Return Of Undertaker
JF-Expert Member
- Jun 12, 2012
- 4,572
- 26,868
KUNA JAMBO LA KUONGEA KAMA TAIFA HAPA.
Na Thadei Ole Mushi.
Niliwahi kuandika Mara Moja tu kuhusu uchaguzi wa Serikali za Mitaa. Niliandika Sababu ya watu kutokutaka kujiandikisha. Leo naomba niandike tena kidogo kuhusu uchaguzi huu.
Naandika haya nikiwa ni mwanaccm, naandika haya nikiwa ni Mtanzania. Kama kuna atakayesema Mimi sio ccm au sio mtanzania kwa nitakachoandika namruhusu tu kusema kwa kuwa ndio Uhuru wenyewe wa kujadiliana kwa mustakabali mpana wa Nchi yetu Mimi na wewe.
Naona kila siku wapinzani wanalalamika kuhusu kuonewa, kutokutendewa haki nk. Sijui ni kwa kiasi gani hawajatendewa haki lakini hebu tujadiliane kwa maslahi mapana ya Taifa letu. Kuna ujumbe nimeuona wa Askofu Bagonza, sijui chama chake lakini nimeona kama ana Mantiki katika alichokiongea.
Askofu Bagonza kuna jambo ambalo ameligusa kuwa Upinzani umesusiwa na kila Mtu, waandishi, viongozi wa dini, asasi za kiraia, Serikali yaani kila mtu kawasusia. Askofu Bagonza katumia neno "stigmatization" (the act of treating someone or something unfairly by publicly disapproving of them) kwa Lugha ya Kikwere ni hali ya kutomtendea haki tena na hadhara yaani kila mtu anakudharau.
HILI KWANGU NI LOGIC.
Hivi mnafikiri kwa nini Watu hujinyonga? mnafikiri kwa nn watu hujitoa mhanga? Chukulia mfano huu Binti aliyekuwa anasoma anapata ujauzito, nyumbani kila mtu akamtenga kuanzia baba, mama, ndugu zake nk. Akienda shuleni hadi marafiki wanamtenga kwa kifupi huyu anapata shambulio la kisaikolojia na kitakachotokea aidha atajidhuru au atadhuru wengine.
LOGIC
Najua kuna wana CCM hawatanielewa, anyway Mwanamikakati wa Jeshi la China Sun Tzu katika kitabu chake cha art of war aliwahi kusema " To a surrounded enemy, you must leave a way of escape" akiwa na maana kuwa usimbane adui kila pembe mpe nafasi ya kutoroka. Ukimbana kila pembe hatakubali kufa kirahisi atapambana kujiokoa na anaweza kukuletea madhara. Wakati mwingine hata kama adui una uhakika wa kumpiga mwachie nafasi ya kutoroka utakuwa umepata ushindi mkubwa bila kutumia nguvu.
SIKIA.
Sikuwahi kusoma Falsafa au Saikolojia kwa kiwango kikubwa sana, nilisoma katika ngazi za awali nikachepukia kwenye masomo ya ujalalani huku kwenye chaki na madaftari aliyokimbia Prof Kabudi ila nitawaambia kitu kidogo sana kwa mustakabali wa taifa hili Siku za usoni.
Kuna faida Kubwa sana ya wapinzani kutokuwatenga na kila kitu, wanapatwa ugonjwa wa Sonoma, Sijui ni kwa kiasi gani wametendwa kama wanasingizia au kweli wamefanya makosa ila kuna kila sababu ya kuwasikiliza, kuna kila sababu asasi za kiraia kuwasemea, kuna kila sababu ya viongozi wa dini kuwasemea nk.
Hii itatusaidia sisi CCM kushusha msononeko huo walionao, hili litasaidia kutokujidhuru au kudhuru wengine, hili litatuleta pamoja zaidi kama taifa, hili litatusaidia kutokuzaa vikundi vya uhalifu nchini, vikundi vya kujitoa mhanga, hili litatusaidia kuwachelewesha kwenye uasi kama watapata mtu wa kuwasemea.
Naandika haya kwa maslahi ya taifa sio chama wala mtu. CCM Msinichukie tujadili hii hoja kwenye vichwa vyetu.... Nishukuru maeneo ambayo yameanza kusikiliza baadhi ya malalamiko yao.
Karibu jalalani
Ole Mushi
0712702602
Na Thadei Ole Mushi.
Niliwahi kuandika Mara Moja tu kuhusu uchaguzi wa Serikali za Mitaa. Niliandika Sababu ya watu kutokutaka kujiandikisha. Leo naomba niandike tena kidogo kuhusu uchaguzi huu.
Naandika haya nikiwa ni mwanaccm, naandika haya nikiwa ni Mtanzania. Kama kuna atakayesema Mimi sio ccm au sio mtanzania kwa nitakachoandika namruhusu tu kusema kwa kuwa ndio Uhuru wenyewe wa kujadiliana kwa mustakabali mpana wa Nchi yetu Mimi na wewe.
Naona kila siku wapinzani wanalalamika kuhusu kuonewa, kutokutendewa haki nk. Sijui ni kwa kiasi gani hawajatendewa haki lakini hebu tujadiliane kwa maslahi mapana ya Taifa letu. Kuna ujumbe nimeuona wa Askofu Bagonza, sijui chama chake lakini nimeona kama ana Mantiki katika alichokiongea.
Askofu Bagonza kuna jambo ambalo ameligusa kuwa Upinzani umesusiwa na kila Mtu, waandishi, viongozi wa dini, asasi za kiraia, Serikali yaani kila mtu kawasusia. Askofu Bagonza katumia neno "stigmatization" (the act of treating someone or something unfairly by publicly disapproving of them) kwa Lugha ya Kikwere ni hali ya kutomtendea haki tena na hadhara yaani kila mtu anakudharau.
HILI KWANGU NI LOGIC.
Hivi mnafikiri kwa nini Watu hujinyonga? mnafikiri kwa nn watu hujitoa mhanga? Chukulia mfano huu Binti aliyekuwa anasoma anapata ujauzito, nyumbani kila mtu akamtenga kuanzia baba, mama, ndugu zake nk. Akienda shuleni hadi marafiki wanamtenga kwa kifupi huyu anapata shambulio la kisaikolojia na kitakachotokea aidha atajidhuru au atadhuru wengine.
LOGIC
Najua kuna wana CCM hawatanielewa, anyway Mwanamikakati wa Jeshi la China Sun Tzu katika kitabu chake cha art of war aliwahi kusema " To a surrounded enemy, you must leave a way of escape" akiwa na maana kuwa usimbane adui kila pembe mpe nafasi ya kutoroka. Ukimbana kila pembe hatakubali kufa kirahisi atapambana kujiokoa na anaweza kukuletea madhara. Wakati mwingine hata kama adui una uhakika wa kumpiga mwachie nafasi ya kutoroka utakuwa umepata ushindi mkubwa bila kutumia nguvu.
SIKIA.
Sikuwahi kusoma Falsafa au Saikolojia kwa kiwango kikubwa sana, nilisoma katika ngazi za awali nikachepukia kwenye masomo ya ujalalani huku kwenye chaki na madaftari aliyokimbia Prof Kabudi ila nitawaambia kitu kidogo sana kwa mustakabali wa taifa hili Siku za usoni.
Kuna faida Kubwa sana ya wapinzani kutokuwatenga na kila kitu, wanapatwa ugonjwa wa Sonoma, Sijui ni kwa kiasi gani wametendwa kama wanasingizia au kweli wamefanya makosa ila kuna kila sababu ya kuwasikiliza, kuna kila sababu asasi za kiraia kuwasemea, kuna kila sababu ya viongozi wa dini kuwasemea nk.
Hii itatusaidia sisi CCM kushusha msononeko huo walionao, hili litasaidia kutokujidhuru au kudhuru wengine, hili litatuleta pamoja zaidi kama taifa, hili litatusaidia kutokuzaa vikundi vya uhalifu nchini, vikundi vya kujitoa mhanga, hili litatusaidia kuwachelewesha kwenye uasi kama watapata mtu wa kuwasemea.
Naandika haya kwa maslahi ya taifa sio chama wala mtu. CCM Msinichukie tujadili hii hoja kwenye vichwa vyetu.... Nishukuru maeneo ambayo yameanza kusikiliza baadhi ya malalamiko yao.
Karibu jalalani
Ole Mushi
0712702602