Uchaguzi 2020 Oktoba 2020 - Hali inaonesha Magufuli kushinda kwa zaidi ya asilimia 90, wabunge na madiwani wakutosha

Environmental Security

Senior Member
May 21, 2020
181
261
Kama tunavyofahamu kuwa mwaka huu ni mwaka wa uchaguzi, na kama ilivyo katika chaguzi zilizopita, hali ya hewa huwa inaanza kujulikana mapema kwa kuzingatia mambo mbalimbali, kwa kuanzia na utekelezaji wa ahadi, kukubalika kwa wagombea, uimara wa chama hadi kufikia kipindi cha uchaguzi ikiwemo pamoja na mambo mengine.

Kama ilivyo kawaida tayari hali katika mitaa, vijiji, kata, wilaya na mikoa, inaonesha kuwa Rais wetu mpendwa ndugu. John Pombe Joseph Magufuli ataashinda kwa idadi kubwa sana ya kura, na hii inatokana na uungwaji mkono mkubwa sana alionao kutoka kwa waTanzania wa kada mbalimbali. Hii ni kutokana na ukweli kwamba kasi yake katika kuleta maendeleo na kushughulikia changamoto mbalimbali za kitaifa hadi za watu binafsi katika ziara zake, lakini pia jinsi ambavyo ameshughulikia janga la corona ambapo amezingatia sana hali ya WaTanzania walio wengi hivyo kuamua kutumia mbinu ambazo zinawezekana na zina matokeo kwa mazingira yetu na maisha yetu, hasa ikizingatiwa kuwa yapo mataifa makubwa ambayo yameumizwa na yameshindwa kudhibiti janga hili pamoja na uwezo wao wa kisayansi na kiteknolojia, amedhihirisha kuwa si kila wakati lazima uendeshe mambo kwakuwa fulani anafanya hivyo - (katika hili nafahamu viongozi wa dini wanauthibitisho wa wazi na ni mashahidi muhimu sana), barabara, vituo vya afya, watalam wa afya, vifaa tiba, reli, elimu bure, mikopo vyuo vikuu, reli, ndege, kukuza uchumi, nidhamu serikalini, kuondoa ufisadi na urasimu, pamoja na hayo yapo mengi sana lakini kwa kadiri siku zanavysonga nitakuwa nakueleza kwa kina kila alichofanya kwa kila eneo, najua wajua lakini napenda kukujuza zaidi ili wote tutembee kifua mbele kwa alichofanya kwa taifa letu kwa kipindi hiki.

Jambo jingine ni jinsi alivyoweza kukiimarisha Chama Cha Mapinduzi kwa nafasi yake ya uenyekiti, (bila kusahau wasaidizi wake katika chama) hivyo wanachama wote kuwa proud na chama chetu, na hivyo wote kwa pamoja kuwa wakwanza kuhakikisha tunampatia kura zetu, kwakuwa sasa chama kinaisimamia serikali katika utekelezaji wa ilani yetu makini, chama kina mapato yakutosha toka katika vyanzo vyake vinavyosimamiwa vizuri, chama kinakubalika na ni chama pekee Tanzania ambacho ni mali ya wananchi, sio mali ya mtu fulani au kundi fulani.

Kingine ni kuwa wapinzani wamekosa kabisa ajenda ya kusimama nayo, wamebaki kudandia matukio na kutoa matamko ambayo ni ya kitambo tu na baadae kudakia jingine, maana kasi ya Chama Cha Mapinduzi kwasasa ni kushughulikia kila changamoto ya wananchi na kuleta maendeleo kwa vitendo, sio kwa bahati mbaya kwamba wapinzani hawana ajenda ni kwasababu kila waliyodhani wataitumia imeshughulikiwa tayari, hadi imefikia wale walio wa kweli na wanaoamini katika maendeleo ya kweli wameamua kuunga mkono juhudi za Rais na serikali katika kuwaletea wananchi maendeleo.

Ushindi ni halali kabisa kwa Chama Cha Mapinduzi, Rais, wabunge na madiwani maana kazi inaonekana na wananchi wanaona na kuridhika,

Pamoja tunajenga taifa letu.
 
Mimi nahisi umshauri Raisi ( Mwenyekiti wa CCM) afute uchaguzi mwaka huu , hizo pesa za uchaguzi zitumike kwa ajili ya miradi ya maendeleo.

Ikiwa tayari mnaona mnashinda kwa asilimia hiyo 90 halafu baada ya uchaguzi mutumie pesa nyengine muwanunue hao asilimia 10 ya viongozi walo bakia huo utakuwa ubadhirifu wa pesa za wananchi.

Jiwe alisema atahakikisha ifikapo 2020 hakuna upinzani, kwahiyo kama hutaki upinzani kuna haja gani ya uchaguzi? Ukumbuke kwamba matumizi ya miradi mingi ya Serikali hii kuanzia 2015 hadi sasa haijapitishwa wala kujadiliwa na bunge , basi bora pia umshauri mkuu wa mihimili yote avunje bunge ili tupate kubana matumizi tuzitumie hizo pesa kwa watanzania wanyonge.
 
Mimi nahisi umshauri Raisi ( Mwenyekiti wa CCM) afute uchaguzi mwaka huu , hizo pesa za uchaguzi zitumike kwa ajili ya miradi ya maendeleo.
Ikiwa tayari mnaona mnashinda kwa asilimia hiyo 90 halafu baada ya uchaguzi mutumie pesa nyengine muwanunue hao asilimia 10 ya viongozi walo bakia huo utakuwa ubadhirifu wa pesa za wananchi. Jiwe alisema atahakikisha ifikapo 2020 hakuna upinzani, kwahiyo kama hutaki upinzani kuna haja gani ya uchaguzi? Ukumbuke kwamba matumizi ya miradi mingi ya Serikali hii kuanzia 2015 hadi sasa haijapitishwa wala kujadiliwa na bunge , basi bora pia umshauri mkuu wa mihimili yote avunje bunge ili tupate kubana matumizi tuzitumie hizo pesa kwa watanzania wanyonge.
Bila uchaguzi justification (Uhalali) wa serikali unapatikana vipi? Uchaguzi ni takwa la kikatiba ni lazima twende hivyo hivyo..na tume hii hii kwani tusipofanya uchaguzi mataifa watatutenga na tutaonekana sisi ni madikteta mtuelewe wadanganyika.
 
Kama atotoa mil 50 kila kijiji ahadi za 2015 / .....Basi atashindwa vibaya sana. Ataishia kubebwa napolis vilaza +Time fake ya uchaguzi




chadema , Is political party which power belongs to the people.
 
Sawa bana ,kwa Sababu mna Dolla hakuna shaka yoyote..
IMG-20200525-WA0016.jpg
IMG-20200525-WA0016.jpg
 
Kwajinsi anavyo kubarika JPM atashinda hata Kama msimamizi wa uchaguz atakua Trump...

Sent using Jamii Forums mobile app
ha ha ha sawa chief, sasa fanyeni yafuatayo ili walau uchaguzi uwe na mantiki kidogo.

Kwanza, Waondoeni makada wenu watiifu wa CCM (Wakurugenzi ) wasiwe wasimamizi wa uchaguzi, Pili Kura za Urais zihesabiwe kwenye kila kituo na Tatu Mgombea wa Kiti cha URAIS anaweza kupinga matokeo ya mwenzake aliyeshinda mahakamani.
 
Kama tunavyofahamu kuwa mwaka huu ni mwaka wa uchaguzi, na kama ilivyo katika chaguzi zilizopita, hali ya hewa huwa inaanza kujulikana mapema kwa kuzingatia mambo mbalimbali, kwa kuanzia na utekelezaji wa ahadi, kukubalika kwa wagombea, uimara wa chama hadi kufikia kipindi cha uchaguzi ikiwemo pamoja na mambo mengine.

Kama ilivyo kawaida tayari hali katika mitaa, vijiji, kata, wilaya na mikoa, inaonesha kuwa Rais wetu mpendwa ndugu. John Pombe Joseph Magufuli ataashinda kwa idadi kubwa sana ya kura, na hii inatokana na uungwaji mkono mkubwa sana alionao kutoka kwa waTanzania wa kada mbalimbali. Hii ni kutokana na ukweli kwamba kasi yake katika kuleta maendeleo na kushughulikia changamoto mbalimbali za kitaifa hadi za watu binafsi katika ziara zake, lakini pia jinsi ambavyo ameshughulikia janga la corona ambapo amezingatia sana hali ya WaTanzania walio wengi hivyo kuamua kutumia mbinu ambazo zinawezekana na zina matokeo kwa mazingira yetu na maisha yetu, hasa ikizingatiwa kuwa yapo mataifa makubwa ambayo yameumizwa na yameshindwa kudhibiti janga hili pamoja na uwezo wao wa kisayansi na kiteknolojia, amedhihirisha kuwa si kila wakati lazima uendeshe mambo kwakuwa fulani anafanya hivyo - (katika hili nafahamu viongozi wa dini wanauthibitisho wa wazi na ni mashahidi muhimu sana), barabara, vituo vya afya, watalam wa afya, vifaa tiba, reli, elimu bure, mikopo vyuo vikuu, reli, ndege, kukuza uchumi, nidhamu serikalini, kuondoa ufisadi na urasimu, pamoja na hayo yapo mengi sana lakini kwa kadiri siku zanavysonga nitakuwa nakueleza kwa kina kila alichofanya kwa kila eneo, najua wajua lakini napenda kukujuza zaidi ili wote tutembee kifua mbele kwa alichofanya kwa taifa letu kwa kipindi hiki.

Jambo jingine ni jinsi alivyoweza kukiimarisha Chama Cha Mapinduzi kwa nafasi yake ya uenyekiti, (bila kusahau wasaidizi wake katika chama) hivyo wanachama wote kuwa proud na chama chetu, na hivyo wote kwa pamoja kuwa wakwanza kuhakikisha tunampatia kura zetu, kwakuwa sasa chama kinaisimamia serikali katika utekelezaji wa ilani yetu makini, chama kina mapato yakutosha toka katika vyanzo vyake vinavyosimamiwa vizuri, chama kinakubalika na ni chama pekee Tanzania ambacho ni mali ya wananchi, sio mali ya mtu fulani au kundi fulani.

Kingine ni kuwa wapinzani wamekosa kabisa ajenda ya kusimama nayo, wamebaki kudandia matukio na kutoa matamko ambayo ni ya kitambo tu na baadae kudakia jingine, maana kasi ya Chama Cha Mapinduzi kwasasa ni kushughulikia kila changamoto ya wananchi na kuleta maendeleo kwa vitendo, sio kwa bahati mbaya kwamba wapinzani hawana ajenda ni kwasababu kila waliyodhani wataitumia imeshughulikiwa tayari, hadi imefikia wale walio wa kweli na wanaoamini katika maendeleo ya kweli wameamua kuunga mkono juhudi za Rais na serikali katika kuwaletea wananchi maendeleo.

Ushindi ni halali kabisa kwa Chama Cha Mapinduzi, Rais, wabunge na madiwani maana kazi inaonekana na wananchi wanaona na kuridhika,

Pamoja tunajenga taifa letu.
Raisi Magufuli hashindani,hakuna ushindani.
Kama hakuna ushindani uchaguzi wa nini?

Wakati wa utawala wa chama kimmoja tulikuwa na ndio au hapana ya mgombeaji wa uraisi.
Bora tufanye hivyo.
 
Mtu akiongelea uchaguzi Tanzania nasikia kichefuchefu, Under Magufuli nchi inanuka ufisadi wa uchaguzi
 
Back
Top Bottom