Ofisa Usalama wa Taifa atumbukia ufisadi BoT

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,790
288,004

Ofisa Usalama wa Taifa atumbukia ufisadi BoT
Waandishi Wetu, Dodoma
Daily News; Saturday,February 02, 2008 @19:01

KAMPUNI mbili ambazo zimetumiwa kuchota mabilioni Benki Kuu (BoT) zimegundulika kuwa zinamilikiwa na Ofisa wa Idara ya Usalama wa Taifa mwenye cheo cha juu kabisa. Kampuni hizo ni Clayton Marketing Ltd na Excellent Services Ltd ambazo ni miongoni mwa kampuni 22 zilizotumiwa kuiba Sh bilioni 133 za BoT kupitia Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA).

Habari zimeeleza kuwa ofisa mmoja wa ngazi ya juu ndani ya idara hiyo ndiye anatajwa kama mmoja wa wakurugenzi. Habari za uhakika ambazo gazeti hili limezipata zinaeleza kuwa kampuni hizo zilitumiwa kuchota kiasi kikubwa cha fedha kwa kisingizio cha kazi maalumu ya kitaifa.

Kampuni ya Clayton inatajwa kuchota kwa wakati mmoja dola za Marekani 500,000 kutoka Benki Kuu. "Nyaraka tu iliandikwa kwenda Benki Kuu kwamba tafadhali lipa hizo pesa kwa kazi maalumu, unajua wakati huo hatukujua hizo fedha zinakwenda wapi, sasa tunafahamu," kilidokeza chanzo kimoja cha habari.

Kampuni hizo mbili ni miongoni mwa kampuni zilizolipwa Sh bilioni 42.9 na hakuna nyaraka yoyote iliyowasilishwa kuthibitisha malipo hayo. Kampuni zingine katika kundi hilo ni G&T International Ltd, Mibale Farm, Liquidity Service Ltd, M/S Rashtas (T) Ltd, Kiloloma and Brothers, Karnel Ltd na Malegesi Law Chambers (Advocates) inayomilikiwa na Bedery Malegesi.

Pia gazeti hili limebaini kuwa ofisa huyo kutokana na nafasi yake, ni miongoni mwa watu ambao idara yake imehusishwa katika kuundwa kwa tume maalumu iliyoundwa na Rais Jakaya Kikwete kuchunguza tuhuma hizo. "Kwa kazi yake yeye ni mtu mkubwa katika kamati ile kwani ndiye anayeshughulikia masuala yote ya kigaidi, kiuhalifu wa kimataifa ndani ya Idara ya Usalama wa Taifa," kilidokeza chanzo chetu cha habari.

Mwenyekiti wa kuchunguza ufisadi huo, John Mwanyika alipofuatwa na gazeti hili mjini Dodoma aeleze uhusiano wa Ofisa huyo wa Usalama wa Ikulu na kamati yake alisema kwamba hamfahamu huyo mtu na kamati yake inahusisha watu watatu na wala haihusishi watu wa Usalama wa Taifa.

"Sina taarifa za hizo kampuni unazoniuliza na wala huyo mtu simfahamu," alisema Mwanyika wakati akizungumza na gazeti hili ambalo lilitaka ufafanuzi kama ofisa huyo anahusika kwenye kamati yake. Tume ya kuchunguza suala hilo inaongozwa na Mwanasheria Mkuu kwa kushirikiana na Mkuu wa Polisi na Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa.

Lakini vyanzo vya habari vilithibitisha kuwa Ofisi ya Usalama wa Taifa imeombwa kuhusishwa katika kuchunguza suala hilo kama ambavyo imekuwa inashiriki katika matukio mengine ya uhalifu. Kampuni ya Excellent Service Ltd ambayo imesajiliwa kama inashughulika na masuala ya upokeaji na usafirishaji wa mizigo, wakurugenzi wake wakati huo walimiki asilimia 100 kila mmoja akiwamo Ofisa Usalama huyo.

Kampuni hiyo ofisi zake zinaelezwa kuwa ziko Mtaa wa Sokoine kitalu namba 11649. Oktoba 5, 2004 mwenzake alijiuzulu na akateuliwa mtu anayeitwa Massimo Fanneli kuwa Mkurugenzi. Hisa za Sabbas ambazo ni 100 zilihamishiwa kwa Fannel baada ya kulipwa Sh milioni 5. Kampuni hiyo hadi kufikia Desemba 19 mtaji wake uliongezeka kutoka 500,000 hadi kufikia milioni 5.

Alipotakiwa kuzungumzia kama kampuni zilizoanzishwa na Ofisa Usalama huyo zilikuwa ni kwa ajili ya shughuli za Serikali, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Utawala Bora), Philip Marmo alisema jana kuwa Serikali haijafikia hatua ya kuanzisha kampuni katika idara yake nyeti ya kama ya Usalama wa Taifa.

Alisema kutokana na hali hiyo ni wazi kuwa kampuni anazodaiwa kuanzisha ofisa huyo mwandamizi zilizotajwa katika ubadhirifu wa Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA) hazihusiani na Idara ya Usalama wa Taifa.

"Mimi sifahamu kama ana kampuni lakini kwa mujibu wa Azimio la Zanzibar, anaruhusiwa kuwa na kampuni, lakini zisiingiliane na nafasi yake kwa maana asitumie nafasi yake katika uendeshaji wa kampuni zake. Sasa hivi suala hilo la kampuni zilizohusika na ubadhirifu linashughulikiwa na vyombo vya sheria, mimi siwezi ku comment kitu hapo, tusubiri sheria ifanye kazi," alisema.
 
afisa usalama, mtu huyo nk. hana jina?

kama magazeti yanashindwa kutaja moja kwa moja
si waende brela na kuchukua orodha na kumwaga
majina ya wahusika bila kuonyesha yupi na afisa
usalama. ninahakika wakuu wa kumkoma nyani giladi
watamuumbua tuu hapa jf.
 
sasa kama habari hizi ni za uhakika na vyanzo vyake vimethibitishwa si wangemtaja. Vinginevyo naomba hilo jina mimi nitamtaja. Pleaaase.. but you better back up with some data!
 
Azimio la Arusha lilileta haya ya kuwa na makampuni na huku unatumia Serikali sasa JK kaja na Azimio la Kikwete . Sina uhakika linataka kufanya nini but I think is another hoax.
 
Ningependa kufahamu jina lake.Ningependa kujua uhusiano waKe na Apson Mwang'onda.Mwenye Data anitumie katika PM na mie nitamuanika hadharani.
 
Majina yote yanatajwa hapa chini:

Uchunguzi wa gazeti hili unaonyesha kuwa kampuni za Bencom International Ltd, B. V Holdings Ltd, Venus Hotels Ltd, V.B Associates Company Ltd, Bina Rosort Lt na Bora Hotels & Apartment zote zilisajiliwa kwa siku moja.


Jayantkumar Patel na Devendra Vinodbahi Patel wanatajwa kama wakurugenzi wa kampuni hizo ambazo ziliandikishwa Aprili 4, 2005 zote zikiwa na malengo yanayofanana ya kuagiza na kusafirisha bidhaa mbalimbali nje ya nchi.


Kampuni zote hizo kila moja imeandikishwa kwa mtaji wa Sh milioni 1, kila kampuni ina hisa 100 ambazo zina thamani ya Sh 10,000 kwa kila hisa moja. Kiasi cha Sh bilioni 133 zimechotwa BoT kwa kutumia kampuni 22 ambazo zililipwa kwa kutumia nyaraka bandia.


Patel peke yake anamiliki kampuni nyingine tatu hivyo kufanya aongoze katika wizi wa fedha hizo za umma. Katika mwaka 2005, kampuni nyingi zilizotajwa kuchota mabilioni ziliandikishwa na kusajiliwa.


Kuna kampuni ya Mibale Farms iliandikishwa Septemba 6, 2005, wakurugenzi wake wanatajwa kuwa ni Kiza Selemani na Farijara Hussein, Clayton Marketing Ltd inayomilikiwa na Edwin Mtoi na Elisifu Ngowi na iliandikishwa Juni 6, 2005.


Mwaka huo huo pia kampuni ya Kiloloma and Brothers iliandikishwa Aprili 14. Mkurugenzi wake anatajwa kuwa ni Charles Kissa. Money Planners & Consultants nayo iliandikishwa Machi 24, 2005 na wakurugenzi wake wanatajwa kuwa ni Paul Nyingo na Fundi Kitunga.


Lakini kampuni hizo mbili ni za mtu mmoja maana zinatumia ofisi iliyoko mtaa wa Iramba nyumba namba 7 Magomeni, Dar es Salaam ingawa zilisajiliwa kwa makusudi tofauti.


Moja imesajiliwa kama inashughulika na usambazaji wa vifaa vya ofisini wakati nyingine shughuli yake ni ukusanyaji wa madeni. Mwaka huo wa 2005 kampuni ya Kagoda Agriculture Ltd pia iliandikishwa Septemba 29 na wakurugenzi wake wanatajwa kuwa ni John Kyamuhendo na Francis William.


Kampuni zingine anazomiliki Patel alizoandikisha miaka ya nyuma ambazo nazo amezitumia kuibia Benki Kuu ni Maltan Mining Company ambayo iliandikishwa Machi 1995. Katika kampuni hiyo Patel aliandikisha kampuni hiyo akiwa na mwanahisa mwingine aliyemtaja kwa jina la Haharier Radhakrishnan.


Lakini Agosti 29, mwaka huo huo, Patel akabadilisha jina la kampuni hiyo na kuiita Noble Maltan. Hata hivyo, tangu iandikishwe mwaka huo hakuwahi kuwasilisha taarifa ya mizania BRELA kama sheria inavyomtaka hali iliyosababisha msajili huyo kumwandikia barua kumtaka awasilishe mizania hiyo.


Patel pia ana kampuni nyingine ya Ndovu Soaps Ltd aliyoiandikisha Februari 18, 1992 na tangu wakati huo hakuwahi kuwasilisha wala kulipia taarifa ya mizania. BRELA pia ilimwandikia barua mwaka jana kumtaka awasilishe na kulipia taarifa hiyo muhimu la sivyo angechukuliwa hatua za kisheria.


Kwa mujibu wa Sheria ya Makampuni kifungu 108, mtu anayeandikisha kampuni anatakiwa kuwasilisha taarifa za mizania kila mwaka (Annual Returns Report). Katika taarifa hiyo lazima uonyeshe wakurugenzi waliopo, mtaji wa kampuni na shughuli inayoshughulika nazo.


Kampuni yake nyingine ni Navy Cut Tobacco Tanzania Ltd ambayo aliiandikisha Oktoba 12, 1995 kwa ajili ya kusafirisha nje Tumbaku na bidhaa nyingine inayohusiana na tumbaku. Lakini pia hakuwahi kufanya malipo yoyote ya taarifa ya mizania.


Kampuni ya Liquidity Services Ltd inayomilikiwa na Thabit Katunda na Rajab Maranda iliandikishwa Desemba 17, 2004, Njake Hotel & Tours inayomilikiwa na familia ya Japhet Lema iliandikishwa Aprili 10, 2003 na ilianzishwa kwa mtaji wa milioni 200.


Lakini Mei 13, 2005 ilibadilishwa jina na kuitwa Njake Tours & Safaris Ltd. Baadaye mtaji wake uliongezeka ghafla na kufikia Sh bilioni nane. Kampuni ya Excellent Services Ltd iliandikishwa 2004 na wakurugenzi wake walikuwa ni Emil Sabbas na Elisifa Ngowi.


Kampuni hiyo ilianzishwa kwa mtaji wa Sh 500,000, lakini baadaye Sabbas alijiuzulu na kumuuzia hisa zake Massimo Fanneli Desemba 19, 2005. Ghafla mtaji wa kampuni hiyo uliongezeka hadi kufikia Sh milioni 50.


Karnel Ltd ambayo shughuli zake ni usambazaji wa vifaa vya kuzimia moto ilianzishwa Agosti 4, 1998 kwa mtaji wa Sh milioni moja; lakini kufikia Desemba 15 mtaji wake uliongozeka hadi kufikia Sh bilioni 10. Wakati kampuni ya Uwakili ya Malegesi yenyewe imesajiliwa tangu mwaka 2001 na inaongozwa na Bedery Malegesi. Nayo inatajwa katika ufisadi huo wa BoT.
 

Ofisa Usalama wa Taifa atumbukia ufisadi BoT
Waandishi Wetu, Dodoma
Daily News; Saturday,February 02, 2008 @19:01

KAMPUNI mbili ambazo zimetumiwa kuchota mabilioni Benki Kuu (BoT) zimegundulika kuwa zinamilikiwa na Ofisa wa Idara ya Usalama wa Taifa mwenye cheo cha juu kabisa. Kampuni hizo ni Clayton Marketing Ltd na Excellent Services Ltd ambazo ni miongoni mwa kampuni 22 zilizotumiwa kuiba Sh bilioni 133 za BoT kupitia Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA).

Habari zimeeleza kuwa ofisa mmoja wa ngazi ya juu ndani ya idara hiyo ndiye anatajwa kama mmoja wa wakurugenzi. Habari za uhakika ambazo gazeti hili limezipata zinaeleza kuwa kampuni hizo zilitumiwa kuchota kiasi kikubwa cha fedha kwa kisingizio cha kazi maalumu ya kitaifa.

Kampuni ya Clayton inatajwa kuchota kwa wakati mmoja dola za Marekani 500,000 kutoka Benki Kuu. “Nyaraka tu iliandikwa kwenda Benki Kuu kwamba tafadhali lipa hizo pesa kwa kazi maalumu, unajua wakati huo hatukujua hizo fedha zinakwenda wapi, sasa tunafahamu,” kilidokeza chanzo kimoja cha habari.

Kampuni hizo mbili ni miongoni mwa kampuni zilizolipwa Sh bilioni 42.9 na hakuna nyaraka yoyote iliyowasilishwa kuthibitisha malipo hayo. Kampuni zingine katika kundi hilo ni G&T International Ltd, Mibale Farm, Liquidity Service Ltd, M/S Rashtas (T) Ltd, Kiloloma and Brothers, Karnel Ltd na Malegesi Law Chambers (Advocates) inayomilikiwa na Bedery Malegesi.

Pia gazeti hili limebaini kuwa ofisa huyo kutokana na nafasi yake, ni miongoni mwa watu ambao idara yake imehusishwa katika kuundwa kwa tume maalumu iliyoundwa na Rais Jakaya Kikwete kuchunguza tuhuma hizo. “Kwa kazi yake yeye ni mtu mkubwa katika kamati ile kwani ndiye anayeshughulikia masuala yote ya kigaidi, kiuhalifu wa kimataifa ndani ya Idara ya Usalama wa Taifa,” kilidokeza chanzo chetu cha habari.

Mwenyekiti wa kuchunguza ufisadi huo, John Mwanyika alipofuatwa na gazeti hili mjini Dodoma aeleze uhusiano wa Ofisa huyo wa Usalama wa Ikulu na kamati yake alisema kwamba hamfahamu huyo mtu na kamati yake inahusisha watu watatu na wala haihusishi watu wa Usalama wa Taifa.

“Sina taarifa za hizo kampuni unazoniuliza na wala huyo mtu simfahamu,” alisema Mwanyika wakati akizungumza na gazeti hili ambalo lilitaka ufafanuzi kama ofisa huyo anahusika kwenye kamati yake. Tume ya kuchunguza suala hilo inaongozwa na Mwanasheria Mkuu kwa kushirikiana na Mkuu wa Polisi na Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa.

Lakini vyanzo vya habari vilithibitisha kuwa Ofisi ya Usalama wa Taifa imeombwa kuhusishwa katika kuchunguza suala hilo kama ambavyo imekuwa inashiriki katika matukio mengine ya uhalifu. Kampuni ya Excellent Service Ltd ambayo imesajiliwa kama inashughulika na masuala ya upokeaji na usafirishaji wa mizigo, wakurugenzi wake wakati huo walimiki asilimia 100 kila mmoja akiwamo Ofisa Usalama huyo.

Kampuni hiyo ofisi zake zinaelezwa kuwa ziko Mtaa wa Sokoine kitalu namba 11649. Oktoba 5, 2004 mwenzake alijiuzulu na akateuliwa mtu anayeitwa Massimo Fanneli kuwa Mkurugenzi. Hisa za Sabbas ambazo ni 100 zilihamishiwa kwa Fannel baada ya kulipwa Sh milioni 5. Kampuni hiyo hadi kufikia Desemba 19 mtaji wake uliongezeka kutoka 500,000 hadi kufikia milioni 5.

Alipotakiwa kuzungumzia kama kampuni zilizoanzishwa na Ofisa Usalama huyo zilikuwa ni kwa ajili ya shughuli za Serikali, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Utawala Bora), Philip Marmo alisema jana kuwa Serikali haijafikia hatua ya kuanzisha kampuni katika idara yake nyeti ya kama ya Usalama wa Taifa.

Alisema kutokana na hali hiyo ni wazi kuwa kampuni anazodaiwa kuanzisha ofisa huyo mwandamizi zilizotajwa katika ubadhirifu wa Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA) hazihusiani na Idara ya Usalama wa Taifa.

"Mimi sifahamu kama ana kampuni lakini kwa mujibu wa Azimio la Zanzibar, anaruhusiwa kuwa na kampuni, lakini zisiingiliane na nafasi yake kwa maana asitumie nafasi yake katika uendeshaji wa kampuni zake. Sasa hivi suala hilo la kampuni zilizohusika na ubadhirifu linashughulikiwa na vyombo vya sheria, mimi siwezi ku comment kitu hapo, tusubiri sheria ifanye kazi," alisema.

iri ribubu ha sirierewi. kama uritaka kureta miapari si ingriireta tu. hujuigi kusema na maububu yako hayo si ujuwege hata kuandikaga. sasa rihapari rote hiro harafu hata rijina ra hiro riusarama ra taifa hurijuwi, harafu rimkapa riripopondaga mianikaji ya hapari ya tanzania mukariona rimkapa rijinga. nani nirijinga kwa miapari namuna hii. si hii mianikaji hapari ndio mijinga.
 
Gembe kuwa mpole mzee hapa hadi kujua majina basi itakuwa baada ya kila kitu kufichwa .Mwanamtandao huwa hatajwi kwa uharaka ila ukiwa nje ndiyo utamsikia Meghji anasema alidanganywa .
 
Lakini vyanzo vya habari vilithibitisha kuwa Ofisi ya Usalama wa Taifa anayeitwa ALI SIWA imeombwa kuhusishwa katika kuchunguza suala hilo kama ambavyo imekuwa inashiriki katika matukio mengine ya uhalifu. Kampuni ya Excellent Service Ltd ambayo imesajiliwa kama inashughulika na masuala ya upokeaji na usafirishaji wa mizigo, wakurugenzi wake wakati huo walimiki asilimia 100 kila mmoja akiwamo Ofisa Usalama huyo.
 
Kulingana na habari hapo juu, jina linalotokea kwenye kampuni hizo zote mbili ni la Elisifa Ngowi, je huyu ni usalama wa taifa?
 
kichefuchefu kam cha uja uzito vile. ina maana hawa tunaowaamini kuwa wanalinda usalama wa taifa letu nao wanahusika kuiporomosha nchi?? sasa uzalendo upo wapi?? maana kama uzalendo utaisha ktk mioyo ya watanzania sisi basi hawa usalama ndiyo mioyo ya uzalendo yenyewe. wanakosa nini mpaka wachote hela zote hizo?? au ndo zile enzi za undugunaizesheni ktk kujiunga na kitengo hicho??

naamini kuwa sio usalama wa taifa wote wameoza ila wapo walio wasafi na sijui wata deal vipi na ishu hii.

Nauliza hiviii.... zaidi ya kuweka kura sandukuni, sisi wananchi tunanafasi ipi tena kidemokrasia (i dont believe in it) kuondoa utata huu??? maana kuwazomea hakutoshi, ni budi tuwavue cyupi na tuwatandike viboko hadharani.... (nina hasira sio siri)
 
Ahsante Mtanzania, ila hawa Habari Leo ni wa ajabu sana. Hii habari hapa chini iliandikwa na habari leo Ijumaa iliyopita na The Citizen wakaandika Jumamosi iliyofuatia bila majina (Jumamosi ya wiki iliyopita) lakini cha ajabu ni kwamba habari ya The Citizen iliwekwa hapa JF na majina tukayaanika. Pia katika ile thread ya Ufisadi Usalama wa Taifa, kuna mtu aliweka data hapa na kuonyesha kwa data za JF hii habari ya Habari Leo si ya leo, ila naambiwa walisubiri kuomba kibali kwa JK na wamepata. Waliongea mpaka na RI. JF walitangulia zamaaani!!. Ajabu lEo watu wamesahau. JF NI KOBOKO.

http://www.jamboforums.com/showthread.php?p=128217

http://www.jamboforums.com/showthread.php?t=9182&page=2

http://www.jamboforums.com/showthread.php?t=9252&page=2

http://www.jamboforums.com/showthread.php?p=132715



Majina yote yanatajwa hapa chini:

Uchunguzi wa gazeti hili unaonyesha kuwa kampuni za Bencom International Ltd, B. V Holdings Ltd, Venus Hotels Ltd, V.B Associates Company Ltd, Bina Rosort Lt na Bora Hotels & Apartment zote zilisajiliwa kwa siku moja.


Jayantkumar Patel na Devendra Vinodbahi Patel wanatajwa kama wakurugenzi wa kampuni hizo ambazo ziliandikishwa Aprili 4, 2005 zote zikiwa na malengo yanayofanana ya kuagiza na kusafirisha bidhaa mbalimbali nje ya nchi.


Kampuni zote hizo kila moja imeandikishwa kwa mtaji wa Sh milioni 1, kila kampuni ina hisa 100 ambazo zina thamani ya Sh 10,000 kwa kila hisa moja. Kiasi cha Sh bilioni 133 zimechotwa BoT kwa kutumia kampuni 22 ambazo zililipwa kwa kutumia nyaraka bandia.


Patel peke yake anamiliki kampuni nyingine tatu hivyo kufanya aongoze katika wizi wa fedha hizo za umma. Katika mwaka 2005, kampuni nyingi zilizotajwa kuchota mabilioni ziliandikishwa na kusajiliwa.


Kuna kampuni ya Mibale Farms iliandikishwa Septemba 6, 2005, wakurugenzi wake wanatajwa kuwa ni Kiza Selemani na Farijara Hussein, Clayton Marketing Ltd inayomilikiwa na Edwin Mtoi na Elisifu Ngowi na iliandikishwa Juni 6, 2005.
Mwaka huo huo pia kampuni ya Kiloloma and Brothers iliandikishwa Aprili 14. Mkurugenzi wake anatajwa kuwa ni Charles Kissa. Money Planners & Consultants nayo iliandikishwa Machi 24, 2005 na wakurugenzi wake wanatajwa kuwa ni Paul Nyingo na Fundi Kitunga.


Lakini kampuni hizo mbili ni za mtu mmoja maana zinatumia ofisi iliyoko mtaa wa Iramba nyumba namba 7 Magomeni, Dar es Salaam ingawa zilisajiliwa kwa makusudi tofauti.


Moja imesajiliwa kama inashughulika na usambazaji wa vifaa vya ofisini wakati nyingine shughuli yake ni ukusanyaji wa madeni. Mwaka huo wa 2005 kampuni ya Kagoda Agriculture Ltd pia iliandikishwa Septemba 29 na wakurugenzi wake wanatajwa kuwa ni John Kyamuhendo na Francis William.


Kampuni zingine anazomiliki Patel alizoandikisha miaka ya nyuma ambazo nazo amezitumia kuibia Benki Kuu ni Maltan Mining Company ambayo iliandikishwa Machi 1995. Katika kampuni hiyo Patel aliandikisha kampuni hiyo akiwa na mwanahisa mwingine aliyemtaja kwa jina la Haharier Radhakrishnan.


Lakini Agosti 29, mwaka huo huo, Patel akabadilisha jina la kampuni hiyo na kuiita Noble Maltan. Hata hivyo, tangu iandikishwe mwaka huo hakuwahi kuwasilisha taarifa ya mizania BRELA kama sheria inavyomtaka hali iliyosababisha msajili huyo kumwandikia barua kumtaka awasilishe mizania hiyo.


Patel pia ana kampuni nyingine ya Ndovu Soaps Ltd aliyoiandikisha Februari 18, 1992 na tangu wakati huo hakuwahi kuwasilisha wala kulipia taarifa ya mizania. BRELA pia ilimwandikia barua mwaka jana kumtaka awasilishe na kulipia taarifa hiyo muhimu la sivyo angechukuliwa hatua za kisheria.


Kwa mujibu wa Sheria ya Makampuni kifungu 108, mtu anayeandikisha kampuni anatakiwa kuwasilisha taarifa za mizania kila mwaka (Annual Returns Report). Katika taarifa hiyo lazima uonyeshe wakurugenzi waliopo, mtaji wa kampuni na shughuli inayoshughulika nazo.


Kampuni yake nyingine ni Navy Cut Tobacco Tanzania Ltd ambayo aliiandikisha Oktoba 12, 1995 kwa ajili ya kusafirisha nje Tumbaku na bidhaa nyingine inayohusiana na tumbaku. Lakini pia hakuwahi kufanya malipo yoyote ya taarifa ya mizania.


Kampuni ya Liquidity Services Ltd inayomilikiwa na Thabit Katunda na Rajab Maranda iliandikishwa Desemba 17, 2004, Njake Hotel & Tours inayomilikiwa na familia ya Japhet Lema iliandikishwa Aprili 10, 2003 na ilianzishwa kwa mtaji wa milioni 200.


Lakini Mei 13, 2005 ilibadilishwa jina na kuitwa Njake Tours & Safaris Ltd. Baadaye mtaji wake uliongezeka ghafla na kufikia Sh bilioni nane. Kampuni ya Excellent Services Ltd iliandikishwa 2004 na wakurugenzi wake walikuwa ni Emil Sabbas na Elisifa Ngowi.

Kampuni hiyo ilianzishwa kwa mtaji wa Sh 500,000, lakini baadaye Sabbas alijiuzulu na kumuuzia hisa zake Massimo Fanneli Desemba 19, 2005. Ghafla mtaji wa kampuni hiyo uliongezeka hadi kufikia Sh milioni 50.


Karnel Ltd ambayo shughuli zake ni usambazaji wa vifaa vya kuzimia moto ilianzishwa Agosti 4, 1998 kwa mtaji wa Sh milioni moja; lakini kufikia Desemba 15 mtaji wake uliongozeka hadi kufikia Sh bilioni 10. Wakati kampuni ya Uwakili ya Malegesi yenyewe imesajiliwa tangu mwaka 2001 na inaongozwa na Bedery Malegesi. Nayo inatajwa katika ufisadi huo wa BoT.
 
Mtanzania, si tu kwamba ni Ofisa Usalama, naambiwa ndiye aliyechukua nafasi ya Siwa, katika Kurugenzi ya Usalama wa Ndani, awali alikua akifanya kazi chini ya Siwa, lakini alikua na nguvu kubwa kutokana na kuwa mtu wa DG aliyeondoka. Mkuu Mambo ni mazito kuliko yanavyoonekana.
 
Mtanzania, si tu kwamba ni Ofisa Usalama, naambiwa ndiye aliyechukua nafasi ya Siwa, katika Kurugenzi ya Usalama wa Ndani, awali alikua akifanya kazi chini ya Siwa, lakini alikua na nguvu kubwa kutokana na kuwa mtu wa DG aliyeondoka. Mkuu Mambo ni mazito kuliko yanavyoonekana.

huierewi mijitu humu inchanganyaga mimbo siyo imesahaugi ni mijinga haina miakiri.inajinyaga mijanja kumbe inareta miapari ya kure kare. miapari ya zamani.
 
Mtanzania, si tu kwamba ni Ofisa Usalama, naambiwa ndiye aliyechukua nafasi ya Siwa, katika Kurugenzi ya Usalama wa Ndani, awali alikua akifanya kazi chini ya Siwa, lakini alikua na nguvu kubwa kutokana na kuwa mtu wa DG aliyeondoka. Mkuu Mambo ni mazito kuliko yanavyoonekana.

Mkuu Halisi,
Nilipoona watu wanashangaa majina hayajatajwa nikashangaa maana mimi nimeyaona hapa mara nyingi kama ulivyosema hapo juu. Nikaamua kutumia search engine na ndio nikaipata hiyo habari tena toka kwenye threads za JF.

Labda watu wanasoma haraka haraka na kusahau, Mimi sisomi threads zote ila nikiamua kujibu kitu basi inabidi nisome kila kitu toka mwanzo ili kutojichanganya.

Asante kwa taarifa mkuu. Inaelekea mikono ya Apson na Mkapa imetapakaa kila sehemu. Hii ngoma ni nzito mno. Mpaka sasa nimeshindwa kupata sababu za JK kumteua Mwang'onda kuwa mbunge, je alikuwa analipa fadhila za babake? Au basi tu ni kwasababu alikuwa kijana wa Mtandao?

Sijui kama tutajua ukweli wote kuhusu BOT maana inaelekea watu wengi mno walikuwa wanaogelea hapo.
 
Ukisoma kwa makini habari hii pia utaona mambo yalikwisha kuandikwa.

Vigogo wawatisha mashahidi kashfa BoT

Mwandishi Wetu Januari 30, 2008

Lengo ni kumwokoa mhusika mkuu
WAKUU wa Serikali na vigogo ndani ya Chama Cha Mapinduzi wanahaha kutokana na kashfa nzito ya wizi wa mabilioni Benki Kuu (BoT), na sasa wanafanya kila liwezekanalo ili kuwakinga baadhi ya watuhumiwa wa moja kwa moja wasianikwe hadharani, Raia Mwema imeambiwa.

Hali hiyo inatokana na ukweli kwamba kama yote yatakuwa yamesemwa na kuwekwa hadharani, kuhusu nani wamehusika, basi sura za vigogo kadhaa serikalini na ndani ya CCM zitakosa pa kujificha.

"Sasa kuna shinikizo kwamba watakaokwenda kuhojiwa na tume ya Rais wasitaje baadhi ya majina yaliyohusika katika kashfa hii, majina ambayo yanajitokeza mara kwa mara katika kushiriki wizi huu mkubwa ndani ya BoT," mmoja wa wanachama wakongwe wa CCM ameiambia Raia Mwema.

Lakini kwa mujibu wa ofisa huyo, suala hilo limeleta mgawanyiko mkubwa ndani ya chama chenyewe, huku baadhi wakisema wahusika wawajibike kwa madhambi yao kama yatadhihirika mbele ya vyombo vya sheria ili chama kisije kuathirika.

" Hilo ni suala ambalo linaendelea ndani ya CCM sasa, tena mpaka hata katika ngazi za juu kabisa za Kamati Kuu, ambako kuna wanaotaka mtu aliyehusika awajibike na wengine ambao wanataka mambo haya yazimwe," anaongeza ofisa huyo.

Raia Mwema imefahamishwa pia kwamba baadhi ya watu, watuhumiwa na wasio watuhumiwa katika wizi huo, wamekuwa wakitafadhalishwa wasitaje jina la kigogo mmoja ndani ya CCM ambaye kwa kupitia kampuni ya kughushi, alishiriki kikamilifu kuchota mabilioni ya fedha ambazo sasa inaaminika ziliingia katika kampeni za uchaguzi wa mwaka 2005.

"Hata kabla ya baadhi yao kuitwa mbele ya Kamati aliyoiunda Rais Jakaya Kikwete kuchunguza wizi huo wa BoT, wamekuwa wakipelekewa ujumbe mahsusi kwamba watakapokuwa mbele ya Kamati, wasitaje jina la kigogo huyo.

"Wameelezwa wataje majina ya wafanyabiashara wawili wenye asili ya Asia ili ionekane kwamba hawa ndio pekee waliochota fedha hizo. Na wanaambiwa kwamba wafanyabiashara hao kwa sasa wako tayari kuchukua mzigo huo badala ya kigogo huyo.

"Mmoja kati ya wafanyabiashara hao wanaotajwa kuchukua mzigo wa kigogo huyo ni Jeetu Patel, mwenye kumiliki kampuni tisa ambazo zimetajwa wazi katika wizi huo na ambaye tangu suala hili litangazwe na Serikali yuko nje ya nchi," anasema ofisa huyo akiongeza kwamba mwingine ni mfanyabiashara wa Dar es Salaam ambaye yuko karibu na CCM na ambaye mara kadha amejitosa kutaka kuwa mgombea ubunge.

Vyanzo mbalimbali vya habari vinaeleza kwamba wingu kubwa limetanda kuhusiana na utendaji wa Kamati ya Rais Kikwete inayoongozwa na Mwanasheria Mkuu Johnson Mwanyika na kufanya baadhi ya watu wajiulize iwapo kweli ukweli wa kashafa hiyo utakuja kufahamika katika mazingira ambayo dola inashiriki kutaka kuficha ukweli kuhusu wahusika wakuu.

Baadhi ya wachunguzi wa masuala nyeti kama haya wameiambia Raia Mwema kwamba hakuna cho chote ambacho Serikali na CCM wanaweza kukiokoa kwa kuweka shinikizo ili baadhi ya wahusika wasitajwe katika uchunguzi.

"Wanachofanya ni kuahirisha tu tatizo. Kesi kubwa katika suala hili si wingi wa fedha hizi na wala si nani alihusika, bali tatizo ni kwamba hawa watu walighushi nyaraka. Kwa vyovyote vile kughushi nyaraka ni kosa zito na upelelezi ukifanyika sawasawa, hatimaye hao ambao wanataka kusafishwa sasa watajikuta wakitajwa na kusutwa na nyaraka.

"Kama kweli kuna utashi serikalini, kama ambavyo Rais Kikwete alijaribu kuonyesha wakati wa kutangazwa kwa hatua dhidi ya wizi ndani ya BoT, basi hakuna namna ila kuliacha suala hili liishe bila Serikali wala CCM kuingilia ili hatimaye wahusika wapatikane," anasema mtoa habari wetu.

Raia Mwema imeambiwa pia kwamba jitihada hizo zinazoendelea zimeigusa pia familia ya aliyekuwa gavana Dk. Daudi Ballali ambayo imepelekewa ujumbe kuwaomba wamwambie Dk. Ballali anyamaze.

"Wamekwenda mara mbili na mara zote wamefikisha ujumbe kwamba wanataka wawasiliane na ndugu yao (Dk. Ballali) Marekani ili afunge mdomo wake. Nimeambiwa kwamba familia imechanganyikiwa.

"Wao kama wanafamilia hoja sasa ni kaka yao apone, lakini mara wanapelekewa ujumbe kwamba dola haitaki azungumzie kokote suala hilo la BoT. Hawaelewi maana ya yote haya ni nini. Na tukumbuke kwamba hawa ni Watanzania tu wa kawaida, ujumbe kama huo lazima utawachanganya," anasema mtoa habari huyo.

Bado Dk. Ballali hajaweza kusema lolote, lakini taarifa za waliokuwa karibu naye zinasema kwa jinsi anavyohisi amechafuliwa, wakati ukifika atasema ili asafishe jina lake.

"Huko aliko anasononeka. Haohao ndio waliokuwa wakimshinikiza alipe yale mabilioni. Na hata alipojaribu kubisha ili taratibu za malipo zifuatwe aliambiwa alipe. Sasa wamekwisha kumtumia hata hawazungumzii afya yake ambayo si nzuri. Wanataka ikiwezekana anyamaze moja kwa moja," anasema mmoja wa watu wa karibu na Dk. Ballali ambaye, kutokana na sababu zinazoeleweka, ameomba asitajwe.

Kwa sasa Dk. Ballali anaelezwa kuwa nchini Marekani na bado ana nia ya kurudi Tanzania pamoja na kuwa siku hasa haijulikani hasa kwa kuwa Serikali ya Marekani imetangaza kumfutia viza yake.

Ubalozi wa Marekani nchini, wiki hii umetoa taarifa ukijivua kuwajibika kumrejesha nchini Dk. Ballali kwa maelezo kwamba jukumu hilo kwa sasa ni la Serikali ya Tanzania.

Lakini baada ya viongozi wote wa juu wa CCM kukanusha hadharani kuhusika kwa chama hicho tawala, Spika wa Bunge, Samuel Sitta, amesema kwamba CCM haihusiki moja kwa moja katika sakata la BoT pamoja na kwamba upo uwezekano wa watu binafsi ndani ya CCM kuhusika.

Kutoka Dodoma inaelezwa kwamba Wabunge wameitaka serikali kuwasilisha bungeni ripoti kamili ya ukaguzi wa BoT, hiyo ikiwa baada ya Waziri wa Fedha, Zakia Meghji kuwasilisha bungeni taarifa ya kuelezea hatua za serikali kuhusu ukaguzi huo.

Hata hivyo Spika Sitta amewaeleza wabunge kwamba ofisi yake imekua na mawasiliano na serikali kuhusu suala hilo.

Wakati hayo yakiendelea, gazeti la The Citizen la Jumamosi, Januari 26, 2008 liliandika kuhusika kwa watu wazito ndani ya serikali na likieleza majina ya kampuni za Excellent Services Limited na Clyton Marketing Limited bila kutaja majina ya wakurugenzi wake.

Hata hivyo, vyombo vya habari ikiwa ni pamoja na gazeti la serikali la Kiswahili la Habari Leo lilitaja wakurugenzi wa kampuni hizo na kuainisha jinsi zilivyosajiliwa na kupanda kwa mtaji wake.

Kwa mujibu wa habari hizo ambazo zimethibitishwa na Msajili wa Makampuni (BRELA), wakurugenzi wa Excellent Services yenye makao yake Sokoine Drive, Namba 11649, waliomo ni pamoja na Emmily Samanya, Peter Sabas, Levis Msiko, Elisifa Ngowi na Massimo Faneli, ilipoanzishwa 2004 kwa mtaji wa Sh 500,000/- kabla ya mtaji kuoanda hadi kufikia milioni 50 mwaka 2005.

Kumbukumbu za BRELA na magazeti zimewataja wakurugenzi wa Clyton Marketing Limited, iliyosajiliwa Juni 6, 2005 kuwa ni pamoja na Edwin Mtoi na Elisifa Ngowi. Anuani ya kampuni hiyo ni Plot Namba 707, Mkwepu Dar es Salaam.

"Mmoja kati ya wakurugenzi katika makampuni hayo mawili (anamtaja jina) anatajwa kuwa mkurugenzi mwandamizi na mwenye nguvu katika Idara ya Usalama wa Taifa na amekuwa humo kwa muda mrefu akiwa karibu sana na Mkurugenzi Mkuu aliyestaafu, Cornel Apson," anaeleza ofisa mwandamizi serikalini na kuendelea:

"...(anamtaja jina) amekua katika kitengo kinachofanya kazi ya kupambana na uhalifu ikiwamo ugaidi, rushwa, biashara ya fedha haramu na uhalifu mwingine wa kimataifa, jukumu linalomsogeza karibu zaidi na kamati iliyoundwa na Rais kuchunguza sakata la BoT."
Wakati hayo yakiendelea, kamati hiyo imekwisha kuanza kuwahoji kwa kina wamiliki wa makampuni 22 yanayotajwa katika sakata la BoT huku ikielezwa kwamba nyaraka zote za makampuni hayo zimechukuliwa kutoka BRELA.

Kwa mujibu wa habari hizo nyaraka hizo hasa baada ya kupatikana kwa makampuni yaliyodaiwa kutosajiliwa zimechukuliwa na kamati iliyoundwa na Rais na hakuna mwenye nafasi ya kusoma majalada hayo kwa sasa.

Makampuni ambayo nyaraka zake zilikosekana ni pamoja na G&T International Limited, ambayo imefahamika kumilikiwa na Octavio Timoth na Beredy Malegesi, ambaye anaelezwa kuwa shahidi muhimu katika sakata hilo na huenda "akazibwa mdomo," kwa mujibu wa vyanzo vya habari ndani ya serikali.

Kampuni nyingine ambayo nyaraka zake zimeonekana ni Changanyikeni Residential Complex Limited inayomilikiwa na Jose Vander Merwe, Samson Mapunda na Charles Mabina ikiwa na makao yake, Sinza, Kumekucha, Dar es Salaam.

Sakata la BoT, linaiweka CCM katika mtego mkubwa kutokana na kuhusishwa kwake moja kwa moja na matumizi ya fedha hizo katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2005, lakini viongozi wake wamekanusha madai hayo.

Sasa inafahamika kwamba sehemu kubwa ya fedha ikiwamo zile zilizotokana na kampuni iliyoghushi nyaraka ya Kagoda Agricultural Limited (KAL) iliyochota Sh bilioni 40/- ziliingia katika uchaguzi huo kupitia wana CCM maarufu waliokua katika harakati za kampeni ya Jakaya Kikwete.

Fedha hizo na nyingine ziligawiwa kwa baadhi ya wabunge kwa viwango vilivyotofautiana, na nyingine zilipotea ama kuibwa kutokana na kutokuwapo utaratibu rasmi wa udhibiti na uhakiki wa fedha kitaalamu.

Kwa ujumla sakata zima limemuelemea Dk Ballali ambaye pamoja na kuhusika kwake, ana siri nzito inayoweza kuibua kashfa ya aina yake katika historia ya siasa za Tanzania kama si ya kimataifa.

Pamoja na maelezo kwamba Dk. Ballali alifanya malipo yenye utata kutokana na wakuu wake wa kisiasa kushinikiza, sakata hiyi nzima iliwahusisha watendaji wa BoT na wana CCM maarufu, bado hakuna kati yao anayetajwa wala kuitwa na kamati ya uchunguzi.
 
kazi ipo
na hili la sitta kumzuia makinda asijadili BOT na Richmond, si inaonesha dhahiri kuwa kuna jambo linachukuliwa kwa tahadhari sana hapo?? Na ikichukuliwa baadhi ya wahusika wametajwa dhahiri ila wale mbegu halisi hawajatajwa hadi sasa. Ninapata shaka kama hiyo ripoti kamili itatolewa kwa bunge kuijadili. Nahisi kuna tukio kubwa la kisiasa au hata kinchi litatokea na kutunyima haki ya kujua kinachoendelea na tuhuma za ufisadi BOT.

Pia ikumbukwe uhuru wa vyombo vya habari Tanzania ni kwa nadharia tu.
 
Wabongo hatuwezi kulala. Ina maana hawa jamaa kwa nguvu na network waliyonayo, kama sheria ikichukua mkondo wake wana uwezo mkubwa wa kutuingiza kule ambapo jirani zetu wanajuta kuwepo.
 
Kwa kiasi fulani naanza kupata mwangaza jinsi Thom Apson alivyopata hizo tenda za Ikulu na Benki kuu Zanzibar.
 
Back
Top Bottom