Oktoba 14: Kumbukumbu ya Kifo cha Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. Imetimia miaka 21 tangu imempoteza Tanzania kifo cha Baba wa Taifa

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Feb 24, 2012
5,000
9,862
Leo ni Kumbukizi ya Kitaifa ya miaka 21 ya kifo cha Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kilichotokea Oktoba 14, 1999 nchini Uingereza alipokuwa anapatiwa matibabu.

Mwalimu Nyerere ni mmoja kati ya waasisi wa Taifa la Tanzania, ambaye alishiriki kikamilifu katika harakati za kulikomboa Taifa kutoka kwa ukoloni wa Waingereza.

Alikuwa Rais wa kwanza wa Tanganyika na aliongoza tangu Taifa lilipopata Uhuru, Desemba 9, 1961 hadi mwaka 1985

Alikuwa muasisi wa falsafa ya Ujamaa na Kujitegemea ambapo aliamini ili Taifa liendelee kunahitajika watu, ardhi, Siasa safi na Uongozi bora.

Endelea kupumzika kwa amani, Mwalimu Nyerere!
===
Wakuu Salaam:

Leo October 14 inatimia miaka 21 tangu muasisi wa Taifa hili atutoke duniani.

Yapo mengi ambayo alifanya na kila mmoja ni shahidi katika hili.
Katika uongozi wake alienzi Siasa safi zenye zilizo na amani ndani yake kama msingi wa maendeleo ya watu na vitu.

Wakati kifo chake kimetangazwa, binafsi mimi sikua na uwelewa kuhusu hilo hivyo sijukujua chochote kinachoendelea. Mwaka wa 2000+ ndiyo naelewa sasa.

Kuuliza uliza, kipindi kile tulikua moshi wakati hiyo taarifa imetoka na ilitangazwa usiku.

Lipo unalokumbuka wakati wa Uongozi wa Mwalimu. Ni kipi?

Na pia wakati kifo cha Mwalimu kinatangazwa, Ulikua wapi kipindi kile?

PIA SOMA
= > Ubalozi wa Marekani wamkumbuka Mwl. Nyerere. Wasema maendeleo ni watu sio vitu
 
Nasikitika siku hii imebaki kwenye makabati hakuna kiongozi aliyejaribu kufuata nyayo zake ,kwamba tunadanganywa tu hakuna ukweli wowote,watu wamerudi kwenye utumwa.

Leo hii kuna ubaguzi wa elimu watoto wa viongozi wanasoma kwenye shule zenye viyoyozi lakini watoto wa masikini wanasoma kwenye mabanda ya makuti huku wakipita njiani kwa kuimba elimu bure ,leo kusoma chuo kikuu imekuwa ni adhabu ya kaburi huku watoto wao wakipewa ada za kodi zetu.

Leo hii mahakama,bunge,na vyama vya wafanyakazi vimekuwa ni vibogoyo nchi imefikia mahala ambapo hata mwanafunzi wa darasa la pili anaweza kuongozo ,vijana ambao ndiyo taifa wamejigeuza wanafiki wa kutetea maovu ya viongozi ,Nyerere hakuwa mnafiki sasa sijui mnamuenzi kwa mambo gani !!Yaani laana juu ya laana
 
Hivi maisha gani mazuri tuliishi wakati wa Nyerere leo tujifanye tunasikitika sana? maisha mabaya umaskini wa kiwango cha lami wakati wa utawala wake. Ila yeye kama Binadamu ni kweli alikuwa mwanasiasa bora kabisa ila sera zake za kiuchumi au niseme chama chake zero.

Yako mazuri alifanya na pia mabaya alifanya katika suala umoja, amani alifanya mengi mazuri ila sera za kiuchumi hapana alichemka..ila ndio hivyo huwa hatutaki kusikia mapungufu. leo ni siku ya kupumzika tu wala hakuna kumbukumbu... kuna watu wazazi wao tu hawakumbuki waliwazika lini watamkumbuka Nyerere
 
Hivi maisha gani mazuri tuliishi wakati wa Nyerere leo tujifanye tunasikitika sana? maisha mabaya umaskini wa kiwango cha lami wakati wa utawala wake. Ila yeye kama Binadamu ni kweli alikuwa mwanasiasa bora kabisa ila sera zake za kiuchumi au niseme chama chake zero. yako mazuri alifanya na pia mabaya alifanya katika suala umoja, amani alifanya mengi mazuri ila sera za kiuchumi hapana alichemka..ila ndio hivyo huwa hatutaki kusikia mapungufu. leo ni siku ya kupumzika tu wala hakuna kumbukumbu... kuna watu wazazi wao tu hawakumbuki waliwazika lini watamkumbuka Nyerere
Unafikiri ingekuwa rahisi kutengeneza uchumi wa taifa changa kwamba leo tu basi uchumi huo umepaa juu..! Alitawala miaka 20 kumbuka wakati huo hata wasomi tu ilikuwa tabu,elimu ilikuwa duni,kilimo nacho ndo kilikuwa kimeshikiliwa na wakoloni! Tofauti na leo wasomi wa Mambo mbalimbali utawakuta tayari we ni kuwatumia tu.. wanauchumi wapo,manguli wa sheria wapo,mainjinia wapo,walimu wapo wakutosha.. Sasa linganisha na kipindi kile watu waliojua kusoma na kuandika tu basi ilitosha..😂

Ulitaka nyerere abebe mangapi ndugu..?
Mi namshukuru kwa utashi wake pia japo kila mtu na mapungufu yake.. na kuepuka lawama zaidi na ndio maana aliwaaachia wengine uongozi.. aliacha shirika la ndege likiwa na ndege kadhaa wakazifusa!,kumbuka nchi yetu kipindi chake pia ililazimika kuingia vitani hivyo uchumi mfinyu uliokuwepo nao uliyumba pia! Vita si lelemama ndugu!.. Kama angekuwa ni mfitini wa kutaka mali hovyo angeruhusu uchimbwaji wa madini tokea kwenye uongozi wake lkn alijua hakuna wataalum na wangepigwa tu!.. I think you know what happened.

Ilitosha nae kushughulika kwa aliyoshughulika nayo na kama muasisi wa taifa lzm apewe sifa yake tu! Yule utake usitake ndio alikuwa dira ya taifa hili alipigia chapuo vyama vingi,aliutumia usomi wake na utashi wake kupambania uhuru hivyo alirisk hata maisha yake (japo hakuwa pekee tu)
Tusijifanye vipofu kwakuwa leo tunaplatform hizi wao ndo waasisi.
 
Wakuu Salaam:

Leo October 14 inatimia miaka 21 tangu muasisi wa Taifa hili atutoke duniani.

Yapo mengi ambayo alifanya na kila mmoja ni shahidi katika hili.
Katika uongozi wake alienzi Siasa safi zenye zilizo na amani ndani yake kama msingi wa maendeleo ya watu na vitu.

Wakati kifo chake kimetangazwa, binafsi mimi sikua na uwelewa kuhusu hilo hivyo sijukujua chochote kinachoendelea. Mwaka wa 2000+ ndiyo naelewa sasa.

Kuuliza uliza, kipindi kile tulikua moshi wakati hiyo taarifa imetoka na ilitangazwa usiku.

Lipo unalokumbuka wakati wa Uongozi wa Mwalimu. Ni kipi?

Na pia wakati kifo cha Mwalimu kinatangazwa, Ulikua wapi kipindi kile?
 
Aliwahi kumtandika viboko kiongozi mmoja ambaye jina lake linaanza na John. Nadhani angekuwa hai angatamani kuirudia hii....
 
Unafikiri ingekuwa rahisi kutengeneza uchumi wa taifa changa kwamba leo tu basi uchumi huo umepaa juu..! Alitawala miaka 20 kumbuka wakati huo hata wasomi tu ilikuwa tabu,elimu ilikuwa duni,kilimo nacho ndo kilikuwa kimeshikiliwa na wakoloni! Tofauti na leo wasomi wa Mambo mbalimbali utawakuta tayari we ni kuwatumia tu.. wanauchumi wapo,manguli wa sheria wapo,mainjinia wapo,walimu wapo wakutosha.. Sasa linganisha na kipindi kile watu waliojua kusoma na kuandika tu basi ilitosha..😂

Ulitaka nyerere abebe mangapi ndugu..?
Mi namshukuru kwa utashi wake pia japo kila mtu na mapungufu yake.. na kuepuka lawama zaidi na ndio maana aliwaaachia wengine uongozi.. aliacha shirika la ndege likiwa na ndege kadhaa wakazifusa!,kumbuka nchi yetu kipindi chake pia ililazimika kuingia vitani hivyo uchumi mfinyu uliokuwepo nao uliyumba pia! Vita si lelemama ndugu!.. Kama angekuwa ni mfitini wa kutaka mali hovyo angeruhusu uchimbwaji wa madini tokea kwenye uongozi wake lkn alijua hakuna wataalum na wangepigwa tu!.. I think you know what happened.

Ilitosha nae kushughulika kwa aliyoshughulika nayo na kama muasisi wa taifa lzm apewe sifa yake tu! Yule utake usitake ndio alikuwa dira ya taifa hili alipigia chapuo vyama vingi,aliutumia usomi wake na utashi wake kupambania uhuru hivyo alirisk hata maisha yake (japo hakuwa pekee tu)
Tusijifanye vipofu kwakuwa leo tunaplatform hizi wao ndo waasisi.
Usinielewe vibaya mimi naamini kabisa alikuwa mwanasiasa bora kabisa na upeo mkubwa wa kuchambua mambo ila katika uchumi alokosea sana sababu ziko nchi zilipata uhuru kama wakati wetu na zilikuwa maskini tu kama Malaysia lakini leo ona tofauti.

Namuheshimu kama baba wa taifa na kiongozi mzuri katika baadhi ya mambo ila kama alichaguwa twende wa ujamaa ndio shida ilipoanzia maana ukatushinda njiani tukarudi kulekule alikokukataa ndio tumechelewa. wanasema ukiona vita chagua upande wa mshindi sisi tukakosea tukubali.
 
Ikiwa leo ni Siku ya kumbukizi ya kifo cha Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. Muasisi wa Taifa hili kupitia jitihada zake tulipata Uhuru.

Kizazi hiki cha leo kimeishi bila mwalimu tangu alipotutoka tarehe 14.10.1999.

Huzuni,vilio na simanzi zilizotawala bila kukoma hazitosahaulika kamwe.
Kwa waliojuwa na kutambua mchango wake katika taifa hili.

Kwa yeyote yule mwenye neno la kumuenzi au kile anachokumbuka au kinachomjia kichwani akisikia neno Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Anaweza akawa na ushuhuda tosha juu ya upekee wa Mwalimu na umuhimu wake kwa taifa.

Je, vijana na kizazi cha leo kinamuenzi vipi Mwalimu?

Ni kweli tumepambana na Maradhi,Ujinga na Maskini?

Vitu gani unavikumbuka kuhusu Mwalimu?

Tufahamishane chochote kuhusu Mwalimu aidha historia yake kwa kifupi nukuu zake na mambo mengine muhimu kumhusu.
 
Back
Top Bottom