Ombi: Ajira TANESCO zipitie Public Sec. Recruitmnent, wengi wameingia kwa kubebwa

Uozo wa namna hii upo kwenye public/ government institutions nyingi.

Nenda kila mahali kupo ivyo ivyo

Undugu, ukanda, ukabila, udini kwenye ajira ni janga kubwa.
Watu maskini huwa wanaongea mengi sana juu ya waliofanikiwa. Hivi mwajiriwa kama ana sifa na anaweza kazi kuna haja gani ya kumfanyia categorization ya uliyoyataja hapo juu? Nchi zilizoendelea maoni ya kugawa kama haya hakuna. Marekani Bush baba Rais tena alichaguliwa, akaja Bush mtoto rais tena wa kuchaguliwa, Bush mtoto Gavana wa kuchaguliwa haya maneno ya ukanda, ukabila, udini, familia wenzetu hawajali wanajali uwezo wako tuu! Mama Clinton naye mke wa Rais wa Zamani naye alipigiwa kura nyingi tu awe rais pamoja na kwamba mumewe alishawahi kuwa rais. Hakukosa kura eti kwa vile ni Clinton wife. Mimi naona ifike mahali watu waajiriwe kwa sifa na uwezo wao siyo kuwanyima kwa ukabila,Undugu, ukanda, udini. Tuache kugawanyika kwa misemo hii. Halafu hivi kama mimi nina wadhifa sehemu kuna fursa ndugu, mtoto ana sifa kwa nini nisimpe? Wakose kwa kuwa nina mahusiano nao? Faida yangu kwao ni nini kama siyo kuwabeba? Ila kama hana sifa simpi!
 
Mfumo wa kuajiri watumuishi katika shirika la umeme Tanzania(TANESCO) ni mbovu , usiofuata misingi wala utaratibu maalum. Tanesco kupewa uwezo wa kuajiri wenyewe imekuwa shida kwao kwani watu wengi wameajiriwa kwa mashinikizo ya wakubwa katika shirika. Naomba serikali ipeleke ajira zote za TANESCO Katika sekretarieti ya ajira ya Taifa. Unakuta shirika linaajiri watu ili kufanya kazi flani lakini hawana uwezo hasa katika kazi za kiufundi.

Taarifa zinasema huko mokoani ndo uozo umejaa, kwani unaweza kukuta meneja ameajiri familia yake nzima na ni watumishi wa eneo husika , jambo kama hili linapunguza ufanisi wa kazi.

Pia promotion za TANESCO Nyingi zimekuwa ni za kujuana, unakuta mtu ana masters , ana PHD lakini hapandi cheo. Matokeo yake mameneja wengi hasa wa mikoani na wilayani wana elimu ya diploma tu, Serikali iangalie sana suala hili, kwani linaleta kuvunjana moyo mtu ana mdegree, masters na ni mtendaji mzuri, inakuaje mtu mwenye elimu ya diploma ndo apewe umeneja. Mabo ya TANESCO ni ya ajabu sana.
TANESCO ni shirika la Umma linalojitegemea kwa kila kitu. (SU) Sidhani kama serikali inaweza kuwaingilia katika kuajiri, promotion.
 
Au kama vipi kazi hizo wapewe watoto wa viongozi tu .
Yaani hakuna watu nawaheshimu nchi hii kama mafundi umeme wa TANESCO. Jamani hawa mafundi wako vizuri kikazi, nikiona vipindi vyao vya kazi wanazofanya za kuzalisha umeme na kuunganisha siamini kama Tanzania tumeweza kusomesha watalaam kama hawa. Fikiria jinsi umeme ulviyo hatari lakini jamaa hawa wanaondoa hiyo hatari. Hizo ajira mnazolilia za TANESCO nadhani ni zile Supportin business siyo Core Business kama Ufundi wa kuunganisha umeme kitaifa! Sidhani kama walishawahi kuacha fundi kwa kuzingatia upendeleo! Kaka yangu alimaliza Electrical Engineering Dar Tech, moja kwa moja Tanesco wali[potangaza ajira bila kumfahamu mtu.
 
Mfumo wa kuajiri watumuishi katika shirika la umeme Tanzania(TANESCO) ni mbovu , usiofuata misingi wala utaratibu maalum. Tanesco kupewa uwezo wa kuajiri wenyewe imekuwa shida kwao kwani watu wengi wameajiriwa kwa mashinikizo ya wakubwa katika shirika. Naomba serikali ipeleke ajira zote za TANESCO Katika sekretarieti ya ajira ya Taifa. Unakuta shirika linaajiri watu ili kufanya kazi flani lakini hawana uwezo hasa katika kazi za kiufundi.

Taarifa zinasema huko mokoani ndo uozo umejaa, kwani unaweza kukuta meneja ameajiri familia yake nzima na ni watumishi wa eneo husika , jambo kama hili linapunguza ufanisi wa kazi.

Pia promotion za TANESCO Nyingi zimekuwa ni za kujuana, unakuta mtu ana masters , ana PHD lakini hapandi cheo. Matokeo yake mameneja wengi hasa wa mikoani na wilayani wana elimu ya diploma tu, Serikali iangalie sana suala hili, kwani linaleta kuvunjana moyo mtu ana mdegree, masters na ni mtendaji mzuri, inakuaje mtu mwenye elimu ya diploma ndo apewe umeneja. Mabo ya TANESCO ni ya ajabu sana.
Kwanza usijaribu kuonesha masters wakati wametangaza wanataka shahada lazima utapigwa chini. Penye watu feki vyeti halisi acha vyeti vikubwa havitakiwi.
 
Ni kweli Tanesco wana ajiri kwa upendeleo, km huna ndugu Tanesco imekula kwako.
Ma HR wanatoa ajira kwa maadizo toka juu tens bila ya haya wanampa asiyestahi
 
Kuna watu wamelaaniwa kwakuwa na fikra au mawazo ya kibaguzi, nikweli unakuta mtu kutoka mkoa furani akishapata madaraka kama CEO, au DG wale wa kabila lake wana anza na viburi kwa dhana yakuwa boss ni kabila lao,baadhi ya watu wana thubutu hata kuwapa vyeo watu wa mikoa au kabila lao kisa tu wanatoka sehemu moja au kabila moja, haya mambo yapo na kuna makabila ambayo yanaongoza kwa tabia hizi za kibaguzi, halafu unaluta wana network ya kulindana.Japo sina uhakika inawezekana hili TANESCO Lilikuwepo kutaokana na mambo yalivyokuwa yanakwenda hovyo hovyo tu.
 
Mfumo wa kuajiri watumuishi katika shirika la umeme Tanzania(TANESCO) ni mbovu , usiofuata misingi wala utaratibu maalum. Tanesco kupewa uwezo wa kuajiri wenyewe imekuwa shida kwao kwani watu wengi wameajiriwa kwa mashinikizo ya wakubwa katika shirika. Naomba serikali ipeleke ajira zote za TANESCO Katika sekretarieti ya ajira ya Taifa. Unakuta shirika linaajiri watu ili kufanya kazi flani lakini hawana uwezo hasa katika kazi za kiufundi.

Taarifa zinasema huko mokoani ndo uozo umejaa, kwani unaweza kukuta meneja ameajiri familia yake nzima na ni watumishi wa eneo husika , jambo kama hili linapunguza ufanisi wa kazi.

