Tabutupu
JF-Expert Member
- Nov 26, 2010
- 13,108
- 18,325
Wanawake hawapendi wanaume wanao otea, wanataka mwanaume mwenye subira na anaye fanya mambo kwa uratatibu. Wakati wanaume wanachokuwa nacho makini ni any hole/ opportunity/njia wazi/ au nafasi yoyote aitumie kufanikisha matakwa yake, bila kujali kesho itakuwaje.
hisia za mwanamke ziko mbali zinahitaji maandalizi kiakili na kimwili, kitu ambacho wanaume wengi hujikutwa wakipuliziwa kipyenga cha kuotea bila wao wenyewe kujua wapi walipo kosea.
Kwa kawaida ili kuwaridhisha wanawake, fanya yafuatayo.
1. Cheza pasi fupi fupi uwanja mzima.
2. Gawa mipira
3. Akichoka na mchakamchaka wa samba, nenda kafunge goli.
Hii si katika swala la ndani ya chumba kile kikubwa. Hata wale walio na wachumba mmsiende haraka kabla hawa viumbe hawaja jua mchezo wako. Ama sivyo atakutega ufanye kosa karibu na penadi box upigwe kadi nyekundu (kibuti) bila idhini yako.
Wekend njema wana jf.