mchajikobe
JF-Expert Member
- Aug 14, 2009
- 2,652
- 1,237
Habari zenu ndugu wana JF,leo hapa jamvini kuna kitu nataka kuwajuza,kwa wale watumiao barabara ya Ali Hassan Mwinyi na ile ya umoja wa mataifa pale karibu na trafic lights za Salender kuna omba omba mmoja mimi binafsi naamini anastahili viboko ili aache utani na awaombao.Huyu ombaomba ni mvulana ambaye amekuwa pale kwa miaka mingi kidogo akijitafutia ridhiki,lakini kinachonisababisha nimtafutie bakora ni kwamba hana ubunifu na kazi yake,huyu jamaa ana kidonda kikubwa sana mguuni na hicho ndicho kimpatiacho ridhiki,kinachonishangaza kwa huyu bwana ni kwamba kila siku anaomba hela ya kwenda kujitibu,lakini kila mwaka kidonda kiko vilevile na hakikauki,sijui kama ni kidonda kweli au ni sanaa,maana kwa mtu wa kawaida ukiwa na kidonda kama kile huwezi fika miezi miwili bila kukatwa huo mguu!Nimetafakari kwa kina nikaona huyu jamaa anatutania sisi ombwaombwa,ile inaweza ikawa ni sanaa,sababu mtu gani hahisi hata maumivu,wala kidonda hakiongezeki wala kupungua?Huyu mimi naona anastahili viboko ili aache ujinga wake huo!!