuna mabo ambayo hayahitaji akili nyingi, lakini ukituliza akili kidogo tu utaona TIMING ya mlolongo wa matukio ni wa kupangwa. hii sio COINSIDENCE....... ni mpango uliopangwa na pande mbili(ambazo tunadanganywa na kuaminishwa kwamba ni pande hasimu) dhidi ya COMMON THREAT.
ZZK IS A COMMON THREAT kwa fisadi yeyote bila kujali kavaa jezi ya chama gani.zzk ni windo linalowindwa na watu hatari sana toka vyama na taasisi zote zilizo na mafisadi ndani yake.wakati jumuiya ya kimataifa inamtambua na kutathamini uwezo na mchango wake(yeye ndiye kijana wa kiafrika anayealikwa zaidi katika majukwaa ya kimataifa na kutoa mada kuliko yeyote africa nzima), sisi tunamuandalia kaburi la mwili wake na kaburi lake kisiasa.vijana wa kitanzania tumekuwa ni MBWA wa kufuata miluzi ya mabwana (masters) hata kama miluzi hiyo inatuelekeza mdomoni mwa chatu.I am confused for what is happening now!!!!!
but my confussion will never lead me astray and miss my point. I WILL SATAND BY HIM(ZZK) no matter what.kama walivyofanya IRGUN kule izrael kuna umuhimu wa kufanya hivyo hapa.... mafisadi toka vyama vyote wameungana dhidi ya wanyonge wa tanzania. na yule anayesimama na wanyonge wanamuandalia kaburi. wengine woote, wanawachukulia wanyonge wa tanzania kama mitaji ya kufikia malengo yao.
ZZK.. HUU NI WOTO WANGU KWAKO....
i know as everybody knows that you are the smartest politician in mordern tanzania.you are the most patriotic leader who prictises his preach. but the stream you are swimming against, is too strong for you to cross it MAN ALONE. out here there are people. people who beleave in you, people who knows dirty politics which surrounds you.
dont go alone man. TAKE US WITH YOU!!!!
 
Mzalendo my foot!!! Tuambieni lile HUMMER alipewa na rafiki yake yupi 2008??!! Hana hata unaibu waziri anahongwa hummer je akiwa raisi atahongwa suit tu??!! Mzalendo anatembelea helicopter za TANAPA??!! Atueleze mgodi wa Buzwagi umekua mzuri baada ya yeye kuwa mjumbe wa kamati ya madini,kupewa mabati na kujengewa shule kule +mwandinga na Buzwagi hao hao????!!!

Mkiwa mnatetea mabwana zenu(utwana na ubwana)) msituragai na maneno ya uzalendo!!!!!
 
mwambie ataje sasa. ngojera zimezidi. usitufanye wapumbavu, kama unayo taja tuanze kuwachukia wao badala ya wewe.
Busara inahitajika katika kutaja. Hata Rais wa Nchi, aliwahinkutamka kuwa anayo majina ya wauza sembe. Ila mpaka sasa hajawahi kuyataja hadharani. Busara ikimuongoza mtu, usitarajie atakurupuka kutajataja tu majina ya watu hadhazani. Kwani hata ukitaja, huna hakika kama itasaidia maana tumeona hata huko mahakamani mambo hayajakaa sawa. Mafisadi wanapelekwa huko lakini tunashuhudia wakiachia, sembuse wamiliki wa akaunti nje ya nchi?
 
Mzalendo my foot!!! Tuambieni lile HUMMER alipewa na rafiki yake yupi 2008??!! Hana hata unaibu waziri anahongwa hummer je akiwa raisi atahongwa suit tu??!! Mzalendo anatembelea helicopter za TANAPA??!! Atueleze mgodi wa Buzwagi umekua mzuri baada ya yeye kuwa mjumbe wa kamati ya madini,kupewa mabati na kujengewa shule kule +mwandinga na Buzwagi hao hao????!!!

Mkiwa mnatetea mabwana zenu(utwana na ubwana)) msituragai na maneno ya uzalendo!!!!!
Mkuu, wewe kwa kuwa ni kutoka ukoo wa kihafidhina, huwezi kumsemea mazuri Kabwe.
 
notradamme Mafisadi wa nchi hii ni magwiji wa siasa.. na wamecheza karata yao vizuri kweli kweli... Vijana wengi wa nchi hii tunaudhaifu mbaya sana na hawa watu wanajua namna ya kutulisha chuki na tukashiba haswa.

Kuna dalili kuwa kati ya majina yaliyopo wapo viongozi wa vyama vya upinzani na chama tawala.
Ndomaana nguvu ya kujua ushahidi aliokuwa nao zitto ni kubwa na yenye kutaka kutimizwa kwa mbinu za hali ya juu.
 
Last edited by a moderator:
Sikutegemea na wala sitarajii kuona na kusikia Godbless Lema anaunga mkono juhudi za Zitto. Lema ni mmoja wa watu wanaofaidi matunda ya ufisadi kupitia kwa mkubwa wake Mbowe

Lema siku zoote ni mpinzani wa zitto naungana na zitto kutotaja majina hawa mafisadi wanapesa pia wako tayari kufanya lolote kwa zitto kama atawataja.

Achane kulalama juu ya zitto kama hamjui ugumu wa haya mambo mbona mbowe alisema anamkanda wa mripuko wa bomu soweto mbona hajautoa hadi leo acheni kutaka majibu mepesi.
 
Jibu hoja kwa mifano hai na sio kuleta porojo za uhafidhina na propaganda zenu za kipumbavu zisizo na masilahi ya taifa wala kwa next generation.
Mkuu, mbona unanilazimisha njibu hoja? Kwani mimi ndo niliyetoa hoja hiyo?
 
MKUU WA NCHI ALISEMA ANAYO MAJINA YA WAUZA UNGA+ZZK NINAYO MAJINA YA WALIOFICHA FEDHA USWIS=:A S-confused1:(CONFUSED) WHY AND FOR WHOM?HAO WATU WANAOOGOPWA KUTAJWA WANA NGUVU KIASI HICHO?AU TUNAWAJUA?AU NI NDUGU ZETU WA KARIBU?AU NI WATU HATARI SANA?=CONFUSED WITH BONGO POLITICS
 

Similar Discussions

29 Reactions
Reply
Back
Top Bottom