Ole wenu CHADEMA!

Mkandara

JF-Expert Member
Mar 3, 2006
15,772
8,958
CCM kumbomoa Mbowe

• Wadai watatumia mbinu iliyommaliza Sumaye

Na Mwandishi Wetu

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimeanza mkakati wa siri wa kubomoa upinzani, na sasa imedhihirka kwamba mlengwa nambari wani ni Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe na chama chake.

Habari zilizoifikia Tanzania Daima zimeonyesha kwamba mkakati wa kumbomoa Mbowe ulianza kusukwa rasmi tangu Novemba mwaka jana, wakati wa kampeni za kugombea urais, baada ya Mbowe kuonyesha makali yake.

Katika uchaguzi huo, Mbowe alikuwa anagombea urais, na alipata nafasi ya tatu nyuma ya Jakaya Kikwete wa (CCM) na Profesa Ibrahim Lipumba wa Civic United Front (CUF).

Vyanzo vyetu ndani ya CCM, ambavyo havikutaka kutajwa majina, vimesema kwa nyakati tofauti kwamba kilichomponza Mbowe ni kauli aliyoitoa akiwa Mererani, mkoani Manyara, akimtuhumu mgombea wa CCM kupewa sh milioni 40 na wawekezaji wa mgodi wa TanzaniteOne, kwa ajili ya kampeni.

Katika mkutano wa Mbowe uliohudhuriwa kwa wingi na wachimbaji wa madini wa mgodini hapo, Mbowe alisema Jakaya Kikwete, aliyekuwa mgombea wa CCM, asingeweza kuwafanya lolote Wazungu wa TanzaniteOne - kama walivyokuwa wanataka wachimbaji - kwa kuwa mwekezaji huyo amechanga sh milioni 40 kwa ajili ya kampeni za CCM.

Mbowe aliwaomba wampe kura ili akiwa rais aweze kuangalia upya mikataba ya madini na hatima ya wachimbaji wazalendo.

Vyanzo vimesema kauli hiyo ilimzulia chuki isiyo ya kawaida miongoni mwa viongozi waandamizi ndani ya CCM, huku wengine wakijiapiza kwamba wakishapata madaraka, kazi yao ya kwanza ni kummaliza Mbowe.

"Sisi tulikuwa tunamwona Mbowe kuwa ni mstaarabu, hana siasa za kubomoana; lakini baada ya hapo tuliona ameanza mambo ya Mrema ya kulipua mabomu.sasa sisi tuko madarakani. Lazima atutambue," kilisema chanzo cha habari.

Kingine kilisema kauli hiyo imeharibu hata uhusiano mzuri uliokuwa unaonekana kuwapo kati yake na Rais Kikwete, kwani hivi sasa Rais Kikwete ni miongoni mwa watu 'wanaomchukia' mno Mbowe, na hawezi kumuachia afurukute. Wengine wamefika mahali pa kusema anamwogopa.

"Unajua hata sisi tumeshangaa. Mzee anamwogopa sana Mbowe.sijui imekuwaje, kwa sababu sisi wengine tunamwona Mbowe kama anatupa changamoto.lakini sasa tumefika mahali hata jina lake linatajwatajwa kwenye vikao vikubwa ndani ya chama chetu.wanamhofia," kilisema chanzo kingine.

Chanzo hicho kilitoa mfano kwamba hata katika hotuba yake kwenye vikao vikuu vya CCM mwezi uliopita, lilipokuwa linajadiliwa suala la mgawanyiko ndani ya CCM na hatima ya watu wanaojiita wanamtandao, baadhi ya viongozi waandamizi walifika mahali pa kumtaja Mbowe kwamba ndiye anayepandikiza dhana ya mgawanyiko ndani ya CCM.

Hata hivyo, msimamo huo umepingwa na baadhi ya wajumbe, wakisema CCM ikitaka kusimama imara isimsingizie Mbowe au kutafuta wachawi nje ya chama, bali ikubali kujikosoa.

Vyanzo vya habari vinasema macho ya watendaji wa CCM sasa yanaelekezwa kwa Mbowe kuliko kwa mwanasiasa yeyote wa upinzani, kwa kuwa ndiye anaonekana kuwa na hoja zenye mvuto mbele ya umma akilinganishwa na wapinzani wenzake.

Kinachosubiriwa sasa ni mabadiliko ya uongozi wa juu ndani ya CCM, ili waanze kujipanga namna ya kumbomoa, kwa kuwa kazi ilishapangwa.

"CCM mpya haitakuwa na simile juu ya Mbowe..nakuhakikishia, baada ya miaka minne CHADEMA haitakuwa ile ile, wala Mbowe hatatamba tena," kilisema chanzo kingine.

Kwa mujibu wa vyanzo hivyo, CCM inadhamiria kumbomoa Mbowe kisiasa na kibiashara kupitia njia mbalimbali za propaganda na kisheria, na kwa kutumia vyombo vya habari.

Uchunguzi unaonyesha kwamba hata sasa kazi hiyo imeanza, lakini inahitaji kuendelezwa kwa kasi hapo baadaye.

Chanzo kimoja kimedokeza kwamba watambomoa kwa mbinu ile ile waliyotumia kummaliza aliyekuwa Waziri Mkuu, Frederick Sumaye.

"Ngoja nikwambie. Unadhani kilichommaliza Sumaye ni nini? Propaganda.Alishughulikiwa mpaka ikafika mahali kila mtu ukimuuliza anasema Sumaye hafai, hata kama hana maelezo. Lakini si kwamba hafai.alishughulikiwa. Bila vyombo vya habari, leo angekuwa mtu tofauti. Kazi iliyopo sasa ni kushusha umaarufu wake kisiasa," kilisema chanzo.

Hata hivyo, baadhi ya wana CCM wanasema Mbowe ni mtu muhimu, kwa kuwa anatoa changamoto zinazowasukuma hata wao kufikiri mara mbili, na kwamba nyingine serikali iliyopo imezitumia kurekebisha kasoro zilizokuwapo. Wanasema kwamba kinachoogopwa kwa Mbowe ni uwezo wake wa kujenga hoja.

"Tofauti ya Mbowe na wenzake ni kwanza, anajua kujenga hoja. Ukimsikiliza utakubaliana naye. Pili, ndiye mwanasiasa ambaye umri unamruhusu kuweka mikakati ya muda mrefu. Halafu usisahau, hana njaa kama wengine hawa. Hatuwezi kumhonga au kumnunua Mbowe.njia rahisi ni kummaliza kisiasa," kilisema chanzo kingine.

Baadhi ya wana CCM wamekiri kwamba chuki dhidi ya Mbowe ilipandikizwa hata miongoni mwa wabunge tangu mwanzo, na ndiyo maana Mbunge wa CHADEMA wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe, alifanyiwa njama akashindwa kwenye uwakilishi wa Bunge la Afrika, Desemba mwaka jana.

"Kwa kuwasikiliza tu, Zitto alionyesha ni mpevu kuliko washindani wenzake. Lakini tulishaamua kumnyima, kwa sababu tuliona kumpa yeye ni kuikuza CHADEMA na Mbowe. Ile tulifanya kisiasa tu.lakini tulijua," kilisema chanzo kingine cha habari.

Habari zinasema kwamba huko nyuma, mbinu zilizotumika kuwamaliza wapinzani ni pamoja na kupenyeza watu wao ndani ya vyama vyao ili walete vurugu, jambo wanaloweza kulifanya kwa CHADEMA pia, ili viongozi na wanachama wagombane, wafukuzane.

Mbinu hiyo ilifanikisha kuimaliza makali NCCR - Mageuzi, kilichokuwa chama kikuu cha upinzani kati ya 1995 na 2000. Baada ya NCCR-Mageuzi kusambaratika kwa tofauti kati ya viongozi wakuu, viliibuka vyama vingine viwili; Tanzania Labour Party (TLP) na CUF, vikiwa vimevuna maelfu ya wanachama waliokuwa NCCR - Mageuzi.

Uongozi mbovu, dharau kutoka kwa jamii na migogoro isiyoisha imeimaliza TLP, huku CUF ikiathiriwa zaidi na propaganda kwamba ni chama cha kigaidi na cha Kiislamu, jambo ambalo limekifanya kihusishwe na baadhi ya matukio yasiyopendeza, kibaki na wanachama wale wale, au wapungue, kisikue zaidi.

Hata idadi ya kura kilizopata mwaka jana, ikilinganishwa na ya mwaka 2000, ukweli unaonyesha kwamba kimedumaa, hakikui.

Chama kinachoonekana kukua, hasa upande wa Bara, ni CHADEMA chini ya Mbowe, huku kikiwa na sera kuu mbili - ya majimbo na elimu - ambazo baada ya ufafanuzi wa Mbowe, zimekitofautisha na vyama vingine.

Mitaani, mwanasiasa anayezungumzwa sana kwa upande wa upinzani, huku akipewa nafasi ya kukua zaidi ni Mbowe.

Vyanzo vya habari vinasema CCM wamefanya utafiti, wamelijua hilo , na hawawezi kumwachia akashamiri, kwa sababu hawataki kusumbuliwa katika uchaguzi wa mwaka 2010.


Chanzo: http://www.freemedia.co.tz/daima/2006/06/11/habari1.php
 
kama kuna mtu anastahili kulaumiwa sana kwa kuvurunda upinzani ni Mbowe. Alikuwa na nafasi kubwa sana mwaka jana kuweza kunyakua viti vingi zaidi lakini akapoteza nafasi hiyo kwa kujaribu kugombea Urais ambao alikuwa ana uhakika asingeupata. Sifikiri kama CCM ina sababu yoyote ya kumbomoa.. nadhani ameishajibomoa mwenyewe!!!!
 
Hili gazeti lililoandika hii article lina utata kidogo, kwani linamilikiwa na baadhi ya viongozi wa CCM wasiokuwa Mtandao, kama uko bongo ukalifuatilia hili gazeti utagundua kuwa siku zote lina habari za ujanja ujanja,

CCM walikutana majuzi kuzungumzia mambo mawili, Independent Candidates na kundi la "MTANDAO" na matatizo yake kwa CCM in general kutokana na vita vikali ambavyo vimezuka ndani ya CCM na katika kikao hicho Mwandosya na Mama Nagu walimshukia vikali mzee JK na kikundi chake cha Mtandao, na JK pamoja na kuleta jeuri kidogo baadaye ilibidi atulie ili asaidiwe namna ya kupambana na Independent Candidates, ambapo aliambiwa kuwa solution ni bunge kuunda sheria mpya na kali against hii issue,

sasa linakuja hili gazeti na hadithi ambayo ni pure uongo! Freeman ni CCM anyway, na anashinda kila siku na kina Kingunge, JM, Chenge, Kinana, Msekwa, Sitta, Rostam, na wengineo wote, sasa kama huyu jamaa angekuwa ni upinzani pure no way hao wazee wa CCM wangekubali kuonekana naye hizo ni simple politics ambazo mtu huhitaji kuwa genius ili kuelewa, Mtandao walioshinda kwa kura 80% leo watakosa usingizi kwa kiongozi wa upinzani aliyepata kura chache kama Freeman! I mean haya ndio magazeti yanayohitaji kufungiwa na yale yote ya Mengi yote yanahitaji kufungiwa kwa kuwapotosha wananchi, JK aliyeinunua kila tool ya siasa wakati akiwa sio rais, leo ni rais, kesho uchaguzi utakapokuja atafanya nini, wakati ana all the powers kufanya analotaka akiwa na new tools za usalama na jeshi?

Off course wanaoandika katika hili gazeti ni marafiki pia wa Freeman, sasa sina uhakika nia na madhumuni yao hapa ni nini? Kuhusu uchaguzi wa mbunge wa EAC wa upinzani ulikuwa ni uamuzi wa JM baada ya viongozi wapya kujaribu kuchagua wakashindwa walimuendea mzee huyo na kumuomba awasaidie, akawaambia kuwa ni lazima wachague mbunge ambaye ni lame duck against CUF ambao ndio waliopaswa kupewa hiyo nafasi kwa kuwa na wabunge wengi bungeni, ili pia kupunguza ruzuku yao kwa mwezi kwani kuwa na huyo mbunge pia kunaongeza ruzuku ya chama anachotoka! CCM wakakubali na hakukuwa na lolote lingine ni uongo wa mchana,

Ninarudia tena kuwa haya ni moja ya magazeti huku yanayohitaji kufungiwa, Sumaye alijimaliza mwenyewe hakumalizwa na mtu yoyote ni wizi wake na tamaa ya mali za haraka haraka zilizomuua kisiasa, hata yule rais aliyempa uPM for ten years mwishoni alikuwa hataki hata kuonekana naye hadharani, na issue iliyommaliza zaidi ni ile ya NMB, kwani alienda mpaka kwa BM kuomba ajiuzulu akakataliwa way before ya uchaguzi wa Dodoma! Mtandao walimuua kisiasa Salim peke yake tena kwa njia chafu sana hiyo sio sir lakini sio Sumaye , yeye alijiua mwenyewe na ni mambo ya ajabu leo tunamsikia anapita huko chini chini akitoa hela zake chafu eti apewe umakamu wa CCM, wakati akiwa waziri mkuu aligombea hiyo nafasi na kupata kura yake mwenyewe, leo ni kitu gani atafanya tofauti!

Sumaye anapaswa kuelewa kuwa Mtandao walitumia hela nyingi sana kumsaidia JM kupita ubunge, nia na madhumuni ilikuwa aje amwaaachie EL nafasi hiyo mwakani, sasa huyu mjinga watu wanamlia hela zake bure! Mzee Sumaye ninajua kuwa unasoma humu kila siku acha ujinga mzee, fuga hao Ngombe wako, siasa waachie wenyewe!

Anyway my point ni kuwa hili gazeti na yale yote ya Mengi wakati umefika yanahitaji kufungwa!
 
Amani iwe kwako,

Namshukuru Kyoma kwa kunishawishi kujiunga na hili jukwaa la majadiliano ingawa bado sijawaza kujiunga na TEF kama asasi.

Nimeingia na kukutana mijadala moto!. Mzee Es, naomba kutofautiana na wewe moja kwa moja kuhusu hoja ulizozitoa.

Ila kwa kuwa hukunilenga, nitanyamaza watu waendelee na mjadala kwanza.

Nashukuru nimeikuta tena timu iliyokuwa BCStimes. Mkandara, naomba tuwasiliane.

JJ

www.chadema.net/blogu/mnyika/
 
Mzee JJ,

Kwanza heshima yako, halafu nafikiri unakumbuka nilikwambia nini kule BCs, Keenja na Sumaye watakuibia kura halafu bado ndugu yangu ninakukumbusha kuwa njoo una great skills politically, ila tu uko kwenye chama kibovu rudi nyumbani CCM tuanze kazi mpya bro!
 
Mzee ES: Nafikiri it is too simplistic kusema kuwa Mbowe ni CCM kwa kuwa ameonekana na baadhi ya wana ccm! Huo ni uchonganishi ambao ccm wamekuwa wakitumia kuanzisha vurugu katika vyama vya upinzani. Tunatarajia more hard facts kwenye forum hii!

It is also too simplistic kusema kuwa ccm hawaiogopi chadema kwa sababu tu ilipata kura chache katika uchaguzi. Nakumbuka wewe mwenyewe uliwahi kutuambia kule business times kuwa ccm hawadharau adui hata awe mdogo namna gani! Iweje leo waidharau chadema kwa sababu tu walipata kura kidogo. Na kama ccm hawaiogopi chadema ilikuwaje wakati wa kampeni kila kigogo wa ccm akiwemo Kingunge alikuwa hawezi kumaliza hotuba hadi ataje chadema na/au Mbowe? Hata JK kabla hajaanguka Jangwani alikuwa anaongelea sera za chadema na Mbowe! Hiyo ni propaganda.

Kwa sasa hivi kuna mambo mawili ambayo ni tishio kwa ccm. 1) kushindwa kukidhi matarajio ya watanzania kutokana na ahadi lukuki walizotoa-na kuna kila dalili kwamba watashindwa 2)umakini wa sera na uongozi wa chadema. Tuna habari za uhahakika kuwa hata hao wasio wanamtandao na wasiokubaliana na mambo ya JK wanafikiria kwenda chadema anytime mambo yasipobadilika. Pamoja na udhaifu wake chadema ndio chama pekee mbadala kwa ccm.

Kwa kiasi kikubwa naamini yaliyoandikwa kwenye hili gazeti maana hata JK alisema sio mara moja au mara mbili, kuwa chadema itakufa kama ilivyokufa nccr baada ya uchaguzi. Kwa nini sasa leo tusiamini kwamba kuna kitu kinaendelea dhidi ya chadema?

Mwisho, ni udekteta kufikiria kufungia magazeti kwa sababu tu yanaandika habari ambazo huzipendi! Hata mimi nakerwa na habari za IPPmedia maana zinaegemea upande mmoja, lakini hiyo hainifanyi nitamani kufungiwa kwao maana hawajavunja sheria, ni tabia yao tu ya kujipendekeza ambayo watanzania wengi tunayo, ila wengine hatujaionesha kwa sababu hatuna njia za kuonesha. Ni bora matamanio ya kufungia magazeti yangetoka kwa mtu mwingine sio kwa mtu kama wewe mwenye mamlaka katika chama kinachotawala na katika chombo cha kutunga sheria kama Bunge!

Otherwise, nakubaliana sana na michango yako na ya Bob Mkandara katika hoja zingine ulizotoa. Naona ule moto wa BCS umerudi. Tuombe hii nayo isiingiliwe.
 
Mwanakijiji,
Good questions. Good questions.
Mr. ES hata kama hii article si ya kweli kuna maswali ambayo ningependa kusikia comments zako. Kwanza ni zile $40 ambazo inasemekana AFGEM/Tanzanite one walimhonga Kikwete kwa ajili ya uchaguzi. Hili alilizungumzia Mbowe hadharani? Kama si kweli mbona hakuchukuliwa hatua zozote? Pili, hili swala la kupitiwa mikataba n.k haikuwa sera ya Kikwete na CCM.Ilikuwa sera ya Chadema. Tatu hao wanamtandao, nina hakika they are very uncomfotable na Freeman. Wao hawana sera. Wameshapata ulaji. Je huoni kuwa kwao wanamwona Freeman kuwa tishio? Kama si 2010 basi 2015
 
Inawezekana kwa mbinu ya kisiasa ya Mbowe! au kama ni kweli CCM wana huo mpango INASIKITISHA SANA NA HAWAITAKII MEMA NCHI YETU. MBOWE ANGALAU ALITOA CHANGAMOTO KATIKA KAMPENI. NA NI VIZURII CHADEMA KAMA CHAMA KIKAIMARIKA ILI CCM KIWEZE KUFANYA KAZI ZAKE KWA UMAKINI ZAIDI KWA FAIDA YA WANACHI NA SIYO YA VIONGOZI WACHACHE WEZI KAMA FORMER PM.

YOU CAN FOOL SOME PEOPLE FOR SOMETIME BUT YOO CANNOT CHEAT THEM AT ALL TIMES!
TUMEAMKA NA HUU MOTO WA FORUM UNAZIDI KUFANYA KAZI NZURI.
WAMEIBA WAMETAJIRIKA LAKINI BADO TU WANAENDELEA KUTAKA KUIBA NA SIYO KUTUONGOZA HADI LINI?

MIKATABA BOGUS WALIYOSAINI ITATUGHARIMU KWA MUDA MREFU SANA!!!
 
Jasusi,

Maswali mazuri. Hivi naibu waziri wa madini LM si nilisikia ana hisa au yumo kwenye bodi ya mojawapo ya kampuni za madini?!, naomba kupigwa shule, kama ni kweli, hii kujichunguza ndio nini?

Mzee Es, viongozi wengi wa upinzani wanatumiwa na CCM hiyo inajulikana, Lipumba alivyokuwa anajibizana na JK sikuamini siku walipokua wakichat na kucheka Bagamoyo kwenye mazishi. Siasa sio uhasama, tatizo wabongo wengi tunafikiria hivyo. Hiyo kuwepo pamoja sio tija. Na nadhani kiongozi wa kwanza CCM kuelewa kuwa siasa sio uhasama ni JK, nampongeza sana kwa hilo.
Ndio maana unamuona Mbowe na hao viongozi, maana Mbowe naye ni muelewa. Ila nitashangaa sana kama mtu ataprove kuwa Mbowe ni kibaraka wa CCM

FD
 
Hivi wabunge walipokula kiapo cha Ubunge walitumia katiba gani? Ya CCM au ya Nchi? Je waliapa kulinda Ilani ya Uchaguzi au Katiba? Kwanini kuna kutilia sana mkazo utii kwa chama kuliko kwa nchi?
 
J J Mnyika,
ndugu yetu karibu sana, huna haja ya kujiunga na TEF kama mwanachama wa TEF, sisi wote ni wachangiaji ktk kijiwe hiki. Kuna maswali tuliwauliza hatukujibiwa hadi leo na hii imetupa ugumu kuelewa nani ni nani ktk chama hiki zaidi ya ahadi zake. Na kuhusu kuwasiliana na dhani mwenzangu ndio uliingia mitini kabla ya uchaguzi na hukurudi tena hadi hii leo. E-mail yangu haijabadilika nadhani kuna mengi sana inabidi sio tu ujifunze toka humu ila ningependa uwatumie sana wanabodi hii kwa sababu wewe umebahatika kupata nafasi ndani ya lingo - Chadema..

Wanabodi,
Jamani msitegemee Mzee Es anaweza kuja na hoja inayopingana na maazimio ya chama chake. Kisha wambieni yeye ni CCM damu kwa hiyo msitegemee anaweza kuwa against ktk swala la chama chake isipokuwa anafanya kile ambacho kila mwanachama wa CCM angetakiwa kukifanya. Kama mmekwisha gundua Mzee Es huwasema watu binafsi ndani ya CCM ambao wanataka kuharibu jina la chama chake.

Kusema kweli maneno ya Free, hata kama yana ukweli kumbukeni kwamba JK hakuvunja sheria kupokea mchango wa TanzaniteOne. Ndivyo inavyokwenda inapofikia demokrasia kwa mtazamo wa nchi za magharibi labda tu kosa kubwa ni kwamba TanzaniteOne ni kampuni ya nje..lakini hii ndiyo sura halisi ya michango inayokubalika ikiwa tumechagua demokrasia kwa sura ya nchi za magharibi.

Kibaya zaidi ni kwamba mfumo huu kwa nchi kama Tanzania ni hatari kubwa sana kwa sababu haukupokelewa kama unavyokuja. Tumeongeza mila zetu ambazo hazihusiani kabisa na siasa. Sio utamaduni wetu kutoa fadhila kwa mategemeo ya kulipwa zaidi, isipokuwa sisi mtoaji kwa nafasi kama hizi huwa yule anayetafuta ushindi - Takrima kwa sura ya pili. Utayaona mambo kama haya ktk kuchumbia mke, Machief wetu enzi zao walipimwa fadhila na mapenzi yao kwa kile kinachotoka mifukoni mwao n.k. Yote haya ni ktk kutafuta ushindi.

Bahati mbaya tumeipokea demokrasia ambayo haina rangi wala kabila, kisha tukaivika msuli kwa kuongezea kijimila chenye rangi mahala pasipohitajika.. Hatuwezi kutaka yote kwa pamoja na ndio maana Takrima kwa sura zote imechukua mkondo mbaya ndani ya siasa.

Mimi binafsi nadhani hatari zaidi ni upokeaji wa fedha toka kwa mtu, mashirika ama nchi toka nchi za nje kwa sababu ya Uchaguzi ndani nchini. Vyama vyote nchini vimepokea misaada toka nje kwa maslahi ya watu, vyama, mashirika ama nchi hizo na malipo yake kwa nchi maskini kama yetu ni kuendeleza unyonyaji na udhalilishaji wa wananchi.

Mzee Es,
Nakubaliana na wewe kwamba Free kajifunga kamba za miguu mwenyewe. Mimi na wewe tulipiga sana makelele kabla ya Uchaguzi na kama Chadema wangependa kupata ushindi hata nafasi ya pili wasingeendelea na mbinu za Free. Tishio la CCM nadhani ni Chadema sio Free. Free mzungumzaji mmoja mzuri sana na anaweza kushika nafasi kubwa ndani ya Chadema lakini sio kuwa kiongozi mgombea Urais. Free sio mgeni kwa vijana wengi mnaoandika humu. Free sio mgeni kwa vijana wengi waliosoma nje ambao wangependa sana kumsaidia ama kukisaidia Chadema lakini navyomfahamu Free ana kile kichwa cha kujiona yeye sii mtu wa kuinama bali kuombwa yeye. Ewaalah, kwake ni utumwa na matokeo ya uchaguzi nadhani yamewadhihirishia Chadema kwamba kunahitajika marekebisho makubwa sana ndani ya chama. Kwanza kabisa Chadema inatakiwa wapate uwezo wa kushinda majimbo mengi kwa kumtumia Free huyohuyo kama msemaji wao mkubwa kwa sababu ndani ya CCM kuna viongozi ambao wako njia panda. Viongozi ambao waki-cross Chadema, Ushindi wa CCM hatarini kabisa. Lakini mbowe hawezi kabisa kuachia kamba kumpisha mtu, hii ndiyo ndoto yake na hawezi kuiachia hadi kifo. Hii ni personal goal, hajari kama ni kwa njia ya Chadema ama chama gani - IKULU that's where he is heading!

Kwa hiyo nitamalizia kwa kusema CCM kumbomoa Mbowe inawezekana ( kufika Ikulu) lakini tatizo kubwa la CCM sio Free ila ni Chadema na Mzee Es mwenyewe ulikiri maneno haya kabla ya uchaguzi.
 
