CHEDU
Senior Member
- Dec 24, 2015
- 198
- 188
Ombi kwa wagombea Ubunge na Urais juu ya lugha ya kufundishia mashuleni kubadilishwa kutoka kiswahili kuwa Kiingereza.
Mnapoelekea uchaguzi mkuu wagombea wote wa ngazi zote na kwa vyama vyote hasa wa chama tawala tafadhali tunaomba mchukue ajenda hii kwa upande wa elimu mkadilishe lugha ya kufundishia kutoka Kiswahili kuwa Kiingereza.
Hali ni mbaya sana kwa shule zetu za serikali wanafunzi wanahangaika sana pale wanapotoka shule za awali kujiunga na sekondar wanapata tabu sana kuyaelewa masomo kwa maana lugha inabadirika na wao wanafunzi awali walizoeshwa kutumia kiswahili katika kujifunza.
Hii imepelekea wanafunzi wengi kutoelewa wanachofundishwa na kuchukia shule, na hata hao wachache wanaofaulu bado shida ipo hasa katika kujieleza kwa lugha ya kiingereza hata baada ya masomo watu wanapata shida sana katika interview wakati wa kutafuta kazi hali ni mbaya sana.
Cha kushangaza viongozi wengi nchi hii wanakumbatia mfumo wa lugha kiswahili mashuleni wakati watoto wao wanawasomesha shule za private ambazo lugha za kufundishia ni za Kiingereza, hii ni roho mbaya na ubinafsi wa hali ya juu sana mnahalibu maisha ya watu.
Namaliza kwa kusema hii kitu ni rahisi kama watia nia na wagombea mkiichukua kama ajenda ili kuwanusuru vijana wetu huku mashuleni bado hamjachelewa, tukianza na chekechea darasa la kwanza hadi chuo kikuu naamini hata viwango vya ufaulu vitapanda.
Mnapoelekea uchaguzi mkuu wagombea wote wa ngazi zote na kwa vyama vyote hasa wa chama tawala tafadhali tunaomba mchukue ajenda hii kwa upande wa elimu mkadilishe lugha ya kufundishia kutoka Kiswahili kuwa Kiingereza.
Hali ni mbaya sana kwa shule zetu za serikali wanafunzi wanahangaika sana pale wanapotoka shule za awali kujiunga na sekondar wanapata tabu sana kuyaelewa masomo kwa maana lugha inabadirika na wao wanafunzi awali walizoeshwa kutumia kiswahili katika kujifunza.
Hii imepelekea wanafunzi wengi kutoelewa wanachofundishwa na kuchukia shule, na hata hao wachache wanaofaulu bado shida ipo hasa katika kujieleza kwa lugha ya kiingereza hata baada ya masomo watu wanapata shida sana katika interview wakati wa kutafuta kazi hali ni mbaya sana.
Cha kushangaza viongozi wengi nchi hii wanakumbatia mfumo wa lugha kiswahili mashuleni wakati watoto wao wanawasomesha shule za private ambazo lugha za kufundishia ni za Kiingereza, hii ni roho mbaya na ubinafsi wa hali ya juu sana mnahalibu maisha ya watu.
Namaliza kwa kusema hii kitu ni rahisi kama watia nia na wagombea mkiichukua kama ajenda ili kuwanusuru vijana wetu huku mashuleni bado hamjachelewa, tukianza na chekechea darasa la kwanza hadi chuo kikuu naamini hata viwango vya ufaulu vitapanda.