#COVID19 Ole Millya apata chanjo ya Uviko-19; asema kama Rais Samia amechanjwa yeye ni nani asichanjwe

waziri2020

Senior Member
May 31, 2019
190
451
Mbunge mstaafu wa jimbo la Simanjiro mkoani Manyara, James Ole Milya leo Agosti 3 mwaka 2020 amechomwa chanjo ya Uviko -19 kama njia mojawapo ya kujikinga na ugonjwa huo hatari duniani.

Ole Milya amejipatia chanjo hiyo aina ya Jansen kutoka kampuni ya Johnson & Johnson katika hospitali ya mkoa wa Arusha ya Mt Meru ambapo aliambatana na baadhi ya wakazi wa jijini Arusha.

Akizungumza muda mfupi Mara baada ya kupatiwa chanjo hiyo Ole Milya alisema kwamba kwanza ameamua kuchanja kama njia mojawapo ya kujikinga na maradhi ya Uviko-19 .

Ole Milya alitaja sababu nyingine iliyomsukuma ni kumuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kupambana na janga la Uviko -19 duniani.

Ole Milya alisisitiza kuwa kama Rais Samia amepata chanjo hiyo yeye ni nani wa kuipinga na kuwataka watanzania kuondokana na hofu kwa kuwa Rais Samia ambaye alimtaja kuwa ni mfariji mkuu wa taifa(comforter in chief) alishawahakikishia kwa vitendo usalama wa chanjo hiyo.

"Kama Rais Samia amechanjwa Mimi ni nani wa kukataa?Mimi ni kiongozi ni lazima nionyeshe mfano kwa wengine wito wangu wa watanzania tuondoe hofu twende tukapate chanjo" alisema Ole Milya

Mwisho.
IMG_20210803_153520.jpeg
IMG_20210803_143050.jpeg
IMG_20210803_143121.jpeg
 
Kwa Hiyo RAIS Asingechanjwa na Yeye Asingechanja? Huyu Jamaa toka Akose UBUNGE akili imemfyatuka
20210716_160047.jpg
 
wenye magonjwa ya;
1.KISUKARI
2.SARATANI
3.UKIMWI
3.TB
4.PRESHA
wapo kwenye hatari kubwa sana ya kupoteza maisha tuchukue tahadhari, piga chanjo, vaa barakoa, nawa mikono, epuka mikusanyiko.
 
wenye magonjwa ya;
1.KISUKARI
2.SARATANI
3.UKIMWI
3.TB
4.PRESHA
wapo kwenye hatari kubwa sana ya kupoteza maisha tuchukue tahadhari, piga chanjo, vaa barakoa, nawa mikono, epuka mikusanyiko.
Safi sana mbunge wetu jamani umeonyesha mfano tunakupenda sana Milly, karibu simanjiro
 
Back
Top Bottom