Olympiki - Target 2012 - Medali 20

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,474
39,987
Ufuatao ni mpango wa ushindi baada ya kuona Watanzania hatuna lengo la kufanya vizuri na tumekuwa wasindikizaji kila olympiki na tumebakia kukumbukia ushindi wa 1980.

NADHARIA INAAYOONGOZA:
Kwa Taifa lolote kuweza kuchukua nafasi yake katika ulimwengu wa siasa na kiuchumi, Taifa hilo halina budi pia kuonesha kuwa lina nguvu na uwezo katika michezo. Ni michezo ambayo ndiyo siasa ya kweli inaonekana na ni siasa ya urafiki zaidi kuliko uadui. Ni kwa sababu hiyo utaonaa nchi kama Marekani, Urusi, Uingereza, China, Ujerumani, Australia na Ufaransa wanafanya jitihada kubwa sana kujiandaa kwa michezo hususan Olympic kwa sababu wanaamini it is the biggest political venue ya kuonesha mafanikio yao ya kiuchumi, kisiasa na kijamii. Tanzania nayo ikitaka kuonesha kweli imeanza kufanikiwa kiuchumi na kijamii haina budi kuonesha hilo kupitia kwenye michezo.

LENGO: Kupata medali zisizopungua 20 kwenye Olympiki ya London 2012. Za rangi yoyote ile.

IDADI YA WANARIADHA: Kuanzia sasa tutaandaa wanariadha wapatao wasiopungua 100 katika sekta zote kubwa za michezo, Soka, riadha, Uogeleaji, riadha na michezo mingine. Kati ya hao timu yetu itaundwa na wanariadha 50. Itaitwa Timu ya Ushindi (Victory Team)

MIKAKATI:

  • 0. Kuunda Kamati ya Ushindi ambayo itasimamia maandalizi haya ya Olympiki. Kamati hiyo itaundwa na watu wote ambao hawajawahi kusimamia maandalizi ya Olympiki kabla! Iundwe na wataalamu wa chakula, wataalamu wa afya, wanamichezo, conditional pyschologists, na iwekwe chini ya mtaalamu wa riadha kutoka China. Huyo Mchina na timu ya wasaidizi wapewe uwezo wote wa kusaka, kutambua, na kukusanya vipaji vya vijana wa Kitanzania na itakapofika 2010 awe tayari na timu ya vijana wasiopungua 100 kuwaandaa kwa Olympiki.

  • 1. Kuanza kusaka vipaji vya wanamichezo kuanzia wenye umri wa miaka 12 sasahivi hadi wenye miaka 16 sasa hivi ili ifikapo 2010 wale wenye miaka 12 watakuwa na miaka 16 ambao ni umri wa chini wa kushiriki Olympiki na wale wenye miaka 16 sasa hivi watakuwa na miaka 20. Lengo letu ni kupeleka timu ya vijana zaidi katika Olympiki. Kwenye timu yetu ya Ushindi mwenye miaka 21 ndiyo atakuwa "mzee" kwenye timu hiyo.

  • Katika hili jitihada ya pekee ifanywe pia ya kuwahusisha Watanzania wanaoishi nje ya nchi hasa nchi zenye vifaa na zana za kisasa za ushindani kama Marekani, Uingereza, Ujerumani n.k na kuwaambia kuwa kama wana watoto wao walio kati ya umri huo hapo juu watoto hao wanaweza kushiriki timu ya Taifa ya Tanzania endapo wataandikishwa na watakuwa tayari kushiriki mashindano ya Tanzania. Msisitizo upewe kwa Watanzania pia watakaokuwa katika vyuo vikuu mbalimbali vya Marekani kuwa wajihusishe na michezo katika vyuo hivyo na watapata nafasi ya kushirki mashindano ya TAnzania ya Taifa kupata timu kwa kadiri ya kipengele cha 2 hapo juu.

  • 2. Miaka hii miwili ya mwanzo kuwa na mashindano ya michezo kila mwezi katika wilaya na mikoa mbalimbali ya kutafuta vipaji. Kuanzia kwenye mashule ya msingi, mitaani n.k Mashindano ya wilaya ya riadha, mashindano ya kijiji ya riadha ili kuibua vipaji mbalimbali. Haya mambo ya kupoteza muda na "umiss wherever" na kucheza "chandimu" peke yake yaanze kuzaa matunda kwani hakuna Olympiki ya urembo! Vijana wetu waanze kutiwa moyo kuwa na wao wanaweza kuwa wanariadha maarufu zaidi duniani kupitia mashindano ya Olympiki.

  • 3. Ndani ya mwaka mmoja wa maandalizi (2008/2009) tushiriki mashindano ya dunia ya riadha na tuhakikishe vijana wetu wanafanya vizuri huko. Wakianza kupata ile fedha ya ushindi (kwenye mashindano ya dunia mita mia moja mshindi anapata karibu dola milioni moja!). Itaanza kuchochea wengine kuelekea 2009/2010.

  • 4. Ili kuweza kufanikisha hilo la (3) hapo juu Serikali (ya Muungano na ya Zanzibar) zitenge kiuiwiano Shs. Bilioni moja kila mwaka kwa ajili ya kujiandaa kwa Olympiki kila mwaka. Kwa hiyo hizo bilioni moja za mwaka huu zitumike kuandaa ofisi, makazi ya makocha, na vitendea kazi vya mwanzo vya "Kamati ya Ushindi na kuandaa mchakato wa awali wa kusaka vipaji na kuanza kuviendeleza mikoani.

  • 5. Mojawapo ya michezo ambayo tunattaka kuushangaza ulimwengu ni kuogelea. Huu ni mchezo ambao naamini tuna nafasi kubwa zaidi kuliko nchi nyingi za kiafrika. Tukiwa tumezungukwa na maziwa makubwa matatu na bahari ya Hindi kuogelea kuko ndani ya damu yetu. Hivyo, tujenge vituo viwili ifikapo 2010 Tanzania National Aquatic Centers. Lengo la vitu hivyo ni kuwapa watoto na vijana na mtu mwingine yoyote nafasi ya kuogelea kitaalamu. Lakini msisitizo mkubwa ni vituo hivyo kutumika kama sehemu za mashindano ya kuogelea. Vituo viwe ni vya kiwango cha Olympiki. Nani tumuombe ajenge kwa fedha zetu wenyewe, you guessed it China. Ifikapo 2010 tuandae mashindano ya kwanza ya Kimataifa ya Afrika ya Kuogelea tunaweza kuyaita TanzaniaaOpen Swimming Competition; na kwa mbwembwe zetu tunatangaza mshindi wa kwanza kupata medali ya Tanzanite!! or something of sort!

  • 6. Ifikapo 2010, kambi ya Olympiki itengenezwe na mchuo ufanyike hadi kufikia kiwango cha kuwa na wachezaji 50 tu ambao wote wawe wawe wamefikia kiwango cha olympiki. Vijana hao 50 na labda 20 ambao ni substitutes ndio wataunda timu ya Olympiki ya Taifa kuelekea London 2010. Watakuwa kwenye kambi ya eneo moja, kama walikuwa kwenye shule nyingine watahamia karibu na kambi hiyo kwa gharama za serikali. Nidhamu itakuwa ni msingi wa ushindi, na uzalendo kwa Taifa iwe ni chachu ya wao kujituma.

  • 7. Ifikapo 2011, timu yetu lazima iwe inashikilia rekodi kadhaa za dunia katika maeneo mbalimbali na hivyo tunapojiandaa kwenda Olympiki 2012 jina la Tanzania linatangulia kuwa ni "washindi wa dunia". Mashindano ya Taifa ya 2011 yatakuwa ni pamoja na kuwaleta wale vijana wa Kitanzania walioko nje kwa mujibu wa kipengele (cha pili) ambao watashinda kupata tiketi ya kushiriki Olympiki na kambi ya Taifa ya Olympiki of a Unified Team itawekwa rasmi. Kabla ya mashindano ya 2012, timu hiyo ya Olympiki ipewe ofa ya nguvu kutembelea sehemu mbalimbali duniani kwa mapumziko ya angalau wiki mbili kuwashukuru kwa muda wote wa kujiandaa na olympiki na wanaporudi wanakuwa kwenye "Lock Down" hadi Olympiki iishe.

  • 8. Timu ya Tanzania ikiwa na wanaridha 50 na rekodi kadhaa za dunia itapita mbele ya jukwaa la wageni siku ya ufunguzi kama tishio la ushindi. Mashindano ya kwanza ya kuogelea, Michael Phelps anaangushwa na kijana wa Kitanzania na kumnyang'anya dhahabu yake ya kwanza kwenye Relay! Tanzania itakuwa imefika.

  • 9. Mwisho wa Olympiki London Tanzania ni nchi ya Afrika iliyofanya vizuri zaidi kwenye Olympiki na kwenye dunia ikiwa ni miongoni mwa nchi 10 bora. Wakati huo mtajua hatukushinda kwa bahati!!!

Yote haya yatawezekana endapo tu kuna NIA na UAMUZI wa makusudi wa KISIASA YA KUFANYA VIZURI KATIKA MICHEZO. Hadi pale wanasiasa wetu watakapoona haja ya kuinua Tanzania katika michezo ndipo tutaweza kufanya vizuri. Lakini kwa kadiri wanavyosubiri watu wafanye vizuri ndio watoe pongezi ndivyo watakavyoendelea kusubiri kuvuna wasichopanda! Vinginevyo wataendelea kusubiri kulia kivulini bila kuchumia juani.
 
Mzee, nashauri ufanye sum-up baada ya mjadala wa wanajamvi na kumtumia Mhe. waziri wa michezo na baraza la michezo. wasipotekeleza tutawashitaki kwa uzembe. Eti hata hiyo michezo ya kulenga shabaha kwa kutumia upinde na mshale hatuwezi? mbona huo ndo utamaduni wetu! Pia wajeshi wetu bila shaka wanashabaha za kutosha kutumia bunduki. naamini kuwa tunaweza kufanya vizuri katika
1. Riadha
2. Kulenga shabaha kwa upinde na mishale
3. Kulenga shabaha kwa bunduki

Big up Mwanakijiji.
 
Some lofty goals for a starving nation with a low Per Capita GDP, rampant illiteracy and a host of other priorities.
 
Mimi nimeweka pa kuanzia tu, tuchangia halafu nitaunganisha mawazo na kuyatoa kama special proposal ya kutaka ushindi maana haya ya kuombea tu kushinda bila kujiandaa kushinda ni ushirikina!!
 
Some lofty goals for a starving nation with a low Per Capita GDP, rampant illiteracy and a host of other priorities.


Ukiangalia vitu katika upana wake utaona matokeo yake ni makubwa zaidi. Tusipotamani kufanya makubwa kwa nafsi zetu, hata madogo hatuwezi. It is about prestige, it is about confidence, and it is about determination. Kama huwezi hata kufanya vizuri kwenye michezo what are you good at? Kama unahishindwa hata kuandaa timu ya kurusha mishale, utaweza kurusha setilaiti?

Ukiangalia pendekezo la Bilioni moja kwa mwaka ni chenji tu ukilinganisha na fedha zinazokwiba na kupotea kila mwaka toka serikali kuu na serikali za mitaa. It could be lofty goals but at least they are goals we can attain if we put our collective mind and pour our resources.
 
Mimi nimeweka pa kuanzia tu, tuchangia halafu nitaunganisha mawazo na kuyatoa kama special proposal ya kutaka ushindi maana haya ya kuombea tu kushinda bila kujiandaa kushinda ni ushirikina!!

Oyaaa...kipi muhimu madawati shuleni, chakula na lishe nzuri, au medali za olimpiki?
 
Oyaaa...kipi muhimu madawati shuleni, chakula na lishe nzuri, au medali za olimpiki?

so far hayo madawati shuleni yapo, chakula na lishe nzuri vipo? Kuna kitu gani kinaitangaza nchi zaidi ya Olympiki? Hivi Jamaica imepata matangazo ya bure kiasi gani kuliko Olympiki? Angalia hata Tunisia juzi walivyomuadhiri mtu hata asiyejua Tunisia iko wapi alijua. SIangalii kama suala la michezo tu naliangalia kama suala la mkakati wa kujitambulisha katika ulimwengu. Mkisha shinda mashindano ya dunia na kufanya upsets 2009, 2010, na 2011 vyombo vya habari vya dunia vitaanza kuangalia Tanzani kwa mwanga mpya na mnapowaambia watu waje kutembelea nchi ya Tanzania hamsemi "the land of Kilimanjaro and Zanzibar" bali mnaweka picha ya Bingwa wa Dunia wa Riadha, Mvunja Rekodi ya Dunia n.k it is bigger than sports my friends...

Hapo utaona madawati, chakula na lishe vinavyoingiliana kwa uzuri kabisa.
 
so far hayo madawati shuleni yapo, chakula na lishe nzuri vipo? Kuna kitu gani kinaitangaza nchi zaidi ya Olympiki? Hivi Jamaica imepata matangazo ya bure kiasi gani kuliko Olympiki? Angalia hata Tunisia juzi walivyomuadhiri mtu hata asiyejua Tunisia iko wapi alijua. SIangalii kama suala la michezo tu naliangalia kama suala la mkakati wa kujitambulisha katika ulimwengu. Mkisha shinda mashindano ya dunia na kufanya upsets 2009, 2010, na 2011 vyombo vya habari vya dunia vitaanza kuangalia Tanzani kwa mwanga mpya na mnapowaambia watu waje kutembelea nchi ya Tanzania hamsemi "the land of Kilimanjaro and Zanzibar" bali mnaweka picha ya Bingwa wa Dunia wa Riadha, Mvunja Rekodi ya Dunia n.k it is bigger than sports my friends...

Hapo utaona madawati, chakula na lishe vinavyoingiliana kwa uzuri kabisa.

Saa ingine Mwanakijiji sijui huwaga unafikiriaga nini tu kichwani mwako...nakumbuka uliwaka sana kuhusu mambo ya priorities pale Lowassa alipochangisha millioni 400 baada ya Stars kushinda kamechi kamoja. Ukahoji sana kuhusu vipaumbele vyetu. Sasa leo unaleta mikakati ya kushinda medali 2012 huko London......sidhani kama suala ni kutangaza Tanzania, suala ni maisha bora, period.
 
Saa ingine Mwanakijiji sijui huwaga unafikiriaga nini tu kichwani mwako...nakumbuka uliwaka sana kuhusu mambo ya priorities pale Lowassa alipochangisha millioni 400 baada ya Stars kushinda kamechi kamoja. Ukahoji sana kuhusu vipaumbele vyetu. Sasa leo unaleta mikakati ya kushinda medali 2016 huko London......sidhani kama swala ni kutangaza Tanzania, swala ni maisha bora, period.

Nyani, wakati mwingine nafikiri kitu kinachowezekana. Walipochangia milioni 400 nilipinga kwa sababu walijaribu kuvuna wasichopanda. Kushinda kule kulikuwa kwa bahati na si matokeo ya maandalizi. Ilikuwa ni kupoteza fedha. Ushindi ambao ninauzungumzia mimi ni ushindi ambao ni bora zaidi kuliko milioni 400.

Sasa tukisema tujiandae kwa bilioni 1 kila mwaka kwa michezo tunachofanya siyo kuwapa wachezaji, kwanza tunatengeneza ajira mpya, walimu, taasisi, ujenzi wa vifaa n.k hivyo tunatengeneza maisha badala ya kumwaga milioni 400 kwa timu isiyoshinda.

Unapowekeza kwenye michezo unawekeza kwenye mafanikio ya kiuchumi. Michezo isionekane kama anasa bali ajira ya kweli ambayo inaweza kuinua maisha ya maelfu ya vijana nchini. Hebu fikiria tukiandaa timu ya Basketball na ikafanya vizuri Olympiki na vijana wetu kuonekana kupendwa na kupewa mwaliko wa kucheza NBA au European leagues hatutakuwa tumeinua maisha yao? Na wao wakifanikiwa kwenye league hizo na wakarudi nyumbani na kukarabati vishule vyao vya awali au hospitali huoni ni worthy investment kama anavyofanya Dikembe Mutombo?

Hivi tukitoa mshindi wa dunia wa mbio fupi, na huyo bwana anapohojiwa na kutangaza Tanzania hauoni faida ya kiuchumi inayotokea. Ninachokipinga mimi hata sasa hivi nitakipinga ni hii tabia ya kupenda kushangalia tusichofanyia kazi na kufurahia ushindi tusiofanyia kazi.

Sisi ni mabingwa wa kusherehekea tusivyofanyia kazi. Leo hii ukisikia Mtanzani amapeta medali ya dhahabu hata CCM watashangalia kuwa ni matunda ya sera zake. Nakumbuka jinsi watu walivyoshangalia BB Richard aliposhinda na ikawa kama Tanzania imeshinda katika mashindano ya kijinga.

Lakini mashindano ya Olympiki is bigger than mechi moja ya kuifunga Togo na hakuna mtu mwingine yoyote duniani. Ukikumbuka criticism yangu ilikuwa based na kuona huwezi kutumia milioni 400 kuchangia timu iliyoandaliwa kushindwa wakati unavijana wanaosota Ukraine. Hata juzi (literally) serikali imetuambia vijana wanne wa kitanzania wamepewa scholarship ya kusoma Harvard kwa doal laki 6! Kiasi hicho kingeweza kuwasomesha vijana wale wa Ukraine wote 29 kwa miaka minne! Huko ni kutokuwa na Kipaumbele.
 
MMKJJ,

Kazi nzuri, lakini nasikitika kwasababu watawala wetu wa sasa hawaangalii mipango ya 2012 bali 2010 (Uchaguzi Mkuu!). Malengo yao kwa sasa ni kutimiza zile "ahadi" za 2005 kabla ya 2010.

Sasa hivi mipango yao yote ni "fast-track" ili watuonyeshe wananchi kabla ya 2010. Hawataki mpango mwingine wowote wa kuvuka hapo 2010!
 
Mheshimiwa Rais JK akifungua Bunge jipya, 30 Desemba 2005 alisema:

Tutaviwezesha vyama mbalimbali vya michezo ili Tanzania iweze kuwa mshiriki mzuri, na siyo kuwa msindikizaji, katika mashindano mbalimbali ya michezo ulimwenguni. Pamoja na hayo nitaanzisha mjadala wa kitaifa wa kuendeleza michezo nchini.

Leo hii ni kipindi cha miaka 3 tangu Rais kutoa kauri hiyo, yaani pamoja na mipango ya serikali na "support" ya Rais bado Tanzania imefanikiwa kupeleka wanamichezo 10 tu kwenye michezo ya Olimpiki! Sitaki kukumbushia mabondia wetu waliokwenda huko Madagascar, wala ushiriki wetu wa katika soka!
 
Think Big, asante kwa nukuu hiyo; tatizo letu hasa viongozi wetu ni kufikiria "in the now". Leo hii tunazungumzia mafuta katika pwani yetu, je tumejiandaa kuyalinda? Hivi leo wakianza kutengeneza rigs za mafuta bahari ya hindi nani atalinda? Jeshi la POlisi lina nyenzo za kulinda intallments za aina hiyo?

Michezo ndiyo njia nyepesi, rahisi, na kubwa zaidi ya Taifa kujitangaza na kujitutumua. Hivi Kenya inajulikana zaidi kwa kitu gani? NI wana michezo wake ndio waliofungulia sana utalii nchini humo siyo nguvu za kiuchumi. Sisi Tanzania hatutaki ukubwa na hatuna hamu ya ukuu, we are just for the bare minimums!
 
Mwanakijiji,

Huwezi kushinda medali 20 toka zero kwa maandalizi ya miaka minne, hiyo sahau kabisa.

Lazima turudi kwenye basics kwa kurudisha michezo kwenye shule za msingi na mashindano yote kama ilivyokuwa zamani.

Labda aim iwe mwaka 2016. Kwasasa tunaweza kupata medali mbili au tatu lakini sio ishirini.

Pia michezo ambayo sisi tunashiriki ina upinzani mkubwa sana, labda tuanze na sisi kuogelea, kuendesha baiskeli nk.

Waingereza nimeona medali moja inawagharimu pounds 2.8 milioni, kwenye riadha medali moja ni zaidi ya pounds milioni tano. Lazima tu invest kwenye michezo kuanzia chini. Na baada ya hapo mashule, vyuo na majeshi yetu wawe na fungu maalumu la michezo. Lakini je mafisadi watashindwa kuzinyofoa zote?

Jambo lingine la kuangalia ni kwamba sehemu kubwa ya washindi kwa wenzetu ni wanafunzi wa vyuo vikuu au waliwahi kuwa wanafunzi wa vyuo vikuu labda ukiachia riadha. Sababu kubwa ni kwamba hao ndio wanaweza kuwa na facilities pamoja na walimu wa kutosha. Kwasisi wanariadha wetu wengi walikuwa ni polisi ama jeshi kwasababu huko ndiko wana facilities na muda. Labda tuwape wanajeshi pesa zaidi na kuwe na kitengo cha michezo. Je mlimani pamoja na kuwa na degree ya michezo, tuna hata mwanamichezo yeyote wa maana?

Tunakokwenda itakuwa ngumu sana kwa nchi za Afrika kushinda. medali siku hizi zinaendana na pesa na wala sio uwezo tu kama ilivyokuwa zamani.
 
Mwanakijiji,

Huwezi kushinda medali 20 toka zero kwa maandalizi ya miaka minne, hiyo sahau kabisa.

Lazima turudi kwenye basics kwa kurudisha michezo kwenye shule za msingi na mashindano yote kama ilivyokuwa zamani.

Labda aim iwe mwaka 2016. Kwasasa tunaweza kupata medali mbili au tatu lakini sio ishirini.

Pia michezo ambayo sisi tunashiriki ina upinzani mkubwa sana, labda tuanze na sisi kuogelea, kuendesha baiskeli nk.

Waingereza nimeona medali moja inawagharimu pounds 2.8 milioni, kwenye riadha medali moja ni zaidi ya pounds milioni tano. Lazima tu invest kwenye michezo kuanzia chini. Na baada ya hapo mashule, vyuo na majeshi yetu wawe na fungu maalumu la michezo. Lakini je mafisadi watashindwa kuzinyofoa zote?

Jambo lingine la kuangalia ni kwamba sehemu kubwa ya washindi kwa wenzetu ni wanafunzi wa vyuo vikuu au waliwahi kuwa wanafunzi wa vyuo vikuu labda ukiachia riadha. Sababu kubwa ni kwamba hao ndio wanaweza kuwa na facilities pamoja na walimu wa kutosha. Kwasisi wanariadha wetu wengi walikuwa ni polisi ama jeshi kwasababu huko ndiko wana facilities na muda. Labda tuwape wanajeshi pesa zaidi na kuwe na kitengo cha michezo. Je mlimani pamoja na kuwa na degree ya michezo, tuna hata mwanamichezo yeyote wa maana?

Tunakokwenda itakuwa ngumu sana kwa nchi za Afrika kushinda. medali siku hizi zinaendana na pesa na wala sio uwezo tu kama ilivyokuwa zamani.


Nimekupata vizuri kabisa Mtanzania. Binafsi maneno haya ya kutoweza kwa kweli hayaniingii, sisi hatuwezi kwa sababu hatutaki kuweza. Tunaweza kufanya lolote lile ambalo tumekusudia na kudhamiria kweli. Kama tukitaka kupata medali zisisopungua 20 kwenye 2012 Olympiki tutaweza kufanya hivyo. Kama italazimu kufanya hivyo kwa kupitia mashule n.k then lets do it; Kama inamaana itabidi tujenge facilities za kusaidia wanariadha wetu, lets do it. Naamini katika kuweza ...
 
I still think, if you put all this in the context of cost benefit analysis, and remove the intangibles (prestige and all that fluff, prestige my foot...) the funds required to prepare a big gamble in the Olympics can be used to realize a sure win with some badly needed social services.

If we do not participate in the Olympics nobody will die as a direct consequence, some officials may not get their per diems and some shoppings, but thats about it.

If we do not have the right equipment to diagnose breast cancer early, some women will surely die.

We have to learn to do without some things, which would you choose, the Olympics or some basic social services?

I know with the Olympics it is a gamble even with the required investment, the same cannot be said for social services.
 
Mwanakijiji,

Huwezi kushinda medali 20 toka zero kwa maandalizi ya miaka minne, hiyo sahau kabisa.

Lazima turudi kwenye basics kwa kurudisha michezo kwenye shule za msingi na mashindano yote kama ilivyokuwa zamani.

Labda aim iwe mwaka 2016. Kwasasa tunaweza kupata medali mbili au tatu lakini sio ishirini.

Pia michezo ambayo sisi tunashiriki ina upinzani mkubwa sana, labda tuanze na sisi kuogelea, kuendesha baiskeli nk.

Waingereza nimeona medali moja inawagharimu pounds 2.8 milioni, kwenye riadha medali moja ni zaidi ya pounds milioni tano. Lazima tu invest kwenye michezo kuanzia chini. Na baada ya hapo mashule, vyuo na majeshi yetu wawe na fungu maalumu la michezo. Lakini je mafisadi watashindwa kuzinyofoa zote?

Jambo lingine la kuangalia ni kwamba sehemu kubwa ya washindi kwa wenzetu ni wanafunzi wa vyuo vikuu au waliwahi kuwa wanafunzi wa vyuo vikuu labda ukiachia riadha. Sababu kubwa ni kwamba hao ndio wanaweza kuwa na facilities pamoja na walimu wa kutosha. Kwasisi wanariadha wetu wengi walikuwa ni polisi ama jeshi kwasababu huko ndiko wana facilities na muda. Labda tuwape wanajeshi pesa zaidi na kuwe na kitengo cha michezo. Je mlimani pamoja na kuwa na degree ya michezo, tuna hata mwanamichezo yeyote wa maana?

Tunakokwenda itakuwa ngumu sana kwa nchi za Afrika kushinda. medali siku hizi zinaendana na pesa na wala sio uwezo tu kama ilivyokuwa zamani.

kurudisha michezo kwenye shule za msingi na mashindano yote kama ilivyokuwa zamani

Huwezi kurudisha michezo kwenye shule za msingi zisizowepo, zilizopo ambazo hazina walimu, zenye walimu ambao hawalipwi mishahara na wanataka kugoma etc etc.Inabidi uende na the basics kwanza, kabla ya kuwa na ambitions za kuwa na shule zenye gymnasiums kwanza tuna walimu? Walimu wanajua kufundisha mambo ya gymnastics au P.E? Isije ikawa mambo ya Kikwete kufungua shule bila walimu.

Waingereza nimeona medali moja inawagharimu pounds 2.8 milioni, kwenye riadha medali moja ni zaidi ya pounds milioni tano

Haya tunaona figures zenyewe zinakabilia point something something ya GDP, halafu tunataka ku gamble kwenye Olympic ambako we can very well not perform, na hata kama tuki perform jamani is it worth that much to us? Kweli tunaweza ku justify kutumia hela hizi sie masikini? Au kuiga tembo kunya tu?

Jambo lingine la kuangalia ni kwamba sehemu kubwa ya washindi kwa wenzetu ni wanafunzi wa vyuo vikuu au waliwahi kuwa wanafunzi wa vyuo vikuu

Narudi kule kule, huwezi kuwa na michezo vyuo vikuu kama huna vyuo vikuu, au una vyuo vikuu visivyo na facilities.Wazo la kuendeleza facilities za vyuo vikuu ni muhimu, lakini vipi kama tukiwa na uchaguzi wa maabara/ vitabu/mishahara ya walimu on one hand na michezo on the other?

We have a long way to go and any unrealistic, utopian, however ambitious, lofty goals must not be more to the detriment of our development than they are worth.

Tuliambiwa inabidi tukimbie wakati wengine wanasimama, kikimbia ni pamoja na ku sacrifice Olympic, hakuna Olympic mpaka tuwe na GDP Per ya angalau $ 3,000.
 
Topic nzuri lakini ipelekwe kwenye MICHEZO.

Kwa kweli itasaidia tatizo la ajira angalau kwa asilimia moja!

Safi sana Mwanakijiji
 
Mimi nadhani kuna vitu vya muhimu na pressing zaidi ya kujiandaa na kushinda medali London. Kuna wagonjwa wanalala chini Muhimbili pale. Hiyo mihela itakayotumika kuandaa wanamichezo wa olimpiki ni bora ielekezwe kwenye vitu muhimu vinavyohusu maisha ya watu. Kuna wazee wa EAC ambao mpaka leo bado hawajalipwa mafao yao. Ninaweza kujaza mikurasa kibao na mambo ambayo tunabidi kufanya. Pia sipingi kuwa na wanamichezo waliopata maandalizi mazuri lakini inabidi tuangalie na kupima kipi ni cha muhimu zaidi. Na kama tunaweza kutenga mihela mingi kwenye maandalizi ya kushinda medali kwenye olimpiki basi pia tunaweza kuondokana na kero za maisha zinazotusumbua kila siku!!!
 
Back
Top Bottom