Ole Naiko: Mnatuonea watu wa Monduli

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,474
39,987
Habari Leo

MKURUGENZI wa Kituo cha Uwekezaji (TIC) Emanuel Ole Naiko, ameituhumu Kamati Teule ya Bunge kwa kumhusisha na kashfa ya Richmond huku akisema anaamini ilifanya hivyo kwa nia ya kumkomoa kwa vile yeye ni mzaliwa wa Monduli.

Akizungumza jana, Ole Naiko alisema kulikuwa na njama za makusudi zilizokuwa zinafanywa na Kamati hiyo ya Bunge kumhusisha yeye, TIC na mkataba uliofanywa kati ya Serikali na kampuni hiyo ya kuzalisha umeme wa dharura ambao umelisababishia Taifa hasara ya mabilioni.

Katika mapendekezo yake yaliyowasilishwa bungeni mapema mwezi huu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge, Dk. Harrison Mwakyembe, alisema Mkurugenzi wa TIC na maofisa wengine walioshiriki katika kuipa upendeleo Richmond wawajibishwe kwani walitenda hivyo kinyume cha sheria.

Akizungumzia suala hilo jana, Ole Naiko alisema yeye binafsi alianza kuhisi kwamba kamati hiyo ilikuwa inamtafuta kumhusisha yeye na TIC katika sakata hilo baada ya kupokea barua ya pili ya kamati iliyomtaka awasilishe vitabu vyote vya wageni tangu mwaka 2006 hadi 2007.

“Barua hii ilinifanya nihisi kwamba kulikuwa na hila za kutuhusisha na sakata hilo,” alisema Mkurugenzi huyo na kuongeza kuwa “Nililazimika kumwandikia Katibu wa Bunge kulalamikia ‘summons’ za namna hiyo ambazo zilikuwa zinaonyesha nia mbaya ya kunitafutia kosa…sikujibiwa.”

Akichambua kile alichokiita nia mbaya ya kamati; Ole Naiko alisema alishtuka baada ya kamati hiyo kumwita ofisa mmoja wa kituo hicho kwa sharti kuwa asiijulishe menejimenti juu ya kuitwa kwake.“Sisi hatukuwa na la kuficha…mimi namwachia Mwenyezi Mungu suala hili.” Katika mazungumzo yake, Mkurugenzi huyo alirejea kauli iliyotolewa na Kiongozi mmoja wa Kanisa mjini Monduli mwishoni mwa wiki akitahadharisha kuwa Watanzania wasihusishe suala la Richmond na watu wanaotoka Wilaya ya Monduli.

Alisema hatari hiyo ni kujenga chuki kwa watu kutoka Monduli na nchi inaweza kutumbukia kwenye migogoro ya kikabila. Alisema kumhusisha Mmasai ama watu wa Monduli na Richmond itaifanya jamii ichukie baadhi ya wananchi kwa sababu tu wanatoka sehemu fulani ya nchi.

Huku akimnukuu Baba wa Taifa hayati Mwalimu Nyerere, Ole naiko alisema chuki za namna hiyo ni sawa na ‘mtu kula nyama ya mtu’ haishii hapo. “Kama nia ni kuondoa watu wa sehemu fulani ya nchi serikalini, tufanye hivyo kwa kuwatendea haki na siyo kuwajengea mazingira ya namna hii.”

Mkurugenzi huyo alisema shutuma kwamba TIC iliwapa upendeleo Richmond zimejengeka katika maswali ambayo mmoja wa wakurugenzi wa Richmond Naeem Gire, alipohojiwa na Kamati ya Bunge. Alisema maswali hayo yalilenga kudhihirisha kwamba Richmond ilipewa umuhimu pekee kuliko wawekezaji wengine jambo ambalo sio la kweli.

Hata hivyo aliongeza kuwa hakuna dhambi kwa kituo hicho kumpokea mwekezaji kama mfalme; “Sisi kwetu wawekezaji ni wafalme awe Richmond…ndio sababu tulipata tuzo ya dunia 2007 kwa kuwakaribisha wawekezaji.”

Ole Naiko alisema kituo chake kimesikitishwa na taarifa ambayo ilijaribu kuifanya jamii iamini kuwa kilipinda taratibu kuipa cheti cha uwekezaji kampuni ya Richmond. Alisema hakuna kosa lolote lile kwani wawekezaji hao walikwenda wakiwa wametimiza masharti yote yanayotajwa na sheria.

Vielelezo hivyo ni cheti cha usajili kilichotolewa na Msajili wa Makampuni (BRELA) cha Julai 12 2006, leseni ya biashara iliyotolewa na Wizara ya Viwanda, Biashara na Masoko, mpango wa biashara ulionyesha mchanganuo wa mradi, hati ya TRA inayoonyesha ilisajili kulipa kodi, fomu ya maombi yenye kiapo na barua ya benki na ushahidi kwamba wana fedha za kutekeleza mradi huo.

Alihoji, “baada ya mwekezaji huyo kusajiliwa na vyombo vingine vya serikali, TIC ingelikuwa na kigezo gani kuwachelewesha ama kuwafanyia ‘due diligence’ kuna tofauti gani kati ya TIC na hivyo vyombo vingine vilivyo wasajili? Mbona vyenyewe havilaumiwi?

Akionyeshwa kukerwa na shutuma za kamati kwa TIC, Ole Naiko alisema Mkataba wa Serikali na Richmond haujawahi kupokewa TIC wala hakukuwa na haja ya kituo hicho kupata mkataba huo kwani suala la mkataba linashughulikiwa na mamlaka nyingine. Alisema kama ni kosa kuipa cheti cha uwekezaji Richmond, basi kosa hilo haliwezi kuisha TIC bali kosa hilo litasambazwa kwa mamlaka zote zilizoipa Richmond usajili wa namna moja ama nyingine.
 
kwa hiyo anataka kusema kuwa kamati teule ya bunge ilikuwa na nia ya kuwaaibisha wote waliotoka monduli!!
naona anatumia mbinu mbaya ya kujivua lawama....ubaguzi na ukabila, coz anajua watu wapo sensitive na mambo hayo.
kama msomi he can do better than that!....na atafute njia nyengine za kujivua lawama na sio kutumia kivuli cha ukabila au uzawa.
 
"MKURUGENZI wa Kituo cha Uwekezaji (TIC) Emanuel Ole Naiko, ameituhumu Kamati Teule ya Bunge kwa kumhusisha na kashfa ya Richmond huku akisema anaamini ilifanya hivyo kwa nia ya kumkomoa kwa vile yeye ni mzaliwa wa Monduli."

1. Hivi TIC ni Ole Naiko?


"Akizungumzia suala hilo jana, Ole Naiko alisema yeye binafsi alianza kuhisi kwamba kamati hiyo ilikuwa inamtafuta kumhusisha yeye na TIC katika sakata hilo baada ya kupokea barua ya pili ya kamati iliyomtaka awasilishe vitabu vyote vya wageni tangu mwaka 2006 hadi 2007."

2. Hapa sijaelewa kitu kimoja. Aliitwa na kamati mara ya pili, je alikwenda hata mara moja kueleza anachojua juu ya Richie?

“Barua hii ilinifanya nihisi kwamba kulikuwa na hila za kutuhusisha na sakata hilo,” alisema Mkurugenzi huyo na kuongeza kuwa “Nililazimika kumwandikia Katibu wa Bunge kulalamikia ‘summons’ za namna hiyo ambazo zilikuwa zinaonyesha nia mbaya ya kunitafutia kosa…sikujibiwa.”

3. Summons zinawezaje kuwa na nia mbaya wakati zinakupa nafasi ya kujieleza kwa uhuru na kujisafisha? Kwa nini unaziogopa summons, na huzipendi?

4. I smell Lowassaism behind Naiko, whether he likes it or not.

5. Hii ya kusema Kamati inajenga chuki dhidi ya kabila la Wamasai au wanaotoka Monduli ni upuuzi unaoanzishwa na mlalamikaji...Ole Sendeka na waArusha wengine hawakuliona hilo, isipokuwa Naiko tu?
 
Naona mZee Ole Naiko yamemfika

OLE NAIKO////????

You are grown up, interlectual, matured, and respected person, PLS, PLS, usijaribu kutulazimisha tuamini ujinga wako. Simply tuambie umetumwa na mfisadi mwenzako EL kumkosha kwa kutumia silka ya ukabila. PLS shut up your MDOMO.
 
Hahaha,
Ujanja mzuri kabisa wa kukimbia kuwajibishwa. Kwanza, Mr.Ole Naiko unaonyesha ni jinsi gani unavyo amini ya kwamba Mbunge wa Monduli Mh. Lowassa is not guilty,Kama nia ni kuondoa watu wa sehemu fulani ya nchi serikalini, tufanye hivyo kwa kuwatendea haki na siyo kuwajengea mazingira ya namna hii
this sound so funny, why Dr. Mwakyembe ameue kuwashambulia wana wa Monduli Mr. Ole, what is so special with Mondoli people?

Huyu jamaa anajua kabisa ya kwamba yeye na wenzie wa TIC waliweza kuwapa vibali Richmond Development LTD pasipo kuchunguza financial statement zao, pasipo kuchunguza uwepo wao wa kikampuni, so Mr. Ole someone need to pay the price of that mistakes and unfortunately ni wewe mwana wa Mondoli. Swali linakuja do we cared about your staments? no we dont care sababu hatujui how many fraud company umeshazisajili up to this moment. So, hizo idea zako ambazo EL amekupa nadhani haziwezi kufanya kazi, nenda katafute jingine la kuwaeleza watanzania.

Statement ya kudai kwamba yeye aliipa richmond green light sababu walikuja na tax ID kutoka TRA that is NON SENSE, kwani TIC hawana vigezo vya kuipitisha kuwekeza nchini. Swali ni moja tuu, did Richmond qualified to be investment company in Tanzania under TIC credentials? If the answer is no, then why didn't you denied their application? If the answer is yes, then why Dr Mwakyembe prove otherwise?

Unajua hawa waandishi wananiboa, how in the world unaweza kumsikiliza mtu akamwaga pumba zote pasipo kumrushia hard ball?
 
Unajua hawa waandishi wananiboa, how in the world unaweza kumsikiliza mtu akamwaga pumba zote pasipo kumrushia hard ball?

Huwa wanakwenda pasipo kujiandaa ama hawana details za subject na hivyo aidha wanaweza kujikuta wanauliza obvious questions ama wanabaki kimya na kusubiri wagawiwe press release na kwenda kuandaa habari ya gazeti. Lakini kwa mtu mwenye details za procedures wanazofuata investors wakati wanapopeleka applications zao TIC sidhani kama angekosa maswali ya kumkaba Bwana Naiko.

Halafu Naiko kuunganisha recommendations za Kamati ya Mwakyembe na watu wa Monduli ni ufinyu wa fikra. Alitakiwa kujitetea pasipo kusema kwamba walikuwa wakimlenga yeye kwa kuwa anatoka Monduli. Ina maana akina Hoseah, Mwanyika, Karamaji, Msambaa, Mwakapugi, Mrindoko na wengineo wote wanatoka Monduli? Hapo ndipo unapoona ufinyu wa watu katika kufikiria ama kujionyesha wazi kwamba wana walakini katika utendaji kazi wao.
 
“Barua hii ilinifanya nihisi kwamba kulikuwa na hila za kutuhusisha na sakata hilo,” alisema Mkurugenzi huyo na kuongeza kuwa “Nililazimika kumwandikia Katibu wa Bunge kulalamikia ‘summons’ za namna hiyo ambazo zilikuwa zinaonyesha nia mbaya ya kunitafutia kosa…sikujibiwa.”


This sounds, huyu jamaa is feeling that he is above the law, kwanini usingeenda kuwasikiliza, nadhani, baada ya kuwasikuliza ungepata melekeo wao wa kukuonea vzr zaidi na ungepata mengi tu ya kusema baada ya kuwaona

OLe Naiko ni walewale ambao wako madarakani muda mrufe sasa wanaona ni haki yao kuwepo hapo wakipata vitu kama huvi wanaanza kuongeea upuuzi mtupu tu kwassb hawajajiandaa kukaa bench na wanaanini wao ni watawala toka mbinguni

OLe Naiko tuna mengi ya kuongea juu yako, tafadhali huo ujinga unaotaka kuuleta WAUKABILA please baki nao, tuachie tanzania yetu
 
kwa hiyo anataka kusema kuwa kamati teule ya bunge ilikuwa na nia ya kuwaaibisha wote waliotoka monduli!!
naona anatumia mbinu mbaya ya kujivua lawama....ubaguzi na ukabila, coz anajua watu wapo sensitive na mambo hayo.
kama msomi he can do better than that!....na atafute njia nyengine za kujivua lawama na sio kutumia kivuli cha ukabila au uzawa.

Wana JF, hakika Ole Naiko amepofushwa na rushwa ya akina EL kiasi kwamba anajifanya hajui kuwa licha ya Dr Mwakyembe kuwa ni Mnyakyusa, yeye na kamati yake walisisitiza kwenye ripoti yao kuwa Arthur Mwakapugi, ambaye pia ni Mnyakyusa, ni mmoja kati ya watu waliozembea na wanastahili adhabu kali...halioni hilo ila tu analalamika kuwa Wamasai wanajengewa chuki loh jamani, kweli rushwa mwanaharamu...

Kutokana na mwendendo huu, wanachama wa Agenda 21 tutaweza kuwaorodhesha kirahisi.

Anayelalamika ukabila ndiye wa kwanza kuendekeza ukabila.
 
"MKURUGENZI wa Kituo cha Uwekezaji (TIC) Emanuel Ole Naiko, ameituhumu Kamati Teule ya Bunge kwa kumhusisha na kashfa ya Richmond huku akisema anaamini ilifanya hivyo kwa nia ya kumkomoa kwa vile yeye ni mzaliwa wa Monduli."

1. Hivi TIC ni Ole Naiko?


"Akizungumzia suala hilo jana, Ole Naiko alisema yeye binafsi alianza kuhisi kwamba kamati hiyo ilikuwa inamtafuta kumhusisha yeye na TIC katika sakata hilo baada ya kupokea barua ya pili ya kamati iliyomtaka awasilishe vitabu vyote vya wageni tangu mwaka 2006 hadi 2007."

2. Hapa sijaelewa kitu kimoja. Aliitwa na kamati mara ya pili, je alikwenda hata mara moja kueleza anachojua juu ya Richie?

“Barua hii ilinifanya nihisi kwamba kulikuwa na hila za kutuhusisha na sakata hilo,” alisema Mkurugenzi huyo na kuongeza kuwa “Nililazimika kumwandikia Katibu wa Bunge kulalamikia ‘summons’ za namna hiyo ambazo zilikuwa zinaonyesha nia mbaya ya kunitafutia kosa…sikujibiwa.”

3. Summons zinawezaje kuwa na nia mbaya wakati zinakupa nafasi ya kujieleza kwa uhuru na kujisafisha? Kwa nini unaziogopa summons, na huzipendi?

4. I smell Lowassaism behind Naiko, whether he likes it or not.

5. Hii ya kusema Kamati inajenga chuki dhidi ya kabila la Wamasai au wanaotoka Monduli ni upuuzi unaoanzishwa na mlalamikaji...Ole Sendeka na waArusha wengine hawakuliona hilo, isipokuwa Naiko tu?

huyu mtu obviously ni mpumbavu asiyeeelewa mambo. nimeisoma taarifa yake na kuna kipengele anajitetea kuwa richmond ni kampuni safi iliyofuata kanuni zote za kuwa mwekezaji.

swali hapa ni moja tu? kama kampuni haukusajiliwa marekani. ilileta certificate ipi ya incorporation? maana ili upate kibali cha uwekezaji lazima iwe ni kampuni iliyosajiliwa.

only a fool will not be able to see this and hence will seek to rely on the richmonduli syndrome!!!
 
Hivi hawa watu wanafikiri wananchi kuwa ni wajinga namna hiyo?

Lowasa alisema eti inaelekea watu wanautaka uwaziri mkuu! Huyu naye anasema watu kutoka monduli wanaonewa..nyie bwana kama mlizoea kuiba mali za wananchi sasa ni wakati wa kulipa.
Wakati mkisaini hiyo mikataba isiyo na kichwa wala miguu na kuiibia serikali mamilioni mnafikiri kuwa hamuwaonei wananchi?

-Wembe.
 
Uozo wa Richmonduli una very loong roots.Ulipitia pia TIC na sasa anajua chambua chambua inakuja na god father wake kesha tema mzigo na yeye anajua TIC si yake ndiyo maana anajaribu ku pre empty .Lakini pia tusiangalie upande mmoja tu wa Naiko .Yule ni Mtumishi wa Serikali kafikia hatua hiyo. Nawakumbusha kwamba JK na kundi lake wako bize kumsafisha Lowasa na sasa oneni men at work .
 
kwa hiyo anataka kusema kuwa kamati teule ya bunge ilikuwa na nia ya kuwaaibisha wote waliotoka monduli!!
naona anatumia mbinu mbaya ya kujivua lawama....ubaguzi na ukabila, coz anajua watu wapo sensitive na mambo hayo.
kama msomi he can do better than that!....na atafute njia nyengine za kujivua lawama na sio kutumia kivuli cha ukabila au uzawa.

Ole Naiko yuko ktk harakati za kumsafisha EL ili agombee urais 2015. Hawa si ndiyo waliokodi magari 200 kumpokea EL uwanja wa ndege? na wakaprint t-shirt za kusema shujaa EL. Watu kama hawa watakuja wengi tu kila mmoja kwa dizaini yake. Hii yote in kutapatapa tu na ukweli utabakia palepale.

Ila ninawasiwasi na mwenendo wa magazeti siku hizi yanajitahidi kuandika sana maoni ya upande wa mafisadi na kuyalemba.
 
"MKURUGENZI wa Kituo cha Uwekezaji (TIC) Emanuel Ole Naiko, ameituhumu Kamati Teule ya Bunge kwa kumhusisha na kashfa ya Richmond huku akisema anaamini ilifanya hivyo kwa nia ya kumkomoa kwa vile yeye ni mzaliwa wa Monduli."

1. Hivi TIC ni Ole Naiko?

2. Je alikwenda hata mara moja kueleza anachojua juu ya Richie?

3. Summons zinawezaje kuwa na nia mbaya

4. I smell Lowassaism behind Naiko, whether he likes it or not.

5. Ole Sendeka na waArusha wengine hawakuliona hilo, isipokuwa Naiko tu?


Hii ni mbinu chafu kabisa ya kujisafisha na Ufisadi, Suala ni Richmond na si Monduli. Huyu Naiko anataka kusema akina Karamangi na Msabaha wote ni watu wa Monduli? Sometimes wawe wanafikiria ni nini cha kuongea Publically.

Nafikiri hapa huyu Lowasa anajaribu kutumia Mbinu zozote na atatumia mbinu zozote hata kama ni chafu kutaka kurudi kwenye chati Jambo ambalo haliwezekani.

Kuwahusianisha watu wa Monduli na ufisadi haiwezekani, kama yeye Naiko kaamua kuungana na Lowasa waungane na si kuijumuisha Monduli na Ufisadi. Mbona Monduli kuna watu Mashujaa kama Marehemu Sokoine ambaye bado tunamkumbuka, Kumheshimu na Kumlilia na kama leo atafufuka tunaweza kumpa nchi na si hawa mafisadi wanaotafuta uongozi wa nchi kwa njia chafu na zisizofaa.


Hatutakubali kukaangwa kwenye mafuta yetu wenyewe, mmetuibia na sasa mnaanza kuleta hisia za ukabila.
 
ole naiko has a point,kama mwakyembe alitaka ku probe usajili mzima wa richmond lazima angetakiwa kuwahoji all licencing authority ambao ni HALMASHAURI YA JIJI[AFISA BIASHARA]-LESENI YA BIASHARA,MAMLAKA YA MAPATO-TAX CLEARANCE CERTIFICATE,BRELA,WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA - LESENI,BANK ILIYOMPA BARUA,WAKILI ALIYEMUAPISHA ets....tofauti na hapo tuache ushabiki..tu,TIC wao hutoa approval ya investment baada ya kuridhika na document za hao wengine...kama wao wamepitisha na mwekezaji ana meet requirement hawawezi kumnyima...

...sioni ubaya kwa aliyoyasema ole naiko..ameamua kusema ukweli ,wakitaka na yeye wamfukuze kazi!!! period!!!
 
OLE NAIKO,

Mfa maji haachi kutapatapa hadi anaishiwa nguvu na kuzama. kujitetea huko hata mtoto hawezi... na pia kutotambua madudu uliyofanya ktk sakata zima la kuwapa Certificate of Incentive wale RDC ni mapungufu ya akili nina mshaka hata hiyo kama uliipata kwa njia ya ufisadi.

Umeshafanya makosa SHARTI UHUKUMIWE kama mkosaji yoyote.

Hizo pesa zenu za ufisadi haziwapi daraja la 'UMUNGU'
 
Nitaendelea kuamini kuwa,watu ambao huwa wanakaa katika madaraka kwa muda hasa kwa nchi zetu hizi za kiafrika huwa wanadhani kwamba hakuna wengine wanaoweza kufanya hizo kazi wanazofanya. Moja kati ya vitu ambavyo Mwl.Nyerere alikuwa anakemea kwa nguvu zote ni ukabila,hivi statement za ukabila ni hatari sana kwa Taifa hili.
Ole Naiko,mtu msomi aliyewezakuaminiwa na nchi na kupewa kitengo muhimu anatoa pumba kama hizi,watanzania wanapata picha gani?Ni kiongozi aliyejaa ubinafsi na ukabila. Si ajbu ukakuta hapo kituo cha uwekezaji pamejaa wamasai aka wanamonduli? Maana kama DM anatoa maneno ya ubaguzi na ukabila,ujue hiyo ofisi ina ukabila sana na ubaguzi.
Lilo wazi,Ole Naiko ulichangia kwa kiasi kikubwa kwa kampuni hii kuweza kutuingiza mjini,mengi yamesemwa,unapaswa kuwajibika.
 
Habari Leo

Akizungumza jana, Ole Naiko alisema kulikuwa na njama za makusudi zilizokuwa zinafanywa na Kamati hiyo ya Bunge kumhusisha yeye, TIC na mkataba uliofanywa kati ya Serikali na kampuni hiyo ya kuzalisha umeme wa dharura ambao umelisababishia Taifa hasara ya mabilioni.


Mkurugenzi huyo alisema shutuma kwamba TIC iliwapa upendeleo Richmond zimejengeka katika maswali ambayo mmoja wa wakurugenzi wa Richmond Naeem Gire, alipohojiwa na Kamati ya Bunge. Alisema maswali hayo yalilenga kudhihirisha kwamba Richmond ilipewa umuhimu pekee kuliko wawekezaji wengine jambo ambalo sio la kweli.

Hata hivyo aliongeza kuwa hakuna dhambi kwa kituo hicho kumpokea mwekezaji kama mfalme; “Sisi kwetu wawekezaji ni wafalme awe Richmond…ndio sababu tulipata tuzo ya dunia 2007 kwa kuwakaribisha wawekezaji.”

Ole Naiko alisema kituo chake kimesikitishwa na taarifa ambayo ilijaribu kuifanya jamii iamini kuwa kilipinda taratibu kuipa cheti cha uwekezaji kampuni ya Richmond. Alisema hakuna kosa lolote lile kwani wawekezaji hao walikwenda wakiwa wametimiza masharti yote yanayotajwa na sheria.

Vielelezo hivyo ni cheti cha usajili kilichotolewa na Msajili wa Makampuni (BRELA) cha Julai 12 2006, leseni ya biashara iliyotolewa na Wizara ya Viwanda, Biashara na Masoko, mpango wa biashara ulionyesha mchanganuo wa mradi, hati ya TRA inayoonyesha ilisajili kulipa kodi, fomu ya maombi yenye kiapo na barua ya benki na ushahidi kwamba wana fedha za kutekeleza mradi huo.

Alihoji, “baada ya mwekezaji huyo kusajiliwa na vyombo vingine vya serikali, TIC ingelikuwa na kigezo gani kuwachelewesha ama kuwafanyia ‘due diligence’ kuna tofauti gani kati ya TIC na hivyo vyombo vingine vilivyo wasajili? Mbona vyenyewe havilaumiwi?

Akionyeshwa kukerwa na shutuma za kamati kwa TIC, Ole Naiko alisema Mkataba wa Serikali na Richmond haujawahi kupokewa TIC wala hakukuwa na haja ya kituo hicho kupata mkataba huo kwani suala la mkataba linashughulikiwa na mamlaka nyingine. Alisema kama ni kosa kuipa cheti cha uwekezaji Richmond, basi kosa hilo haliwezi kuisha TIC bali kosa hilo litasambazwa kwa mamlaka zote zilizoipa Richmond usajili wa namna moja ama nyingine.

TIC kazi yao ni ku-screen watu wote wanaojiita wawekezaji. TIC ikiridhia kuwa hawa Wawekezaji watafaa na wana credibility, dnipo wanapotoa leseni na mwekezaji atakwenda BRELA, TRA na kwingine kupata vyeti na usajili.

Huu ni upumbavu na utoto. Majibu yake ni ya kitoto sana na yanaonyesha ni jinsi gani alivyo dhaifu kiutendaji na hastahili kuwa mkuu wa Taasisi kubwa kama hiyo.

Kauli ya kusema "sisi wawekezaji ni wafalme" ina maana hata wakiambiwa wabong'oe watrainama na kubong'oa midhali mfalme kasema. Sasa kama Mteja ni mfalme, basi inamaana unatawaliwa na mteja/mwekezaji/mfalme na unafanya vitu kwa utashi wa Mfalme!

Who was the boss of TIC in when RDC came? Was it Sitta? and if we go back to 1996 as now Naiko wants to spin and bring back IPTL, who was the boss at TIC?

Aliyewapa hawa jamaa hati na kuwasilisha kabrasha lao BRELA, TRA ndiye alikuwa mhalifu nambari wani! Maana hakufanya uchunguzi wa kina kuhusu hii kampuni.

According to Houston Business Journal la September 11 1998, hawa kina Gire walikuwa ni printers, there is no single citation ya energy innitiative.

Sasa walipokuja, walikuja kama nani? wapiga chapa au wajenzi wa miundo mbinu?

Maana hawa Richmond mafundi Umeme hawakuanza kazi zao za Nishati mpaka mwaka 2001 au 2003 ikitegemeana ni upi ukweli (angalia maelezo yao ya overview kwa hizo linki mbili za Rdevco)!

I hope Naiko will have back up story maana he thinks everyone is Zobwe and he can pull a fast ball any minute he wants!

Mwambieni kama UwT wameshindwa kumpa habari kamili, Jambo Forum itamsaidia kupata habari sahihi!

http://www.bizjournals.com/houston/stories/1998/09/14/focus1.html
http://www.richmondprinting.com
http://www.rdevco.com/
http://www.rdevco.com/overview.html
 
Wakuu safi sana. Huyu kweli ni mpumbavu mtupu.Lakini si tunajua wapumbuvu haelewi hadi umkandamizie kwenye huo ubongo? Hebu tumweleze hivi.

1
.Aliharibu pale alipotoa cheti cha uwekezaji na wakapata tax exemption washikaji wa Richie huku akijua hiyo kampuni ilikuwa feki.​
hili ni kosa kubwa brother ,ebo.

2.Kamati ikiundwa na ukaitwa haina maana unatafutwa.ni kutaka kujua jambo kutokea upande wako.Kuhisi kuwindwa ni upuuzi tu.Nenda kasikilize kwanza .kwani hawakukuliza kwa nini ulitoa cheti kwa Richmund? Hawakukuliza ni nani au kampuni ya aina gani inastahili cheti cha taasisi yako?

3.Kwa kawida ukiletewa summons huwezi kuilalamika hiyo summons kabla hujaenda. Ndio maana katibu wa bunge hakukujibu.In maana hadi leo hujajua kwa nini hakukujibu? Kwani wewe ni mbunge?

5.Ikiwa wewe ni mkongwe hapo TIC ulishindwa vipi kuhakiki identity ya Ricmund hadi wakapewa cheti? Sasa huoni hicho cheti pia nacho ni feki ab initial .Kile cheti chako brother kiliwapa kichwa na mahali popote walikuwa wanakionyesha kwanza hicho kwa hiyo wengine wakaona ni kampuni fresh wala hawakuhangaika na registraion doc. ...Sijui hata kama linaingia kwenye huo ubongo Ah.

4. Mimi na wengine wote wala hatutaki kujua umetoka wapi.Kama wewe Mmasai au Mmeru hatutaki kujua .Unajipeleka huko mwenyewe Halafu kwanza , eti Kwani Lowasa ni Mmasai? kwani hujui Lowasa ni Mmeru by birth? Sasa wewe mmasai unajifanya mmeru halafu unatangaza Wameru tunaonewa and vise versa.Lol

5.Kuna watu safi huko Monduli lakini wewe ni mmoja wao? Kama mlicolude na Lowasa mzee usije ukasingizia Umondoli wenu sisi tunataka hoja ..toa point ...sio uongee upupu kinamna namna ili tukuonee huruma .Ulihusika na ni mmoja wao .Ukimkana Lowasa atatoboa yote siku akiwa kwa Pilato ...mahakamani. period
 
ole naiko has a point,kama mwakyembe alitaka ku probe usajili mzima wa richmond lazima angetakiwa kuwahoji all licencing authority ambao ni HALMASHAURI YA JIJI[AFISA BIASHARA]-LESENI YA BIASHARA,MAMLAKA YA MAPATO-TAX CLEARANCE CERTIFICATE,BRELA,WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA - LESENI,BANK ILIYOMPA BARUA,WAKILI ALIYEMUAPISHA ets....tofauti na hapo tuache ushabiki..tu,TIC wao hutoa approval ya investment baada ya kuridhika na document za hao wengine...kama wao wamepitisha na mwekezaji ana meet requirement hawawezi kumnyima...

...sioni ubaya kwa aliyoyasema ole naiko..ameamua kusema ukweli ,wakitaka na yeye wamfukuze kazi!!! period!!!

Huoni ubaya wa kupotosha maudhui ya kamati kuwa ni kushambulia kabila la Wamasai au wana Monduli?

Hujui kama ripoti ya kamati ilipendekeza kuboreshwa kwa BRELA?
 
Back
Top Bottom