Ole Sabaya anatetewa na Wananchi wasiokuwa na mihemko wala Visasi vya Siasa Uchwara za Jimbo la Hai. Acheni haki itendeke

zanku

Member
Jun 9, 2020
69
149
SABAYA ANASEMEWA NA WANANCHI WASIOKUWA NA MIHEMKO WALA VISASI VYA SIASA UCHWARA ZA JIMBO LA HAI

Kwanza nianze kwa ku- declare interest Mimi sijawahi kumwona ana kwa ana Dc Ole Sabaya bali nimeanza kumfatilia vema kipindi ametatua tatizo la utapeli lililowapata zaidi ya wanafunzi 500 wa Chuo cha ualimu Moshi kilichopo wilayani Hai, ambako mimi nilikuwa na mabinti zangu wiwili wanaosoma pale mmoja mwaka wa kwanza mwingine wa pili.

Tukio lile la urejeshaji wa ada zilizokuwa zimeibwa kitaalam kwa kutumia mifumo ya kibenki na kupelekea wanafunzi kupatiwa payslips zilizodurufiwa na wajanja wa benki fulani, mhasibu wa chuo na wakala wa benki zilisababisha upotevu wa takribani milioni 76, hapo ndio nilimjua Ole Sabaya baada ya kuingilia na kuhakikisha taasisi za wale wahusika zinazilipa deni lile, ndio ilifungua ukurasa wa mimi kujua huyu mtu ni very potential kwenye taifa letu.

Sasa twende kwenye mada, Nampongeza Rais Samia Suluhu kwa kutumia busara ya Kumsimamisha na kuruhusu uchunguzi wakujua pande zote mbili zinamasaibu gani, lakini wameibuka mahakimu walioamua kutoa hukumu zao jinsi waonavyo wao kutokana na machungu yao ya kisiasa mwaka 2020, imefikia hatua watu wamekodi kurasa za gazeti la Raia Mwema kuandika propaganda zao ili kushinikiza DC huyo aondolewe kazini kwa tuhuma za mitandaoni na chuki binafsi za matapeli aliowahi kuwashugulikia wakiongozwa na Cuthbert Swai.

Pili, Sabaya ametenda mambo mengi sana pale hai ya kudhibiti uhalifu ukitaka kujiridhisha pitia mtandao wa YouTube ushuhudie.

Katika kazi hizo amejizolea maadui wenye nguvu kwasababu aligusa matapeli wenye connection na fedha, pia amejizolea kundi kubwa la wanyonge wasiokuwa na connection kubwa ya kusema katika mitandao na wasiokuwa na uwezo wa kununua kurasa kwenye magazeti, hivyo vita hapa inachezeshwa kitaalamu sana ambapo wanasiasa wenye visasi wamelitafuta lile kundi la matapeli na kulipa mbinu na kulisogeza kwa wataalam wa propaganda ili lijaribu kulipa kisasi na kuwasaidia wanasiasa hao walau kuhema maana ilikuwa hali mbaya kwao endapo Sabaya angeendelea ku-exists katika ukanda wao.

Mimi binafsi siingilii siasa zao zilizopita bali nawakumbusha tu wenye mamlaka kuwa Ole Sabaya anayomakundi mawili alioyatumikia kwanini linasikilizwa kundi lililojiungamanisha na wanasiasa wenye chuki na visasi?

Kwanini kundi la wananchi waliotendewa haki halipewi kipaumbele? Au kwa kuwa halina uwezo wa kuajiri wapika majungu wa kuandika mitandaoni? Au kwa kuwa halina uwezo wa kulipia kurasa za magazeti za kuandika mema ya mtu wao?

Tatu, kuna kundi limetokea likijaribu kudhibiti Sabaya asipate utetezi kabisa mahali popote hii ilianza siku alipohojiwa clouds Tv na sasa hawataki watu wamsemee mema aliofanya, wamefika hatua wanadai utetezi juu ya sabaya unaratibiwa na mwenyewe?

Hahaha inachekesha, Mtu mnaesema amekamatwa yuko lokapu anaweza vipi kuratibu masuala ya nje? Kwa waliowahi ingia lupango wanafahamu kuwa hilo ni ngumu mno kutokea, Nyie andikeni mlivyoagizwa na mabosi wenu kuandika lakini acheni demokrasia ya watu wengine kuandika iwepo.

Msimpangie Rais Samia, anaclear doubts zenu juu ya Sabaya msi-take advantage ya kumpangia matokeo ya uchunguzi yaweje, acheni maombi yetu wanyonge yatende kazi ya kufuta uongo za uzandiki mlioutengeneza kwa muda mrefu.

Kumbukeni Kila penye Ukweli, Uongo hujitenga Pembeni. Utafika wasaa wa Uongo kujitenga na ukweli utajidhihirisha, Kwa maana Uongo Unasafiri maili nyingi kwa Kwenda duniani Kabla Hata Ukweli Haujaamka. Ni suala la Muda tu.

Wasalaam Anatory Massawe.
 
Bank ya dunia wasingetangaza Tanzania imefika uchumi wa kati tungedanganywa sana na wapuuzi chadema kama wewe.
 
SABAYA ANASEMEWA NA WANANCHI WASIOKUWA NA MIHEMKO WALA VISASI VYA SIASA UCHWARA ZA JIMBO LA HAI

Kwanza nianze kwa ku- declare interest Mimi sijawahi kumwona ana kwa ana Dc Ole Sabaya bali nimeanza kumfatilia vema kipindi ametatua tatizo la utapeli lililowapata zaidi ya wanafunzi 500 wa Chuo cha ualimu Moshi kilichopo wilayani Hai, ambako mimi nilikuwa na mabinti zangu wiwili wanaosoma pale mmoja mwaka wa kwanza mwingine wa pili.
unahaki ya kumtetea
 
Sijasoma andiko lako lote ila kwa heading naona kama umeongea vyema, ila umesahau kuchukua ushauri wako mwenyewe (kuacha uchunguzi / haki itendeke) naona kama unamtoa kwenye hatia kabla ya uchunguzi
 
Chadema ni genge la majambazi na wahalifu. Ole Sabaya alilijua hilo na ndio maana kama Mwenyekiti wa Kamati Ulinzi na Usalama wa Wilaya alipambana nao kisawasawa. Hasira za kushughulikiwa wamezihamishia mitandaoni na magazeti uchwara! Hawatashinda!
 
Ki kawaida MABAYA hufuta yale yote MAZURI

Nikupe mfano Muigizaji wa prison break alipendwa sana na wadau wa tansina ya maigizo ya action hapa Tz, lkn alipokuja kujitangaza kama shoga alipoteza umaarufu wake kwa kasiiiii
Mwambieni Cuthbert swai, mbowe na lema ,Sabaya ni level ingine
 
Back
Top Bottom