Pia promotion za TANESCO Nyingi zimekuwa ni za kujuana, unakuta mtu ana masters , ana PHD lakini hapandi cheo. Matokeo yake mameneja wengi hasa wa mikoani na wilayani wana elimu ya diploma tu, Serikali iangalie sana suala hili, kwani linaleta kuvunjana moyo mtu ana mdegree, masters na ni mtendaji mzuri, inakuaje mtu mwenye elimu ya diploma ndo apewe umeneja. Mabo ya TANESCO ni ya ajabu sana.
Kwani mashirika yote ya umma ndivyo yanavyofanya ?au sababu tu ni Tanesco
 
Hata sekretarieti ya ajira nao wanabeba ndugu zao tu

Mkuu nakuunga mkono. Secretariate ya Ajira ndiko kuna uozo wa ajabu. Kuna kujuana balaa....Nenda vyuo vikuu..vya umaa, sijui SUA, UDSM, you name it..Ajira ni kujuana mpaka inaboa.
 
1. Kwangu mimi hili ni wazo zuri sanah!
2. Pia wazo hili naushauli lisi ishie TANESCO tu! bali liende kwenye taasisi zote zinazo/zilizo lalamikiwa sana na Watanzania kwamba zinatoa ajira za upendeleo. Mfano mmoja mkubwa ni shirika la NSSF, ambako aliyekuwa director general Alhaji Dr. Ramadhan Dau na Human Resource Bi. Chiku Mattesa walikuwa wakilalamikiwa sanaa kuwa wanatoa ajira zenye upendeleo wa kidini.
 
Tusiilaumu TANESCO jamani....huu mfumo wa kujua upo tena ni CANCER hapa nchini kwetu.

Tunashadadia kwa kua humu ndani mpo mlioingia wa memo kutoka juu na mpo mlioingia kwa kudra za mwenyezi MUNGU.
 
Kwa vile ulitaka ajiea tanesco ukakosa basi umejawa na chuki na tanesco,hata wakihamishia utumishi hutopata hiyo kazi.

Mkitoka hapo aliekosa kazi TRA,TANAPA,TPDC,EWURA,TFDA,TBC,CAG,REA,NHC,BOT,TPA,DAWASCO,SUMATRA,TBS, nk ,nk nao watataka kazi ziende utumishi kisa walikosa kazi huko.

Haya ni mawazo ya kimasikini.
 
Mfumo wa kuajiri watumuishi katika shirika la umeme Tanzania(TANESCO) ni mbovu , usiofuata misingi wala utaratibu maalum. Tanesco kupewa uwezo wa kuajiri wenyewe imekuwa shida kwao kwani watu wengi wameajiriwa kwa mashinikizo ya wakubwa katika shirika. Naomba serikali ipeleke ajira zote za TANESCO Katika sekretarieti ya ajira ya Taifa. Unakuta shirika linaajiri watu ili kufanya kazi flani lakini hawana uwezo hasa katika kazi za kiufundi.

Taarifa zinasema huko mokoani ndo uozo umejaa, kwani unaweza kukuta meneja ameajiri familia yake nzima na ni watumishi wa eneo husika , jambo kama hili linapunguza ufanisi wa kazi.

Pia promotion za TANESCO Nyingi zimekuwa ni za kujuana, unakuta mtu ana masters , ana PHD lakini hapandi cheo. Matokeo yake mameneja wengi hasa wa mikoani na wilayani wana elimu ya diploma tu, Serikali iangalie sana suala hili, kwani linaleta kuvunjana moyo mtu ana mdegree, masters na ni mtendaji mzuri, inakuaje mtu mwenye elimu ya diploma ndo apewe umeneja. Mabo ya TANESCO ni ya ajabu sana.


hili si kwa TANESCO TUU hata taasisi nyingi za serikali, kazi ni kwakujuana...watoto wa wakubwa na ndugu zao...na wengine wanabadili majina ya ukoo ili wasijulikane...

Viongozi wetu wa serikali waangalie hili ni jipu sana.....
Ukijaribu kutumbua hapa kuna ndugu zake ambao watabaki watakuwa wanampa taarifa zoote za ndani wanakumaliza... Hili ni jipu tambaazi hasa, watu wanaajiriwa kwa vimemo, wanafanya interview lkn hata wasipopita wanaajiriwa
 
Back
Top Bottom