Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali imeandika historia kwa kuokoa Tsh Trilioni 11.4 ndani ya mwaka mmoja

Uzalendo wa Kitanzania

JF-Expert Member
Mar 8, 2020
2,156
4,510
Weledi, Uchapakazi na Uzalendo

Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali ya Awamu ya Tano imeokoa Tsh Trilioni 11.4 baada ya kushinda kesi mbalimbali zilizofunguliwa ndani na nje ya Nchi dhidi ya Serikali ya Tanzania.

Aidha Ofisi hiyo imefanikiwa kurejesha Serikalini mali mbalimbali zilizochukuliwa kwa njia zisizo halali ikiwemo mashamba 106, Viwanja, Hoteli na nyumba mbalimbali ikiwemo Hoteli ya Mbeya.

Gabriel Malata - Wakili Mkuu wa Serikali

======

WAKILI Mkuu wa Serikali, Gabriel Malata amesema serikali imefanikiwa kuokoa zaidi ya Sh trilioni 11.4 kwa miaka miwili kutokana na uendeshaji madhubuti wa mashauri ndani na nje ya nchi.

Malata amesema hayo leo wakati akitoa taarifa kwa Waziri wa Katiba na Sheria, Dk Mwigulu Nchemba aliyetembelea ofisi yake.

Wakili huyo mkuu amesema miongoni mwa mafanikio yametokana na kushinda kesi zilizofunguliwa nchini Afrika Kusini na Canada.

Amesema fedha hizo zingeweza kulipwa kwa watu wasiostahili.

CHANZO: Habari Leo (August 2020)
 
So what's the effects of kuokoa... Upupu mtupu hela haionekani kwa watz
 
Tafuta maana ya maneno haya ya Kingereza..

Rescue..
Blackmail..

Kisha futa maada yako..

Msafwa,
Uporoto, Mbeya..
 
Kwa mafanikio hayo yaliyopatikana mbona yule wakili aliyekuwepo kabla ya huyu Malata aliondolewa wakati alifanya hiyo kazi nzuri?
 
Ule uwanja wa ndege uliojengwa uani kwa mfalme umerudi serikalini?
 
Uongo mtupu , trillion 11 za kwenye makaratasi . Hizo hela "walizookoa" kupitia kesi walizoshinda hela kwanini hawatutajii ni kesi namba ngapi ya Jamhuri vs Kampuni au mtu, korti gani nje na ndani ya nchi n.k , Jaji gani aliwapa ushindi na hukumu zake tuzisome.
 
Nyumba za serikali walizogawana mpaka na ndugu zao, zikagharimu mabilioni kuwaweka maelfu ya wafanyakazi hotelini wengine nyota tano, zinarudishwa lini?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom