Ombi kwa rais wa tec (baraza la maaskofu katoliki) kuhusu matatizo ya chuo cha bugando.

CHIETH

Senior Member
Aug 15, 2011
179
67
Tumsifu yesu Kristo,
Ninapenda kutoa taarifa ya hali halisi ya Chuo Kikuu cha Bugando.

Mwezi wa saba wanafunzi wa Udaktari wa mwaka wa tatu waliandika barua kwa mkuu wa kitivo cha udaktari wakiomba mitihani ya management of diseases uhairishwe hadi hapo watakopofundishwa ipasavyo. Kwa bahati mbaya Mkuu huyo aliamua kutumia lugha chafu kuponda darasa kwa maandishi eti darasa kwanza ni weak- yaani wabovu na hawahudhurii darasa. Akaamua kutumia kigezo hicho ilikukandamiza darasa hilo kufanya mitihani hiyo ili kuficha siri ya lecturers husika kutoingia darasani kufundisha. Walimjibu kwa maandishi eti hawatafanya mitihani hiyo hadi watakapo fundishwa kulingana na prospecter ya chuo.

Ni kweli kwamba wanafunzi hawa hawakufanya mitihani kwa kufuata maelezo ya prospecter yao. Bila kuzingatia ukweli huo Mkuu wa kitivo cha udaktari akaamua kutoa maamuzi yake kupitia academic board kuwa darasa hili linafaa lifutiwe udahili. Bahati nzuri kulikuwa na wajumbe wanaofahamu sheria na madhara ya matokeo ya maamuzi kama yake. Hakuzingatia mamilioni ya fedha zilizokwisha potea kugharamia elimu ya wanafunzi hao.
Hivi sasa Huyo Mkuu wa kitivo amejenga uhasama na wanafunzi hao na ameanza kushinikiza kuwa lazima wafeli katika mitihani ya marudio na kutunga mitihani migumu ili baadhi ya wanafunzi hao waDISCO. Sijui kama kweli mkuu huyo anailewa vema prospecter. Anashinikiza supplementary zifanyike mwezi wa tatu na sio mwezi wa 9 kulingana na maelekezo ya prospecter ya chuo. Hii ikiwa ni njama ya kuwabebesha mzigo wale wenye suplementary ya pharmacology washindwe mitihani ya management of diseases mwezi wa 3 ili wa disco.

Naomba mtafute suluhu kati ya hawa wanafunzi na Mkuu wa kitivo la sivyo nina wasi wasi kama wanafunzi hawa watamaliza chuo wote. Ninafikri mkuu huyu anapersonal grudges na darasa hili.
Tatizo la mkuu huyo ni kuwa hana tabia ya kusikiliza matatizo ya wanafuzi ukizingatia Chuo hiki inamatatizo ya walimu wa clinicals. Nikweli 85% ya clinical subjects hazifundishwi ipasavyo na kuna usanii mwingi. Wanafunzi wanapokosa masomo haya wanapoingia wodini huwa wanakutana na hali ngumu sana ikiwa ni pamoja na matusi, kejeli na dharau kutoka kwa madaktari wa bugando. Mwaka wa tano walitungiwa mitihani migumu ya surgery isiyo kuwa na sifa halafu mtungaji akatoka nje akitamba amewakomesha. Hii ndiyo chuo kikuu kweli? Mkufunzi kama huyu hana tofauti na Mwalimu wa primary anayetunga mitihani halafu hutambia wanafunzi wake eti atakaye pata 50 nitampa zawadi. Mkuu huyu wa kitivo hakuona hili kama tatizo. Ina maana hana kamati inayofanya moderation ya mitihani iendane sifa za kimataifa, maana mtu anaweza akatunga mitihani kulingana na interest zake binafsi.

Sasa kama mkereketwa wa swala hili nimeamua kutumia jukwaa hili ili kuomba msaada kwa maaskofu kuuangalia vizuri chuo chao.

Naomba kuwasilisha.
 
Mkuu, malalamiko yenu ni ya msingi sana, kwa ushauri wangu mngepeleka haya malalamiko kwenye uongozi wa chuo au kwa wadhamini wa chuo, na ikiwezekana mpeleke nakala ya malalamiko yenu wizarani... Na hata ikiwezekana kwenye magazeti...! Elimu ni jambo kubwa sana na halipaswi kufanyiwa masihala.
 
Jitahididni naona elimu ya Tanzania bado ina utumwa mwingi sana. Fight foryour rights. Usipofundishwa vizuri masomo ya clinic utaitwa dr. au dk?
 
Chukuenı barua zote zenu na alızowajıbunı,pelekenı wızara ya Elmu na vılevıle pelekenı kwa Askofu,ılı waweze kuwapenı ufumbuzı wa Tatızo lenu,Elımu nı kıtu kıngne kabısa msıkubalı wachezee maısha yenu kabısa.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom