Omba omba huyu anastahili viboko!!

mchajikobe

JF-Expert Member
Aug 14, 2009
2,652
1,237
Habari zenu ndugu wana JF,leo hapa jamvini kuna kitu nataka kuwajuza,kwa wale watumiao barabara ya Ali Hassan Mwinyi na ile ya umoja wa mataifa pale karibu na trafic lights za Salender kuna omba omba mmoja mimi binafsi naamini anastahili viboko ili aache utani na awaombao.Huyu ombaomba ni mvulana ambaye amekuwa pale kwa miaka mingi kidogo akijitafutia ridhiki,lakini kinachonisababisha nimtafutie bakora ni kwamba hana ubunifu na kazi yake,huyu jamaa ana kidonda kikubwa sana mguuni na hicho ndicho kimpatiacho ridhiki,kinachonishangaza kwa huyu bwana ni kwamba kila siku anaomba hela ya kwenda kujitibu,lakini kila mwaka kidonda kiko vilevile na hakikauki,sijui kama ni kidonda kweli au ni sanaa,maana kwa mtu wa kawaida ukiwa na kidonda kama kile huwezi fika miezi miwili bila kukatwa huo mguu!Nimetafakari kwa kina nikaona huyu jamaa anatutania sisi ombwaombwa,ile inaweza ikawa ni sanaa,sababu mtu gani hahisi hata maumivu,wala kidonda hakiongezeki wala kupungua?Huyu mimi naona anastahili viboko ili aache ujinga wake huo!!
 
Hata mimi huwa anainiboa anavyolazimisha tutizame hicho kidonda chake! Kwa kweli tunatatizo kubwa sana. Wengi wa hawa ombaomba wanao uwezo wa kujitafutia kipato bila kuomba.

Hii attitude ya kuomba ni mbaya sana inapokuwa kwa mtu mojamoja lakini ni mbaya zaidi inapokuwa kwa taifa. Viongozi wetu wanazunguka huku na huko kujipendekeza na kuombaomba wakati uwezo tunao (very simila to hawa ombaomba!).
 
Binafsi hii inakera sana,

Jana kwenye luninga eti ombaomba wameandamana kupinga kuwa mwenzao kamgeuza mtu mkono ukawa na manyoya, halafu hiyo stesheni inatupotezea muda kuturushia hewani. Hivi hao ombaomba hawana akili. Kuna mwenzao China ambaye ukimwona hata wao ni wazima sana, lakini anamiliki duka lenye slogan "Half Man, Half Price"
 
Cjui kama ni kweli ila mi niko huku Serengeti National. Huku tunasikia kuwa kuna ombaomba mmoja hapo salender bridge kamwomba mama moja chapaa afu huyo ombwaombwa akaota manyoa, halafu ghafla ombaomba na ombwaombwa wakapotea katika mazingira ya kutatanisha. Yakweli hayo?
 
Habari zenu ndugu wana JF,leo hapa jamvini kuna kitu nataka kuwajuza,kwa wale watumiao barabara ya Ali Hassan Mwinyi na ile ya umoja wa mataifa pale karibu na trafic lights za Salender kuna omba omba mmoja mimi binafsi naamini anastahili viboko ili aache utani na awaombao.Huyu ombaomba ni mvulana ambaye amekuwa pale kwa miaka mingi kidogo akijitafutia ridhiki,lakini kinachonisababisha nimtafutie bakora ni kwamba hana ubunifu na kazi yake,huyu jamaa ana kidonda kikubwa sana mguuni na hicho ndicho kimpatiacho ridhiki,kinachonishangaza kwa huyu bwana ni kwamba kila siku anaomba hela ya kwenda kujitibu,lakini kila mwaka kidonda kiko vilevile na hakikauki,sijui kama ni kidonda kweli au ni sanaa,maana kwa mtu wa kawaida ukiwa na kidonda kama kile huwezi fika miezi miwili bila kukatwa huo mguu!Nimetafakari kwa kina nikaona huyu jamaa anatutania sisi ombwaombwa,ile inaweza ikawa ni sanaa,sababu mtu gani hahisi hata maumivu,wala kidonda hakiongezeki wala kupungua?Huyu mimi naona anastahili viboko ili aache ujinga wake huo!!
KWA TAARIFA YAKO ILE NI NGOZI YA NG'OMBE ANACHUKUA MACHINJIONI KILA SIKU. Bado yupo mbona nasikia ndiye aliyehusika na manyoya ya mkononi yaani nyaunyau?
 
Hakuna kidonda pale angeshakufa kwa kidonda kama ile tangu nimuone zamani sana huwezi kuishi na kidonda kama ile..feki
 
KWA TAARIFA YAKO ILE NI NGOZI YA NG'OMBE ANACHUKUA MACHINJIONI KILA SIKU. Bado yupo mbona nasikia ndiye aliyehusika na manyoya ya mkononi yaani nyaunyau?
Duu wewe kiboko ulifanyaje utafiti mgumu kiasi hicho hadi ukagundua hilo gozi la ng'ombe,sasa huwa ananunua au hupewa bure?
 
Pale yupo na kijana mwingine mikono yake kama vile imeathirika na ukoma, yule kijana alifukuzwa kwenye kituo cha kulelea watoto yatima kwa kuwa ni mlevi kupindukia na anavuta sana bangi.,waliokuwa wanamlea wanasema kuwa alikuwa pia ana kamchezo ka kulawiti wenzake hapo kituoni na mara kwa mara alikuwa anatoroka na kuingia mitaani kuomba mwisho wake wakamtimua kabisa na hata sasa inasemekana kila jioni akifunga mahesabu anaenda bar na kuanza kuangusha moja moja, sasa mtu kama huyu hata kama mikono yangu haitaota manyoya kwanini nimsaidie .
 
Una maana hata Muungwana ni Omba Omba?

Tena yeye ndio kiongozi wa ombaomba.,hebu imagine tunaomba michango ya sherehe, pesa za maendeleo ya nchi, wazee wa manyoya nao wanaomba pesa za kujikimu kimaisha n.k. sasa ni nini hiki kama si taifa la ombaomba.
 
Anajiita papaa ya pesa nyingi.
Hana kidonda wala nini, usiku huwa anakuwa mzima,
akimaliza kuzungukazunguka, huwa anaenda kupooza koo pale kona bar, afrika sana.
Pitapita usiku utamuona.
 
Anajiita papaa ya pesa nyingi.
Hana kidonda wala nini, usiku huwa anakuwa mzima,
akimaliza kuzungukazunguka, huwa anaenda kupooza koo pale kona bar, afrika sana.
Pitapita usiku utamuona.
Unanitia hasira sana kama ni kweli,yaani watu watoke jasho kwaajili ya mzembe kama huyu,ole wake nimuone leo ni mikwaju kwa kwenda mbele!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom