Ole Sendeka akaribia kuzipiga kavu kavu na RC wa Manyara kwenye mkutano

Dark City

JF-Expert Member
Oct 18, 2008
16,253
11,598
Habari zilizorushwa na TBC1 kutoka Manyara zimeonesha kuwa Mkuu wa Mkoa wa Manyara Henry Shekifu amepandishiana live na Ole Sendeka baada ya kutofautiana wakati wakihudhuria mkutano wa vijiji viwili huko Simanjiro. Kama kawaida ya wakubwa, RC ametishia kumweka ndani Sendeka kwani sheria inamruhusu kufanya hivyo kwa msaa 48 bila kutakiwa kutoa maelezo.
 
Shekifu ajue kuwa Olesendaka anaingia mjengoni kuzitunga hizo sheria , kwa maana hiyo zi simpe kiburi kwa mtindo wowote ule.
Tupe kisa basi mbona ipo ki aina fulani hivi hii story au bado Lowasa anamtafutia kisa cha kumfanya asigombee ubunge tena?
 
huyu RC SI MBWA MWENZAKE SHEKIFU ANAENDEKEZA SIASA KWENYE MASLAHI YA WATANZANIA
SENDEKA CHAPA MAKOFI..AKA WEWE RC NA SHEKIFU WAKO
 
simpingi sendeka kwani imefikia sasa watu kupata ujasiri wa kusimamia haki za watu tunaowawakilisha, lakiniit depends on who called for the meeting, kama ni wa kimkoa then sendeka amekosea... ila kama ni kikao cha kijimbo then he was right
 
hiyo safi kama ikiwezekana kupigana makofi kupigania taifa hili na tufanye hivyo
 
Usilolijua ni usiku wa giza!!!

Sendeka hana adabu hata kidogo na wala hajafunzwa kwao kuheshimu wakubwa wake. Kikao kile kiliitishwa na RC kwa ajili ya kuzungumza na wananchi wa kijiji cha Sukuro, na kulikuwa na mkutano wa hadhara lengo ni kuhusu ugawaji wa vitongoji wa kata ya Sukuro, ambao sasa ina vijiji viwili Sukuro na Kitiangare.

Sendeka hakubaliki katika kijiji cha Sukuro hivyo aliandaa watu kutoka kijiji cha Kitiangare kuja kufanya vurugu, wakati RC anaongea mtu mmoja wa Sendeka akafanya vurugu, RC akaomba atolewe nje, ndipo Sendeka alipokurupuka na kumgongea meza RC sambamba na kumfokea OCD.

RC alimuomba kwa sauti ya chini Sendeka atulie lakini aliendelea kumfokea RC ndipo akaomba Sendeka atoke nje.

Nimeanza kwa kusema kuwa usilolijua ni usiku wa giza, watu wengi wakiwemo na wadau wa Jamii Forums hawamfahamu Sendeka zaidi ya kumuona ITV na kumsoma katika magazeti ya IPP, nendeni katika jimbo lake ndipo mtamjua Sendeka ni mtu wa aina gani? Ni mfanya vurugu, hamuheshimu yeyote, ni mbabe asiye na chochote kichwani, elimu yake ni duni na ndicho kinachomponza. Si mchambuzi wa mambo na mvivu wa kufikiria sana, kwani angeweza kufikiri haraka kabla ya kumshambulia RC kwa maneno.

Na ni mara ya pili hii Sendeka anamkosea adabu Shekifu. Na sioni sababu ya kumtaja Lowasa kwa kila baya linalofanywa na Sendeka!!!!!!!!!!
 
Usilolijua ni usiku wa giza!!!

Sendeka hana adabu hata kidogo na wala hajafunzwa kwao kuheshimu wakubwa wake. Kikao kile kiliitishwa na RC kwa ajili ya kuzungumza na wananchi wa kijiji cha Sukuro, na kulikuwa na mkutano wa hadhara lengo ni kuhusu ugawaji wa vitongoji wa kata ya Sukuro, ambao sasa ina vijiji viwili Sukuro na Kitiangare.

Sendeka hakubaliki katika kijiji cha Sukuro hivyo aliandaa watu kutoka kijiji cha Kitiangare kuja kufanya vurugu, wakati RC anaongea mtu mmoja wa Sendeka akafanya vurugu, RC akaomba atolewe nje, ndipo Sendeka alipokurupuka na kumgongea meza RC sambamba na kumfokea OCD.

RC alimuomba kwa sauti ya chini Sendeka atulie lakini aliendelea kumfokea RC ndipo akaomba Sendeka atoke nje.

Nimeanza kwa kusema kuwa usilolijua ni usiku wa giza, watu wengi wakiwemo na wadau wa Jamii Forums hawamfahamu Sendeka zaidi ya kumuona ITV na kumsoma katika magazeti ya IPP, nendeni katika jimbo lake ndipo mtamjua Sendeka ni mtu wa aina gani? Ni mfanya vurugu, hamuheshimu yeyote, ni mbabe asiye na chochote kichwani, elimu yake ni duni na ndicho kinachomponza. Si mchambuzi wa mambo na mvivu wa kufikiria sana, kwani angeweza kufikiri haraka kabla ya kumshambulia RC kwa maneno.

Na ni mara ya pili hii Sendeka anamkosea adabu Shekifu. Na sioni sababu ya kumtaja Lowasa kwa kila baya linalofanywa na Sendeka!!!!!!!!!!

Hata wewe ni mtu wa Lowassa tu..... hata na Shekifu..... ni mtandao wa mafisadi nyie
 
Hata wewe ni mtu wa Lowassa tu..... hata na Shekifu..... ni mtandao wa mafisadi nyie
mkuu tuache makundi kwenye hili sendeka kama ameteleza basi na tunaompenda lazima tumwambie aisee... he needs to calm down a bit!

tutapata ukweli very soon
 
Nimeanza kwa kusema kuwa usilolijua ni usiku wa giza,watu wengi wakiwemo na wadau wa jamii forum hawamfahamu sendeka zaidi ya kumuona ITV na kumsoma katika magazeti ya IPP,nendeni katika jimbo lake ndipo mtamjua sendeka ni mtu wa aina gani?ni mfanya vurugu ,hamuheshimu yeyote,ni mbabe asiye na chochote kichwani,elimu yake ni duni na ndicho kinachomponza si mchambuzi wa mambo na mvivu wa kufikiria sana,kwani angeweza kufikiri haraka kabla ya kumshambulia RC kwa maneno,na ni mara ya pili hii sendeka atamkosea adabu Shekifu.Na sioni sababu ya kumtaja lowasa kwa kila baya linalofanywa na sendeka!!!!!!!!!!

Kwa jinsi ulivyomwelezea Ole Sendeka nashindwa kukuamini. Inawezekana ni kweli ana mabaya lakini kitendo chako cha kuelezea mabaya yake tu na kwa makusudi kuacha mazuri yake inatia shaka. Kwa maana ya kazi aliyotumwa na wananchi pale bungeni sina shaka ole Sendeka anafanya kazi nzuri kupita wabunge wengi tu ninaowafahamu hasa ukizingatia anatoka chama tawala. Kwa kifupi mimi namwona kama mmoja kati ya wabunge wa ccm wenye ujasiri
 
mkuu tuache makundi kwenye hili sendeka kama ameteleza basi na tunaompenda lazima tumwambie aisee... he needs to calm down a bit!

tutapata ukweli very soon

De Novo!
Pamoja na Sendeka kuwa mbabe Lowassa amezidi kumwandama. Laiti ungejua mkakati wa Lowassa kuelekea uchaguzi wa 2010 na 2015..... Ni kwanini autafute urais kwa nguvu namna hii? Yaani yeye kaamua kila anayemwona ni kikwazo kwa yeye kupata urais 2015 amshugulikie mapema....!!!
 
usilolijua ni usiku wa giza!!!Sendeka hana adabu hata kidogo na wala hajafunzwa kwao kuheshimu wakubwa wake.sendeka hakubaliki katika kijiji cha sukuro hivyo aliandaa watu kutoka kijiji cha kitiangare kuja kufanya vurugu,wakati RC anaongea mtu mmoja wa sendeka akafanya vurugu,RC akaomba atolewe nje,ndipo sendeka alipokurupuka na kumgongea meza RC sambamba na kumfokea OCD,RC alimuomba kwa sauti ya chini sendeka atulie lakini aliendelea kumfokea RC ndipo akaomba sendeka atoke nje.Na sioni sababu ya kumtaja lowasa kwa kila baya linalofanywa na sendeka!!!!!!!!!!

