Ombi kwa mbunge wa Kigoma Kaskazini mh. Z.Z Kabwe kuhusu Mwandiga..

sexologist

JF-Expert Member
Dec 5, 2010
2,283
976
Nimetazama taarifa ya habari leo kupitia chanel ten, pamoja na mambo mengine, nimevutiwa na habari ya Kigoma eneo la Mwandiga..

Habari yenyewe ni particularly kuhusu soko la Mwandiga ambalo linahudumia vijiji sita na wakazi zaidi ya 20,000.. Cha ajabu, soko halina choo hata kimoja. Watu wanajihudumia kwenye vibanda vya biashara, na wafanyabiashara wanalalamika sana mbunge wao kuwatelekeza, vibanda vimechoka mno..

Habari hii kwangu na kwa baadhi ya watu ni sensitive kutokana na umaarufu wa mbunge wa huko na nguvu yake ya ushawishi kwa sponsors.. ukikumbuka aliwahi kuanzisha utaratibu wa kuwakopesha vijana pesa, ambazo alidai kupewa na wafadhili wa nje..

Ndugu Zitto Zuberi Kabwe, kwa heshma na taadhima naomba uwakumbuke ndugu zako na wapiga kura wako wa Mwandiga..

Acha kuzunguka kila kona 'kujisafisha'.. Wewe ni mbunge wa Kigoma Kaskazini sio wa taifa. Hivyo saidia kwako kwanza ndio uje na kwangu!!

Naamini umenielewa!

Source: Chanel 10

am a free mind!
 
Hapo ni sawa na kumpigia mbuzi gitaa ukitegemea acheze. Zitto ni sawa na kenge. Hasikii hadi umpige atokwe na damu masikioni ndio atasikia.
 
Zitto sio wa mwandiga kwao ni mwanga kisangani. Ingawa ndio ngome yk kubwa kw jimbo lake.
 
kwa hiyo ulitaka akachimbe choo? hizi siasa zinatupeleka pabaya sasa. we zito njoo hapa akina lema naona wameanza tena
 
kwa hiyo ulitaka akachimbe choo? hizi siasa zinatupeleka pabaya sasa. we zito njoo hapa akina lema naona wameanza tena


Mwaka huu Zito chochote atakachofanya hata kiwe kizuri vipi kitapondwa na kuonekana kama mavi!
 
kwa hiyo ulitaka akachimbe choo? hizi siasa zinatupeleka pabaya sasa. we zito njoo hapa akina lema naona wameanza tena

wabunge wanakazi kubwa ya kutuongoza sisi wenye akili ndogo, ila bora huyu kapendekeza mbunge akachimbe choo, wapo wanategemea kupata soksi za shule kutoka kwa wabunge wao.
Kila mtu awajibike katika ngazi yake aliyopo.
 
Back
Top Bottom