soine
JF-Expert Member
- Nov 22, 2010
- 2,113
- 2,329
We sio mtu huru wa kufanya uchambuzi huru kwahiyo sisi wengine tunakupuuza tu.
No wonder japo wewe ni mwanahabari, siku hizi uko kimya kabisa kuhusu uminywaji wa uhuru wa vyombo vya habar na ni wazi wewe ukipewa uwaziri wa habari, utakandamiza sana media na hata hii JF unaweza kuigeuka
Mtu mwenye akili timamu,alie-civilised hawezi kuwa-influenced na maendeleo ya vitu kiasi cha kupuuza kukosekana kwa utu kunakofanywa au kufumbiwa macho na watawala.
Pia jiulize hayo maendeleo ya vitu, yote ni vipaumbele sahihi na yanafanywa kwa kuzingatia taratibu na sheria za nch?
Kwa kifupi,uko biased kwa malengo yako binafsi na nyinyi ndio aina ya watu ambao Bwana yule anapenda kufanya nao kazi.
Mwisho:Siku ukipewe uteuzi,usisahau kuishukuru JF.
Kaka Pascal naomba nikuambie tu kuwa waweza kuwa na akaunti ya benki iliyojaa pesa, ukawa na miradi mingi sana na kila kitu cha ufahari. Ila unapokosa amani na furaha ndani ya maisha yako, hizo mali zote ni hazina maana, ni karaha tu.
Amani kwanza.
Hata maandiko yanasema utafuteni kwanza ufalme wa mbinguni na mengine yote mtazidishiwa.