Freeman,

(1). Kwanza ni rafiki yangu, na ninajua kuwa ni wachangiaji wawili tu hapa wanaomjua personally, Bob na Jasusi, lakini ninaamini kuwa part yake ya siasa ninaifahamu kuliko wengine wote. Free is a good man na ni visionary man, nimemuona kwa macho yangu akiigeuza Mbowe Hotel kutoka just another Guest house mpaka kuwa Hotel ya kweli, na mpaka sasa Bilicanas. Hata siku moja siwezi kusema Free ni msaliti, hapana! lakini I believe kuwa within his heart Free ni CCM, cham cha marehemu baba yake, na ni kupitia Azimio la Arusha ndipo baba yake aliweza kuinunua hilo jengo kupitia (CCM-TANU), baada ya kazi kubwa ya mzee Haikaeli kumsaidia sana Mwalimu enzi zile.

Katika uchaguzi uliopita CCM kama kawaida yao, waliingia na full gears, lakini toka baada ya Dodoma kulikuwa na wasi wasi mkubwa ndani ya CCM kuwa wananchi walioendelea ni vigumu kumpigia kura mgombea wao, maana hakuwa na record, na mikoa iliyoendelea sio siri inafahamika kuwa ina wananchi ambao sio rahisi kuwadanganya, na sio siri Free aliwika sana kwenye hiyo mikoa, sasa matokeo ya uchaguzi ndiyo yaliyowashangaza sana CCM, kwani hakuna aliyetegemea kuwa Freeman angepata kura chache vile, na mpaka leo hii hakuna anayeelewa exactly what happened? Na hata Freeman mwenyewe haelewi ni nini kilitokea? Sio kwamba angeweza kushinda, no! lakini ilitegemewa kuwa wabunge wengi wangetoka Chadema, ukweli ni kwamba hata mimi binafsi niliamini kuwa bunge lingekuwa nusu kwa nusu, kati ya CCM na Upinzani na hasa Chadema, kwa hiyo yes!, wakati wa uchaguzi Free alikuwa tishio lakini matokeo yalimaliza kabisa nguvu yote ya Free kisiasa kwa maoni yangu, na Chadema itafanya makosa makubwa kumsimamisha tena uchaguzi ujao.

Freeman alikuwa ni a strong candidate kuliko wote waliogombea kwa maoni yangu, na JK alikuwa ni the weakest candidate, Free alikuwa na strong political points kuliko wote, lakini tatizo ni kuwa alikuwa peke yake mtu mmoja, akiwa Songea maana yake ni Chadema nzima iko huko, as opposed to CCM! Halafu vyama vyote upinzani vinaendelea kuwa tatizo moja sugu, nalo ni kwamba wako mijini tu! Hawako vijijini, kura karibu zote za CCM zinatoka vijijini, kama vile kura za Bush kwenye uchaguzi wa mwisho zilitoka vijijini. Halafu Free alisindwa kuzi-simplify point zake ili zieleweke na wananchi wa chini, kwa mfano majimbo ilikuwa ni a very strong one kuliko zote alizokuwa nazo, lakini baada ya kushindwa kuisema vizuri CCM wakai-simplify kuwa ni chanzo cha kuleta ukabila na udini na wananchi wakakubali kuwa ni kweli!

(2). Kufunga magazeti yasiyokuwa na muelekeo ambayo kazi ni kuwapotosha tu wananchi na kupandikiza chuki za bure miongoni mwa wanajamii ni hatua moja muhimu sana katika kufanikisha kuwaelimisha wananchi na taifa na kuwaamsha kisiasa, wewe mwenyewe unajua kuwa tatizo letu kubwa bongo ni wananchi wasioelewa kitu chochote, wakipewa pilau tu wanakuja na kukupa kura! Media ni a very powerful tool ya kuwapotosha wananchi,

ninasema haya magazeti yazungumzie our real problems, kama vile rais kusafiri na wajumbe 50, yaulize EL alikwenda kufanya nini huko Majuu ambalko rais tayari alikuwa huko majuzi tu, magazeti yaulize ni nani aliyeruhusu wabunge kupewa shillingi millioni 40 za magari, badala ya 30 kama ilivyokuwa ni nani aliyeruhusu nyongeza ya millioni 10? Magazeti aulize ni kwa nini tunjenga bunge jipya na wakati tuna Karimjee na Dodoma tayari, wakati hospitali zetu zinatisha kwa uchafu na umasikini? Wananchi wanahitaji kujua ni kwa nini tunagawana umeme? Yapige kelele kuhusu mikataba mbuzi? Wote tumeona jinsi Media ilivyosimama kidete juu ya nyongeza za wabunge mpaka rais mwenyewe akaogopa na kujitoa kuwa yeye hahusiki, sasa kwa nini wasifanya hivyo kwenye issue zote? Badala yake wanakuja kuandika ujinga, I mean NONESENSE! CCM kummaliza Free wanahitaji kukaaa kikao kizima cha CCM?, badala tu ya kumtumia TRA kufunga biashara zake? I mean ukifunga biashara za Free basi na siasa zake zimekwisha kwa sababu aslimia 80% ya shughuli zake za kisiasa Free anatumia hela zake binafsi kwa hiyo akiwa tatizo ni kufunga njia za kuingia pesa zake!

Kwa hiyo mzee kuhusu magazeti, kinyongo changu ni kuwa hayazungumzii real issues ambazo ni muhimu kwa wananchi, na ndio maana hayauzi tena siku hizi, yamebakia kutegemea vikundi vya vyama vya siasa! Isipokuwa kama wananchi kama wewe wanaona kuendelea kuandika ujinga badala ya issues ni sawa, basi yadumu!

(3). Mzee Jasusi,

Swali la mil 40, ninaona mzee Bob amelijibu vizuri, kuhusu sera ni kweli sera almost zote za JK, originally zilikuwa za Free lakini akaweza kuziwahi na kuzigeuza kuwa zake, kama vile Bill Clinton alivyokuwa akiwafanya Republicans, kwa mfano ile issue ya Welfare mwaka 1996, politically sio dhambi ila sasa tatizo linakuja utekelezaji, sasa magazeti yetu yalipaswa kuanza kumuuliza JK vipi zile ahadi za ajira millioni moja kwa mwaka au mwezi?

Kwa kumaliza ninasema kuwa Free alijitahidi, na laifanya kazi nzito na inahitaji kupewa heshima, lakini katika siasa tunaangalia umeangukia wapi sio umeangukaje! Ndio maana huko majuu uchaguzi ukiisha tu, kina Gingrich wanaambiwa wajitoe waingie wengine, huu ni wakati muafaka kwa Free na chadema kuanza kumpromote JJ, na wengine, Free akae pembeni na kuendeleza chama chake, mamboi mengine kama ninavyosema siku zote siwezi kuyaingilia kiundani mno maana tunamuamini Mungu na kufunga milango ya magari yetu!
 
Mwanakijiji, Mkandara na Mzee Es,

Nadhani nikiendeleza ukimya na kusoma tu sitakuwa nimechagiza vizuri mjadala.

Naowaomba nirushe kidogo “chakula cha fikra”


1. Tuisome na kuijadili habari husika kwa ujumla- kichwa kinasema Mbowe lakini habari imedokeza kuwa CCM inataka kumharibu “Mbowe na chama chake”. Sijui kama mwandishi alitumia “chama chake” kama lugha ya picha au ulikuwa akimaanisha umiliki. Yote kwa yote, kwenye ‘chama chake’ tuweke “CHADEMA”. Utamaduni wa chadema ni kutoamini katika chama mtu bali chama taasisi.

2. Niweke bayana kwamba nitakayosema ni maoni yangu binafsi, si kauli ya chama kama.

3. Naamini ni kweli CCM ina mpango wa kubomoa upinzani, au niweke vizuri- “kundi fulani” ndani ya CCM. Wanajitahidi kupandikiza migogoro(Rejea mtiririko wa matukio ndani ya vyama), wanajitahidi kutaka kuhonga(vyeo, fadhila nk) baadhi ya viongozi wanaochipukia katika upinzani lakini kubwa kuliko yote wanajenga kupitia vyombo vya habari propaganda dhidi ya upinzani(kwa walio nyumbani rejea mtiririko wa habari na makala katika magazeti mbalimbali kuhusu upinzani, utajiuliza kwanini makala kuhusu masuala nyeti haziandikwi kwa wingi lakini kuna makala nyingi za namna hii tena katika hoja zisizo na mshiko). Huu ni mkakati.(media spin)

4. Ni kweli vyombo vya habari vilitumika wakati wa kura za maoni ndani ya CCM sasa nguvu imeelekezwa katika kuupamba utawala na kubomoa upinzani.

5. Lakini Rais Kikwete anajiweka mbali kabisa na haya, alianza kwa kusema upinzani usibezwe baada ya matokeo, akaendelea kusema katika hotuba yake ya kufungua bunge kuwa mwenye kuwepo CHADEMA ni haki yake, asibuguziwe, akaendelea kusema Moshi Mjini kwamba hata waliochagua upinzani hawatanyimwa maendeleo. Na kwamba hakutakuwa na ubaguzi wala kunyanyaswa. Haya ni maneno matamu! Lakini hali halisi ardhini ni tofauti. Je, rais kama kikwete mwenye kupenda kuwa karibu na watu hajui kinachoendelea?Je usalama wa Taifa hawamwambii?. Nini chanzo cha mgogoro wa CCM Tarime kama sio kuchukia upinzani? Wananchi wa Karagwe wanafanywa nini hivi sasa? Angalia mwenendo wa Tendwa katika sakata la TLP!. Ya Mahita je?Najua wengine mtasema, serikali iliomba msamaha kwa CUF, je kwa kiasi gani imesadia CUF kusafishika? Lakini mimi nasema, CCM ilianza kuua upinzani siku nyingi kabla ya uchaguzi na kwenye uchaguzi wenyewe. Hoja ninazo, ila si sehemu ya mjadala huu.

6. Mzee mwanakijiji, umekuja na nadharia kwamba Mbowe ndio kaua upinzani kwa kuamua kugombea urais. Hii si kweli. CHADEMA imefanya tathmini na kuona ni jinsi gani chama kimepata faida kwa kusimamisha mgombea urais. Macho ya wananchi, asasi mbalimbali, na hata vyombo vya habari yasingekuwepo kwa CHADEMA kama isingekuwa na mgombea urais. Uzito wa Mbowe wakati wa kampeni usingekuwa mkubwa kama angezunguka kama mwenyekiti( Waulize Mbatia na Mvungi). Kuna baadhi ya maeneo matokeo ya wagombea ubunge na udiwani yamebebwa na kampeni za urais kupitia mabango, vipeperushi na nguvu ya helikopta kuwafikia watu wengi. Na ingekuwa vigumu kuwianisha muda katika ya haja ya CHADEMA kuendelea kutawala Hai na siasa za nchi nzima. Kwa ujumla, CHADEMA iliwasha mwamko mpya katika siasa za Tanzania uchaguzi uliopita kwa kuamua kumsimamisha Mbowe kama mgombea urais.(Hili nalo ni suala pana linalohitaji makala ya peke yake yenye uchambuzi wa matokeo kwa kina).

7. Yote kwa yote, mimi siamini kama upinzani ulishindwa kwa kiasi kile cha matokeo ya tume. Siamini kama zile ndio kura za Mbowe na wala siamini kama ndio kura za CUF kama ambavyo siamini ndio kura za hata Mrema pamoja na kushuka kwake kisiasa. Unayaamini matekeo ya Temeke, Karagwe, Bukoba mjini, Ubungo na kwingineko? CHADEMA imeeleza sababu za kwanini haidhani kama yale yalikuwa matokeo sahihi ya uchaguzi( rejea http://www.chadema.net/uchaguzi/ripoti1.php ). Hili nalo ni suala linalohitaji mjadala wa peke yake!

8. Mzee Es, si kweli kwamba gazeti la Tanzania Daima linamilikiwa na viongozi wa CCM wasiokuwa wanamtandao. Tena ukichambua kwa makini habari za magazeti utaona kuwa Tanzania Daima ni moja ya magazeti yanayoandika sana habari za wanamtandao likizidiwa kiasi na magazeti ya Habari Corporation. Kwa jinsi ninavyofahamu ulivyomjuzi wa mengi, naamini mkono uliteleza!

9. Sitaki kwa sasa kuingia kwenye mjadala wa Independent candidates na mwelekeo kwa siasa za Tanzania aliouchokonoa Mzee Es. Kuna maswali mengi ya kujiuliza: Utanufaisha CCM, upinzani ama wananchi? Tufanyeje? Nashauri tuweke kwenye mjadala wa peke yake ili tusipoteze mtiririko.

10. Mzee Es umesema Freeman ni CCM. Kama alivyosema Mwanasiasa-Tupe ushahidi. Kwa maoni yangu mimi siyo. Ilinichukua muda sana kuamua kuingia CHADEMA. Mimi napenda Utomaso!. Niliwachunguza sana viongozi wa CHADEMA kabla sijajiunga. Wengi nawaamini. Kama watabadilika huko mbele hiyo ni silika nyingine tofauti ya binadamu. Nimekaa karibu sana na Freeman, msimamo wake kuhusu masuala mbalimbali ya maisha naufahamu. Kama watu wa jamii hiyo ni wanaendana na yanayofanyika CCM basi watanzania wengi ni CCM. Lakini siamini hivyo. Kumbuka Freeman ana mizizi katika CHADEMA kama mmoja wa waasisi miaka kumi na ushee nyuma. Unataka kusema toka wakati huo alikuwa CCM? Sitaki kuzungumza sana, labda niulizwe-maana ningependa kuzungumzia zaidi masuala, sio watu. Walau kidogo naweza kuzungumzia matukio. Nachelea kuingia katika mizani ya busara nyepesi, busara za kawaida na busara zilizotukuka.

11. Umeghafilika pia katika suala la wabunge. Habari imezungumzia ubunge wa Afrika(AU), umeingiza ubunge wa EAC. Lakini umeenda mbali zaidi kusema kwamba ubunge huu ulipaswa kupewa kwa chama cha upinzani chenye wabunge wengi..nk ..nk..nk. Kwanza rejea kwenye mjadala wa bunge la AU kwa kuwa wa EAC bado(hata ukija ni yoyote anaweza kugombea si lazima awe mbunge. Pili, hitaji ni mbunge wa upinzani bila kujali kama anatoka chama chenye wabunge wengi au la suala ni awe mbunge. Ukweli ni kwamba CCM walifanya vikao kabla wakakubaliana kwamba wasimchague Zitto Kabwe wa CHADEMA wala Fatma Maghimbi wa CUF na kumfuata Mzee Phares wa TLP agombee. Wakampa kura nyingi. Walitumia uhuru wao, lakini siamini kama walitumia busara zao-hawakutanguliza utaifa wala sifa za kiuongozi. Mmoja alisema kabisa hatumtaki Zitto kwa kuwa tutaipa nguvu CHADEMA. Hii ni ishara ya wazi ya kuwa CCM imedhamiria kubomoa upinzani!

12. Ya Sumaye, JM na umakamu mwenyekiti tuyaache kwa sasa. Sumaye alichafuliwa na alilamika wazi- “Anayeingia madarakani kwa kalamu atatawala kwa risasi”. Lakini walichofanya ni kutumia udhaifu wa Sumaye, kuuweka wazi. Utasemaje sasa ya Mwananchi, uarabu wa Salim Ahmed Salim na mauaji ya Karume? Haya yalitokea Mzee Es. Tusipingane na ukweli. Ni wazi baada ya kumaliza kazi hiyo sasa nguvu imehamishiwa kwa majukumu mawili niliyoyataja.

13. Sasa kwani nini CHADEMA ilengwe zaidi na sio chama kingine? Mwandishi ametoa sababu mbili- Mosi, Kampeni kali za CHADEMA uchaguzi uliopita(nakubaliana naye), Pili-Mbowe na kashfa ya Kikwete ya pesa Mererani(nakubaliana naye kidogo), Tatu, Hoja ya Mbowe kuhusu wanamtandao(Nakubaliana naye ingawa amefinya sana hoja hii- sababu hapa ni tamko la CHADEMA la siku mia za kikwete-ukitaka kuthibitisha rejea http://www.chadema.net/makala/mbowe/mbowe_10.html ). Mimi nasema, sababu kuu ni tatu: Moja, CHADEMA ilikuwa tishio kwa CCM uchaguzi uliopita(ndio maana CCM iliitaja sana CHADEMA). Pili, CHADEMA imekubalika sana kutokana na uchaguzi uliopita(sasa na wakati wa kubomoa kukubalika huku); tatu, CHADEMA ndio chama pekee cha upinzani kilichokuwa kisiasa na kuonyesha matumaini ya kuchukua dola chaguzi zijazo na Mbowe ndio tishio zaidi kwa Kikwete na mgombea ajaye wa CCM( rejea http://www.chadema.net/uchaguzi/ripoti1.php -hivyo CHADEMA itazamwa kuwa adui namba moja wa CCM na utawala wake). Lakini kwa nini haraka hivi? Ni kutokana na sababu ya tatu, Uamuzi wa CHADEMA na Mbowe kuukosoa utawala wa Kikwete-hivyo mtandao unaona umaarufu wa Kikwete unapunguzwa. Ndio maana utasikia kauli si tulidhani Mbowe ni mstaarabu kumbe sio. Tulitegemea CHADEMA isikosoe nk nk. Ndio maana tamko limetolewa siku nyingi lakini mpaka leo CCM wanaendelea kulikanusha( rejea www.chadema.net kwenye tamko la Vijana wa CHADEMA kuhusu UVCCM). Hivyo kwa mtu yoyote makini anajua pamoja na idadi ndogo ya wabunge, CHADEMA sio chama cha kupuuza. CCM wanajua kuwa idadi ndogo ya kura sio nguvu ya kweli ya CHADEMA, mashushu wao wanaujua ukweli uliopo nyuma ya matokeo ya uchaguzi 2005.

14. Sitaki kuingia katika mjadala na Mzee Es kuhusu rai yake ya kutaka magazeti ya IPP na Tanzania Daima yafungiwe.

15. Mzee Es,nawe heshima yako, nakumbuka. Nilikwambia Sumaye na Keenja hawataaniibia. Na ukweli ndio. Walioiba Ubungo ni system. Wala sio kwa nguvu ya Keenja. Yeye alisha-surrender. Mkurugenzi wa manispaa wakati huo ambaye ndiye alikuwa msimamizi wa uchaguzi alitamka kuwa alipewa maagizo toka juu( yeye alisema ikulu) atangaze matokeo. Na kweli mwishowe baada ya kumaliza kuhesabu za urais akatoka nje aliporudi akatangaza matokeo bila kujumlisha matokeo ya Ubunge kituo hadi kituo kama sheria inavyohitaji. So my heart is sober on this, I belief the residents and young people were the winners in Ubungo what ever the results. Anyway, huu ni mjadala tofauti.

16. Mzee Es, narudia tena. Matokeo ya uchaguzi hayawezi kunifanya niingie CCM. Kwa nini sikuingia in a first place. I differ in its leadership principles and policies!. Sijaingia kwenye siasa kwa ajili ya “Mkate na Jibini”. There is a vision and mission I am pursuing. Sorry for using strong language but as Shaban Robert puts it, ‘’ ‘’Msema kweli hukimbiwa na marafiki zake nikipatwa na ajali kama hiyo sitawaonea wivu wale wanaodumu na marafiki zao siku zote. Siwezi kuikana kweli kwa kuchelea upweke wa kitambo na kujinyima ushirika wa milele unaotarajiwa kutokea baada ya kushindwa kwa uongo”.

17. Mwanasiasa, nakubaliana na hoja zako.Asante.

18. Jasusi, yafungulie mjadala hayo maswali- Masha, Kikwete na Madini ya Mererani. Tujadili humu, kutoka Afgem mpaka TanzaniaOne. Kutoka IMMA mpaka kauli za Tundu Lissu. Yapo mengi. And Let them respond!. There are issues on minerals, let me reserve them for now.

19. Mkira, naendeleza ulipoishia..as Bob says…but now you see z light..STAND UP FOR YOUR RIGHT.

20. Mwanakijiji-maswali yako kuhusu loyalty ya wabunge naomba uyafungulie mjadala wa pekee. Kuna masuala nyeti humo! Ila Mimi naamini katika kuishi beyond partisan politics. Vyama mbalimbali ni muhimu, muhumu sana. Ndio maana namshangaa yoyote mwenye kutaka kuua upinzani. I know politics is about power, but a good politician or citizens must know absolute power corrupts absolute. Ndio maana nataka kwa pamoja tuvilee vyama lakini kulea kwetu vyama kusitufanye tupoteze utaifa.

21. Mkandara, ni kweli kuwa JK hakuvunja sheria. Na wala Free hakusema alivunja sheria. Alichosema ni kuwa Kikwete hawezi kuwatetea wana Appolo akiwa rais kwa kuwa amechangiwa na wale wale waonaowanyanyasha wanamerereni. This was a policy attack. But CCM took it as a personality assault which is tantamount to cropping enemity!

22. Ya takrima nakubaliana nawe. We profaned the essence of our traditional hospitality and even abused the dictationary meaning on the word “Takrima”.

23. Nakubaliana nawe kuwa tumeipokea demokrasia kichwa kichwa. We the new generation have the role to change this trend!

24. Mkandara, Free wa mwaka juzi si wa mwaka jana na si wa leo. He is one of the everyday readers and learners I have seen. Perhaps sasa umuandikie kwa kirefu. You may send him direct your plans or through me. Anapokea sana mawazo.

25. Ila narudia tena, CHADEMA ilifanya vizuri sana kumsimamisha kugombea. Nakubaliana nawe kuwa CHADEMA inahitaji kujipanga, na ndicho tunachofanya hivi sasa. Tulianza kwa kutengeneza Mpango Mkakati wa Miaka mitano na Mpango kazi wa Mwaka. Sasa tumeanza kutekeleza. Tuko kwenye mchakato wa kubadili katiba, mwezi wa nane tutafanya mkutano mkuu. Mwakani tunafanya uchaguzi. Viongozi wote wa chama wamefupisha muda wao wa uongozi kupata fursa ya kukipanga chama vizuri ikiwemo kuweka muundo thabiti kwa mapambano.

26. Mkandara, sikubaliani sana na dhana ya kutoa viongozi toka CCM. Mko vijana makini wengi na watanzania wengi mahiri ambao hawana vyama. Karibuni tujenge upinzani wenye manufaa kwa taifa. Somo la Njelu Kasaka na wengine linafundisha mengi kuhusu watokao CCM. But I don’t close my door. There are some good people the likes of Dr. Slaa, Balozi Ngaiza, Pesha etc.

27. Mkandara, Mbowe kuwa na ndoto ya kwenda ikulu sio nongwa. Ni fursa. As JF. Kenedy said- mwanasiasa yoyote lazima autake uongozi ndipo ataweza kupata uongozi na kuongoza. But what is important is shunning away from Machavellianism!. Suala la msingi ni unataka kwenda ikulu kwa nia gani? Is Ikulu a means or an end?. Kiongozi yoyote anayetaka kwenda ikulu kwa nia njema atajenga taasisi. Naamini ndicho Mbowe anajitahidi kufanya CHADEMA. Na katika hatua kilipofika hivi sasa CHADEMA sio Mbowe, CHADEMA ni taasisi. Katika hatua hii maamuzi ya mwachama mmoja hayawezi kubomoa chama. Hii ndio CHADEMA inayopaswa kulindwa dhidi ya hujuma za chama tawala ambacho ni chama dola ili Tanzania tuendelee kuwa na upinzani wenye maslahi kwa wote.

Mungu atubariki tuendelee kutofautiana bila kugombana. Kama nilivyosema mwaka jana SIASA sio UADUI





ma kweli hukimbiwa na marafiki zake nikipatwa na ajali kama hiyo sitawaonea wivu wale wanaodumu na marafiki zao siku zote. Siwezi kuikana kweli kwa kuchelea upweke wa kitambo na kujinyima ushirika wa milele una‘’Msema kweli hukimbiwa na marafiki zake nikipatwa na ajali kama hiyo sitawaonea wivu wale wanaodumu na marafiki zao siku zote. Siwezi kuikana kweli kwa kuchelea upweke wa kitambo na kujinyima ushirika wa milele unaotarajiwa kutokea baada ya kushindwa kwa uongo’’.otarajiwa kutokea baada ya kushindwa kwa uongo’’.
 
Mzee Es,

Naona jumbe zetu zimepishana. Wakati naingiza ujumbe wangu nawe umetuma wa kwako. Hivyo hoja zangu za juu hazijumuishi majibu kwa hoja zako za chini. Nimejibu hoja zako za mwanzoni.

Nakupongeza kwa ujumbe wako wa sasa ambao walau umeita panga "panga" na sio kisu kikubwa.

Naomba nisitoe maoni yoyote kwa sasa niache wengine wachangie kwanza. Nitakujibu!

Thanks 4 ur compliments.


Ps: Rekebisho katika post yangu iliyopita...weka neno "in" katika ya leadership na principles. Isomeke: I differ with their leadership in principles and policies. Nazungumzia misingi yao ya kimatendo
 
Very convincing JJ very convincing!

Sina chama bado, na CCM ndio ilikua chaguo langu la kwanza, ila argument zako zimenifanya nikiangalie CHADEMA kwa mwanga mpya!

Shukran!
 
Mzee JJ,

Kwanza nitoe shukrani zangu kwako kwamba finally you have come out kama wewe, unajua siku zote toka BCs ulikuwa hujawahi kutoka rasmi kama safari hii, huu ni ushindi kwa forum na ninaamini kuwa the more mawe yakirushwa huko wote watakuja,

(1). kwa kifupi suala la magazeti na viongozi sio refu sana, kwani viognozi ndani ya CCM wanajulikana kutokana na magazeti wanayoyasoma, hata siku moja wahusika huwezi kuwakuta na magazeti ya opposite, tena yakiandika habari za matusi kwa opposite huwa tunaletewa nyumbani kabisaa na wale viongozi kwa kuwatuma wapambe wao, ninajua hili gazeti ni la nani ndani ya CCM, kwani huyu mzee hasomi gazeti lolote zaidi ya hili! Na halijawahi kumtukana hata siku moja, lakini chochote mtakachosema nitakubali!

(2). Ushahidi kuwa Free ni CCM sina, isipokuwa sijawahi kuwaona kina Lipumba, Mrema, Mtikila, Mapesa, Mbatia wakishinda majumbani kwa wazee wa CCM, hata siku moja ninarudia! Baada tu ya uchaguzi kulikuwa na mkutano mkubwa wa mzee wa CCM na Free, nyumbani kwa huyu mzee WHY? Waliongelea nini? Sasa sio mara ya kwanza ninasema haya, toka BCS nilishasema kuwa Free ni CCM, na at the right time atapewa uwaziri na ninajua kuwa hiyo siku inakuja sio mbali, ila ushahidi sina! Halafu ninajua kuwa Mapesa alipoanza kuwa tishio, CCM walimnyang'anya nyumba kwa kusingizia ana madeni, sasa leo Free anawezaje kuwa tishio kwa CCm halafu wakamuachia kuendelea na biashara? Na kwa nini alipoikuwa mbunge ilikuwa taabu kwake ku-socialize na wabunge wenzake wa upinzani? Hawa kina Chenge alikuwa anaongea nao nini kila siku? Ushahidi sina ila ninasema Freeman ni mfanyabiashara sio mwanasiasa, mimi ndivyo ninavyomfahamu maana kama unataka kuwachukia viongozi wa CCM kwa madhambi yao kwa wananchi ni lazima uhakikishe kuwa wewe pia huna hayo madhambi, hivi nyinyi kina Mwanasiasa na JJ, mnaweza kutuambia kuwa Free ni clean kiasi kwamba anaweza kuyasimamia madhambi ya CCM? Ndio maana ninasema kuwa ni the right thing amuachie mwingine, yeye na CCM hawana tofauti yoyote, tena nimesema akuachie wewe mzee JJ,

(3). Sio watu wote tulioko CCM tumefuata dhambi za mikate na jibini, hapana! Wewe ukija huku utatutasaidia kuleta mabadiliko ya kweli ambayo tunayahitaji, mapinduzi ndani ya mapinduzi, lakini hakuna haraka mzee JJ, pole pole tu mpaka utakapokuwa tayari, hakuna haraka maana huko uliko uwezekano wakuingia ni mdogo kwa sababu ninajua kuwa wewe ni kama mimi hatua hela za kumwaga bila sababu!

(4). Bunge la Africa ni kwamba huwezi kuingia mpaka uwe mbunge ndani ya nchi yako, ndio maana rafiki yangu Kommando kule alipigwa vita vikali na CCM kwa ujumla kwenye kugombea ubunge wa Ukerewe kwa kutaka kumtoa yule mama ambaye ni rais wa bunge la AU, ni CCM ndio wanaoamua nani aende EAC na AU, na ni CCM hao hao waliompeleka Shija kuwa katibu Commonwealth, ila siwezi kusema zaidi!

(5). Kuhsus kura zako ninaamini kuwa wewe ndie unayefahamu zaidi kwa hiyo siwezi kukubishia,

Kwa hayo ninasema tuendelee na mapambano, labda somehaow tutawasaidia wananchi na serikali yetu, ila usipotee tena! Sio mpaka tuseme Freeman ni CCm ndio utokeee!

(5).
 
Mzee JJ

Mzee ES amegusia suala la uchaguzi na wizi wa kula. Mimi ningefurahi sana kama ungekuwa mwakilishi wa jimbo letu. Mwenzako natokea maeneo ya kwa Mfuga Mbwa. Ingawa mimi sina chama, lakini nakubaliana na wazo lako la kuondoa dhana ya kufikiri kuwa Tanzania hakuna vijana wenye mawazo mazuri ya kuiongoza nchi. Sio lazima viongozi watoke CCM na kujiunga na CHADEMA. Sidhani kama uliwahi kuwa kiongozi wa ngazi za juu wa CCM lakini natambua mchango wako kwa taifa ni mkubwa kuzidi hawa waheshimiwa wanaoiuza nchi.

Hata Zamoyoni Mogella alichoka, akajiunga na timu ya wakongwe na sasa hata hiyo timu hawezi kuichezea tena. Tukubaliane kuwa inafikia wakati hata akili inachoka kadiri unavyokula chumvi. Hawa akina Kingunge wanakata mbuga zaidi ya miaka arobaini sasa. Itakuwa ni kichekesho kuwashawishi hawa waheshimiwa ili wajiunge na kuleta mawazo mapya ndani ya CHADEMA. Suala la msingi lililo mbele yetu ni kuwapuuzia wote pamoja na kambi zao. Vizazi vipya tunahitaji kuanzisha majadiliano ya nguvu na kuyachapisha kwenye vijarida na vijitabu vya kudumu. Hii itakuwa taasisi tofauti ambayo haiwezi kununuliwa na mtu yeyote. Tutavipinga na kuviweka sawa vyombo vya habari, Bunge, Viongozi, na Raisi wetu ambaye ana madaraka makubwa kupita kiasi.

Kukosa kwako Ubunge kuliniuma sana Mzee JJ, mpaka sasa hivi najiuliza maswali mengi bila majibu. Nchi yetu bado ni changa kisiasa, hivyo, tunahitaji utaratibu wa kuwahusisha wananchi moja kwa moja katika masuala ya uwakilishi. Napinga utaratibu wa sasa wa “the winner takes all” hautufai. kuwapata washindi kwenye uchaguzi kwa msingi wa wingi wa kura hauzisaidii nchi masikini kama yetu. Utaratibu huu hauzingatii kikamilifu matakwa ya wananchi kwani chama cha siasa kinaweza kupata idadi ya wabunge iliyo kubwa au ndogo ukilinganisha na uwiano wa kura za wananchi kwa ujumla.

Mfumo tulionao sasa unatetea zaidi uwakilishi wa vyama vya siasa na viongozi wetu wanautumia kuondoa uwakilishi wa wananchi. Badala ya kuzingatia haki za wananchi unawekwa msingi wa haki za vyama vya siasa. Binafsi, ningependelea tuwe na utaratibu wa kutumia mchanganyiko wa ushindi wa wingi wa kura na uwiano wa kura ambao ni mwanzo mzuri wa kufikia uwakilishi halali zaidi.

Kuna dosari gani kwa mfano, tukiamua kwamba mikoa yote iwe majimbo ya uchaguzi kwa kura za uwiano. Viti vya uwiano pia vigawanywe kwa mikoa kwa uwiano. Chama cha siasa kitapata mwakilishi kama kikifikia asilimia fulani ya kura. Kama tungekuwa na utaratibu huu katika uchaguzi wa mwaka jana, basi mzee JJ ungekuwa Bungeni unawatimulia vumbi hawa waheshimiwa wanaojiwakilisha wenyewe pamoja na vyama vyao badala ya kuwawakilisha wananchi.
 
J J Mnyika,
Kushindwa kwako ktk uchaguzi uliopita ni moja ya sababu kubwa ambazo sisi vijana inatakiwa kujifunza. Mimi sii mwanasiasa na sipendi kabisa kujihusisha na Uongo unaokubalika kwa sababu haiwezi kubadilisha matekeo ama kutuongoza ktk mwanga zaidi. Umeshindwa kwa sababu ya hao wazee wa CCM ambao hawapendi na wala sio utamaduni wetu kurithisha vijana wao. Kama nilivyokwisha sema hapo awali mirathi ya aina yeyote ile ni utamaduni uliokwisha potea mara tu baada ya kupata Uhuru. Baba zetu wengi walirithishwa na babu zetu kulingana na mila zetu lakini baada ya Uhuru tulianza kuchanganya tamaduni za kigeni ambazo tulifanya kuiga tu bila kuzifanyia utafiti. Baba zetu leo hii hawapendi kabisa kutoa mirathi na ndio maana watu kama Kingunge wanakimbilia 90 lakini hadi leo hii hawana will na bado wanaendesha biashara ama kazi zao wenyewe. Kesho wakiondoka wanaacha ugonvi wa mirathi nyuma.

Mnyika, mara nyingi mimi napoandika hoja kwanza kabisa naamini hakuna mtu anayekubaliana nami. Hil sio jambo geni kwangu, mara nyingi huwa napingwa sana mawazo yangu hadi pale ukweli unapojitokeza baada ya wao kushindwa kufikia malengo kutokana na dhana zao. I'm a thinker!....Hekima na Busara hazipatikani kwa elimu ya darasa wala ujanja wa mtaani isipokuwa Umri. Shikamoo haipatikani kwa fedha wala elimu na ndio maana sote hutakiwa kuwasikiliza wazazi na wazee wetu bila kujali elimu zao. Wale wanaopinga shikamoo na kuuita utumwa ni haohao wanaojidhalilisha kwa kuwaita ma- boss wao Sir, na wasione utumwa ndani ya neno hilo.

Hata hivyo turudi kwenye mada, - Mnyika Chadema mnahitaji sana vichwa vinavyoheshimika ili kuvunja nguvu ya kijimila hiki kichafu cha wazee kutokubali kuachia ngazi. Na huwezi kuondoa kijimila hiki kama huna mbinu na uwezo wa kuleta mabadiliko. Nakumbuka kuna hoja fulani tumeizungumzia humu kuhusu Shujaa!

Ndugu yetu Ogah, kama sikosei alisema kuwa Shujaa ni yule tu anayeleta Ushindi...kushindwa kwa kiongozi hata kama alikuwa na nia nzuri ni moja ya udhaifu wa kiongozi huyo ktk strategies za kupata ushindi. Kwa hiyo mtu kama Kinjeketile hawezi kuitwa shujaa machoni pa wanamapinduzi kwa sababu shujaa ni yule anayehakikisha ushindi unapatikana. Hii ni theory ambayo hata mimi sikubaliani nayo lakini ina nguvu sana kwa wafuasi wake. Kama vile mpira wa miguu, mafanikio ya timu huhesabiwa kwa ushindi na sio kujihusisha kwake ktk legue.

Sasa basi kama Free ameweza kuweka malengo yake kufika Ikulu na Chadema mnakubaliana na lengo lake, je huoni kama Chadema inamsukuma Free kufikia malengo yake na sio Chadema kuwa bus ambalo linaelekea kufikia ushindi!..Ikiwa free ataendelea kushindwa ina maana Chadema nao wameshindwa!... Akiondoka Free, Chadema nayo itabaki jina... ndugu yangu hii strategy ni mbovu na hatari kubwa sana kwa maendeleo ya chama. Rejea hoja ya Mzee Es hapo juu utaona uhusiano wahoja hii na hiyo ya utaratibu wa uchaguzi.

Nachoona mimi Chadema mnafanya kupanda mlima kwa kutumia ngazi.. yaani chama kizima kinamsukuma Free aweze kufika juu, kwa sababu Chadema mnaamini ngazi haipandwi na watu wawili kwa wakati mmoja. Kwa hiyo, Free atakapo fika juu mnategemea yeye kuanza kuwatupia kamba ya kurahisisha upandaji mlima. Kosa kubwa mnalofanya ni kuangalia physical structure ya mgombea bila kufahamu experience (umri) ni muhimu zaidi kufika kilele cha mlima wa siasa.

Mwisho ndugu yangu, Kubali usikubali..leo hii CCM watakuwa wana-focus sana ktk kumwangusha Mbowe kwa sababu ndiye pekee anayepanda mlima na kuwa tishio kwao. Hii inaifanya kichwa cha habari cha gazeti kuleta maana zaidi ya ile -CCM kuibomoa Chadema, kwani ndani ya Chadema hakuna wazee ambao wanaweza kubadilisha tamaduni mbovu ya kutorithisha. Wewe na mimi Mnyika ni warithi tu, hatuwezi kabisa kutoa madai yetu yakakubalika ikiwa WILL haina majina yetu. No matter how much right, evidence na kadhalika tutakuwa tumebeba. Free karithishwa Chadema na ndio maana ana kila nguvu ya sauti ndani ya Chadema, Kitaifa anaonekana mbabaishaji tu kwa sababu Mwinyi, Mkapa na JK wote wanakubalika kuwa warithi wa JKN. Ndio maana Free alikuwa tishio kubwa alipodai kwamba anataka kufuata nyayo za JKN, ile ilikuwa mbinu kali sana kuliko zote alizowahi kuzitumia na ilitingisha CCM nzima. Alipozimwa na Kingunge hakuwa na mtu (mzee) nyuma yake kuhalalisha madai yake ya mirathi.
 
Wandugu heshima zenu .Kwanza niwape pongezi kwa kuongelea hoja hii kwa undani .Maana hapa kuna habari za ukweli lakini kama kawaida ya wana CCM wamezoea uongo basi ukweli unapindwa tena .Mzee ES lisemwalo lipo na kama halipo linakuja .Naamini you are just being terrified for the news to be disminated before time sasa unataka ku lcover up .Ukisema Mbowe is nothing and was nothing unanifanya nijiulize maswali mengi sana juu ya ulichokisema hapo juu .Wapuuzi wote ambao hawawatakii mema Tanzania waliibuka wazi wazi na kuanza kumsakama Mbowe wakati wa kampeni .Kuanzia Kingunge , JM na kila mmoja ambaye anadhani CCM ni bora kuliko Tanzania alisimama na kuanza maneo yenu ya Ki CCM ya uongo .

Unasema JK alipita kwa 80% nami nasema ni kweli lakini alipita kwa nguvu za akina Mahita na usalama wa Taifa .Ubungo matokeo yalitangazwa kwa lazima Mnyia kasema , nilikuwa Arusha matokeo yalitangazwa kwa lazima na mawakala walifanya kazi ya ziada kuiondoa TLP nawajua baadhi ya mawakala mmoja wapo ni mwanasheria wa manispaaa ya Arusha alikiri wizi wa kura ili kuwazuia kuingia ofisini maana wangeulizwa uuzwaji wa viwanja na mambo mengi machafu pale AR .

Nilikuwa Musoma huko FFU walipiga watu na kuhakikisha Matayo anapita watu wengine hawakupiga kura kwa uoga .Musoma Matayo alichinga nyumba 40 watu wakala wakaenda kupiga kura fika Musoma utasikia live .Musoma hata JK na Makamu wa Rais walichoka kabisa hawakutakiwa na hawatakiwi hadi sasa CCM iliweza kushinda kwa kishindo eneo hilo jiulize .Si muujiza ndiyo maana unalia na kila mara na JM JM hana lolote ila kuwanyima watanzania haki zao kama kuiona CCM ndiyo pekee na uchafu huu .Kuweni macho iko simu tutawahoji kama akina Saddam najua hutakubali kwa sasa lakini sisi ni watu na kila lilo na mwanzo lina mwisho .

Unajua Tarime kulitokea nini ?? Maana JM alisema ukipoteza jimbo unaacha ukuu wa Wilaya lakini Wakurya walisimama wakasema no FFU unajua ni gari ngapi zilitinga Tarime zikiwa na polisi na FFU wakitaka kuiba kura ? Kazi ikawa ngumu sana .Unajua kuna ma box 5 yalikamatwa yakiwa na kura na yaliingiziwa Kenya na kwenye vijiji ambayo walidhani wataweza kuchomeka lakini wananchi walikaa macho wale wenye nyumba zile hawakutoka kwenda nje na walio kuwa nje hawakuingia hadi matangazo ya wangwe Mbunge .

CCM kushinda kwa fujo hata JK haamini maana anajua alikuwa hakubaliki na bado JK hakubaliki bwana .Unasema magazeti yafungwe ama yaandike habari nyeti wakati yana ndoa na JK je jawajipendi ?Maana uchafu tutaanza kuusikia pale ndoa itakapo kufa .Kwa sasa hatutasikia habari zozote za maana na hasa wale wakulima hawatajua lolote mbali na Radio na magazeti kupiga debe .

Tuacheni na Nchi yetu msitugawe kwa maslahi yenu.Leo mnakaa mnaanza kuipinga Mahakama na uamuzi wa Mgombea binafasi kama kweli JK na kampuni yake wanafanya kazi na kweli CCM mliibuka na asimilia 80% na kama kweli mnadhani mnathaminiwa na kuaminiwa na wananchi who worry about Mgombea binafasi ?? CCM haina nguvu hizo ila ina dola na mnatumia vibaya dola .Kuiba sera za Chadema ni kuishiwa kabisa lakini Mbowe katulia ana angalia wapi aipeleke Chadema na atakuja na hoja mpya .Ni aibu kusema kwamba mlitumia hoja ya majimbo na kubadili ikaonekana kama ni mwanzo wa vita .Aibu aibu aibu usingalisema hili ni siasa hizi .
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom