Ofisi ya Taifa Takwimu (NBS) yakanusha kupungua kwa ajira Serikalini

Ukweli tuu uwezo wa serikali kutoa ajira umeshuka ...ata sekta binafsi nyingi zimepunguza wafanyakazi na ata kufa
 
0DDAF66A-1518-4FD9-BA89-2B58B13438AC.jpeg
0DDAF66A-1518-4FD9-BA89-2B58B13438AC.jpeg


Najafibu kuwaza tu
 
Eti Watanzania 22m wameajiliwa. Tena ni Mashetani wa kufa mtu. Mimi hata kama sina utafiti nakuambia waalimu wako laki 7, polisi laki 8, JW wako milioni 1, magereza wako laki 3, manesi wauguzi na madokta laki 6, wafanyakazi wengine wote laki 7. Haya jumla inakuwa 4.1m. ukija sekata binafsi utakuta wako 3m hapo jumla unapata 7.1m. Eti milioni 22, hata uongo hawawezi. Na hapo nimekupa idadi kabla ya vyeti feki kupita. Ukiweka vyeti feki basi watabaki jumla 3m walioajiliwa serikalini.
Mnataka sema kuwa Serikalini haijapungua ila Kwetu ndio zimepungua. Mkisema walioajiriwa ni 22mil maana yake Nusu ya Watanzania wameajiriwa....

Hamjui Nusu ya Watanzania karibia 25mil ni under 18?

Hamjui kuwa wazee 55 na kuendelea ni zaidi ya 10mil

Kwanini ikiguswa serikali mnakuwa wakali sana?
 
TAARIFA KWA UMMA KUHUSU KUKANUSHA HABARI ILIYOSAMBAZWA KATIKA MITANDAO YA KIJAMII YA KUPUNGUA KWA AJIRA SERIKALINI

Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) inakanusha habari iliyosambazwa katika baadhi ya mitandao ya kijamii hususan Jamii Forum yenye kichwa cha habari “NBS yakiri ajira sekta binafsi zimepungua kwa 42.6%, Serikalini zimepungua kwa 78.1% ndani ya mwaka mmoja."

Habari hii imepotosha kuhusu kupungua kwa ajira Serikalini na hivyo jamii inaombwa kuipuuza kwa kuwa haina ukweli wowote.

Ifahamike kwamba, wakati NBS ikijiandaa kufanya utafiti wa Watu wenye Uwezo wa Kufanya Kazi (Intergrated Labour Force Survey) utakaofanyika mwaka 2019/20, ilifanya maoteo mwaka 2018 (projections) ya mwenendo wa hali ya Soko la Ajira Nchini ambayo yanabainisha mabadiliko yaliyotokea katika soko la ajira tangu mwaka 2014 hadi mwaka 2018. Taarifa hii inapatikana kwenye tovuti ya NBS (www.nbs.go.tz - Tanzania in Figures 2018 Uk. 40).

Maoteo ya takwimu hizo yanaonesha kuwa, idadi ya watu walio na ajira imeongezeka kutoka milioni 20.0 mwaka 2014 hadi milioni 22.0 mwaka 2018.

Aidha, takwimu zilizowekwa kwenye Tanzania in Figure 2018 Uk. 41 zinazotokana na taarifa za kiutawala (administrative records) ambazo zinasaidia kupata takwimu za ajira ambazo hazikusanywi kwenye tafiti za kawaida. Takwimu hizi hutumika pia kama kigezo cha kufanya maoteo ya hali ya ajira (proxy indicators) katika vipindi ambavyo hakuna tafiti zilizofanyika ili kutoa hali ya soko la ajira katika vipindi vifupi vifupi na vya kati.

Tafsiri halisi ya Jedwali lililopo uk. 41 wa Tanzania in Figures ni kwamba, mwaka 2017/18 kulikuwa na jumla ya ajira 552,063 zilizozalishwa nchini ikilinganishwa na ajira 453,466 kwa mwaka 2016/17. Hili ni ongezeko la ajira 98,597 sawa na asilimia 21.7 kati ya mwaka 2016/17 na mwaka 2017/18.

Kati ya ajira 552,063 zilizozalishwa nchini mwaka 2017/18, ajira 415,009 sawa na asilimia 75.0 zilikuwa ni ajira kutoka Serikalini; ajira hizi zinajumuisha ajira 18,000 kutoka Serikali Kuu na ajira 397,009 kutoka katika miradi ya maendeleo kupitia Mpango wa Pili wa Maendeleo wa Taifa wa mwaka 2016/17 hadi 2020/21.

Hali hii inatokana na ukweli kuwa, wananchi wengi huajiriwa kwenye miradi ya kimkakati ya maendeleo inayoendelea hapa nchini ambapo Serikali imejikita kwa dhati kuitekeleza kwa ajili ya kufikia uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025 na kupunguza umaskini.

Kwa upande mwingine, ajira 137,054 sawa na asilimia 25.0 ya ajira zote zilizozalishwa na Sekta Binafsi zimepungua kutoka ajira 239,017 mwaka 2016/17 hadi ajira 137,054.

Hivyo, hali halisi kwa jedwali hilo ni kuongezeka kwa ajira Serikalini kutoka 214,449 mwaka 2016/17 hadi 415,009 mwaka 2017/18 sawa na ongezeko la ajira 200,560 (asilimia 94) ya ajira zilizozalishwa mwaka 2016/17.

Ikumbukwe kwamba, Ofisi ya Taifa ya Takwimu hutumia taarifa za kiutawala za ajira kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu; Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu kubaini kiwango cha ajira zilizozalishwa kwa kila mwaka. Huu ndio uzoefu wa nchi nyingi duniani hususan nchi za Afrika.

Utafiti wa Watu wenye Uwezo wa Kufanya Kazi hufanyika kila baada ya miaka mitano ambapo kwa mara ya mwisho ulifanyika mwaka 2014 wakati Utafiti wa Ajira na Mapato katika Sekta Rasmi hufanyika kila mwaka na kwa mara ya mwisho ulifanyika mwaka 2016.

Takwimu hizi za ajira hukusanywa na viashiria mbalimbali vya ajira (Labour Market Indicators) na hutolewa kwa kushirikiana na wadau mbalimbali ikiwa ni pamoja na Shirika la Kazi Duniani (ILO) zikiwa na lengo la kufuatilia na kutathmini sera zilizowekwa na Serikali katika Soko la Ajira.

Mwisho, Ofisi ya Taifa ya Takwimu inausisitiza Umma kupuuza habari hiyo potofu ya kupungua kwa ajira Serikalini na inatoa wito kwa wananchi kuendelea kufanya kazi kwa bidii na maarifa zaidi ili kuunga mkono juhudi zinazoendelea za kujenga uchumi. Aidha, NBS inawaasa wachambuzi wote kufuata matakwa ya Sheria ya Takwimu ya mwaka 2015 kila wanapofanya uchambuzi wa takwimu mbalimbali.

Imetolewa na:

Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS),
DODOMA

14 Agosti 2019


View attachment 1181119
View attachment 1181120



Kuhusu habari inayolalamikiwa, soma:


Hili tamko halipingi chochote kwenye chati tuliyosoma mwanzo,, tamko linajumuisha idadi ya ajira tu, lakini halitoi mchakato baina ya ajira za serikali na ajira za sekta binafsi ambazo ndizo watu walikuwa wanapigia kelele. Kwa jumla za ajira wako sahihi, na hata mimi nilisema hivyo, ila ajira kwa sekta moja moja ndizo naona walalamikaji wanataka majibu hasa kuhusu sekta binafsi
 
Yaani bora wasingekanusha maana ndio wanazidi kuharibu. Hivi kweli NBS wanatuona sisi ni wajinga eti kuna ajira 22m+ nchi hii? Kwa mantiki hii kwakuwa tuko 50m+, maana yake kila watanzania watatu mmoja ana ajira!!
 
Wapumbavu sana, eti Watanzania 22m wameajiliwa. Tena ni Mashetani wa kufa mtu. Mimi hata kama sina utafiti nakuambia waalimu wako laki 7, polisi laki 8, JW wako milioni 1, magereza wako laki 3, manesi wauguzi na madokta laki 6, wafanyakazi wengine wote laki 7. Haya jumla inakuwa 4.1m. ukija sekata binafsi utakuta wako 3m hapo jumla unapata 7.1m. Wapumbavu hao eti milioni 22, hata uongo hawawezi. Na hapo nimekupa idadi kabla ya vyeti feki kupita. Ukiweka vyeti feki basi watabaki jumla 3m walioajiliwa serikalini.

