Saguda47
JF-Expert Member
- May 1, 2016
- 10,766
- 18,620
Taifa limepata msiba mkubwa Sana, limepoteza mkuu wa nchi, amirijeshi mkuu, mkuu wa serikali na mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi!
Kama ilivyo kawaida wa wanadamu, tupo tunaohuzunishwa na ukomo wa maisha yake hapa duniani, wapo pia waliongojea kifo chake Kama siku ya furaha, wengine wanajitokeza hadharani na kudai bado wanakesha baani wakilewa na kufurahisha nafsi zao.
Tunamhukumu Sana John Pombe tukimnyooshea vidole kuwa alikuwa muovu na mtenda mabaya dhidi ya wengine.
Tunasahau kuwa hata sisi hatuishi vizuri na majirani, ndugu na hata familia zetu.
John Magufuli amelala milele, na wengine tunaamini maisha yetu yatakuwa marefu na tutafurahi Sana hapa duniani. Ila hatujui lolote ambalo Mwenyezi Mungu aliamua katika sekunde ya mwisho ya kupokea roho ya Magufuli.
Inawezekana Mungu anatutizama kwa huruma sana tunaoendelea kufurahishwa na kifo Cha huyu mtu tunayeamini alitunyima maisha Bora na raha.
Ndugu zangu! Sisi Ni wadhambi sana, hatuna tofauti na wale tunaosherehekea mauti yao, hatujui Ni lini tutaitwa hukumuni, hatujui tutakuwa baani tukila na kunywa! Mwisho wetu utakuwaje?
Kama Mungu Muumbaji alivyonena ya kuwa tumetokana na mavumbi, hakika mavumbini tutarejea!
Mungu atupe hekima na busara, tuache kuhukumu ambao tayari Bwana ameshahukumu tayari!
Pumzika unapostahili Ndugu John Pombe Magufuli, mema yako yatalinufaisha taifa, nasi tu karibu kuingia hukumuni mwa Bwana.
Kama ilivyo kawaida wa wanadamu, tupo tunaohuzunishwa na ukomo wa maisha yake hapa duniani, wapo pia waliongojea kifo chake Kama siku ya furaha, wengine wanajitokeza hadharani na kudai bado wanakesha baani wakilewa na kufurahisha nafsi zao.
Tunamhukumu Sana John Pombe tukimnyooshea vidole kuwa alikuwa muovu na mtenda mabaya dhidi ya wengine.
Tunasahau kuwa hata sisi hatuishi vizuri na majirani, ndugu na hata familia zetu.
John Magufuli amelala milele, na wengine tunaamini maisha yetu yatakuwa marefu na tutafurahi Sana hapa duniani. Ila hatujui lolote ambalo Mwenyezi Mungu aliamua katika sekunde ya mwisho ya kupokea roho ya Magufuli.
Inawezekana Mungu anatutizama kwa huruma sana tunaoendelea kufurahishwa na kifo Cha huyu mtu tunayeamini alitunyima maisha Bora na raha.
Ndugu zangu! Sisi Ni wadhambi sana, hatuna tofauti na wale tunaosherehekea mauti yao, hatujui Ni lini tutaitwa hukumuni, hatujui tutakuwa baani tukila na kunywa! Mwisho wetu utakuwaje?
Kama Mungu Muumbaji alivyonena ya kuwa tumetokana na mavumbi, hakika mavumbini tutarejea!
Mungu atupe hekima na busara, tuache kuhukumu ambao tayari Bwana ameshahukumu tayari!
Pumzika unapostahili Ndugu John Pombe Magufuli, mema yako yatalinufaisha taifa, nasi tu karibu kuingia hukumuni mwa Bwana.