Oktoba 28 ni mashindano kati ya Reality vs Ahadi Hewa? Je, Watanzania watachagua nini kati ya visible, tangible Deliverables vs The Empty Promises?

We sio mtu huru wa kufanya uchambuzi huru kwahiyo sisi wengine tunakupuuza tu.

No wonder japo wewe ni mwanahabari, siku hizi uko kimya kabisa kuhusu uminywaji wa uhuru wa vyombo vya habar na ni wazi wewe ukipewa uwaziri wa habari, utakandamiza sana media na hata hii JF unaweza kuigeuka

Mtu mwenye akili timamu,alie-civilised hawezi kuwa-influenced na maendeleo ya vitu kiasi cha kupuuza kukosekana kwa utu kunakofanywa au kufumbiwa macho na watawala.

Pia jiulize hayo maendeleo ya vitu, yote ni vipaumbele sahihi na yanafanywa kwa kuzingatia taratibu na sheria za nch?

Kwa kifupi,uko biased kwa malengo yako binafsi na nyinyi ndio aina ya watu ambao Bwana yule anapenda kufanya nao kazi.

Mwisho:Siku ukipewe uteuzi,usisahau kuishukuru JF.

Kaka Pascal naomba nikuambie tu kuwa waweza kuwa na akaunti ya benki iliyojaa pesa, ukawa na miradi mingi sana na kila kitu cha ufahari. Ila unapokosa amani na furaha ndani ya maisha yako, hizo mali zote ni hazina maana, ni karaha tu.

Amani kwanza.

Hata maandiko yanasema utafuteni kwanza ufalme wa mbinguni na mengine yote mtazidishiwa.
 
Swali fikirishi: Je, kuna mtu timamu kiakili atamchagua John Magufuli kwenya uchaguzi wa 2020
NAHITAJI MAJIBU
Mkuu, Kodi ya Kireativiti, kabla ya kujibu swali lako, pitia hoja za bandiko hili, yaani mtu mwenye macho, na anaona kilichofanyika, halafu akachague ahadi hewa?, nani hapo atakuwa hana akili timamu?.

Kiukweli nimeguswa sana na uchapakazi wa Rais Magufuli!. Je, kuna uhusiano kati ya kabila la mtu, na uchapakazi wake?. Je, 2020 kuna haja ya...

Kwa Kasi hii ya Magufuli, kuna haja Kufanya Uchaguzi wa Rais 2020?

Magufuli is Doing Good For This Nation, Tumuassess kwa Positive Attitude, Kwa Mazuri Tumpongeze, Tumuunge Mkono Kumsupport, lakini kwa Mabaya Tumkosoe

Magufuli is Getting Better and Better, He is Changing for The Better!. Hongera Sana!

Rais Magufuli, so far, is the best president this country has ever had. Msikivu, ana upendo na huruma. Atabarikiwa sana. Tanzania itabarikiwa!

Kama umezipitia na una akili timamu, hakuna mtu Mtanzania mzalendo mwenye akili timamu, ataacha kumchagua Dr John Pombe Magufuli!.

Tarehe 28 ni kazi moja tuu!, unachukua, unaweka...

P
 
Kanda ya Ziwa wanaenda na mtoto wao piga, ua garagaza, isistoshe hata kura za huruma Kanda ya Ziwa chadema haipati kwa maana Tundu Lisu katumia muda wake mwingi kumtukana na kumdhalilisha mwana wao JPM, hivyo ondoa kichwani na akilini kwako kabisa hilo, kwanza Tundu Lisu hata kwao Singida hatopata kura za kutosha, kura pekee chache Tundu lisu atakazopata ni labda za wanafunzi wa sheria tena siyo wote, huyo jamaa mmejitwisha zigo la mwiba, ...
Huyo mtu wenu sio Msukuma..watu wamekesha hotelini kwa Lissu Geita..jamaa arudi kwao tu
 
Suala hapa sio 'visible tangible ...whatever', suala ni at whose, LIFETIME, COST?
JINSI MAGUFULI ANAFANYA MAMBO, TUTABAKI NA MASHIMO MATUPU ILIPOKUWA MIGODI, MIUNDOMBINU YA KUKATA SHOKA NA RAIA MAFUKARA WA KUTUPWA WASIO NA MITAJI NA, END OF THE DAY, ANARCHY!
 
Wasaliti wa Nchi Lissu atapigiwa kura na robert tu
Sisi Watanzania tuliowengi tutamchagua Rais Magufuli kipenzi cha Watanzania
 
Zimebaki siku 18, tuingie kwenye mechi kati ya matekelezo vs ahadi hewa!.
P
Kaka siku hizi umekuwa kama kalai,kwani huyo unayemsema utekelezaji 2015 si alikuwa na ahadi hewa pia?
1.Tunataka atleast mtu anayetuahidi kuhusu haki na uhuru huyu mwingine hayo hayasemi kabisa
2.Uku mwingine akisema ataongeza mishahara huyu mwingine hasemi kabisa
3.Uku mwingine akiahidi kurejesha makato ya bodi ya mikopo kule 8% tulikokuwa badala ya hii 15%huyu mwingine hasemi kabisa
4.Uku mwingine akiahidi kurejesha fao la kujitoa huyu mwingine hasemi kabisa
5.Uku mwingine akiahidi kurejesha ule mfumo wa kikokotoo uyu mwingine anasema 2023 kikokotoo kipya kitatumika.

SASA MKUU SI BORA UMPE KURA ZAKO YULE AMBAYE ANGALAU ANASEMEA HAYO,NGOJA 28 TUKAONESHANE MAKALI.
 
Kila mtu atajinadi kwa anayoenda kufanya na siyo yaliyofanyika. Yaliyofanyika hata kama yalikosewa huwezi kuyabomoa tena. Pia hayatasaidia chochote kile kwenye uchaguzi maana ni kazi lazima serikali iliyopo izifanye. Mtu akija na porojo za eti nilifanya au tulifanya nitamuona mjinga wa aina yake.

Pia naomba uelewe kuwa katika uongozi huwa tunaangalia "extra ordinary"
Sasa alichofanya Magufuli ni mambo ya kawaida ambayo hata wewe Mayalla pamoja na njaa zako ukipewa uongozi unayafanya. Kitu cha ajabu sana alichofanya Magufuli ni kuwanyanyasa wasio wanyonge hasa wasomi na wafanya kazi! Hilo kulifanya inakuhitaji uwe na roho Jiwe!

Sasa kama watanzania watamchagua kwa maajabu hayo ya roho jiwe ni wao ila kujenga sijui barabara kwa kufyeka haki za msingi za watumishi na wawekezaji halafu ukajisifia ni jambo la KIPUMBAVU na linafanywa na WAPUMBAVU waliopitiliza!

Halafu siku hizi una hoja za akili ndogo sana mkuu, uccm usikulemaze kiasi hicho.

Halafu pia ulinikera ulivyoandika eti "Wapo watu wenye nia ya kugombea ubunge kwa dhati ya kumsaidia Magufuli"
Naomba nikueleze kuwa kazi ya bunge siyo kumsaidia Magufuli, kazi ya bunge ni kusimamia na kuiongoza serikali iliyopo madarakani. Kuza akili yako mzee, uccm usikulemaze kiasi hicho!
Well said
 
Zimebaki siku 18, tuingie kwenye mechi kati ya matekelezo vs ahadi hewa!.
P
Paskali ameona isiwe shida" if you can't defeat them join them" amewakosoa mwishowe wakamuita Bungeni wakamchimba mkwara, kaufyata kaona isiwe taabu kaungana nao! Kasahau kwamba mwandishi mwenzake Azory alitekwa na hajulikani alipo. Ila nimekumbuka aliambiwa Mayalla maana yake ni Njaa, huenda njaa imehamia kichwani kama ya Polepole,"nimewanukuu Jpm na Lipumba"
 
Suala hapa sio 'visible tangible ...whatever', suala ni at whose, LIFETIME, COST?
JINSI MAGUFULI ANAFANYA MAMBO, TUTABAKI NA MASHIMO MATUPU ILIPOKUWA MIGODI, MIUNDOMBINU YA KUKATA SHOKA NA RAIA MAFUKARA WA KUTUPWA WASIO NA MITAJI NA, END OF THE DAY, ANARCHY!
 
Back
Top Bottom