Mimi siamini kama kuna uwezekano wa kiongozi mzuri kutoka CCM. JK alikuwa chaguo la wengi na wengi tulimpenda ila baada ya JK kutuangusha kwa jinsi tulivyoweka matumaini kwake sioni kama kuna mtu mwingine ndani ya ccm anaweza kuibadili ccm kiwe chama kizuri. Nakiri, nampenda sana Dr Slaa kwa kuwa namwona kama ni mkombozi, mtu asiyeweka maslahi yake binafsi mbele lakini hata Dr Slaa akigombea kwa tiketi ya ccm sitampa kura kwa vile tatizo ni chama si mtu au watu.
Maombi yangu kwa uongozi wa chadema ni kwamba kwa kuwa watanzania tunaiona chadema kama chama mbadala, kizogezeni zaidi chama kwa watu ili kiwe chama cha watu na si cha viongozi. Naomba mzingatie yafuatayo, ni maoni yangu tu yapo subject to criticism ila nayatoa kwa nia njema ya kujenga chama chetu.
(i) Kwanza, tutenge siku moja kwa mwaka, nadhani siku ya kumbukizi ya kuzaliwa chama, tufanye mikutano nchi nzima, lakini badala ya kuhutubia tuwape wananchi nafasi wao wazungumze. Ni ukweli kwamba Tz tuna brains nyingi sana na ufumbuzi wa matatizo yetu tunayo ila tatizo ni kukosa uongozi wa kuyaweka mawazo yetu pamoja na kuyatekeleza. katika mikutano hiyo ya wananchi wa kada mbalimbali na makundi mbalimbali, tuwaulize wana matatizo gani na wanataka matatizo yao watatuliwe vipi. Tukiyakusanya maoni ya watanzania kwa miaka minne, tunaya summarize na kuyatumia kutengeneza ilani ya uchaguzi ya mwaka 2015.
Hapa tutakuwa na mawazo na maoni yanayohusu jimbo kwa mfano wananchi wa ubungo wanaweza kutoa maoni kuhusu jimbo lao na nini kifanyike kuwakomboa, hapa tutatengeneza ilani ya mgombea ubunge na udiwani, yale ya kitaifa basi yanatumika kujenga ilani ya mgombea urais. Kwa kuwa watu wanapigia kura ilani za vyama na kwa kuwa ilani ya chadema itakuwa si imposed bali imetoka kwa watu basi si rahisi watu waipinge.
Kikubwa zaidi ni kwamba sidhani kama malengo yetu ni kushinda uchaguzi tu bali kuisukuma Tz mbele. Kama ilani itatokana na wananchi wenyewe basi itakuwa yao na itatekelezeka. Fuatilia kwa mfano mijadala kuhusu umeme, watu wana mawazo makubwa mno namna ya kuondoa tatizo hili, kama tukichukua mawazo haya na kushirikiana na wananchi wenyewe hakika tutashinda. tatizio la ccm ni kwamba mambo hayatoki kwa watu bali yanatoka juu. Mfano mwingine, tatizo la ajira ya vijana lina ufumbuzi unaotokana na vijana wenyewe, kaa na vijana wasomi, wamachinga, mama ntilie waulize nini kifanyike watakupa mawazo makubwa hadi utashangaa. Tukitumia mawazo yao na kuwatumia wao kutekeleza tutashinda hakika.
(ii) Pili nashauri chama kiajiri on part time basis washauri rasmi wa chama. Watafutwe watu makini na waliobobea katika fani mbalimbali walipwe vizuri kazi yao iwe kufikiri na kufanya utafiti kuhusu mambo ya chama. Naomba tuanze na washauri wanne, wa uchumi, siasa, mambo ya nje na gender. hawa washauri wasiwe wajumbe wa kamati kuu bali wawe watu huru na hata si lazima wawe wanachama ila wanaweza kuhudhuria vikao kama observers tu. natoa tu mfano, ukimchukua Jenerali ulimwengu kama mshauri wa siasa, unamlipa vizuri, kazi yake iwe ni kutafiti, kufuatilia siasa ya nje na ndani na kushauri nini kisemwe wakati gani na chama ki react vipi kuhusu mambo mbalimbali, tuwe na ilani ya jinsi gani, hatuba zibebe nini nk tutapata advantage sana. hata mambo kama maandamano ,kutoka nje bungeni nk lazima mtu huyu ashauri political implication.
Week end njema, tupo pamoja kwa mapambano.
Maombi yangu kwa uongozi wa chadema ni kwamba kwa kuwa watanzania tunaiona chadema kama chama mbadala, kizogezeni zaidi chama kwa watu ili kiwe chama cha watu na si cha viongozi. Naomba mzingatie yafuatayo, ni maoni yangu tu yapo subject to criticism ila nayatoa kwa nia njema ya kujenga chama chetu.
(i) Kwanza, tutenge siku moja kwa mwaka, nadhani siku ya kumbukizi ya kuzaliwa chama, tufanye mikutano nchi nzima, lakini badala ya kuhutubia tuwape wananchi nafasi wao wazungumze. Ni ukweli kwamba Tz tuna brains nyingi sana na ufumbuzi wa matatizo yetu tunayo ila tatizo ni kukosa uongozi wa kuyaweka mawazo yetu pamoja na kuyatekeleza. katika mikutano hiyo ya wananchi wa kada mbalimbali na makundi mbalimbali, tuwaulize wana matatizo gani na wanataka matatizo yao watatuliwe vipi. Tukiyakusanya maoni ya watanzania kwa miaka minne, tunaya summarize na kuyatumia kutengeneza ilani ya uchaguzi ya mwaka 2015.
Hapa tutakuwa na mawazo na maoni yanayohusu jimbo kwa mfano wananchi wa ubungo wanaweza kutoa maoni kuhusu jimbo lao na nini kifanyike kuwakomboa, hapa tutatengeneza ilani ya mgombea ubunge na udiwani, yale ya kitaifa basi yanatumika kujenga ilani ya mgombea urais. Kwa kuwa watu wanapigia kura ilani za vyama na kwa kuwa ilani ya chadema itakuwa si imposed bali imetoka kwa watu basi si rahisi watu waipinge.
Kikubwa zaidi ni kwamba sidhani kama malengo yetu ni kushinda uchaguzi tu bali kuisukuma Tz mbele. Kama ilani itatokana na wananchi wenyewe basi itakuwa yao na itatekelezeka. Fuatilia kwa mfano mijadala kuhusu umeme, watu wana mawazo makubwa mno namna ya kuondoa tatizo hili, kama tukichukua mawazo haya na kushirikiana na wananchi wenyewe hakika tutashinda. tatizio la ccm ni kwamba mambo hayatoki kwa watu bali yanatoka juu. Mfano mwingine, tatizo la ajira ya vijana lina ufumbuzi unaotokana na vijana wenyewe, kaa na vijana wasomi, wamachinga, mama ntilie waulize nini kifanyike watakupa mawazo makubwa hadi utashangaa. Tukitumia mawazo yao na kuwatumia wao kutekeleza tutashinda hakika.
(ii) Pili nashauri chama kiajiri on part time basis washauri rasmi wa chama. Watafutwe watu makini na waliobobea katika fani mbalimbali walipwe vizuri kazi yao iwe kufikiri na kufanya utafiti kuhusu mambo ya chama. Naomba tuanze na washauri wanne, wa uchumi, siasa, mambo ya nje na gender. hawa washauri wasiwe wajumbe wa kamati kuu bali wawe watu huru na hata si lazima wawe wanachama ila wanaweza kuhudhuria vikao kama observers tu. natoa tu mfano, ukimchukua Jenerali ulimwengu kama mshauri wa siasa, unamlipa vizuri, kazi yake iwe ni kutafiti, kufuatilia siasa ya nje na ndani na kushauri nini kisemwe wakati gani na chama ki react vipi kuhusu mambo mbalimbali, tuwe na ilani ya jinsi gani, hatuba zibebe nini nk tutapata advantage sana. hata mambo kama maandamano ,kutoka nje bungeni nk lazima mtu huyu ashauri political implication.
Week end njema, tupo pamoja kwa mapambano.