Ofisi za Ruge na Singh Zilipaswa Kufungwa; Ushahidi Kukusanywa

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,474
39,987
Wenzetu - hasa kwenye nchi zilizoendelea sana - wanapoamua kuwakamata mafisadi hawafanyi kwa kificho na wakiamua kufanya wanafanya kweli kweli. Pamoja na kuwakamata watuhumiwa, nyumba zao zinasachiwa, ofisi zao zinasachiwa, kompyuta na vielelezo mbalimbali vinakusanywa ili kuhakikisiha kuwa ushahidi wote unaowezekana kukusanywa unapatikana.

upload_2017-6-19_12-21-38.jpeg


Maofisa wa FBI, IRS (TRA ya Marekani) na wengine wakitoka na nyaraka mbalimbali toka ofisi za chama cha Democrat ambapo kulikuwa na tuhumiwa wea ufisadi huko New York na California (Soma Hapa)

upload_2017-6-19_12-26-3.jpeg


Maofisa wa FBI Walipovamia ofisi ya Dkt Salomon Melgen kwa tuhuma za ufisadi ikiwemo kusababisha hasara serikali kupitia uhujumu taasisi za bima mbalimbali za afya. Soma Hapa

Hapa kwetu Detroit hivi majuzi maofisa wa FBI walivamia ofisi ya daktari mwingine kwa mambo hayo hayo, siyo tu ofisi lakini pia hadi nyumbani kwake ili kukusanya ushahidi mbalimbali.

upload_2017-6-19_12-31-28.jpeg


Yote hii ni mifano michache tu ya jinsi gani unapoamua kupambana na ufisadi unapambana mzima mzima. Haitoshi kuwapigisha magoti kina Rugemalira na Singh bila kuhakikisha kuwa mali zao zote, ofisi zao zote zinapekuliwa pamoja na majumba yao yote ili kukusanya ushahidi wote unaowezekana.

Haitoshi tu kusema unawashtaki kwa tuhuma zipi wakati hujatumia muda wa kutosha kukusanya ushahidi mzito dhidi yao. Sijui hadi hivi sasa kama kuna warranti zimetoleaw dhidi yao zina upana gani.

Ni matumaini yangu kuwa DPP na vyombo vya dola vitatumia nguvu zote za uwezo wote wa sheria kukusanya ushahidi na kutengeneza mashtaka ambayo yatakusanya wote waliohusika na kashfa hii na kuwashtaki to the full extent of the law!
 
Lazima tujue kwamba tuna safari ndefu kabla hatujafika huko sio safari ya mchezo mchezo tu .

Ingekua kwa wenzetu sidhani kama hiyo ingelitokea maana nafasi hiyo isingetokea.
 
Wasiwasi wangu mkubwa ni kama waendesha mashitaka wana ushahidi wa kutosha kuweza kupata conviction.

Masuala kama haya si busara kwenda nayo public namna hii kama huna ushahidi wa kutosha kuweza kupata conviction.

Sijui pia kama wanaweza kupewa plea deal ili waweze kufunguka zaidi.
 
Wenzetu - hasa kwenye nchi zilizoendelea sana - wanapoamua kuwakamata mafisadi hawafanyi kwa kificho na wakiamua kufanya wanafanya kweli kweli. Pamoja na kuwakamata watuhumiwa, nyumba zao zinasachiwa, ofisi zao zinasachiwa, kompyuta na vielelezo mbalimbali vinakusanywa ili kuhakikisiha kuwa ushahidi wote unaowezekana kukusanywa unapatikana.

View attachment 527143

Maofisa wa FBI, IRS (TRA ya Marekani) na wengine wakitoka na nyaraka mbalimbali toka ofisi za chama cha Democrat ambapo kulikuwa na tuhumiwa wea ufisadi huko New York na California (Soma Hapa)

View attachment 527145

Maofisa wa FBI Walipovamia ofisi ya Dkt Salomon Melgen kwa tuhuma za ufisadi ikiwemo kusababisha hasara serikali kupitia uhujumu taasisi za bima mbalimbali za afya. Soma Hapa

Hapa kwetu Detroit hivi majuzi maofisa wa FBI walivamia ofisi ya daktari mwingine kwa mambo hayo hayo, siyo tu ofisi lakini pia hadi nyumbani kwake ili kukusanya ushahidi mbalimbali.

View attachment 527146

Yote hii ni mifano michache tu ya jinsi gani unapoamua kupambana na ufisadi unapambana mzima mzima. Haitoshi kuwapigisha magoti kina Rugemalira na Singh bila kuhakikisha kuwa mali zao zote, ofisi zao zote zinapekuliwa pamoja na majumba yao yote ili kukusanya ushahidi wote unaowezekana.

Haitoshi tu kusema unawashtaki kwa tuhuma zipi wakati hujatumia muda wa kutosha kukusanya ushahidi mzito dhidi yao. Sijui hadi hivi sasa kama kuna warranti zimetoleaw dhidi yao zina upana gani.

Ni matumaini yangu kuwa DPP na vyombo vya dola vitatumia nguvu zote za uwezo wote wa sheria kukusanya ushahidi na kutengeneza mashtaka ambayo yatakusanya wote waliohusika na kashfa hii na kuwashtaki to the full extent of the law!
Kwani umeambiwa Takukuru hawajafanya hayo? Usilolijua no kama usiku wa Giza bushman!
 
1. Wenzetu?

2. Wamarekani ni wenzetu hapo tu?

3. kwenye uhuru wa kujieleza sio wenzetu?
4.uhuru wa kukosoa serikali sio wenzetu?
1. ndiyo
2....
3. Occupy Wall Street unajua iliishaje?
4. Unajua habari za Snowden aliyetoa maoni yake kuwa kupekua usiri wa raia si sawa tena akatoa na ushahidi. Amevuliwa uraia a US kwa ku revoke passport yake.
 
Marekani wanayo katiba isiyowalinda wahusiku wakuu wa wizi, katiba isiyotazama sura ya mtu wala wadhifa na katiba inayozingatia uhuru na haki...sisi ni kama watoto wadogo vile, tunaishia kucheza tu kwenye dimbwi la maji, baharini lazima tutazama tu.

Katiba kama hiyo watu kama Magufuli lazima wataiogopa kama ukoma, ni katiba inayoweza kukutia kitanzini kama unaropoka hovyo kama tunavyoshuhudia hivi sasa ikimpa tabu Rais wao Trump. Hapa kwetu wakururpukaji hawa hujificha nyuma ya vyombo vya dola.

Naomba tusiilinganishe Marekani na mambo ya kijinga.
 
Mkurugenzi wa IPTL anapaswa agongwe "subpoena" aelezee kila kitu mahakamani or else inatafuna kwake
 
Mzee Mwanakijiji Umeshachanganyikiwa na kubeba mabox, njoo umsaidie Magufuli huku nawe upate Ukuu wa wilaya.

Sikiliza Wanaume walishasema siku nyingi mno sio huyu Magufuli wako anayefanya siasa kwenye Maisha ya Watanzania
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom