Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) na Jeshi la Polisi wajitafakari, watanzania sio wajinga

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Nov 25, 2010
6,135
17,802
Hebu tazama kuhusu Kabendera na wengineo:

Kwanza, watu 'wasiojulikana na wasiotaka kujitambulisha' wanafika nyumbani kwa anayetaka kukamatwa. Wananchi wakisogea na kutaka kujua kulikoni, watu hao hudai ni polisi.

Pili, Mkamatwaji hufikishwa Polisi na mahojiano hufanyika. Huhojiwa kwa mambo mbalimbali ynayodhaniwa kutendwa au kushiriki kwa Mkamatwaji. Mahojiano huambatana na Mkamatwaji kuwekwa mahabusu.

Kabrasha lenye nyaraka za taratibu zote zilizofuatwa kuanzia kukamatwa hadi kuhojiwa kwa Mkamatwaji hupelekwa Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka nchini almaarufu kama DPP. Mkuu huyo hupaswa kulipitia kabrasha hilo na kuona kama kuna kosa au makossa yaliyotendwa.

Ofisini kwa DPP, kulingana na nyaraka za mahojiano ya Polisi na Mkamatwaji, huandaliwa Hati ya Mashtaka yenye shtaka au mashtaka kadhaa. IELEWEKE KUWA mashtaka huchipukia kwenye malalamiko ya Mlalamikaji aliyefungua malalamiko Polisi na maelezo aliyoyatoa Mkamatwaji wakati akihojiwa na Polisi. Si chini wala zaidi ya hapo.

Wananchi wanapenda wakosaji wapelekwe Mahakamani na sharia kuchukua mkondo wake. Lakini, hawaridhishwi na namna Mkamatwaji anavyokamatwa, kuwekwa mahabusu na kuhojiwa.Tena wananchi hawaridhishwi na ama na aina ya mashtaka wanayoburuzwa nayo mahakamani Wakamatwaji. Mashtaka hutofautiana na mahojiano ya Polisi na Mkamatwaji.

Vile vile, mashtaka ya sasa kutoka kwa DPP 'huonwa na kuaminiwa' na wananchi kama makossa ya kukomoana. Imekuwa kawaida hivisasa Wakamatwaji kushtakiwa kwa makossa yasiyo na dhamana kama uhujumu uchumi, utakatishaji fedha na ugaidi.

Kutokana na malalamiko ya wananchi, ambao ndiyo hasa wateja wa Mkurugenzi wa Mashtaka na Polisi, Ofisi hizi zinapaswa kujitafakari na kujirekebisha. Si vyema vyombo vinavyopaswa kuaminika na kuwa kimbilio la wananchi wanyonge kutiliwa shaka kila dakika. Watanzania sio wajinga!

Makosa yasiyo na dhamana yasiwe kichaka cha mateso ya kisheria!

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Muleba, Kagera)
 
Inaonekana wameambiwa na aliyewatuma kumkamata Kabendera kuwa lazima wahakikishe ananyamazishwa. Wamemhoji kuhusu uraia wakakosa pa kumkamatia. Wamemhoji kuhusu kumtusi Rais mtandaoni (cyber crime) hata hapo wamemkosa. Sasa DPP ameleta mahakamani mashitaka ambayo hayakuwemo kwe mahojiano. Hawa ni watu wa ajabu sana lakini yote ninkwa sababu ya njaa tu!

Mungu amlinde Kabendera dhidi ya maovu yote huko mahabudu na ampatie uvumilivu. Hili nalo litapita!
 
Inaonekana wameambiwa na aliyewatuma kumkamata Kabendera kuwa lazima wahakikishe ananyamazishwa. Wamemhoji kuhusu uraia wakakosa pa kumkamatia. Wamemhoji kuhusu kumtusi Rais mtandaoni (cyber crime) hata hapo wamemkosa. Sasa DPP ameleta mahakamani mashitaka ambayo hayakuwemo kwe mahojiano. Hawa ni watu wa ajabu sana lakini yote ninkwa sababu ya njaa tu!

Mungu amlinde Kabendera dhidi ya maovu yote huko mahabudu na ampatie uvumilivu. Hili nalo litapita!
Huyu alisha pangiwa baya zaidi ya hilo ukamataji wake uliibumbuluwa mipango hiyo
 
taja majina ya watesaji, hao dpp na mpolisi w
Hebu tazama kuhusu Kabendera na wengineo:

Kwanza, watu 'wasiojulikana na wasiotaka kujitambulisha' wanafika nyumbani kwa anayetaka kukamatwa. Wananchi wakisogea na kutaka kujua kulikoni, watu hao hudai ni polisi.

Pili, Mkamatwaji hufikishwa Polisi na mahojiano hufanyika. Huhojiwa kwa mambo mbalimbali ynayodhaniwa kutendwa au kushiriki kwa Mkamatwaji. Mahojiano huambatana na Mkamatwaji kuwekwa mahabusu.

Kabrasha lenye nyaraka za taratibu zote zilizofuatwa kuanzia kukamatwa hadi kuhojiwa kwa Mkamatwaji hupelekwa Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka nchini almaarufu kama DPP. Mkuu huyo hupaswa kulipitia kabrasha hilo na kuona kama kuna kosa au makossa yaliyotendwa.

Ofisini kwa DPP, kulingana na nyaraka za mahojiano ya Polisi na Mkamatwaji, huandaliwa Hati ya Mashtaka yenye shtaka au mashtaka kadhaa. IELEWEKE KUWA mashtaka huchipukia kwenye malalamiko ya Mlalamikaji aliyefungua malalamiko Polisi na maelezo aliyoyatoa Mkamatwaji wakati akihojiwa na Polisi. Si chini wala zaidi ya hapo.

Wananchi wanapenda wakosaji wapelekwe Mahakamani na sharia kuchukua mkondo wake. Lakini, hawaridhishwi na namna Mkamatwaji anavyokamatwa, kuwekwa mahabusu na kuhojiwa.Tena wananchi hawaridhishwi na ama na aina ya mashtaka wanayoburuzwa nayo mahakamani Wakamatwaji. Mashtaka hutofautiana na mahojiano ya Polisi na Mkamatwaji.

Vile vile, mashtaka ya sasa kutoka kwa DPP 'huonwa na kuaminiwa' na wananchi kama makossa ya kukomoana. Imekuwa kawaida hivisasa Wakamatwaji kushtakiwa kwa makossa yasiyo na dhamana kama uhujumu uchumi, utakatishaji fedha na ugaidi.

Kutokana na malalamiko ya wananchi, ambao ndiyo hasa wateja wa Mkurugenzi wa Mashtaka na Polisi, Ofisi hizi zinapaswa kujitafakari na kujirekebisha. Si vyema vyombo vinavyopaswa kuaminika na kuwa kimbilio la wananchi wanyonge kutiliwa shaka kila dakika. Watanzania sio wajinga!

Makosa yasiyo na dhamana yasiwe kichaka cha mateso ya kisheria!

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Muleba, Kagera)
anaotoa hizo amri ili watu wasioe kwao wala kununua biashara zao
 
Tanzania inakadiriwa kuwa na watu milioni 55! Wataweza kuwanyamazisha wote? Hakuna lenye mwanzo likakosa mwisho. Hizi tawala zinakuja tu na kupita, ila Tanzania itabakia milele.
 
I believe they wanted him dead!

United Republic of Gangsters na kuna watu na "heshima" zao wamenyamaza kimya.

Kuna watu wana miaka miwili mpaka mitatu wapo jela kwa kesi zisizokuwa na dhamana na upelelezi haujaisha. Mahakamani kesi zinahairishwa kwa sababu upelelezi haujakamilika. Wanateswa tu!
 
Zamani adui Mkubwa alikuwa Umasikini,Ujinga na Maradhi.

Leo hii adui Mkubwa wa Serikali ni Mwananchi Mwenyewe.

Ama kupotezwa kabisa ukinusurika ndiyo kama hivi Kabendera.

Unapewa kesi ambayo haina kichwa wala Miguu.
 
"...Watanzania sio wajinga..." JPM remaks on Mo case.
Sasa sijui sisi wenye upeo mdogo, uwezo mdogo na uelewa mdogo tushike lipi na kuacha lipi!
 
Afande Mambo ya Kale ananifurahisha sana. Alitupiga biti ya kueneza uongo na uchochezi sasa cha ajabu ile press conference yake ni dhahiri inaonyesha kuwa kuna wakati vyombo vyetu vina watu waongo sana au hawajui wanalolitenda. Tunakosa weledi. Hati raia wema walishuku uraia wa jamaa, mara ikawa issue ya uchochezi na cyber crime, kuingia mahakamani ghafla bin vuu ikageuka kuwa ni "ujambazi", utakasishaji fedha etc sasa jiulize uchunguzi wa hayo umefanyika lini? Sasa watakukamata ndio waanze uchunguzi. Haya ndio mambo mwanaJF mmoja amesema hutokea kule "SHENZISTAN" au kwa lugha ya Trump "SHITHOLE" countries. Ni terms zinazo udhi zikitumika zidi ya nchi yako, lakini wakati mwingine waweza sema tuna stahili, kwani USTARABU wetu unatia mashaka sana.
 
Afande Mambo ya Kale ananifurahisha sana. Alitupiga biti ya kueneza uongo na uchochezi sasa cha ajabu ile press conference yake ni dhahiri inaonyesha kuwa kuna wakati vyombo vyetu vina watu waongo sana au hawajui wanalolitenda. Tunakosa weledi. Hati raia wema walishuku uraia wa jamaa, mara ikawa issue ya uchochezi na cyber crime, kuingia mahakamani ghafla bin vuu ikageuka kuwa ni "ujambazi", utakasishaji fedha etc sasa jiulize uchunguzi wa hayo umefanyika lini? Sasa watakukamata ndio waanze uchunguzi. Haya ndio mambo mwanaJF mmoja amesema hutokea kule "SHENZISTAN" au kwa lugha ya Trump "SHITHOLE" countries. Ni terms zinazo udhi zikitumika zidi ya nchi yako, lakini wakati mwingine waweza sema tuna stahili, kwani USTARABU wetu unatia mashaka sana.
... nimeipenda hii Shenzistan!
 
... nimeipenda hii Shenzistan!
Tuache sheria ifuate mkondo kama amekosa atahukumiwa kwa makosa aliyotenda na kama hajatenda kosa atakuwa huru.Tusijifikirishe kwa mambo tusiyoyajua undani wake.Pia Usalama ni taaluma za watu.
 
....ni kazini ya watu' wanapoitekeleza kwa weledi na kwa misingi ya sheria. Hata wizi na ujambazi ni kazi za watu, kwa kuwa wanavunja sheria, wanakuwa ni waharifu.
Tuache sheria ifuate mkondo kama amekosa atahukumiwa kwa makosa aliyotenda na kama hajatenda kosa atakuwa huru.Tusijifikirishe kwa mambo tusiyoyajua undani wake.Pia Usalama ni taaluma za watu.
 
Back
Top Bottom