mtarimbo
JF-Expert Member
- Jul 12, 2015
- 1,529
- 3,919
Muungano wa upinzani nchini Kenya National Super Alliance (Nasa) umetoa wito kwa wafuasi wake kususia bidhaa na huduma kutoka kwa kampuni tatu ambazo unadai zimekuwa zikimpendelea Rais Uhuru Kenyatta.
Bw Kenyatta alitangazwa Jumatatu kuwa mshindi wa uchaguzi wa marudio uliofanyika 26 Oktoba, ambao kiongozi wa Nasa Raila Odinga alisusia akisema haungekuwa huru na wa haki.
Bw Odinga alitangaza kabla ya uchaguzi huo kwamba muungano huo utabadilika na kuwa Kundi la Pingamizi dhidi ya Serikali na baadhi ya hatua ambazo ulisema utachukua ni kususia bidhaa na huduma kutoka kwa kampuni ambazo alidai zinamfaa Bw Kenyatta.
Kampuni ambazo Nasa wamesema wafuasi wao wanafaa kususia ni:
•Kampuni ya mawasiliano ya Safaricom, ambayo ndiyo tajiri zaidi miongoni mwa kampuni za Kenya
•Kampuni ya maziwa ya Brookside, inayomilikiwa na familia ya Kenyatta
•Kampuni ya kutengeneza mafuta ya kupikia na sabuni ya Bidco
HUU NDIO UPINZANI WA KIAFRIKA
Bw Kenyatta alitangazwa Jumatatu kuwa mshindi wa uchaguzi wa marudio uliofanyika 26 Oktoba, ambao kiongozi wa Nasa Raila Odinga alisusia akisema haungekuwa huru na wa haki.
Bw Odinga alitangaza kabla ya uchaguzi huo kwamba muungano huo utabadilika na kuwa Kundi la Pingamizi dhidi ya Serikali na baadhi ya hatua ambazo ulisema utachukua ni kususia bidhaa na huduma kutoka kwa kampuni ambazo alidai zinamfaa Bw Kenyatta.
Kampuni ambazo Nasa wamesema wafuasi wao wanafaa kususia ni:
•Kampuni ya mawasiliano ya Safaricom, ambayo ndiyo tajiri zaidi miongoni mwa kampuni za Kenya
•Kampuni ya maziwa ya Brookside, inayomilikiwa na familia ya Kenyatta
•Kampuni ya kutengeneza mafuta ya kupikia na sabuni ya Bidco
HUU NDIO UPINZANI WA KIAFRIKA