Ofisi za Serikali na picha ya Rais

hata mimi

JF-Expert Member
Oct 17, 2017
1,356
1,437
Ushauri wangu kama inawezekana tuachane na hii kitu badala yake (picha ya) nembo ya taifa pekee ndio iwekwe maofisini

Hoja yangu inakuja kwa sababu kwanza urais ni taasisi na si mtu kama mtu ingawa rais ni mtu mmoja.

Pili mihimili ya dola ile mingine haijaipa umaalumu picha ya kiongozi mkuu vinginevyo tungeona maofisini picha nne (ya Baba wa Taifa, ya Rais, ya Spika wa Bunge na ya Jaji Mkuu)

Tatu na mwisho kabisa ni kwamba Raisi akitoka madarakani picha yake inakosa thamani kabisa utafikiri haikugharamiwa maelfu ya shilingi kuifikisha hapo

Nina mfano mmoja mashuleni walimu walipelekeshwa sana kuwa na picha ya Raisi awamu ya tano muhula wa pili kisha alipoapishwa Rais awamu ya sita kukatolewa amri ya kuondoa/kutungua picha ya Rais awamu ya tano haraka sana na kuweka/kutundika picha ya Raisi awamu ya sita

Picha zile zilizotunguliwa kukasemwa zitunzwe kwenye kasiki mpaka kutakapotolewa utaratibu wa wapi zipelekwe lakini cha ajabu ni zaidi ya mwaka sasa picha zinaharibika tu bure mashuleni hakuna mwongozo wowote

Matokeo yake sasa baadhi yao wamezitupa na wengine wamediriki kuziweka mpaka chooni ili tu zisiwabane. Sasa kama haikuwa na umuhimu hivyo ni kwanini ilinunuliwa kwa gharama kubwa kiasi kile?
 
Nashauri iwekwe picha ya Nyerere tu.



#MaendeleoHayanaChama
Au waweke, wakipenda, hata ya Jamhuri ya Muungano wa Watazamaji, Kazi Haiendelei.

Nasema hiviii, yote tisa, kumi kamilisheni miradi mikubwa ya maendeleo aliyoiacha JPM. Kile chuma haifutiki ligacy yake adhimu na ladhimu, hata mkithubutu kutumia conc. H2SO4
 
Habari za picha ni kujitukuza tu kwa viongoz, Rais anatambulika nchi nzima kwa Sura sioni umuhim wa picha, Ila vituo vya polisi huwa naona picha ya IGP na hii imekaaje?
 
Ushauri wangu kama inawezekana tuachane na hii kitu badala yake (picha ya) nembo ya taifa pekee ndio iwekwe maofisini

Hoja yangu inakuja kwa sababu kwanza uraisi ni taasisi na si mtu kama mtu ingawa raisi ni mtu mmoja.

Pili mihimili ya dola ile mingine haijaipa umaalumu picha ya kiongozi mkuu vinginevyo tungeona maofisini picha nne (ya Baba wa Taifa, ya Raisi, ya Spika wa Bunge na ya Jaji Mkuu)

Tatu na mwisho kabisa ni kwamba Raisi akitoka madarakani picha yake inakosa thamani kabisa utafikiri haikugharamiwa maelfu ya shilingi kuifikisha hapo

Nina mfano mmoja mashuleni walimu walipelekeshwa sana kuwa na picha ya Raisi awamu ya tano muhula wa pili kisha alipoapishwa Raisi awamu ya sita kukatolewa amri ya kuondoa/kutungua picha ya Raisi awamu ya tano haraka sana na kuweka/kutundika picha ya Raisi awamu ya sita

Picha zile zilizotunguliwa kukasemwa zitunzwe kwenye kasiki mpaka kutakapotolewa utaratibu wa wapi zipelekwe lakini cha ajabu ni zaidi ya mwaka sasa picha zinaharibika tu bure mashuleni hakuna mwongozo wowote

Matokeo yake sasa baadhi yao wamezitupa na wengine wamediriki kuziweka mpaka chooni ili tu zisiwabane. Sasa kama haikuwa na umuhimu hivyo ni kwanini ilinunuliwa kwa gharama kubwa kiasi kile?
Acha kuhangaika na vitu vidogo visivyo na tija,jadili mambo ya maana badala ya ku misuse ubongo wako..

Hapa ni Senegal sijui napo utasemaje 👇
 

Attachments

  • Screenshot_20220707-210141.png
    Screenshot_20220707-210141.png
    205.8 KB · Views: 3
Back
Top Bottom