Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS) yakiri ajira sekta binafsi zimepungua kwa 42.6%, serikalini zimepungua kwa 78.1% ndani ya mwaka mmoja

Quinine

JF-Expert Member
Jul 26, 2010
21,271
47,269
NBS Report “Tanzania in Figure 2018”
Agosti 10, 2019

Kwa kifupi.
  • Ajira rasmi zilizotengenezwa na sekta binafsi zimepungua kutoka 239,017 mwaka 2016/2017 hadi kufikia ajira 137,054 mwaka 2017/2018.
  • Pia ajira rasmi zilizotengenezwa na Serikali zilipungua kutoa 82,302 hadi 18,000 ikiwa ni sawa na anguko la asilimia 78.1 katika kipindi hicho cha mwaka mmoja.
Dar es Salaam. Ripoti mpya ya takwimu za Tanzania imeeleza kuwa ajira zinazotengenezwa na sekta binafsi zimepungua kwa asilimia 42.6 ndani ya kipindi cha mwaka mmoja uliopita, jambo linalotoa changamoto kwa vijana na wadau wa maendeleo kubuni njia mbadala za kuondoa tatizo la ajira nchini.

Ripoti hiyo iliyopewa jina la “Tanzania in Figure 2018” iliyotolewa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Juni 2019, inaonyesha kuwa ajira rasmi zilizotengenezwa na sekta binafsi zimepungua kutoka 239,017 mwaka 2016/2017 hadi kufikia ajira 137,054 mwaka 2017/2018.

Screen Shot 2019-08-14 at 12.39.50.png


Hiyo ni sawa na anguko la asimilia 42.6 ndani ya kipindi cha mwaka mmoja katika sekta hiyo inayotegemewa kuajiri watu wengi nchini.

Hali hiyo inaweza kuwa imesababishwa na kupungua kwa shughuli za biashara katika kipindi ambazo zilikuwa zinakabiliwa mazingira yasiyoridhisha kwa wawekezaji ikiwemo urasimu katika upatikanaji wa vibali na utitiri wa kodi na tozo.

Hata hivyo, katika bajeti ya mwaka 2019/2020, Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango alisema Serikali imekusudia kuboresha mazingira ya biashara kwa kuondoa kodi na tozo zinazowaumiza wawekezaji.

Pia ajira rasmi zilizotengenezwa na Serikali nazo zilipungua kutoa 82,302 hadi 18,000 ikiwa ni sawa na anguko la asilimia 78.1 katika kipindi hicho cha mwaka mmoja.

bdfdf377f36ef9f4716d4b1a91a79bac9acf70e3.png


Wakati ajira rasmi serikalini na sekta binafsi zikipungua, ajira zilizotokana na miradi ya maendeleo inayotekelezwa na Serikali ikiwemo ujenzi wa barabara, majengo na reli ziliongezeka na kuifanya sekta hiyo kuongoza kwa kuajiri watu wengi zaidi mwaka mmoja uliopita.

Licha ya kuongezeka kwa mahitaji ya ajira Tanzania, kiwango cha watu wasio na ajira kimeendelea kupungua katika kipindi cha miaka mitano iliyopita.

Mathalani, kiwango hicho cha ukosefu wa ajira nchini kimepungua kutoka asilimia 10.3 mwaka 2014 hadi asilimia 9.7 mwaka 2018.

SOURCE: Nukta

My Take: Namba huwa hazidanganyi.

======

UPDATES: 14 AUG 2019

Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) inakanusha habari iliyosambazwa katika baadhi ya mitandao ya kijamii hususan Jamii Forum yenye kichwa cha habari “NBS yakiri ajira sekta binafsi zimepungua kwa 42.6%, Serikalini zimepungua kwa 78.1% ndani ya mwaka mmoja."

Habari hii imepotosha kuhusu kupungua kwa ajira Serikalini na hivyo jamii inaombwa kuipuuza kwa kuwa haina ukweli wowote.

 
Anaweza tumbuliwa mtu kwa takwimu kama hizi zinazopingana na ukuaji wa uchimi ktk nchi ya viwanda.

Takwimu hizi zinamaanisha kuna kudorora kwa uchumi nchini japo takwimu zao zinadai uchumi umekuwa.

Nasubiri wapingaji kwa hoja waje
 
Tutafika tu wanakotaka tufike!!

Wengine tumeseme kupitia hapa JF kuhusu hili tatizo siku kadhaa zilizopita.

 
NBS Report “Tanzania in Figure 2018”
Agosti 10, 2019

Kwa kifupi.
  • Ajira rasmi zilizotengenezwa na sekta binafsi zimepungua kutoka 239,017 mwaka 2016/2017 hadi kufikia ajira 137,054 mwaka 2017/2018.
  • Pia ajira rasmi zilizotengenezwa na Serikali zilipungua kutoa 82,302 hadi 18,000 ikiwa ni sawa na anguko la asilimia 78.1 katika kipindi hicho cha mwaka mmoja.
Dar es Salaam. Ripoti mpya ya takwimu za Tanzania imeeleza kuwa ajira zinazotengenezwa na sekta binafsi zimepungua kwa asilimia 42.6 ndani ya kipindi cha mwaka mmoja uliopita, jambo linalotoa changamoto kwa vijana na wadau wa maendeleo kubuni njia mbadala za kuondoa tatizo la ajira nchini.

Ripoti hiyo iliyopewa jina la “Tanzania in Figure 2018” iliyotolewa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Juni 2019, inaonyesha kuwa ajira rasmi zilizotengenezwa na sekta binafsi zimepungua kutoka 239,017 mwaka 2016/2017 hadi kufikia ajira 137,054 mwaka 2017/2018.

Hiyo ni sawa na anguko la asimilia 42.6 ndani ya kipindi cha mwaka mmoja katika sekta hiyo inayotegemewa kuajiri watu wengi nchini.

Hali hiyo inaweza kuwa imesababishwa na kupungua kwa shughuli za biashara katika kipindi ambazo zilikuwa zinakabiliwa mazingira yasiyoridhisha kwa wawekezaji ikiwemo urasimu katika upatikanaji wa vibali na utitiri wa kodi na tozo.

Hata hivyo, katika bajeti ya mwaka 2019/2020, Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango alisema Serikali imekusudia kuboresha mazingira ya biashara kwa kuondoa kodi na tozo zinazowaumiza wawekezaji.

Pia ajira rasmi zilizotengenezwa na Serikali nazo zilipungua kutoa 82,302 hadi 18,000 ikiwa ni sawa na anguko la asilimia 78.1 katika kipindi hicho cha mwaka mmoja.

View attachment 1179274

My Take: Namba huwa hazidanganyi.
we are on the right track tembeeni tu kifua mbele
 
Tukisema hii nchi uchumi wake umeshajifia siku nyingi sana kutokana misplacement of priorities! akina Pascal wanakuja kupinga na maelezo meeeengi tena yanayokinzana na uhalisia.

Uchumi hauchangamani na siasa hata siku moja.

Utawaficha watu hali halisi ya kiuchumi kwa porojo za kisiasa kwa muda lakini itafika mahali hizo porojo zako hazitakuwa na msaada tena bali ni hali halisi ndio itaongea ambayo kila mtu atajionea.
 
Back
Top Bottom