Hili tupate mtiririko mzuri please toa ufafanuzi wa vurugu aliyoifanya huyo "mtu mmoja" na zingatia kutofautisha suala la mtu kupinga/kueleza/kutoa hoja tofauti(freedom of speech) na ya mkuu na vurugu. Heshima ya uoga na wananchi kutojua haki zao ndivyo vitu vinavyolifanya taifa hili liendelee kuwa hovyohovyo.
 
usilolijua ni usiku wa giza!!!Sendeka hana adabu hata kidogo na wala hajafunzwa kwao kuheshimu wakubwa wake.kikao kile kiliitishwa na RC kwaijili ya kuzungumza na wananchi wa kijiji cha sukuro,na kulikuwa na mkutano wa hadhara lengo ni kuhusu ugawaji wa vitongoji wa kata ya sukuro,ambao sasa ina vijiji viwili sukuro na kitiangare,sendeka hakubaliki katika kijiji cha sukuro hivyo aliandaa watu kutoka kijiji cha kitiangare kuja kufanya vurugu,wakati RC anaongea mtu mmoja wa sendeka akafanya vurugu,RC akaomba atolewe nje,ndipo sendeka alipokurupuka na kumgongea meza RC sambamba na kumfokea OCD,RC alimuomba kwa sauti ya chini sendeka atulie lakini aliendelea kumfokea RC ndipo akaomba sendeka atoke nje.Nimeanza kwa kusema kuwa usilolijua ni usiku wa giza,watu wengi wakiwemo na wadau wa jamii forum hawamfahamu sendeka zaidi ya kumuona ITV na kumsoma katika magazeti ya IPP,nendeni katika jimbo lake ndipo mtamjua sendeka ni mtu wa aina gani?ni mfanya vurugu ,hamuheshimu yeyote,ni mbabe asiye na chochote kichwani,elimu yake ni duni na ndicho kinachomponza si mchambuzi wa mambo na mvivu wa kufikiria sana,kwani angeweza kufikiri haraka kabla ya kumshambulia RC kwa maneno,na ni mara ya pili hii sendeka atamkosea adabu Shekifu.Na sioni sababu ya kumtaja lowasa kwa kila baya linalofanywa na sendeka!!!!!!!!!!

nafikiri si vibaya nikisema sendeka ni mpenda sifa, unajua duniani kuna watu wanafiki wanaopenda kufanya jambo ili waonekana na kusifiwa na watu. mwangalie tu hata anapotoa hoja bungeni, utakuta imekaa kisifasifa fulani hivi, ama kama vile ana bifu na mtu, nafikiri mtu mzima anaitwa mtu mzima kwa kufikiria kwanza kabla ya kufanya jambo lolote lile, ukiona mtu anafyatuka tu kufanya jambo kubwa bila kufikiri kwanza madhara yake,mtu huyo huitwa ana akili za kitoto. wabunge wengi kwasasa wanataka kutetea jimbo, hivyo watafanya chochote kile ilimradi wananchi wawaone kuwa wanawafaaa. si huyu jamaa likuwa na kesi kule arusha? ni aibu, unajua ktk nchi zingine ukiona mbunge au kiongozi anakuwa mgomvi, hiyo ni sababu tosha ya kujiuzuru aondoke kabisa, kwasababu anafundisha wananchi wake kuwa matumizi ya ubabe ndo solution. vijana wetu wanapata fundisho gani hapo, na kwanini watu wazima kuaibishana mbele za watu? jambo gani kubwa kiasi hicho hadi watake kuzipiga? hatutaki image kama hii tz. watz wote tukiwa kama yeye si tutakuwa kama kenya au congo? what kind of image does this mbunge anatuletea watz hapa, tuwe wafanya fujo?
 
Bila shaka wakati huu hakuna kulala kule Umasaini -- kuna communication kali kati ya EL na huyo RC, akimshawishi amwekeOS ndani au amfungulie mashitaka ya jinai. Polisi, kama kawaida wao kuwasujudia hawa maRC badala ya kusimamia haki, watafata amri na kumkamata. Kumbukeni hilo jim bo la Simanjro linatakiwa kupokonywa kutoka kwa OS.
 
macho mbidiliko huyo lowasa alikufanyanyia nini???????sendeka hafai hata nusu sekunde na hana zuri lolote alilofanya,angekuwa na familia tungemuuliza mkewe labda,lakini hata mke hana huyo ana watoto tu!!!!na siku zote huficha hekima zake na kuonyesha upumbavu wake,na kusema kuwa huwa anawasaidia wananchi wa simanjiro si kweli hakuna alilofanya kwa waliompa kura hata moja!!!jamani'' USILOLIJUA NI USIKU WA GIZA''.Sendeka ana akili finyu lakini mwili mkubwa!!!!!
 
Nakubaliana na wote wanaosema kuwani stahili kwa viongozi hawa wa CCM kupigwa makofi ikibidi, kwani wanaudhi mno. Kuna haja ya kuyataja maudhi wanayofanya kwa Watanzania? Narudia kusema CCM itarudishwa madarakani kwa sababu this country has flocks of sheep instead of humans! Vinginevyo sioni kwa nini serikali ya kifisadi irudishwe madarakani.
 
macho mbidiliko huyo lowasa alikufanyanyia nini???????sendeka hafai hata nusu sekunde na hana zuri lolote alilofanya,angekuwa na familia tungemuuliza mkewe labda,lakini hata mke hana huyo ana watoto tu!!!!na siku zote huficha hekima zake na kuonyesha upumbavu wake,na kusema kuwa huwa anawasaidia wananchi wa simanjiro si kweli hakuna alilofanya kwa waliompa kura hata moja!!!jamani'' USILOLIJUA NI USIKU WA GIZA''.Sendeka ana akili finyu lakini mwili mkubwa!!!!!

Nitaingilia hapa: Mimi kwa mfano, huyo EL alin iharibia biashara yangu baada ya kukosekana kwa umeme kmwa miezi kadha kutokana na kuidhinisha kwake mkataba wa wa kjifisadi wa kufua umeme. Hilo moja linatosha kumchukia huyu mtu saaaana!!!!!! Alijiuzulu kwa aibu baada ya kuwa cornered na Bunge. Namchukia sana.
 
Shekifu ajue kuwa Olesendaka anaingia mjengoni kuzitunga hizo sheria , kwa maana hiyo zi simpe kiburi kwa mtindo wowote ule.
Tupe kisa basi mbona ipo ki aina fulani hivi hii story au bado Lowasa anamtafutia kisa cha kumfanya asigombee ubunge tena?

Mimi nimeona hiyo habari TBC1. Kasheshe limeanza baada ya mwananchi mmoja kupingana na RC kuhusu mgawanyo wa vitongoji. Ndipo RC akatoa amri atolewe nje ya mkutano. Sendeka alianza kumtetea kwa sauti ya chini ila baada ya hapo ndio wakaanza kupandishiana na RC. Kweli Sendeka alionekana anagonga meza lakini hata RC alikuwa anatembeza vitisho. Ndipo wakubwa wa wawili wa polisi walipofika kwenye meza kuu na kuanza kuongea na Sendeka ambaye alisikika akisema kuwa ameamua kunyamaza. Na hapo hapo RC akaendelea kurusha maneno mazito mazito ya vitisho na kwamba anaweza kumsweka ndani (detention). Siwezi kusema nani kamkosea mwenzake ila kitendo walichofanya ni cha utovu wa nidhamu kwani hakukuwa na haja ya kuzusha kasheshe kama hilo kwenye mkutano. Hata hivyo nadhani hawa wakubwa wanatakiwa kupunguza vitisho vya matumizi ya dola.
 
Hiyo ni pressure inapanda, inashuka, inapanda, inashuka. Kama hujafanya la maana jimboni, hii miezi hii ni mwanaharamu. Waliopanda vizuri, wanasubiri kuvuna tu, hawa wengine wanasubiri kipigo.
 
Back
Top Bottom