Kwa taarifa nilizo nazo ambazo sio sahihi sana, wafanyakazi wa umma hawazidi 1m.
 
Dah mbona kiwango cha walipa kodi wanakuwa wachache Mkuu analalamika daily wakati 22m wanakipato???
 
TAARIFA KWA UMMA KUHUSU KUKANUSHA HABARI ILIYOSAMBAZWA KATIKA MITANDAO YA KIJAMII YA KUPUNGUA KWA AJIRA SERIKALINI

Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) inakanusha habari iliyosambazwa katika baadhi ya mitandao ya kijamii hususan Jamii Forum yenye kichwa cha habari “NBS yakiri ajira sekta binafsi zimepungua kwa 42.6%, Serikalini zimepungua kwa 78.1% ndani ya mwaka mmoja."

Habari hii imepotosha kuhusu kupungua kwa ajira Serikalini na hivyo jamii inaombwa kuipuuza kwa kuwa haina ukweli wowote.

Ifahamike kwamba, wakati NBS ikijiandaa kufanya utafiti wa Watu wenye Uwezo wa Kufanya Kazi (Intergrated Labour Force Survey) utakaofanyika mwaka 2019/20, ilifanya maoteo mwaka 2018 (projections) ya mwenendo wa hali ya Soko la Ajira Nchini ambayo yanabainisha mabadiliko yaliyotokea katika soko la ajira tangu mwaka 2014 hadi mwaka 2018. Taarifa hii inapatikana kwenye tovuti ya NBS (www.nbs.go.tz - Tanzania in Figures 2018 Uk. 40).

Maoteo ya takwimu hizo yanaonesha kuwa, idadi ya watu walio na ajira imeongezeka kutoka milioni 20.0 mwaka 2014 hadi milioni 22.0 mwaka 2018.

Aidha, takwimu zilizowekwa kwenye Tanzania in Figure 2018 Uk. 41 zinazotokana na taarifa za kiutawala (administrative records) ambazo zinasaidia kupata takwimu za ajira ambazo hazikusanywi kwenye tafiti za kawaida. Takwimu hizi hutumika pia kama kigezo cha kufanya maoteo ya hali ya ajira (proxy indicators) katika vipindi ambavyo hakuna tafiti zilizofanyika ili kutoa hali ya soko la ajira katika vipindi vifupi vifupi na vya kati.

Tafsiri halisi ya Jedwali lililopo uk. 41 wa Tanzania in Figures ni kwamba, mwaka 2017/18 kulikuwa na jumla ya ajira 552,063 zilizozalishwa nchini ikilinganishwa na ajira 453,466 kwa mwaka 2016/17. Hili ni ongezeko la ajira 98,597 sawa na asilimia 21.7 kati ya mwaka 2016/17 na mwaka 2017/18.

Kati ya ajira 552,063 zilizozalishwa nchini mwaka 2017/18, ajira 415,009 sawa na asilimia 75.0 zilikuwa ni ajira kutoka Serikalini; ajira hizi zinajumuisha ajira 18,000 kutoka Serikali Kuu na ajira 397,009 kutoka katika miradi ya maendeleo kupitia Mpango wa Pili wa Maendeleo wa Taifa wa mwaka 2016/17 hadi 2020/21.

Hali hii inatokana na ukweli kuwa, wananchi wengi huajiriwa kwenye miradi ya kimkakati ya maendeleo inayoendelea hapa nchini ambapo Serikali imejikita kwa dhati kuitekeleza kwa ajili ya kufikia uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025 na kupunguza umaskini.

Kwa upande mwingine, ajira 137,054 sawa na asilimia 25.0 ya ajira zote zilizozalishwa na Sekta Binafsi zimepungua kutoka ajira 239,017 mwaka 2016/17 hadi ajira 137,054.

Hivyo, hali halisi kwa jedwali hilo ni kuongezeka kwa ajira Serikalini kutoka 214,449 mwaka 2016/17 hadi 415,009 mwaka 2017/18 sawa na ongezeko la ajira 200,560 (asilimia 94) ya ajira zilizozalishwa mwaka 2016/17.

Ikumbukwe kwamba, Ofisi ya Taifa ya Takwimu hutumia taarifa za kiutawala za ajira kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu; Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu kubaini kiwango cha ajira zilizozalishwa kwa kila mwaka. Huu ndio uzoefu wa nchi nyingi duniani hususan nchi za Afrika.

Utafiti wa Watu wenye Uwezo wa Kufanya Kazi hufanyika kila baada ya miaka mitano ambapo kwa mara ya mwisho ulifanyika mwaka 2014 wakati Utafiti wa Ajira na Mapato katika Sekta Rasmi hufanyika kila mwaka na kwa mara ya mwisho ulifanyika mwaka 2016.

Takwimu hizi za ajira hukusanywa na viashiria mbalimbali vya ajira (Labour Market Indicators) na hutolewa kwa kushirikiana na wadau mbalimbali ikiwa ni pamoja na Shirika la Kazi Duniani (ILO) zikiwa na lengo la kufuatilia na kutathmini sera zilizowekwa na Serikali katika Soko la Ajira.

Mwisho, Ofisi ya Taifa ya Takwimu inausisitiza Umma kupuuza habari hiyo potofu ya kupungua kwa ajira Serikalini na inatoa wito kwa wananchi kuendelea kufanya kazi kwa bidii na maarifa zaidi ili kuunga mkono juhudi zinazoendelea za kujenga uchumi. Aidha, NBS inawaasa wachambuzi wote kufuata matakwa ya Sheria ya Takwimu ya mwaka 2015 kila wanapofanya uchambuzi wa takwimu mbalimbali.

Imetolewa na:

Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS),
DODOMA

14 Agosti 2019


View attachment 1181119
View attachment 1181120



Kuhusu habari inayolalamikiwa, soma:



Hahahaa bora wazifute zile jedwali zao.. Au the best wangezipika tuu basi. Ile habari inasema wazi AJIRA RASMI zimepungua na jedwali inaonyesha hivyo hivyo -78%.
Na kweli AJIRA ZISIZO RASMI yaani VIBARUA zimeongezeka kidogo. Ila kiujumla ajira zimeshuka..
Full stop.
 
Wanamdanganya Nani? Kwanza tulitegemea kabisa watakuja kukanusha kwa hiyo hakuna jipya ukweli ni wa awali.
 
Kwamba 2017/2018 kulikua na ajira 400,000 za seeikali hahahah hawa jamaa bila shaka watakua wamejumuisha wamachinga, mama ntilie, yani hata upikeje data huwezi pata hizo ajira 400,000+ kwa mwaka huo
yaani wanatuona mabwege sana ! hivi hii ndio ajira kweli ?
FB_IMG_1549369100113.jpeg
 
Hii idara ya Takwimu, tukipata serikali ya watu wenye weledi, inatakiwa kufutwa na kuitengeneza upya. Na hawa waongo wa sasa, wafikishwe mahakamani kwa kula njama za upotoshaji.
 
TAARIFA KWA UMMA KUHUSU KUKANUSHA HABARI ILIYOSAMBAZWA KATIKA MITANDAO YA KIJAMII YA KUPUNGUA KWA AJIRA SERIKALINI

Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) inakanusha habari iliyosambazwa katika baadhi ya mitandao ya kijamii hususan Jamii Forum yenye kichwa cha habari “NBS yakiri ajira sekta binafsi zimepungua kwa 42.6%, Serikalini zimepungua kwa 78.1% ndani ya mwaka mmoja."

Habari hii imepotosha kuhusu kupungua kwa ajira Serikalini na hivyo jamii inaombwa kuipuuza kwa kuwa haina ukweli wowote.

Ifahamike kwamba, wakati NBS ikijiandaa kufanya utafiti wa Watu wenye Uwezo wa Kufanya Kazi (Intergrated Labour Force Survey) utakaofanyika mwaka 2019/20, ilifanya maoteo mwaka 2018 (projections) ya mwenendo wa hali ya Soko la Ajira Nchini ambayo yanabainisha mabadiliko yaliyotokea katika soko la ajira tangu mwaka 2014 hadi mwaka 2018. Taarifa hii inapatikana kwenye tovuti ya NBS (www.nbs.go.tz - Tanzania in Figures 2018 Uk. 40).

Maoteo ya takwimu hizo yanaonesha kuwa, idadi ya watu walio na ajira imeongezeka kutoka milioni 20.0 mwaka 2014 hadi milioni 22.0 mwaka 2018.

Aidha, takwimu zilizowekwa kwenye Tanzania in Figure 2018 Uk. 41 zinazotokana na taarifa za kiutawala (administrative records) ambazo zinasaidia kupata takwimu za ajira ambazo hazikusanywi kwenye tafiti za kawaida. Takwimu hizi hutumika pia kama kigezo cha kufanya maoteo ya hali ya ajira (proxy indicators) katika vipindi ambavyo hakuna tafiti zilizofanyika ili kutoa hali ya soko la ajira katika vipindi vifupi vifupi na vya kati.

Tafsiri halisi ya Jedwali lililopo uk. 41 wa Tanzania in Figures ni kwamba, mwaka 2017/18 kulikuwa na jumla ya ajira 552,063 zilizozalishwa nchini ikilinganishwa na ajira 453,466 kwa mwaka 2016/17. Hili ni ongezeko la ajira 98,597 sawa na asilimia 21.7 kati ya mwaka 2016/17 na mwaka 2017/18.

Kati ya ajira 552,063 zilizozalishwa nchini mwaka 2017/18, ajira 415,009 sawa na asilimia 75.0 zilikuwa ni ajira kutoka Serikalini; ajira hizi zinajumuisha ajira 18,000 kutoka Serikali Kuu na ajira 397,009 kutoka katika miradi ya maendeleo kupitia Mpango wa Pili wa Maendeleo wa Taifa wa mwaka 2016/17 hadi 2020/21.

Hali hii inatokana na ukweli kuwa, wananchi wengi huajiriwa kwenye miradi ya kimkakati ya maendeleo inayoendelea hapa nchini ambapo Serikali imejikita kwa dhati kuitekeleza kwa ajili ya kufikia uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025 na kupunguza umaskini.

Kwa upande mwingine, ajira 137,054 sawa na asilimia 25.0 ya ajira zote zilizozalishwa na Sekta Binafsi zimepungua kutoka ajira 239,017 mwaka 2016/17 hadi ajira 137,054.

Hivyo, hali halisi kwa jedwali hilo ni kuongezeka kwa ajira Serikalini kutoka 214,449 mwaka 2016/17 hadi 415,009 mwaka 2017/18 sawa na ongezeko la ajira 200,560 (asilimia 94) ya ajira zilizozalishwa mwaka 2016/17.

Ikumbukwe kwamba, Ofisi ya Taifa ya Takwimu hutumia taarifa za kiutawala za ajira kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu; Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu kubaini kiwango cha ajira zilizozalishwa kwa kila mwaka. Huu ndio uzoefu wa nchi nyingi duniani hususan nchi za Afrika.

Utafiti wa Watu wenye Uwezo wa Kufanya Kazi hufanyika kila baada ya miaka mitano ambapo kwa mara ya mwisho ulifanyika mwaka 2014 wakati Utafiti wa Ajira na Mapato katika Sekta Rasmi hufanyika kila mwaka na kwa mara ya mwisho ulifanyika mwaka 2016.

Takwimu hizi za ajira hukusanywa na viashiria mbalimbali vya ajira (Labour Market Indicators) na hutolewa kwa kushirikiana na wadau mbalimbali ikiwa ni pamoja na Shirika la Kazi Duniani (ILO) zikiwa na lengo la kufuatilia na kutathmini sera zilizowekwa na Serikali katika Soko la Ajira.

Mwisho, Ofisi ya Taifa ya Takwimu inausisitiza Umma kupuuza habari hiyo potofu ya kupungua kwa ajira Serikalini na inatoa wito kwa wananchi kuendelea kufanya kazi kwa bidii na maarifa zaidi ili kuunga mkono juhudi zinazoendelea za kujenga uchumi. Aidha, NBS inawaasa wachambuzi wote kufuata matakwa ya Sheria ya Takwimu ya mwaka 2015 kila wanapofanya uchambuzi wa takwimu mbalimbali.

Imetolewa na:

Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS),
DODOMA

14 Agosti 2019


View attachment 1181119
View attachment 1181120



Kuhusu habari inayolalamikiwa, soma:

Andiko la Quinine hapa ukumbini kuhusu kupungua ajira serikalini na sekta binafsi lilizua mjadala mrefu hadi ikalazimu NBS kukanusha maelezo ya Quinine kwa kueleza kuwa ametafsiri vibaya takwimu zilichapishwa katika kitabu cha Tanzania in Figures cha mwaka 2018. Lakini hata pale NBS ilipotoa ufafanuzi bado mjadala unaendelea. Sasa Quinine imekuwa kama vile Cloroquine yaani kila mgonjwa anapopata nafuu ya ugonjwa wa malaria ndivyo mwili unavyozidi kuwasha! Maana naona mjadala hausimami lakini zaidi hofu yangu unakwenda arijojo.

Mjadala wa tangu juzi unanipa fundisho moja kuu ambalo ni kukosekana kwa ufahamu unaofanana wa dhana ya ajira kati ya NBS na wachangiaji wa majadala hapa ukumbini. Kwa maana nyingine, ni kusema kuwa NBS wanaposema ajira wanamaanisha kitu tofauti na sisi tunaochangia mjadala hapa.

Baada ya kufuatilia kwa makini mjadala huu tangu ulipoanza inaonesha dhahiri kuwa wengi humu hata mimi kabla ya kufanya rejea mbili tatu tukisema ajira tunamaanisha wale tu walioajiriwa Serikalini au wanaofanya kazi kwenye makampuni na kuwaacha wale wote waliofanya shughuli nyingine za kiuchumi.

Hii inajidhihirisha wazi pale baadhi ya wachangiaji wanapohoji Tanzania kuwa na ajira milioni 20.0 mwaka 2014 idadi ambayo inatokana na Utafiti wa Watu wenye Uwezo wa Kufanya Kazi na maoteo ya ajira milioni 22.0 zilizokuwepo mwaka 2018! Nimeufuatilia sana mjadala huu kwa sababu baadhi ya wachangiaji wamekuwa wakionesha ufuatiliaji mzuri wa masuala ya kitakwimu hata wengine kuonesha vielelezo vya kitakwimu kutoka NBS kukazia hoja zao.

Kitaalamu tafsiri ya dhana ya ajira ni pana na imejikita zaidi kwenye dhana ya nzima ya Nguvu Kazi ya Taifa kwa kingereza wanasema Economically Active Population. Dhana hii ndio inayotumika katika tafiti za watu wenye uwezo wa kufanyakazi kama ambao Tanzania ilifanya mwaka 2014 pamoja na maoteo ya ajira ya mwaka 2018. Dhana hii inahusisha watu wote wenye umri wa miaka 15 au zaidi ambao walikuwa na ajira au hawakuwa na ajira lakini walikuwa tayari kufanya kazi, hata kama hawakuchukua hatua yoyote kutafuta kazi katika kipindi rejea cha utafiti.

Je, ni zipi hizo zinazoitwa shughuli za kiuchumi? Katika muktadha huu, shughuli za kiuchumi zinaweza kuwa ni kufanya shughuli yoyote kwa malipo ya fedha taslimu au malipo ya vitu (payment in-kind); kujiajiri binafsi kwenye shughuli za kilimo au zisizo kilimo kwa ajili ya kujipatia faida au kwa ajili ya matumizi binafsi au ya kaya; kusaidia kazi za kiuchumi za kaya bila malipo pamoja na wale wote ambao hawakuwa kazini kwa muda, lakini walitarajia kurudi kazini ndani ya muda mfupi wa kipindi rejea cha Utafiti.

Kwa upande mwingine, watu wote walio nje ya Nguvu Kazi ya Taifa (Economically Inactive Population – Out of Labour Force) ni wale ambao walikuwa hawana ajira katika kipindi rejea cha utafiti na hawakuwa tayari kufanya kazi hata kama kazi zingekuwepo. Kundi hili linahusisha watu kama wanafunzi waliopo masomoni muda wote; wagonjwa wasiojiweza na wale ambao hawataki kufanya kazi yoyote kwa sababu mbalimbali.

Kwa hivyo, utaona kuwa takwimu ambazo NBS walizitoa zilitumia tafsiri hizo ambazo ndio zinazotumiwa kwa mujibu wa miongozo inayotumika katika kukokotoa takwimu za ajira kote ulimwenguni.

Nadhani sasa tunaweza kuendelea na mjadala wetu vizuri zaidi baada ya maelezo haya mafupi ambayo nina hakika yatatusaidia wengi katika mjadala wetu hapa ukumbini.
 
Back
Top Bottom